Kitendo cha Lema na Familia yake kupewa Asylum Canada kinaashiria Taifa limeanza kutengeneza wakimbizi wa kisiasa, jambo ambalo halina afya

Ukimbizi wanajitengenezea wenyewe, mbona huo Ubalozi wa Canada haukumuuliza Lema kipindi akiwa jambazi wa kuiba magari aliua watu wangapi kama kweli kafanyiwa veting ya kutosha kabla ya kupewa hifadhi ya ukimbizi?
Jambazi ni magufuri anayeongoza squad za maua
 
Lema kala shavu la ukweli,aibu kwa ccm na wizi wao wa kura.
 
Wewe ni mmoja ya wale wanaoamini "wazungu" wanatupandikizia mbegu ya chuki, kutugawa ili watutawale? Kwa nini sisi watu weusi tu ndio tunawezwa kwa ujinga huu wa "kugawanywa"?

Inakuwaje mataifa mengine hayafanyiwi huu ujinga? Halafu, hii hoja kwamba wazungu "hawatupendi" ina umuhimu gani? Tangu lini taifa makini likahangaikia "kupendwa"na mataifa mengine hapa duniani? Taifa linakuwepo na linaendelea kwa mikakati thabiti; na sio kwa hisia za mapenzi! hizo ni kwa viumbe.

Huyo "mzungu" kwanza ni nani hasa? Ndio mkoloni wetu mpya? Unasema "mzungu ana plan hata za miaka 100 mbele ..."! Sisi je? Tuna plan za upeo upi?

Maelezo marefu lakini yamekosa "coherence". Kwa kifupi matatizo ya bara la Afrika yataanza kutatuliwa siku Waafrika watakapoamua kuacha ulaghai na unafiki na kuwa makini na mustakabali wao. Huyo fictitious "mzungu" ni kisingizio tu cha kukwepa kuwajibika kwa ubadhirifu unaofanywa na viongozi wa Kiafrika dhidi ya watu wao.

Hii hoja ya "kuchukiwa" na "kugawanywa" na wazungu sio nzuri inaonyesha kuwa sisi waafrika ndio watu duni sana hapa duniani; kwamba hatuna akili; hatuoni mbali; na tunanunulika kirahisi kwa manufaa ya mataifa mengine; ndio sababu tukauzana utumwani kwa wingi kuliko mataifa yote. NI AIBU.
 

Better for everybody. Angefanya kazi gani baada ya kukosa ubunge? Kukata magari vipande ili wauze spear, asingebaki salama.
Naamini muda unazidi kuongea. Hawa jamaa hawakustahili kukabidhiwa dola
 
Wakimbizi wapo tangu kipindi cha Mkapa wengi tuu, wapo kila kona ya dunia, US, UK, Canada, Belgium, Sweden, nk nk. Sio big deal kihivyo mnavyofikiria, sana sana kaongeza namba ya wategemea benefits, ila ni nzuri kwa watoto wake watasoma vizuri kama wako seerious.
 
Hivi ule unyama mliokuwa mnatenda kwa miaka yote mitano na mauaji, utekaji na utesaji wa raia kwenye uchaguzi, huku ikiagizwa Lema auliwe ama apewe kesi isiyo na dhamana mnadhani dunia ilikuwa haioni?

Mzee mwenyewe anaelezea jinsi kwenye vikao vyao vya Dunia wanavyoona 😂😂😂😂😂
 
Mabeberu wana akili sana, yeye kalilia ukimbizi wakaona wampe lakini mbali na mipaka ya Tanzania, hivyo atakuwa mbali na maisha ya Bongo ambayo ni mazuri sana kuliko huko, hivyo furaha yake ni short lived. Na hali hii haionyeshi kama Tanzania tumeanza kuzalisha wakimbizi, kwani ilitokea 2000 wale wa Pemba n.k UK na Momba
 
Ni kweli,lakini hebu tuwaze.Hivi kweli unapata taarifa ya kuwa kuna kesi ya madawa ya kulevya unaandaliwa utasubiri?
Tujikumbushe kidogo,
  1. Lwakatare aliyekuwa mbunge alipatiwa kesi ya ugaidi na wote mlishuhudia alivyokuwa anaingizwa mahakamani na msafara wake
  2. Rugemalila alifanya biashara na serikali katika circle za juu (sio kupeleka mchele sekondari) leo anaozea rumande
  3. Juzi kuna watu wamekaa rumande 133 days na mwisho wa siku unaambiwa "hatuna interest na hiyo kesi tena"
Police,DPP na judiciary system yetu hebu ijitathmini.Binafsi simtetei mhalifu lakini kubabimbikia watu kesi inaelekea kuwa kama fashion fulani hivi ya kumkomoa usiyemtaka.
 
Sidhani kama Lema ni desparate kiasi unachotaka kuonyesha
 
Ukimbizi wanajitengenezea wenyewe, mbona huo Ubalozi wa Canada haukumuuliza Lema kipindi akiwa jambazi wa kuiba magari aliua watu wangapi kama kweli kafanyiwa veting ya kutosha kabla ya kupewa hifadhi ya ukimbizi?
Alishtakiwa?alipatikana na hatia?
 
Kama kambona alirudi why lema. Hii mijitu ya Kanda ya ziwa roho mbaya Sana ikipewa leseni ya udereva
 
Hapana hilo lisikusumbue kabisa; Kanada hupokea mtu yeyote anayetaka kuhamia kule. Kanada ni nchi kubwa sana yenye eneo takriban kilomita za mraba 10m lakini ambayo idadi ya watu ni ndogo sana kiasi cha 37.6m tu ukilinganisha na Tanzania yenye eneo la kilomita za mraba 1.0m lakini ina watu zaid ya 56.3m; kwa hiyo Kanada wana nafasi nyingi sana za kuweka watu na kuongeza idadi yao.

Canada wanapenda sana nguvu kazi, na unapoona maendeleo ya Canada mengi yanaletwa na hiyo nguvu kazi ya wahamiaji. Hata wewe ukiomba kuhamia Canada leo utapata kirahisi tu mradi usiwe na rekodi ya uharifu. Ila ukishafika, lazima ufanye kazi kweli kweli, siyo mambo ya misheni town tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…