Honestly, sijawahi kuona mchina kwenye mambo professional alafu akawa ana bahatisha, maoni yangu kwa kuwatazama.
1. Juhudi na focus kwenye kila kitu wanachotakiwa kufanya.
2. Nidhamu kwenye maisha, afya, muda, kuwaheshimu wakubwa zao na ndugu zao.
Binadamu yoyote asiye na tatizo la Ubongo anaweza kufanya na kujifunza lolote, binadamu ni most intelligent organism kwenye uso wa dunia.
Namba 1 na 2 utaipata kwa Wayahudi wengi.
Sababu inayotufanya tuwe na tofauti ya wazi, "Ulazima wa kuwa hivyo", au naweza sema "Necessity is mother of invention."
Bara la Africa, lina hali nzuri ya hewa kwa ajili ya kilimo, kuna misitu na mahitaji ya msingi ya jamii kuishi na kusurvive, kwa hiyo inatufanya tusiwe na haja ya kutumia akili yetu yote.
Wazungu/Wachina/Wakorea wao wamekuwa wanaishi kwenye baridi na mazao, wanyawa na vitu vingine muhimu vinahitaji uunde zana tofauti za uwindaji, ujenge makazi maalumu.
Pia kwa sababu wako kwenye eneo dogo risilo na mahitaji mengi inawapelekea kushindania rasilimali ndogo zilizopo, mwisho wa siku wakaanzisha tawala, na civilization baadae na kupelekea kuwa na mifumo au Taasisi za kielelimu na kuchochea maendeleo na tafiti. Wakati, Waafrika hatukuwa au tulichelewa kuwa na concepts za centralized governments, mwisho wa siku kuna traces ndogo sana Taasisi zetu za Elimu, zaidi ya ngoma za asili.