Kitu gani cha kawaida hujawahi kufanya?

Kitu gani cha kawaida hujawahi kufanya?

Farolito

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2018
Posts
12,001
Reaction score
27,175
Wakuu,

Kuna vitu katika maisha ambavyo ni kawaida kufanywa na watu kila Siku,lakini inawezekana kwa wengine wakawa hawajawahi kufanya kabisa.

Sababu inaweza kuwa kutopenda,kukosa muda,sababu za kiimani nk.

Nikianza na mimi:

1. Sijawahi kabisa kutengeneza juisi ya matunda (Shalubati) katika maisha yangu, pamoja na kwamba huwa natumia ila ni ile iliyotengenezwa na wengine.

2. Sina kabisa akaunti kwenye mitandao maarufu hii mitatu ya Facebook, Instagram na Twitter, habari nyingi napata JF na vyanzo vingine.

Je, wewe ni kitu gani ambacho wengine huona ni cha kawaida kufanya ila kwa upande wako hujawai kufanya?

images.jpg
images%20(1).jpg
 
Sijawahi kupigana.. Ule ugomvi wa kurushiana ngumi..
Uwiii!! Hadi dada yako nimekushinda mana kimtaani mtaani nliwahi kupigana na mvulana kipindi hicho niko mdogo wee alinidunda nakumbuka kulikuwa na mtaro mdogo tu pembeni akanidumbukiza humo nikaanza kulia hadi dada zangu wakaja kunitowa mana sikupigana tena ikabakia nalia tu huku huyo mvulana ananisubiria kwa juu nitoke aniongeze.

Ila toka hapo sijawahi kupigana mana nikawa mwoga hadi kwa wanawake wenzangu kwa hofu nikipigana nao watanipiga. 😅😅
 
Back
Top Bottom