Pre GE2025 Kiukweli 2025 simuoni Rais Samia akishinda kwenye Boksi la kura kama upinzani wakiweka mtu mahiri

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Luhaga Joelson Mpina akimtimua CCM chadema anapata mgombea takayebwaingizia kura nyingi sana Kwa kutumia jina la magufuli. Kula za ngosha atazibeba

Mpina añaweza kushawishi Watu katika kuongea lakini bado ni mchanga kwa level ya kuhama na kupata Wafuasi wa Chadema kisha wananchi wa taifa zima. Kidogo atapata kanda ya ziwa
 

Wala sio jambo la wahuni.
Ni jambo lililowazi

Sidhani kwa mtu muungwana kama yeye hataelewa na kukubali uhalisia.

Unajua kutembea nchi nzima back to back, kushawishi Watu kwa sauti za kisiasa sio jambo dogo

Hata wakati wa Lowasa, moja ya mambo yaliyomuangusha Lowasa ni Suala la hotuba zake.
 
Anaweza akagombea Mkuu.
Upinzani sioni wa kum-challenge.

Lisu sina hakika kama atapewa nafasi nyingine ya kupeperusha chama chake.

Pia Lisu sio chaguo la watanzania wengi. Siasa za Lisu sio pendwa kwa Watanzania wengi.
Lisu mfumo wa siasa zake nae pia haungwi mkono na walio wengi,
 
Upinzani hauna uwezo huo kwa sababu nao ni sehemu ya haohao ccm

..sio kwamba hawana uwezo.

..kinachowavunja moyo ni ukwasi wa Ccm na mbeleko ya vyombo vya dola.

..niambie ni kiongozi gani wa Ccm unaamini angejulikana na kufanikiwa kisiasa hata kama angekuwa upinzani.

..mtu kama Mswiga inabidi tuheshimu kipaji chake kwasababu amefikia umaarufu baada ya kuruka vihunzi vya kila aina.

..viongozi kama Makamba, Biteko, ...unadhani bila mbeleko ya Ccm nani angewajua nchi hii?
 
Tuache maelezo ya thread yako mtu makini/nani ni yupi?
Tuanzie hapo
 

Tatizo la upinzani wengi wao ni mamluki. Hilo tuu
 

Wapinzani gani hao unaowazungumzia?
 
Taja mpinzani unayemwamini leo hapa halafu nakuletea ccm wanamlipa bei gani, lema ushamsikia anamsema tena makonda

..sasa si kubadilisha tu ili Makonda naye awe analipwa na Lema?

..mimi nimeshachoka ni ligi kuu ambayo timu moja inakuwa mabingwa kila mwaka.

..hoja kwamba wapinzani wananunuliwa na Ccm haina maana tena.

..Nataka kuwapa wapinzani madaraka ili Ccm nao wawe wananunuliwa.
 
Hoja yako ya kwanza nakupinga.

Ila hoja ya pili upo sahihi. Anauwezo wa kawaida katika kufafanua mambo na kwenye kushawishi hapo ndio mtihani

..hoja yangu kwamba Maza havutii kwa sura na maumbile umeipinga kinyonge sana.

Nadhani unakubaliana nayo ili huna ujasiri na unaona haya.
 
..hoja yangu kwamba Maza havutii kwa sura na maumbile umeipinga kinyonge sana.

Nadhani unakubaliana nayo ili huna ujasiri na unaona haya.

Nina heshima Mkuu.
Rais ni mtu mzima, ni kama mama yangu.
Kuanza kumchambua uzuri wa maumbile yake ni utovu wa nidhamu.

Ni sawa useme nimchambue mama yangu.


Angekuwa rika langu atleast ningefikiria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…