Kituko gani alikufanyia mtoto wa mwenyeji wako ulipokuwa ugenini huwezi kukisahau hadi leo hii?

Kituko gani alikufanyia mtoto wa mwenyeji wako ulipokuwa ugenini huwezi kukisahau hadi leo hii?

Mimi nilikuwa nimeenda kujitambulisha ukweni(nyumbani kwao demu wangu)
Sasa kama ujuavyo familia za kishua tunavua viatu mlangoni tunaingia na kukaa sitting room ghafla kuna katoto ka miaka kama 7 hivi kakarudi kutoka shule kalipofika mlangoni kakachukua soksi zangu kakazibana na kijiti kakaingia nazo sebureni kanauliza kwa sauti "eti mama hizi soksi za nani chafu zimechanika halafu zinanuka vibaya kama mavi ya fungo"
Sebure nzima walicheka kwa sauti yaani niliaibika sana siku hiyo
[emoji23][emoji23] "mavi ya fungo"
 
Mimi nakumbuka siku moja nikiwa ugenini, huyu mtoto wa mwenyeji wangu aliing'ang'ania radio yangu na mwenyeji wangu akaniambia tumsubirie asinzie watamnyang'anya nakumbuka walinipatia radio yangu saa nne usiku toka saa 12 jioni

Niliwamindi familia yote ila basi tu hawakujua

Weka na wewe cha kwako hapa,
" Anko utakula kwetu"' Nikawa najifanya sijasikia, nakapotezea lkn bado kanauliza kwa ku-shout!
 
Katoto kadogo darasa la awali namfundisha tuition hapa (do not comment [emoji1787]) jana tu alinisimulia jinsi bibi yake alivyochimba au tuseme alivyouza mchanga eneo la hifadhi akakamata.

Mtoto anamtaja hadi mtu aliyemfitini bibi yake.

Alimtaja hadi aliyemtolea bibi yake hela ya dhamana.

Akaniambia siku ya kesi ni tarehe 8, nimeona mtoto mdogo mwenye uwezo mkubwa wa uelewa.
Kuna mambo watu wazima mkiongea watoto hawatakiwi wasikilize la sivyo unakuja kupata aibu kwa majirani.
Kuna mtoto alisema baba yake kaombwa mchango wa laki na jirani fulani hatatoa kwanza hana hela na maneno mengine kibao aliyoyazungumza baba yake ambayo sio mazuri mbaya zaidi baba huyo aliombwa awe baba wa ubatizo wa mjukuu wa jirani huyo japo wana undugu ila wa mbali kidogo.
Hebu fikiria yule aliyeomba atakaposikia hayo maneno tena kwa mtoto wa miaka sita anayasema kwa watu atajisikiaje.
Mama anasema wazi simpendi fulani kwasababu hii na hii na mtoto akitoka anasema mama yangu kasema hampendi fulani kwanza hataki aje kujisaidia uani kwetu wakati hapo wamepanga wala wenzie hawana shida.
Yaani mtoto anatoo maneno mnayoongea ndani anapeleka nje tena kama ulimsema fulani anamwambia kabisa.
Mtoto anakuwa mmbea toka mdogo badala mzazi akemee anaona kawaida
 
Mimi nilikuwa nimeenda kujitambulisha ukweni(nyumbani kwao demu wangu)
Sasa kama ujuavyo familia za kishua tunavua viatu mlangoni tunaingia na kukaa sitting room ghafla kuna katoto ka miaka kama 7 hivi kakarudi kutoka shule kalipofika mlangoni kakachukua soksi zangu kakazibana na kijiti kakaingia nazo sebureni kanauliza kwa sauti "eti mama hizi soksi za nani chafu zimechanika halafu zinanuka vibaya kama mavi ya fungo"
Sebure nzima walicheka kwa sauti yaani niliaibika sana siku hiyo
Bro ulioa huko kweli?
 
Vituko vya kina junya,, nisivyopenda ujinga wanangu wananyooshwa sawasawa kuna siku walikuwa wanaambizana eti mama ni mkali sana kuliko baba, hataki upuuzi
Upo kama mie, wanajua kabisa Mama hataki masikhara, ila baba yao wanavyomchezea sharubu sasaa, basi nawaangalia nasema ujinga uishie huko sio kwangu.
 
Niliendaga kwa anko

Mwanae wa miaka minne,nimekaazangu nachart si aKaanza kulia,mama yake akamuuliza unataka nini??,,,,,,,,,kakasema kanataka simu yangu kaangalie vichekesho,

Mama yake akaniambia warda mpe mtoto simu achezee maana amezoea kuchezea simu yangu sasa ni mbovu

Nikamwambia sinaga hayo mambo kwenye simu yangu na ata kama zingekuwepo nisingempa katu,atafute cha kuchezea,,,auntie alinuna,,Mtoto wanamlelea kwapani.
Mungu wangu!! Yaani Mtoto analilia Simu anapewa hehehehe ningekafurusha kasingerudi tena, wangu anapenda Simu Baba ake imebidi amnunulie ila anajua fika Simu yangu ni kituo cha polisi iite hapo ataniita na sio kuibeba kuniletea.... Naona kuna sehemu mnafika vitoto vinaomba Simu vicheze Game, Ma Anti wazuri wanawapa Simu zao, Mimi hapana acha nionekane bandidu tu.
 
Upo kama mie, wanajua kabisa Mama hataki masikhara, ila baba yao wanavyomchezea sharubu sasaa, basi nawaangalia nasema ujinga uishie huko sio kwangu.
Yani maza nimenyooka sawasawa sipendi upuuzi kabisa siongei mara mbili mbili,, na hawachezei vitu vyangu hata niiache simu masaa nitaikuta salama,,
 
Pitia uone vituko vya kinajunia[emoji23][emoji23]
Mimi nilijua kuwa ni DENNIS THE MENACE kumbe sasa kuna JUNIOR THE MENACE
dennis-the-menace-EWEA8G.jpg
 
Niliendaga kwa anko

Mwanae wa miaka minne,nimekaazangu nachart si aKaanza kulia,mama yake akamuuliza unataka nini??,,,,,,,,,kakasema kanataka simu yangu kaangalie vichekesho,

Mama yake akaniambia warda mpe mtoto simu achezee maana amezoea kuchezea simu yangu sasa ni mbovu

Nikamwambia sinaga hayo mambo kwenye simu yangu na ata kama zingekuwepo nisingempa katu,atafute cha kuchezea,,,auntie alinuna,,Mtoto wanamlelea kwapani.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Niliendaga kwa anko

Mwanae wa miaka minne,nimekaazangu nachart si aKaanza kulia,mama yake akamuuliza unataka nini??,,,,,,,,,kakasema kanataka simu yangu kaangalie vichekesho,

Mama yake akaniambia warda mpe mtoto simu achezee maana amezoea kuchezea simu yangu sasa ni mbovu

Nikamwambia sinaga hayo mambo kwenye simu yangu na ata kama zingekuwepo nisingempa katu,atafute cha kuchezea,,,auntie alinuna,,Mtoto wanamlelea kwapani.
😂😂😂 anataka vichekesho aliviweka
 
Kwa aunt analmtoto 5years wa kiume,yaani anawasha gesi inshot ana mambo ya hatari sana,muharibifu,binti wa kazi anakoma,

Nilikuwa zangu jikoni nimepika nikatoka,nikasimama dinning natizama nje,

Yule mtoto sijui alipita muda gani kuelekea jikoni,nashtuka nimebandikwa na kisu cha moto mkononi aisee nilitamani ardhi ipasuke,,,,,alidundwa na mama yake na Mungu akamlaani siku ya pili alikuwa anachezea moto wa mkaa akaukanyaga kwa miguu yote miwili,aliungua vibaya sana,

Siku naondoka kananiambia usiondoke mie nitabaki na nani,aunt nikikumisi utakuja kuniona huku kanalia,

Sijaendaga tena,wanaishia tu kuniambia utakuja lini,

Maana aunt analalamika adumu na wasichana wa kazi,,nikagundua shida ni tabia za mwanae maana mwenyewe yupo poa tu

nahisi inasababishwa pia na malezi ya mama pekee
Siku hizi uncle unaongea sana
 
Malezi ya kulea watoto kwapani siwafichi ndugu zangu ndio yanayosababisha kuwe na ongezeko kubwa sana la mashoga siku hizi,hizi tabia za kufumbia macho kila wanachofanya kina Junia ipo siku huko mbeleni tutakuja kujuta..Hii nimewachana jana tu kwenye basi wakati natoka Dodoma kwenda Dar kuna vitoto viwili vilikuwa na wazazi wao basi walikuwa hawatulii kelele wao,mara wapande juu ya siti gari ikiwa mwendo kasi,mara wavute nywele wakubwa halafu wazazi wao wanawaangalia tu nilikaa siti tatu kwa nyuma kutoka kwao si ndio mmoja akajitela bwana kujifanya kuja kwangu ananiuliza maswali kuhusu screen zile zilizopo kwenye siti za Shabiby nikawa namjibu fresh tu huku nikichukua tahadhari maana niligundua ni mtundu,eh!!! si akabonyeza ghafla kitufe kimojawapo cha cha screen nikamsukumia ghafla kuelekea uelekeo wa wazazi wao na mineno juu watu wakaniunga mkono "hawa watoto watundu kweli" hapo ndipo nikaanza kupiga madongo kuhusu malezi ya watoto wazazi wao wakisikia..Sema niligundua hata mzazi wake wa kike pia hana malezi mazuri maana mtu mwenye malezi mazuri hawezi kula hovyohovyo alikuwa na rundo la mivyakula mara miwa,zabibu,mayai,tambi,biscuti,juice,sambusa na vyote alikuwa anakula kwa wakati mmoja
Miwa+ sambusa [emoji1787][emoji1787] shenzi..
 
Mimi nilikuwa nimeenda kujitambulisha ukweni(nyumbani kwao demu wangu)
Sasa kama ujuavyo familia za kishua tunavua viatu mlangoni tunaingia na kukaa sitting room ghafla kuna katoto ka miaka kama 7 hivi kakarudi kutoka shule kalipofika mlangoni kakachukua soksi zangu kakazibana na kijiti kakaingia nazo sebureni kanauliza kwa sauti "eti mama hizi soksi za nani chafu zimechanika halafu zinanuka vibaya kama mavi ya fungo"
Sebure nzima walicheka kwa sauti yaani niliaibika sana siku hiyo
Mimi ningeaga na kuondoka, wangejua pa kunitafuta
 
Mimi nakumbuka siku moja nikiwa ugenini, huyu mtoto wa mwenyeji wangu aliing'ang'ania radio yangu na mwenyeji wangu akaniambia tumsubirie asinzie watamnyang'anya nakumbuka walinipatia radio yangu saa nne usiku toka saa 12 jioni

Niliwamindi familia yote ila basi tu hawakujua

Weka na wewe cha kwako hapa,
Ilinibidi nicheke tu
 
Back
Top Bottom