Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Si ni kama vile wewe unavyomuona mke wako mzuri wakati wengine Wala hatuuoni huo uzuri wake. Maana yake nini...ni kwamba mapenz yamekufanya umekuwa kipofu huoni. Sasa kama kitu kidogo hivi kimekushinda kuona ndo utaona paranormal activities!??[emoji1783]

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
🤣🤣🤣Ila mke si yupo...na anaishi so kila mtu atamuona...Sasa we utuambie umemwona jini sijui chumbani kwako...we ni chizi
 
Kuvaa kama Superman hakuna shida

Kuweka sherehe kwa ajili ya Superman iko sawa???

Mkuu acha ujinga kila unachokiona Africa na ulaya kipo...Acha kuwa mtumwa wa fikra
🤣🤣🤣🤣Nenda bac..ulaya makanisa yanageuzwa bar club restaurant kisa watu hawaendi...huku Africa watu ndo wanatajirika na makanisa kisa watu wajinga na Washirikina. Nimekuambiaje Halloween ipo kwa sababu ni tradition. Jamii zao ziliamini uchawi ndio..Ila saa hivi ni fun tu. Ni kama kujikumbushia. Ndo maana watoto wanavaa nguo za mavampires, na vingine kutishana for fun. Ila hawaamini. 🤣Kama unabisha Wikipedia Halloween. Mtu hujui Halloween ni Nini afu unapiga kelele. Yaani ni kama Valentine's day tu, ni siku fulani special kwa ajili ya tradition fulani
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Ila mke si yupo...na anaishi so kila mtu atamuona...Sasa we utuambie umemwona jini sijui chumbani kwako...we ni chizi
Yupo wapi wakati kwenye huu uzi ni wewe peke Yako ndo unamjua mbona sisi hatumuoni na Bado unatuambia yupo!? Na huu ni uchizi pia[emoji2]

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
We Fala mazingaombwe yapo tokea enzi za Musa, behind ze sini ipi tena hiyo unayoongelea[emoji1][emoji1]

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
🤣🤣🤣🤣Aaaah kumbe unaamini Musa alikuwa mtu real. Naamini unafuatilia historia ya misri..ipo kwenye history na science channels kibao..how comes from Egypt history au hata Israel history as a secular (sio ya kidini) hamna records zozote za mtu aitwayo Musa, wamisri hawakumiliki wayahudi Kama watumwa, wayahudi hawakukaa jangwani miaka 40(na hamna archaeology inayoonyesha hivyo) na Canaan ilikuwa Egypt colony by the time...🤣🤣🤣so Musa nae katungwa tu Kama story nyingine ..Kama unabisha fuatilia history ya dunia sio story za mababu za kutungwa
 
1:Kazi ya huyo pope ilikua ni kutoa majini na wachawi

2:Trick gani?? Leta hiyo video itakayoprove hizo tricks za huyo dada acha kuongea kwa maneno
1. Pope saa hivi anatoa mapepo? No why? Coz wameelimika na science wanajua mapepo hamna...
2. Tafuta mi sio field yangu hii..
 
Kuna siku nilikuwa natoka kwenye mihangaiko yangu. Sasa kufika maeneo ya njia panda ya Mwenge nikawa navuka barabara. Wakati navuka, kuna jamaa naye akawa anavuka in opposite direction (tukawa tunaangaliana).

Sasa tukawa kama tunataka kupamiana. Maana nikienda kushoto, jamaa nae anaenda kushoto. Nikienda kulia, jamaa nae anaenda kulia, hadi tukawa tumekaribiana kabisa. Nikaganda kidogo ili kumruhusu yeye afanye uhamuzi, then tupishane, jamaa nae akawa kama vile ananisikilizia Mimi ndo nifanye uhamuzi. Haya yote yalitokea kwa haraka sana, ndani ya muda mfupi, na muda huo kuna cruiser ipo speed inatokea uelekeo wa Kawe inakuja uelekeo wetu Mimi na yule jamaa maana tupo katikati ya barabara, na muda huo zimeruhusiwa gari zinazotoka upande wa Kawe kwenda makumbusho na zinazokata Kona kwenda mawasiliano, za kutokea Makumbusho zimepigwa pini.

Baada ya kuona yule jamaa nae kasimama hanipishi, nikaamua kupita kushoto kwake, ili yeye apite kulia, cha ajabu na yeye akaja upande ule ule, tukawa tumekaribiana kabisa. Baada ya kuhisi hapa tutagongwa na Ile cruiser kwa uzembe, nilijikusanya nguvu zangu zote, nikaamua kumpiga push yule jamaa ili wote tuangukie upande wake, maana sikuwa tena na namna.

Ajabu ni kwamba nilivyojipeleka kumpush, nilijikuta napush hewa, alaf nikaangukia upande wa pili, yule jamaa hakuwepo aisee. Kile kitendo cha kuanguka, Ile cruiser ilipita speed, ikanikosa kidogo sana na haikusimama Wala kupunguza mwendo. Watu waliokuwa maeneo Yale walijua nijirusha kukwepa Ile cruiser, kumbe Mimi nilikuwa nataka kumpush mtu, na wao hawakuona mtu yoyote.
Mkuu itakuwa ulikuwa umelewa
 
Yupo wapi wakati kwenye huu uzi ni wewe peke Yako ndo unamjua mbona sisi hatumuoni na Bado unatuambia yupo!? Na huu ni uchizi pia[emoji2]

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
🤣Ila si wanawake wapo. Mi Nikisema nimeona mbwa hatakama sijawaaminisha na video ya mi kuwa na mbwa tayari mnajua nimemwona coz possibility ipo...Sasa wewe ukisema umelala umeamka Jupiter au umeona ng'ombe anapaa lazma nitaomba uthibitisho coz hii ni extraordinary claim and it requires extraordinary evidence
 
Mi skia kwa mjomba...nimepanga naishi Mimi na mke wangu...🤣au mpaka nije mtaani kwako..okay ukiachana na Hilo. Je Kuna watu ambao hawakai kwa mjomba wao Ila bado hawaamini uchawi? Yes wapo...😁so wao unawapa ushauri gani waone mambo ya kichizi unayoona we na wenzako
Tatizo sio wewe kutoamini uchawi ila tatizo hoja zako ni za kitoto mengi unaongea kwa sababu hujui hata mtaani maisha yakoje.
 
Shida yao hawa watu wa sayansi wanataka kutuambia kuwa hapa duniani hakuna mapepo,kila kitu watakujibu kisayansi kwao
uchawi upo tena sana ila kama haijakutokea utaweka sna hizo theories za kizungu n.k,Kuna mzungu mmoja maeneo flani walikuwa wanachimba mchanga kutafiti dhahabu na Ile sehemu kuwa wachawi wengi tu si akawa anabisha kuwa hakuna uchawi Dunian,usiku alilala kuamuka kesho yake kanyolewa sehemu za Siri mbona aliacha kulala pale kijijini ikawa Kila siku jioni anenda kulala town NB:uchawi upo ila usiepende Kwa waganga ndo utateseka zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
🤣We huna elimu...behind the scenes sio lazma iwe movie .hata live shows Kama Mieleka, dances, etc performance za wasanii Zina behind the scenes. Acha kuwa ignorant sawa. Behind the scenes namaanisha maelezo ya hiyo performance au practice zake hivyo
Ndugu, unajivua nguo. Nimekuambia movie kama mfano tu wa computer fictions unazofikiri ndio Mazingaombwe.

Nikujuze tu, Mazingaombwe ni kitu live hadharani pasipo manuva yoyote ya computer. Yapo na yalikuwepo hata kabla ya kuja kwa mzungu.
 
🤣🤣🤣🤣Okay tiba asilia hata mi naweza kula mmea nikapona. Tuje kwenye tunguli, nyota, nyungu, makaburi...una evidence ya ulisemalo au unaongea kwa hisia...
Mara ngapi nakuambia kwamba ukitaka kushuhudia hayo nitafute, Gharama ni nauli yako tu.
Tiba Asilia aiishii na kula mizizi ya muarubaini dogo, Mawanda yake ni mapana, nimekupa mfano tu wa kulala makaburini, na vipo zaidi ya hapo.
 
Hujui Sayansi ni Nini ..Sayansi haiishi darasa la Saba ulipoishia wewe...Sayansi ipo katika maisha .ukitembea ni Sayansi Kuna skeletal movement, kuna friction, Kuna energy ndo science sawa...elewa bac
Nilishakuambia, Kinachoitwa Uchawi ni Sayansi. Inakoishia Sayansi yako ya darasani ndipo inapoanzia hiyo mnayoita Uchawi.
Sasa hapo ujiulize mwenyewe ni nani ameishia na Sayansi yake ya Newton.

Unajiona uko huru kumbe ni kondoo uliyenona.
 
Mnapoteza sana mda kuwajibu atheist sisi Huwa hatuwajibu maswali yao hayo ya kitoto
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Bas kamwambie mganga wako aniue ..toka hapa na story zako....we na umaskini wako unaenda zahanati yenu ya mtaa hamna hata kipima joto unasema huoni ugonjwa...🤣Hizi story ziishie kwa mwamposa sio hapa
Usipende kuamini kwa maono yako, ulicho nacho ww baki nacho hvyo hivyo na usilazimishe kila mtu aamini kitu unacho kifikilia ww
 
It's not real...mbona inawatokea watu wachache na watu wasio na elimu na wenye maisha duni..mbona watu wanazaliwa mpaka kufa na miaka zaidi ya 50 wasione hivi vitu. Au uchawi unachagua wajinga tu
umekaa na wasomi wote haijawatokea!? Na wasomi Gani hao,mbona wapo wameshatokewa na hayo mambo na hata masikini si wote waliwahi kutokewa,wapo wasomi waliofanyiwa uchawi mpaka Leo akili zao hazipo sawa na wameenda hospitals kubwa hawaoni ugunjwa nalo unasemaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom