Kituko gani alikufanyia mtoto wa mwenyeji wako ulipokuwa ugenini huwezi kukisahau hadi leo hii?

Kituko gani alikufanyia mtoto wa mwenyeji wako ulipokuwa ugenini huwezi kukisahau hadi leo hii?

Nimesoma hizi, zinafurahisha lakini pia kuhuzunisha.
Nawashauri hasa vijana wa kiume ambao wamemaliza chuo au kurudisha mpira kwa kipa ni heri waende kwao kabisa au kwenda kwa mshikaji wako mkapambane pamoja kuliko kwenda kuishi kwa ndugu

Nakumbuka kipindi fulani miaka hiyo ya nyuma nilikuwa nimemaliza chuo, na nimepambana ila mambo magumu ikabidi nirudi mkoani huko kanda ya ziwa na kufikia manispaa kwa mama mdogo ambae anamfuatia mamaangu. Kiuchumi walikuwa poa sana na mme wake na walikuwa na mtoto wao mmoja darasa la 5 ambae anasoma hizi international school
Nimekaa pale mara zikaanza mambo za kuhakikisha kanakula, mara kuosha vyombo ingawa mfanyakazi yupo mara siku nyingine mpo wote na wazazi wake katoe taarifa ya Habari kanaweka katuni yaani vurugu tu.
Siku niliyoamua kutoenda kwa watu
Ni ile kamerudi shule kakaenda kucheza na nguo za shule halafu mamaake akanifokea kwanini nmekaacha kacheze na nguo hizo aiseee nilikakamata nikakapiga. Kakalia kanasema "uondoke uende kwenu sisi hatukutaki hapa, huku kanagalagala chini" na mzee wake akatoka huku anafoka anasema nani Kampiga mwanangu akamchukua akaenda nae town kukanunulia zawadi. Aiseee nilikaa siku mbili nikaondoka nikarudi dsm nikafikia kwa mshikaji tukapambana tukapata ajira na sikuwahi kurudi tena mpaka ingawa huwa tunawasiliana tu. Hata nikienda kikazi kanda ya ziwa sijawahi fikia kwa hao ndugu ingawa wamejenga sana. Mtoto wao huyo alifika six akazingua wakamfanyia mchakato akasoma chuo wakampa asimamie sehemu kapigisha hasara mpaka mzee wake ana sukari, starehe kwa sana kazi anazingua
Jamani malefic ndio kila kitu. Unajitahidi, unapambana unatoboa halafu wanao unawalea kimayai huwaonyeshi namna hela inapatikana ili wawe na nidhamu eti hutaki wateseke ona sasa unasema eti amepata mental health wakati ulimjengea entitlement ya kila kitu bila kumfanya atake responsibilities kwa kila maamuzi anayofanya.
Ni hayo tu tusijisahau kwenye malezi kisa uzungu
Mimi kukaa kwa ndugu hapana unakuwa huna uhuru

Bora kwenu hata kama njaa kali
 
Mtoto mkubwa wa sister ni mkubwa tuu 18 years now kamaliza form 4. kaja home. kufika kakuta wamepika makange akasema yeye hali makange. nkampa hela akaenda nunua chips. asubuh chai tukanunua mihogo kasema halagi mihogo anataka chapati za maji, akapewa. inshu ikaja kwenye kusaidia kazi. hakuna kazi anayoweza labda vyombo tuu kuosha na sio masufuria. kitu pekee anaweza pika ni chai. hata ugali wa mtu mmoja hawezi pika. nkamuuliza vizuri akasema yeye hata kwao wakipika ugali yeye hataki basi anapewa hela anaenda kula mgahawani.

nguo zake anafuliwa. na sio kwamba kwao ni matajiri hapana kipato chao ni cha chini sana.
Aloooh!! Eti halagi nini? Na hela mnampa!!
Nilitembelea sister nikakuta binti eti hafanyi kazi yoyote nyumbani. Dada wa kazi anaamka yeye anaendelea kulala ataamka muda anaojisikia. Weeeh mbona nilimnyoosha. Hadi naondoka anafanya kila kazi. Huwa akiniona tu anajua hakuna ujinga.
 
Mmenikumbusha enzi za utoto wangu .Chakula nilichokuwa napenda sana ni wali ndondo na lazima ndondo lipikwe daily kwa ajili yangu.Sasa ikafika kipindi no wali no ndondo.Sasa kwa kuwa nilikua sitaki ugali nikaamua kuunyea unga uliokuwa umehifadhiwa safi kabisa kwenye kilindo.Jiweke kwenye nafasi ya mzazi unatoka kwenye mihangaiko yako unakuta mwanao kanyea unga.Simu ni moja tu tukutane benki.
 
Mimi mpaka wife ananipiga mkwara kuwa mtoto wetu ndio wa mwisho hazai tena kwa sababu "sipendi" watoto. Ila sio kwamba sipendi watoto, sipendi upuuzi wa watoto. Tena upuuzi wa makusudi.
Sipendi ujinga kabisa.
 
Mjukuu wa mama mwnye nyumba ana miaka kama 3 hivi. Siku hiyo kametoka huko kalikotoka kakaja kunitukana umbwa wewe… aiseeee nilivua lapa nilikapiga halafu nikakabeba nikakapekeka kwa bibi yake nikamwambia nimempiga mjukuu wako huyo hapo. Tangu siku hiyo akiniona ni shikamoo tuu kapuuzi kale
 
Mimi nilikuwa nimeenda kujitambulisha ukweni(nyumbani kwao demu wangu)
Sasa kama ujuavyo familia za kishua tunavua viatu mlangoni tunaingia na kukaa sitting room ghafla kuna katoto ka miaka kama 7 hivi kakarudi kutoka shule kalipofika mlangoni kakachukua soksi zangu kakazibana na kijiti kakaingia nazo sebureni kanauliza kwa sauti "eti mama hizi soksi za nani chafu zimechanika halafu zinanuka vibaya kama mavi ya fungo"
Sebure nzima walicheka kwa sauti yaani niliaibika sana siku hiyo
 
Mimi nakumbuka siku moja nikiwa ugenini, huyu mtoto wa mwenyeji wangu aliing'ang'ania radio yangu na mwenyeji wangu akaniambia tumsubirie asinzie watamnyanganya nakumbuka walinipatia radio yangu saa nne usiku toka saa 12 jioni

Niliwamindi familia yote ila basi tu hawakujua

Weka na wewe cha kwako hapa,
Mwaka flani wageni walikuja nyumbani mtoto akamuomba mama ake simu acheze game mama yake akamwambi imezima chaji na hapakuwa na umeme toka asubuhi

Mama wa huyo mtoto akanambia mpe Basi simu yako acheze game maana ataanza sumbua hapa..nikamjibu haina ilioko ni ya kutumia akili sana sio game last kitoto ..mama yake akasema kuliko Alie we mpe ashindwe🤔

Au mpe a download anajua kutafuta game zake...nikamjibu mwache Alie hii sio PS
 
Back
Top Bottom