Kitwanga atoa ufafanuzi wa suala la Lugumi na uhusiano wake kuhusu kutumbuliwa kwake

Kitwanga atoa ufafanuzi wa suala la Lugumi na uhusiano wake kuhusu kutumbuliwa kwake

Kuhusu iwapo kufukuzwa kwake kuna uhusiano na sakata la Lugumi au la, Kitwanga alitumia majibu aliyedai kuwa ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere kwa waandishi jijini Nairobi Kenya kwa kuhoji:

"Hivi mtu akikueleza mimi ndiye mume wa mama yako utakubali? Naomba hii ndio iwe jibu langu kwa Watanzania na wote wanaozungumzia suala hili na wasiniuize tena suala," alisema Kitwanga
 
Sasa kama lugumi hakua na uwezo wa kufunga hivyo vifaa alishindaje tenda?? Wasilete story story hapa. Wamepiga dili na huo ndio ukweli.

Dili gani tena...of course Kitwanga amejibu vizuri sana, hakuna dili hapo...hayo ni mambo ya biashara, na kama inforsystems walifanya lobbying wao ndio wafunge vifaa hivyo, hizo ndizo mbinu za biashara...sasa kama vilikuwa havijafungwa wa kuulizwa ni LUGUMI na kampuni ya DELL na siyo KITWANGA...tuache longo longo, leo KITWANGA nimemwelewa...Watanzania wengi tumejaa umbea, wivu, majungu na fitina...hawataki mwenzao afanikiwe...Mimi naichukia tabia hii ya sisi watanzania yaani muda wote kulalamika tu na kuleta habari ambazo ziko half cooked...Sasa waandishi wa habari walishindwa vipi kutueleza kama alivyofanya KITWANGA???
 
Mkuu utaratibu haikufwata..Haiwezekani tenda itangazwe leo kesho watu wawe wameshasainishana tenda..Huyo jamaa hakuwa na uwezo na ilikua ni dili tu hilo.
Hayo ndio mambo iwapo yatazungumzwa kwa ushahidi wa takwimu usiotia shaka.
 
Mbona kama alikuwa tila lila tena huyu baba jamani, lazima a join AA iliyopo jirani naye duh
 
Sasa kama lugumi hakua na uwezo wa kufunga hivyo vifaa alishindaje tenda?? Wasilete story story hapa. Wamepiga dili na huo ndio ukweli.

Ilikuwa ikiwezekana katka miaka 10 ya " Maisha bora kwa kila Mtanzania"
 
Ninachosikitika ni hilo tatizo analolisogelea au sijui tayari keshanasa! Ni ulevi wa kupindukia ni dhihari hapo alipo Ameshazitwanga
 
Masuala kama hili la Lugumi ndo yanayompunguzia Magufuli credibility kwenye vita yake dhidi ya ufisadi. Anaonekana anachagua aina ya ufisadi wa kushuhulikia. Na huo nao ni ufisadi.
 
Aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga akiongea na waandishi wa habari leo amezungumzia suala la Lugumi leo baada ya kutumbuliwa kwake
Amesema Lugumi aliingia mkataba na kampuni ya marekani ambayo ina uwezo wa kufanya kazi na polisi, kampuni hiyo ikanunua vifaa Dell na na kampuni hiyo ikaiomba Dell vifaa hivyo ivifunge Tanzania, Dell wakamchagua Inforsystems hivyo Infosys haina uhusiano wowote na polisi wala Lugumi bali ilikuwa inafanya kazi kwa niaba ya Dell
Pia akijibu swali la kuhusu kutumbuiwa kwake kama linahusiana na Lugumi Kitwanga alitumia majibu aliyedai kuwa ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere kwa waandishi jijini Nairobi Kenya kwa kuhoji ''Hivi mtu akikuuliza mimi ni mume wa mama yako utakubali?'' na kutaka asiulizwe tena swali hilo

Ila alivokuwa anaongea sina uhakika kama ndio ongea yake au alikuwa 'ametupia' tena


Haya wandishi kanjanja endeleeni kumuuliza. Sababu za kutenguliwa uteuzi wake upo wazi na ulikuwa unajua halafu leo unakuja kuuliza kitu hichohicho. Hongera Kitwanga Jibu mujarabu kwa waandishi mufilisi.
 
Dili gani tena...of course Kitwanga amejibu vizuri sana, hakuna dili hapo...hayo ni mambo ya biashara, na kama inforsystems walifanya lobbying wao ndio wafunge vifaa hivyo, hizo ndizo mbinu za biashara...sasa kama vilikuwa havijafungwa wa kuulizwa ni LUGUMI na kampuni ya DELL na siyo KITWANGA...tuache longo longo, leo KITWANGA nimemwelewa...Watanzania wengi tumejaa umbea, wivu, majungu na fitina...hawataki mwenzao afanikiwe...Mimi naichukia tabia hii ya sisi watanzania yaani muda wote kulalamika tu na kuleta habari ambazo ziko half cooked...Sasa waandishi wa habari walishindwa vipi kutueleza kama alivyofanya KITWANGA???
Kwa hiyo umeridhika kabisa na maelezo ya Kitwanga.
 
Kwa hiyo umeridhika kabisa na maelezo ya Kitwanga.
Kiasi chake, ila bado yapo maswali yanayohitaji ufafanuzi bahati mbaya hatuna waandishi wa habari wazuri...kwa mfano wangemuuliza hiyo Infosystems ilipewa muda gani kufunga...na mkataba wa kufunga vifaa hivyo ukoje...Lakini waandishi wa habari nao wameandamwa na mihemuko kama ilivyo wananchi...wanatafuta sensational news tu na siyo kufanya analysis ya issues kwani hawana uwezo huo, sitashangaa hata kidogo kama baadhi ya magazeti yatakuja na stori ya 'KITWANGA ajifananisha na Nyerere'...
 
Kitu bunge lishakizima yeye anatoa ufafanuzi wa nini tena wakati tulia ashatulia nayo tayari au ndo alikua Israeli alipoenda kuungama
 
Analeta longolongo kwenye mambo ya msingi
 
Kiasi chake, ila bado yapo maswali yanayohitaji ufafanuzi bahati mbaya hatuna waandishi wa habari wazuri...kwa mfano wangemuuliza hiyo Infosystems ilipewa muda gani kufunga...na mkataba wa kufunga vifaa hivyo ukoje...Lakini waandishi wa habari nao wameandamwa na mihemuko kama ilivyo wananchi...wanatafuta sensational news tu na siyo kufanya analysis ya issues kwani hawana uwezo huo, sitashangaa hata kidogo kama baadhi ya magazeti yatakuja na stori ya 'KITWANGA ajifananisha na Nyerere'...
Swala la mkataba kusainiwa siku moja baada ya tenda kutangazwa sio ishu kwako?? Kampuni ikiomba tenda ni vigezo gani lazima vifwate ili iweze kupata?? Je Jeshi la polisi lilijirisha kuipa Lugumi tenda siku moja baada ya kutangaza tenda?? Hiyo mikataba ya Lugumi na kampuni ya kimarekani,Dell na Infosys ilikuwepo kwenye mkataba kati ya Lugumi na Jeshi la polisi?? Kama haikuwepo kwa nini izungumziwe na wakati serikali imeingia mkataba na Lugumi?? Kwa nini Lugumi alipwe 99% ya fedha zote na wakati amefanya kazi kwa 10% na alikua hajamaliza vuzuri katika hiyo 10%??
Hayo maswali yakijibiwa vizuri nitajua kwamba hakuna harusu ya ufisadi kwenye huo mkataba.
 
Najiuliza ni je aliwaita waandishi wa habari? kama ndio hivyo kwa nini aansema msiniulize maswali?????? halagu waandishi bana bado hawajakomaa badala ya kumwuliza wote wakaganda duuh jamani hii kazi zinahitaji ujasiri
 
Eti "Mtu Akikuuliza Mimi ni Mume wa Mama Yako Utajibuje..."
ahahaha

Aliuliza "hivi mtu akikuambia mimi ni baba yako utakubali tu?". Tafsiri mwenyewe maana ya kauli hiyo ya kuudhi ya mzee wa mjini.
 
Khaa, kutupia tena? huyu jamaa ni noumer, ile siku Magufuli alipokua akilalamikia usafirishwaji wa GBM (Gold Bearing Materials) inaonekana ni yeye tu ndio aliyekua kutupia. Kweli jamaa anajua kutwanga aise.
 
Huyu Kitwanga anazidi kumharibia JPM. Keshatumbuliwa kiaina. Inatosha; aridhike. Atulie sasa vumbi litue JPM arejee kasi yake ya utumbuaji.
 
Back
Top Bottom