Kituko cha mwaka - Wananchi wa Vunjo wamtuma mwakilishi wao Bungeni kuomba kupewa rasmi ardhi na Serikali ili kufanya makazi mapya

Kituko cha mwaka - Wananchi wa Vunjo wamtuma mwakilishi wao Bungeni kuomba kupewa rasmi ardhi na Serikali ili kufanya makazi mapya

Labda wamekuamsha wewe mkuu na kabila lako, sisi waha na wamanyema wa kigoma hatukuamshwa na wachaga na ndio maana babu zeti waliweza kumiliki ardhi kariako na miji mikubwa mingi leo hii tunakula kodi kwa ujanja wa babu zetu kujenga mijini.
Kuna bibi yangu aliuza nyumba kariaKoo milioni mia tano akaenda kununua pembezoni heka za kutosha nazo kauza sana viwanja.Usijumlishe makabila yote, kuna makabila yalishajanjaruka kitambo waha waliwatoa kwenye reli wachaga mikoa ya kanda ya ziwa miaka ya 90 sijui kwa sasa nilihamaga huo ukanda.
Unaota ndoto mkuu,Yan muha amtoe mchaga kwenye reli? Are you serious? Hebu nitajie bilionea mmoja tu wa kigoma [emoji3][emoji3]
 
Kwa hio nyiewachaga kabila zima mmeendelea? Hivi nyinyi wachaga na wasukuma ni nani wanaolisha nchi hii? Ni nani anachangia pato kubwa serikalini?
Nyinyi mmeendelea kwenye nini na wasukuma hawajaendelea kwenye nini? Lile Jiji la mwanza nyinyi wachaga ndio mlili jenga eti?
Kahama nyie wachaga ndio mmeijenga eti? shinyanga nyie ndio mmeijenga eti? Acheni ujinga wa kizamani.
Soma takwimu bwana mdogo,mwanza Ni ya 3 kuchangia Pato la taifa, Kilimanjaro Ni ya 6
Mwanza Ni ya 3 kwa umaskini ,wakati Kilimanjaro Ni ya 2 kwa utajiri,jiji la mwanza pale wachaga wamewekeza pia,maduka makubwa ya spea za magari, maghorofa nk pia au niyakutajie?
 
Kweli kabisa, utawaweza wapi mashoga, wachawi wasiofika kwao, wanaoishia mjini?
sikuwahi kujua kama wachaga mna mambo mengi hivi..
Niendelee?
Wewe una matatizo
Kwamba wachaga hawaend vijijin KWAO? Unajua mkoa unaoongoza kwa makaz bora vijijin ni upi?
Kuhusu uchawi unajua makao makuu ya uchawi Africa mashariki Ni gamboshi? Gamboshi ipo UCHAGANI?
 
Yaani Mbunge wa Vunjo mwenye PhD anamwomba Waziri wa Ardhi awapatie Wachagga wa Vunjo ardhi kwingineko katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sababu ni ili walime kwani kwao wamegawana ardhi kwa mila zao na kujikuta na vipande vidogo sana ambavyo mtu hawezi kulima. Eti wamesongamana, si mpunguze kuzaana.

Hivi huyu Mbunge na hao wachagga wenzie hawaijui Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu freedom of movement?

Hivi yeye mhe. Dr Kimei alipojenga Dar es Salaam na kupata ardhi kubwa Dar mbunge wake wa wakati huo ndio alienda bungeni kumuombea hiyo ardhi? Yaani kabisa anataka annexation ya mkoa wa Kilimanjaro! Au Vunjo nzima ni registered company?

Hivi hao Wasukuma waliojaa huko Mbeya na Morogoro waliomba wapewe hayo maeneo bungeni kupitia wawakilishi wao?

Kwa fikra zake kama hizi huyu bwana hafai kabisa kuwa kiongozi wa juu katika taifa hili kutokana na misingi yake.


Kila mtu anajua toka zamani Kilimanjaro Ina uhaba wa ardhi,labda kwa wavulana km wewe ndiyo hawajui hilo.

Kigezo kuwa wanazaana Sana Ni kukosa uwezo mzuri wa kureason kihesabu(mathematical reasoning) na kutoielewa jiografia ya huo mkoa.
 
Yani huku NJINJO LINDI tunahangaika poli linatuzidi uwezo kumbe kuna watu huko hawana ardhi?.hebu fanyeni mje huku akina Laswai,Tesha,Muro,Lema,Mtei,ila msisahau akina Manka..Serious hili jambo kwangu nalichkulia so positive.Imagine vijiji vyenye mapori makubwa unaletewa wageni elfu 2,within two years utakuwa mji mdogo
 
Wewe usipotoshe. Wakati wa ukoloni eneo hilo liliitwa Jimbo la Kaskazini na Makao yalikuwa Arusha na wala eneo hilo halikuitwa mkoa wa Kilimanjaro kama unavyodanganya. Jimbo hilo lilijumisha eneo kote la mkoa wa Arusha na Manyara ya sasa na mkoa wa Kilimanjaro wa sasa bila kujumlisha wilaya za Same na Mwanga ambazo zilikuwa Jimbo la Tanga. Kwa hiyo kueleza kwamba eti mji wa Arusha ulimegwa kutoka mkoa wa Kilimanjaro ni upotoshaji wa Historia. Baada ya kupata uhuru ndipo yaliyokuwa majimbo yakaanza kugawanywa na kuunda mikoa mipya kutoka majimbo tisa yaliyokuwepo. Katika kuligawa Jimbo la Kaskazini ndipo ukazaliwa mkoa wa Kilimanjaro wenye wilaya mbili kwa wakati huo ambazo ni Moshi kutoka jimbo la kaskazini na Pare kutoka Jimbo la Tanga. Kwa hiyo ni uongo kudai kwamba eti Mji wa Arusha ulimegwa kutoka mkoa wa Kilimanjaro wakati kabla ya uhuru hapakuwa na kitu kilichoitwa mkoa wa Kilimanjaro bali ni Jimbo la kaskazini lenye Makao Makuu Arusha.
Pengine umeadithiwa au una ujinga kichwani ambao hautaki kuutoa, hebu kasome tena historia, hilo jimbo la kaskazini, kabila gani lilikuwa linatawala mkoa wa arusha.

Nenda kajifunze tena kuhusu historia ya wameru, ujue kwamba wachagga wapo kwa sehemu zao, wachagga wa rombo, marangu, old moshi, kibosho, uru, machame, masama na siha, kugawanywa kwa mji wa arusha kuliwagawa wachagga wa meru, ambao baadae waliitwa wameru kutokana na mlima meru, lakini kimantinki hakuna kabila la wameru, maana wameru ni moja ya sehemu ya wachagga na wameru na wachagga hasa wa machame wanasikilizana pure. Hata wao wameru wanajua fika kuwa asili yao ni wachagga asilia. Ni sawa na kuugawa mji wa machame kisha uwaite kabila la wamachame ambapo kimantiki ni makosa ya kijiografia. Au wamarangu alafu uwaite kabila la wamarangu. Hivyo ukiongelea mji wa arusha unaongelea wakazi wake wa asili wameru ambao kwaasili ni sehemu ya wachagga. Utaniuliza kuhusu wa arusha, kabila la wa arusha sio kabila ni wamaasai ambao waliacha kuchunga ng'ombe kwa kuhama hama wao wakaanza kulima mazao, kimila wamaasai hawalimi wala kuchimbua ardhi hata mtu akifa walikuwa hawamziki Bali wanamtelekeza ndani ya boma na kuhama, sasa basi baadhi ya wamaasai wenzao walioamua kulima na kuwa na makao ya kudumu walitengwa na kuanzisha kabila lao ambalo waliita waarusha. Lakini kimsingi waarusha sio kabila kiasilia Bali ni wamaasai walioacha kuchunga na kuanza kulima na kujenga permanently, wengi wao hawa walistaarabika sana.wanaishi arusha .asili hasa ya wamaasai ni maeneo ya monduli, ngorongoro na maeneo ya huko, sio arusha mjini. Kwahiyo bado kumegwa mji wa arusha (meru) na kuwa makao makuu ya mkoa wa arusha kulifanyika kwa kulimega kabila la wachagga na sehemu zake hasa meru kisha wale wachagga wameru wakaitwa wameru kutokana na mlima meru, rudi kasome historia acha kupuyanga ovyo!

Sio wameru tu hata wapare (chasu) wa ugweno, au wagweno asili yao ni uchaggani, kiasi kwamba hawa usikilizana sana na wachagga kwalugha hata koo usishangae ukakuta koo za minja, kesi au kimario/kimaro(na koo nyingine nyingi za asili ya wachagga) huko ugweno. Ambapo wachagga waliamia huko na kuanzisha makazi miaka mingi sana. Sasa kwaupeo wako mdogo usiofahamu historia ukarupuka tena kukanusha. Rudi kasome historia.
 
Msukuma ni level nyingine kwenu. Huwezi kulinganisha watu milioni kumi na ka kikundi ka watu mil. Mbili. Pole sana.
Ukubwa wa pua sio wingi wa Makamasi,

Hata mngekuwa bilioni moja, kama mnanuka umasikini ni buree tu,

Unakuwa wingi kama nyumbu, wakianza safari wanasafiri zaidi ya milioni tatu kutoka Serengeti Tanzanianhadi hadi Maasai Mara Kenya, lakini Simba haogopi huo wingi wa Nyumbu zaidi ya millions tatu ana wala kama mchezo tu.

Wingi bila nguvu ni buree ni kama wingi wa nyumbu tu porini ambao simba wala haogopi, wingi wa ujinga, na umasikini utasababisha mtawaliwe tu kwenye nguvu na utajiri, wachagga, huo ndio ukweli mchungu!
 
Kwa nini hawakupigana wapate ardhi kubwa? Kama wachaga wamekosa ardhi kubwa huwezi nishawishi kuwa walikuwa imara kuliko wamasai, mchaga angeweza kunyang'anya ardhi ya masai au mang'ati acha utani.
Sikulaumu maana hujui Kilimanjaro ikoje,

Ngoja nikuelimishe kidogo japo nikishalisema hili huko juu, wachagga walipofika eneo la Kilimanjaro wakipigana na wenyeji waliowakuta hapo , lengo kuu la wachagga lilikuwa KUPATA ARDHI YENYE RUTUBA zingatia hili neno ARDHI YENYE RUTUBA, na katika eneo la Kilimanjaro kama umewahi kubahatika kufika au hata kusoma historia yake, eneo la ardhi yenye rutuba ni kwenye miteremko ya mlima Kilimanjaro, ambako kutokana na kumwagika kwa volcano miaka ya nyuma na mvua nyingi inayotokana na kuvutwa na mliman huo (dedani) eneo hilo la miteremko ya kuzungika mlima Kilimanjaro likawa lenye rutuba kubwa kwa kilimo na ufugaji.

Hivyo wachagga walipovamia eneo hilo waliliteka na kuishi maeneo hayo, hawakuwa na na maeneo mengine ambayo kiasili ni makame semi arid area, such as simanjiro, upareni , ukambani n.k.

Swali kwanini hawakuteka maeneo mengine jibu ni rahisi sana walikuwa wanatafuta maeneo yenye rutuba ambayo ni kuzunguka mlima Kilimanjaro, ukiangalia maeneo mengine utaona hayana rutuba kama eneo hilo. Lakini kuhusu ushujaa wa wachagga hilo halina ubisha nenda kasome kuhusu wakina mangi Meli, Sina, Mandara n.k. nenda kasome kuhusu impact ya kina Mango Shangali na Mareale katika kuleta Uhuru hapa nchini, hata historia inajieleza wazi kuhusu kabila hill na ushujaa wake kwenye resistance dhidi ya ukoloni hasa wajerumani, tafuta vitabu vya historia ujisomee sina muda wa kuandika hapa,


Wachagga tayari lilikuwa kabila lenye jeshi lake na bendera yake, kiasi cha mwl nyerere kutaka kwanza wachagga wavunje jeshi lao na kushush bendera yao kabla ya kupandisha bendera ya Tanganyija, myerere alidai hatuwezi kuwa na majeshi mawili na bendera mbili ndani ya nchi moja. Rudi kasome kwanini Gavanna wa kiingereza Richard Turnbull alimwandikia barua malikia wa uingereza akinshauri kuwakabidhi Uhuru wa Tanganyika Wachagga?! Akiwasifu kwa akili muundo mzuri wa utawala, uchapakazi na maarifa?!

Rudi kasome historia kuna mengi huyajui kuhusu the great tribe of chagga
 
Hujui kuwa KILIMANJARO tunailisha Nairobi,Mombasa,dar, kwa ndizi na parachichi?
Huko kwenu tunakuja kupiga hela,Kwan wazungu wanapokuja huku tz inamaanisha kuwa tz Ni tajiri kuliko ulaya? Use your common sense
Mchagga hana nafasi kanda ya ziwa ni wachuuzi tu wachache na shoe shiners. Biashara za meli, mahotel, madini na uvuvi ambazo ni uti wa mgongo wa Jiji la Mwanza ni za wenyeji wa kanda hii akina Kitano, Kishimba na wengineo. Kwa mfano Tai five hotel pale kona ya Bwiru ambayo ilikuwa ya mchagga tayari imeisha nunuliwa na msukuma kupitia benki baada ya mchagga kufilisika. Kote huko Geita na Kahama hakuna mchagga mwenye biashara ya maana ni wazawa tu akina Bugomola, Mongo na wenzao wa Kanda ya Ziwa ndio wenye hela. Wadanganye wasioishi kanda hii.
 
Soma takwimu bwana mdogo,mwanza Ni ya 3 kuchangia Pato la taifa, Kilimanjaro Ni ya 6
Mwanza Ni ya 3 kwa umaskini ,wakati Kilimanjaro Ni ya 2 kwa utajiri,jiji la mwanza pale wachaga wamewekeza pia,maduka makubwa ya spea za magari, maghorofa nk pia au niyakutajie?
Nitajie maghorofa matano tu wanayomiliki wachgga hapo Mwanza.
 
Pengine umeadithiwa au una ujinga kichwani ambao hautaki kuutoa, hebu kasome tena historia, hilo jimbo la kaskazini, kabila gani lilikuwa linatawala mkoa wa arusha.

Nenda kajifunze tena kuhusu historia ya wameru, ujue kwamba wachagga wapo kwa sehemu zao, wachagga wa rombo, marangu, old moshi, kibosho, uru, machame, masama na siha, kugawanywa kwa mji wa arusha kuliwagawa wachagga wa meru, ambao baadae waliitwa wameru kutokana na mlima meru, lakini kimantinki hakuna kabila la wameru, maana wameru ni moja ya sehemu ya wachagga na wameru na wachagga hasa wa machame wanasikilizana pure. Hata wao wameru wanajua fika kuwa asili yao ni wachagga asilia. Ni sawa na kuugawa mji wa machame kisha uwaite kabila la wamachame ambapo kimantiki ni makosa ya kijiografia. Au wamarangu alafu uwaite kabila la wamarangu. Hivyo ukiongelea mji wa arusha unaongelea wakazi wake wa asili wameru ambao kwaasili ni sehemu ya wachagga. Utaniuliza kuhusu wa arusha, kabila la wa arusha sio kabila ni wamaasai ambao waliacha kuchunga ng'ombe kwa kuhama hama wao wakaanza kulima mazao, kimila wamaasai hawalimi wala kuchimbua ardhi hata mtu akifa walikuwa hawamziki Bali wanamtelekeza ndani ya boma na kuhama, sasa basi baadhi ya wamaasai wenzao walioamua kulima na kuwa na makao ya kudumu walitengwa na kuanzisha kabila lao ambalo waliita waarusha. Lakini kimsingi waarusha sio kabila kiasilia Bali ni wamaasai walioacha kuchunga na kuanza kulima na kujenga permanently, wengi wao hawa walistaarabika sana.wanaishi arusha .asili hasa ya wamaasai ni maeneo ya monduli, ngorongoro na maeneo ya huko, sio arusha mjini. Kwahiyo bado kumegwa mji wa arusha (meru) na kuwa makao makuu ya mkoa wa arusha kulifanyika kwa kulimega kabila la wachagga na sehemu zake hasa meru kisha wale wachagga wameru wakaitwa wameru kutokana na mlima meru, rudi kasome historia acha kupuyanga ovyo!

Sio wameru tu hata wapare (chasu) wa ugweno, au wagweno asili yao ni uchaggani, kiasi kwamba hawa usikilizana sana na wachagga kwalugha hata koo usishangae ukakuta koo za minja, kesi au kimario/kimaro(na koo nyingine nyingi za asili ya wachagga) huko ugweno. Ambapo wachagga waliamia huko na kuanzisha makazi miaka mingi sana. Sasa kwaupeo wako mdogo usiofahamu historia ukarupuka tena kukanusha. Rudi kasome historia.
Wewe kumbe ni mjinga fulani asiyejua kitu ! Nani kakudanganya kama kuna kabila la wachagga ? Wachagga ni muunganiko wa makabila madogo madogo mengi kama wamachame, wakibosho n.k. tena kwa taarifa yako wengine hawasikilizani. Mrombo akiongea mmchame haioni ndani. Unadai wachagga walitawala Arusha, kama wewe unaijua historia ya nchi hii nitajie ni Mangi gani wa kichagga aliyetawala Arusha na Manyara ya sasa ? Unaposema wachagga walitawala Arusha, unajua maana ya kutawala ? Umekumywa mbege na kuvuta mmea wa Arusha na unakuja na hoja mfu ? Nikuulize swali dogo tu, je, unamfahamu chifu Dodo alikuwa wa wapi ? Acheni kujikweza mbuzi nyie. Kabla ya Uhuru Moshi ilikuwa Wilaya tu katika Jimbo la Kaskazini ambalo makao yake makuu yalilkuwa Arusha na wala hapakuwa na mkoa wa Kilimanjaro kabla ya uhuru. Mkoa Kilimanjaro ulipatikana baada ya kuchukua wilaya ya Moshi toka Jimbo la Kaskazini na Wilya ya Pare toka Jimbo la Tanga na kuunda mkoa wa Kilimnjaro mwaka 1963. Leo unasema eti Arusha ilimegwa toka Kilimanjaro. Pole sana.
 
Back
Top Bottom