Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Tarehe 10/07/2023 asubuhi ya saa moja na dakika kadaa watoto wangu wawili darasa la sita na mwingine la kwanza, walianza kupiga kelele kama kushangaa. Kitendo kilichokera mama yao na mimi pia. Kutoka wananionesha bundi aliye kuwa akidodoka kutokea juu ya bati/ paa ya nyumba yangu. Alipo fika chini alionekana amekufa miguu juu yaani alikufa akiwa chali. Hivyo nikaishia kushangaa tu. Nikawaelekeza watoto wasimwambie mtu yeyote tendo lile. Mwezi mmoja nyuma njiwa poli alikutwa amekufa upenyuni mwa nyumba yangu kubwa amabayo imebakia marumaru na baadhi ya vitu ikamilike. Nilichunguza nikagundua njiwa alijigonga kwenye alminium/ kioo cha dirisha akafa. Sikujali ila niliwaelekeza pia watoto wasiongelee lile tukio.

Sasa huyu bundi baada ya kuonekana amekufa nikarudi ndani kuoga na kujiandaa ili tuelekee kazini na watoto waelekee shule. Sasa mke wangu ana mtoto mwingine wa tatu mwaka mmoja na miezi miwili. Tumemuajiri binti wa jirani anakuja kumchukua na kushinda naye halafu mke wangu anamchukua anapotoka kazini mida ya saa tisa au kumi jioni.
Hivyo alikuja kumchukua mtoto kama ilivyo ada. Kwa kuwa niliwataka watu wasijue mke wangu alipo sikia kengele ina gonga akaniambia yule binti atakuwa ameijia mtoto kwa hiyo nikamtoe yule bundi ili asione ikajulikana kwa kuwa nimeamua iwe siri yetu.

Kweli nilitoka nikamtupe nje ya fensi. Cha kushangaza nilipo msogelea akainuka kama anataka kuruka. Nikachukua fimbo ya ufagio wa ndani nikampiga nayo kwa nguvu mara moja tu akaonekana amekufa. Nikashika bawa lake moja na kumrusha nje ya fensi. Nikaondoka kazini kama kawa.

Kilichofuata mida ya saa nne asubuhi kulitokea kutoelewana na mke wangu kwa kiasi kikubwa na kila nikielezea sababu ya ugonvi huo ndugu wananishangaa kuonesha eti mimi ndiyo mwenye makosa. Ila kiukweli toka hiyo siku sijisikii kumkubali wife hii hali napambana nayo kwa kiasi kikubwa na ninaona speed yangu ya kufanikisha malengo yangu inapungua sana na ninakosa ule umotomoto wa hamasa ya maendeleo kutokana na chuki kwa wife. Hata leo nimeamka na hali ya kutompenda wife, bila sababu ya msingi kwa kukelwa na kosa alilotenda siku hiyo nashindwa kusamehe, japo alikosea sharti langu la kumtaka asiwe anapakizwa na watumishi wenzie wa kiume sipendi na ndicho alifanya. Japo alieleza sababu ya kutenda vile nimekuwa mzito kusamehe.

Sasa wanajamii forum niwaulize sababu ni huyu bundi au ni nini? Hali yangu kwa sasa nimbaya kutokana na sonona takribani mwezi huu wote siko sawa kabisa. Najisikia kukata tamaa.
This is the effect of superstition Sasa
..wote humu mmeona...sorry kwa kinachotokea na mke wako.. ila it's better wote muongee vizuri muelewane what's wrong kuliko kumsingizia mnyama kuhusu ndoa yako...that doesn't solve the problem
 
Hii sio mada kuhusu maendeleo yanayoletwa na uchawi ni kuhusu visa vya ajabu ambavyo vimewahi kumtokea mtu, sasa hayo maendeleo yanakujaje.
Hapa dogo tunasimuliana visa tu unadivert mada eti uchawi haujawahi kumletea mtu maendeleo, kwa hiyo kwa akili yako wanaosimulia hivyo visa unadhani wanategemea uchawi kutafuta maendeleo.
Mi ninajua kuwa uchawi upo lakini sijawahi hata kukanyaga kwa mganga na sitegemei kufanya hivyo my inner power is enough to conquer all dark entities pamoja na hilo haibadilishi ukweli kwamba uchawi upo.
Yaani kumbe upo nje ya topic afu unakaza fuvu kubisha na kujichekesha, tunakuomba uache kurukia comment za watu, we usiyejua haya mambo nenda jukwaa la intelijensia ukacomment kwenye mada za kisayansi hapa tuachie tunaojua visanga tulivyowahi kukutana navyo hapakuhusu period
🤣Nikisema ninajua kucheza mpira utaniambia Nini? Nikuonyeshe si ndio. Nitakuonyesha utaamini kwamba najua? Nikisema jua lipo, nitakuonyesha utaliona utaamini na tayari unajua jua lipo coz it's really there. Huwezi kusema unajua kitu kipo halafu huwezi kukiprove Kama kipo au hakipo, apo sio kujua ni kudhani au kuamini. Unaposema kitu unakijua unajipa majukumu wewe mwenyewe kudhibitisha kwa watu wengine ambao hawajui... Ukisema unadhani au unahisi, u r in a safe position from criticism
 
Eti unanielimisha kwa elimu gani uliyonayo we mtumwa wa fikra, hao mabwana wako wazungu wenyewe sijui pschologist, psychiatrists siwasikilizi pumba zao wala sisomi vitabu vyao kiufupi hawana somo la kunielimisha ndo ije wewe kibaraka, mtumwa brainwashed negropean, eti unielimishe.
Unasema wanaoona hivi vitu ni vichaa wanaona maluweluwe sasa unaanzaje kuwaelimisha vichaa kama we sio kichaa zaidi yao. We dogo utakuwa sio riziki maana hata ushoga ni mental illness.
🤣🤣🤣🤣Acha matusi shoga ni mtu ambae haamini uchawi au? Shoga pia sio mental illness ni sexuality get ur biology ryt au kadai ada...🤣we Kama huna hoja against me tulia...sio unamtukana mtu bila sababu...,🤣 wajinga wakikosa hoja bana
 
Niliwahi kutumia hii kwangu, kuchoma na kimwaga. Hiyo sehemu ilikuwa kila mara bundi wanasogea na kusumbua, mtu aliyekuwa anaishi pale alikuwa hapati usingizi. Mwezi wa 4 huu, bundi hawajai kusogea tena, jamaa analala vizuri na lepe la usingizi.
🤣
 
Uthibitisho wa vp? Elezea unataka uthibitishiwe vp?
We si unaamini uchawi upo, na sitegemei uchawi uwe na limitations za mipaka au umri au elimu ya watu, nataka uyarushe mauchawi huku niyaone na Mimi...🤣kwani shida ni Nini...
 
Inaonyesha hata hauelewi kuhusu psychic reading ni nini ndio mara ya kwanza kusikia hicho kitu halafu cha kusikitisha unalazimisha kubisha tu huku hujui, acha niendelee kukufungua.

Hizi ni baadhi tu ya Psychic abilities ambazo hutumika kwenye psychic reading: Psychometry,Clairvoyant,Clairrecognizance,Clairaudience.
🤣🤣🤣🤣Dogo Nikisema sijui namaanisha ni kitu ambacho tayari nimegundua ni uhuni...mambo ya kusoma karata nyota etc si ndo yote yapo humo..it has nothing to do na uchawi..ni kama mazingaombwe tu nayo unajifunza tu...ni mind games yaani Kama tapeli tu
 
Wametumia jina gani?
🤣 Nimekuambiaje tafuta bible yako niambie sehemu wameandika jinns...mi nakuambia ni Imani ya ancient Arabia Tena kabla ya Muhammad kuja na dini yake waarabu waliamini majini. Sasa wewe unalazimisha sio Arab exclusive nionyeshe jinns kwenye Bible mstari gani
 
Anakera sana huyu jamaa pamoja na wenzake,amejikita hapa kwa watu wenye imani potofu [emoji1787][emoji1787][emoji1787]badala aende kwenye majukwaa ya sayansi huko wakajadiliane namna ya kufika mars,yeye kakaza fuvu mara uchawi haupo z z z z kwani kuna mtu kamlazimisha aamini uchawi
Skia...hivi vitu vinaeffect katika jamii husika. Umeona now mtu hapatani na mke wake badala ya kusolve the problem through communication anaamua kumlaumu bundi mwishowe waachane na watoto wapate shida etc all because of Mila potofu...ndo maana watu wengi wanajaribu kuelimisha watu coz we unaweza ona aaah si Mimi tu naamini shida yako nini, lakini the effect from jamii kuamini hivi vitu ni kubwa leading to conflicts, diseases, deaths, divorces, poor education and health, poverty na kadhalika
 
Nashangaa sijui lisomi la wapi linashindwa kwenda kujadili Artificial Intelligence za kuwafanya binadamu wasitumie tena ubongo mpaka ulemae, limekazana kupambana na watu wasiomuhusu sijui lintafuta nini bwege hili.
Acha matusi leta hoja
 
Back
Top Bottom