Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu,Mkuu itakua ni drone, UFO huwa hazina sauti kwa mujibu wa maelezo ya waliozishuhudia..
View attachment 2018708
View attachment 2018709
Sijapaelewa hapoKwa sekunde kadhaa kilikuwa angani kikielekea uelekeo wa mawio ya jua. Lakini tofauti na ndege nyingine ziwapo angani, ambapo husafiri kwa upande mrefu kuwa ndio muelekeo wa chombo, chenyewe kilioneka kama vile kinasafiri kwa ulekeo wa mapana yake
Kina shape gani??na kina rangi gani?Nashauri tuzidi kusubiri kwa mashuhuda wengine pia. Pengine ikawa ni mojawapi ya zana za kisasa za kivita zq makamanda wa JWTZ kutoka Lugalo Barracks. Kwa maana hawapo mbali kutoka hapa.
kuna jani flani hivi la kipuuzi likichomwa na moshi wake ukiuvuta lina uwezo wa kumkuza mbu hadi kuwa na ukubwa sawa na size ya bombadia!je hapo mlipokuwa watatu kuna moshi wowote ulikuwa unafuka ndugu mtoa ujumbe?
Isijekuwa uliona mwanga wa taa za Disco.Sijui ni mimi pekee yangu na jirani zangu wawili ambao ndiyo tulikishudia chombo hicho, ama ilitokea pia kwa watu wengine. Ilikuwa jana yapata saa moja jioni, giza ndiyo kwanza limeingia, ile tu natoka nje ya geti la uzio wa nyumba yangu kwenda club kuangalia pambano la soka kati ya Liverpool na Arsenal, nikaanza kusikia sauti ya mvumo kama ule wa sauti za nyuki wengi wawapo angani.
Ilikuwa ni sauti ambayo haiko endelevu, bali inasikika kwa muda na hatimaye inakatika na kubakia kimya kwa kitambo. Nilitembea kama hatua kumi na tano, hivi nikawakuta jirani zangu wawili.
Baada ya kusalimiana walinionyesha kushangazwa na kitu hicho cha ajabu kilichokuwa kikitoa mlio wa ajabu. Licha ya sauti yake pia kilikuwa kikitoa mianga ya taa nyingi za rangi ya bluu.
Kwa sekunde kadhaa kilikuwa angani kikielekea uelekeo wa mawio ya jua. Lakini tofauti na ndege nyingine ziwapo angani, ambapo husafiri kwa upande mrefu kuwa ndio muelekeo wa chombo, chenyewe kilioneka kama vile kinasafiri kwa ulekeo wa mapana yake.
Je! Kuna mtu mwingine pia alilishuhudia jambo hili siku ya jana? Ingalikuwa ni mimi pekee yangu ndiye ambaye nilishuhudia jambo hili ningelipotezea, na hata ningevuta subiri ili atokee shuhuda mwingine ambaye angesimulia.
Sasa mashuhuda tulikuwa ni watatu, tena wote watu waxima. Je! Kuna mtu mwingine aliweza kulishuhudia hapa jukwaani.
Mkuu nami pia nakubaliana na wewe. Lakini andiko langu halikujielekeza kwenye ushawishi ili watu wakubaliane nalo. Bali lilikuwa na ujumbe wa kile ambacho nimekishudia kwa macho yangu mwenyewe.Nadhani maana yangu hujaielewa
Maana yangu haikuwa wewe kutoshea na sisi hiyo habari
Maana yangu ni kwa namna gani unaweza kuwahakikishia wasomaji kua tukio hilo ni kweli
Au kwa maoni yako ni kipi ambacho ukikisoma kwenye hayo maelezo yako kinakupa confidence inayoipa nguvu habari hiyo ionekane ni kweli?
SawaMkuu nami pia nakubaliana na wewe. Lakini andiko langu halikujielekeza kwenye ushawishi ili watu wakubaliane nalo. Bali lilikuwa na ujumbe wa kile ambacho nimekishudia kwa macho yangu mwenyewe.
Suala ni muhimu ni kwamba kama ninasema na kushuhudia uwongo basi uwongo huu uwe juu yangu na Mola wangu. Lakini pia kama ninasema ukweli juu ya hili, basi Mola wangu mwenye haki anashuhudia pamoja nami.
Ndege ya kawaida huwa ni nyembamba kwa upana lakini ni ndefu kwa urefu. Lakini hicho ninachokisema mimi ni tofauti nilipokiona kikiwa angani.Sijapaelewa hapo
Unamaanisha kama ni ndege inakwenda upande yaliko madirisha ya abiria?Ndege ya kawaida huwa ni nyembamba kwa upana lakini ni ndefu kwa urefu. Lakini hicho ninachokisema mimi ni tofauti nilipokiona kikiwa angani.
Nilikiona kikiwa kinatembea angani kikiwa na muonekano wa upana wake lakini ni kifupi kwa urefu wake.
Mfano labla tuseme rula jinsi ilivyo. Ndege za kawaida hutembea angani kwa kuzingatia urefu wake, lakini hiki ninachokisema ni kama kilikuwa kinatembea kwa upana wake.
Nafikiri alimaanisha kilikuwa kinaenda upande upandeSijapaelewa hapo