Kituo cha Mabasi cha Magufuli kimegeuka soko kwa sababu ya usimamizi mbaya

Kituo cha Mabasi cha Magufuli kimegeuka soko kwa sababu ya usimamizi mbaya

Hakuna kituo kibaya kama cha Magufuli, mara mia turudi ubungo.
Hakuna sehemu ya kula..siku nimewahi asubuhi natafuta sehemu ninywe chai sikupata, wamejaa mama ntilie walioweka vyakula kwenye ndoo.
Kwenda toilet...vyoo vimejaa tumepanga foleni. Nilikereka sana

Kuna kanjia ukitokea stand ya daladala usipokuwa na miguu mikakamavu unavunja kiuno
 
Nani ataweka mgahawa sehemu ya mamantilieni wengi na bei iwe hiyo hiyo wakati mwenye mgahawa atahitajika kulipa Kodi na gharama zingine, twende kwenye toilet hiyo stendi imejengwa kwaajili ya abilia na toilet kwaajili ya abilia sasa machinga wengi maana yake ndo watatumia hizo toilet muda wote na abilia watajiju wenyewe kweli haki ya abilia imeminywa kwenye hiyo stendi na pa kusemea hakuna, labda abilia waende bungeni kudai haki zao wabunge wawatete kwenye serikali.
Sio kila mtu anaweza kula kwa mama ntilie, binafsi nilishindwa nikasafiri na njaa yangu. Migahawa iwepo
 
dah pale magomeni sheli nimekanyaga bahati mbaya viatu chini vinauzwa, yani utaratibu hakuna watu wanaweka vitu sehem yoyote wanayojisikia..
 
Hakika inashangaza na Kusikitisha kabisa. SERIKALI inashindwa kuweka na kusimamia Utaratibu Mzuri wa Uendeshaji wa Kituo cha Mabasi cha Magufuli kwa kumwaachia Wafanyabiashara kutandaza na kupanga bidhaa zao kwenye Corridor na sehemu za kupumzika Abiria.

Hivi kusimamia hilo mpaka aje Mzungu? Mbona Viongozi wetu wazembe sana kwenye mambo ya Msingi?

Tunawaomba Wahusika wawaondoe wafanya Biashara wanaopanga na kutandaza bidhaa zao kinyume na Utaratibu.
Mwenye jina la kituo aliwataka wauze bidhaa popote, ndio wanyonge hao.
 
Tatizo la Marehemu Jiwe alitaka kutengeza 'cult' (kama kadini kake mwenyewe chenye wafuasi wanaomuona masiha). Na ili kulitimiza hili akatarget wale wa kipato cha chini sana na kujitwika utetezi hewa.

Kutimiza dhamira yake alikwenda kinyume na mfumo wa kistaarabu ili tu aonekane anajali sana, alifanikiwa kupata wa kumuabudu lakini athari yake inakera wengi zaidi.

Leo hii kupita kariakoo ni tabu maana kumejaa wamachinga kila sehemu, ukija ilala boma barabara imekuwa soko la nyanya na vitunguu.

Na hiyo stendi ya mabilioni ishakuwa kama tandika tayari, yote sababu ya kiumbe mmoja tu aliyetaka kuwa mungu na leo hayupo tena.
Kwa kuongezea ni kwamba lengo kuu la kutengeneza hilo kundi la kumuabudu ni angelitumia kuandamana 2025 ili aongezewe muda wa kutawala. Hilo ndo lilikuwa lengo wala sio kwamba alikuwa anawapenda.
 
Waruhusuni basi wapange bidhaa hadi ikulu..ushen.z kabisa huu.

Mji umekuwa kama wa matahira vile..lazima kuwe na taratibu za kufanya biashara..hii kupanga panga kila sehemu ni ujinga mtupu.
Me sijawahi fika huko mkuu ila nina elewa kinacho zungumzwa kwa lugha ya picha sasa kama wataona ni ajira wanaongeza wafanye mpango na Airport pembeni mwa sehemu ya kurukia ndege pana sehemu ya kupanga nyanya pia!
 
Yaani wamachinga wamekua sio watanzania tena. Yaani ni ubaguzi wa hali ya juu kwa hawa vijana wamachinga. Badala ya watu walete hoja nzuri ya kuwasaidia ndio kwanza wao wanaona kero hawavijana kuwepo hapo na kutafuta rizki zao. Ni kweli ndani ya hao vijana kuna vibaka lakini ingekua vizuri tuwe na roho za huruma. Hata kama leo tuna weza kula na kushiba na kulala mahali pazuri lakini ya kesho tusisahau, mungu ni kubwa na mwenye uwezo wa kutupiga chini mara mmoja na sisi tukahangaika kama hao vijana.
Ushauri ni kwa serikali tu. Wajitahidi kuleta mipango mizuri ya maeneo ya biashara humo humo ndani ya stendi. Watengenezewe mazingira mazuri na wapewe ikiwezekana kwa bei nafuu na Pia wote watakao fanya biashara hapo wapewe elimi kwanza kabla hawajaanza biashara zao.
😍😍😍🙏
 
Kila nchi kuna kumwaga na sehemu kama hizo! Hata London! Wewe ukiona hapa kufai huko chagua sehemu za posta posta, Agakhan, oysterbay na kwingineko penye watu wachache. Watanzania walio wengi maisha ya miksanyiko ndiyo wanapenda!

Hebu fafanua London mtaa gani uko hivyo? Twende na facts hatutaki porojo
 
Hakika inashangaza na Kusikitisha kabisa. SERIKALI inashindwa kuweka na kusimamia Utaratibu Mzuri wa Uendeshaji wa Kituo cha Mabasi cha Magufuli kwa kumwaachia Wafanyabiashara kutandaza na kupanga bidhaa zao kwenye Corridor na sehemu za kupumzika Abiria.

Hivi kusimamia hilo mpaka aje Mzungu? Mbona Viongozi wetu wazembe sana kwenye mambo ya Msingi?

Tunawaomba Wahusika wawaondoe wafanya Biashara wanaopanga na kutandaza bidhaa zao kinyume na Utaratibu.
Ukishalitoa jini kwenye chupa huwezi kulirudisha.
TZ kila kitu tumegeuza chini juu na ujinga ndio maarifa.
 
Nimegundua wa Tz hatuna utaratibu mzuri wa kutunza miundombinu,kabisa hii stand haijatendewa
haki katika kuboresha mfumo mzuri wa kuwapangia wafanyabiashara wadogo kupata rizki zao.naona viongozi wamekaa
kimya kama haiwahusu ili baadae waje kusema jiwe aliharibu.
 
Hakika inashangaza na Kusikitisha kabisa. SERIKALI inashindwa kuweka na kusimamia Utaratibu Mzuri wa Uendeshaji wa Kituo cha Mabasi cha Magufuli kwa kumwaachia Wafanyabiashara kutandaza na kupanga bidhaa zao kwenye Corridor na sehemu za kupumzika Abiria.

Hivi kusimamia hilo mpaka aje Mzungu? Mbona Viongozi wetu wazembe sana kwenye mambo ya Msingi?

Tunawaomba Wahusika wawaondoe wafanya Biashara wanaopanga na kutandaza bidhaa zao kinyume na Utaratibu.
Tatizo sio usimamizi. Tatizo stand haikustahili kuwepo pale kabisa kabisa kabisa. Tumesababisha usumbufu na hasara isiyo na sababu. Tumshauri rais arudishe stand Ubungo na pale pawe chuo kikuu.
 
Unapotimiza haki yako usiziue haki ya mwingine huwezi fanya biashara service road then watembea kwa miguu wapite wapi?
 
Back
Top Bottom