Kizungumkuti cha mtu akifa anaenda wapi? Maoni ya watu na imani mbalimbali duniani

Kizungumkuti cha mtu akifa anaenda wapi? Maoni ya watu na imani mbalimbali duniani

Hichi ndio kipimio binadamu hatujakamilika full kuhangaika, tunatafuta vya nje ili hali vya ndani vinatushinda, ikiwa ulijikuta ndani ya hii dunia fanya yakupasayo
 
nimekupata mkuu.
unatuzungumziaje tunaoamini yasiyoonekana kwamba, pamoja na yote tunawajibika kwa maisha yetu Siku ya Hukumu.
Unazungumziaje ufufuo kwa nguvu ya wasioonekana (Mungu), kwa mtu ambaye amekwishakuwa medically confirmed dead.

Kama ulivyosema ni Imani. Haina basis ya scientific proof

Ndo mana Imani ziko nyingi,kila mtu ana uhuru wa kuamini anachotaka.Ila hawezi kuki parade kama fact kwasababu akijathibitishwa kisayansi
 
Mimi nimechagua kuwa mkristo... Mwamini katika Mungu mmoja kwakuwa nimeuona ukweli
Uchaguzi bora kabisa katkati ya dunia ya mashaka na kizungumkuti wakifa bila kuwa na tumaini ambalo Mungu ametuletea sisi viumbe wake anaotupenda kupitia Yesu Kristo.
 
mkuu kama ndiyo hivyo. ilitokeajetokeaje bila kupanga watu bila kujali imani au sayansi zao za kijamii kukuta wanaamini mkanganyiko wa mambo haya na afterdeath scenario.

hukumu ya haki nayo vipi, ipo au haipo. ukifa unakufa tu kama afanyo unintellegent being yoyote kama vile mbu au nyumbu serengeti mto mara.
Hiyo ndiyo imani yangu,kama hukuwepo sehemu kabla ya kuzaliwa,hutokuwepo sehemu kabla ya kufa.....wanyama wengine watajua wenyewe.
 
Sasa nikuulize swali, gari si limetengenezwa na binadamu na lina asli yake (yaani mavyuma) sasa nani aliyemfanya mwanadamu?
Mkuu, ni vyema ukimalizia swali lako kwa kisema binadamu wa kwanza kabisa. Ukiuliza aliyemfanya binadamu, jibu ni binadamu. Kila mtu amezaliwa. Ila, swali kuu ni mwanzo wa kila kitu.

Hakuna kilichopo bila wewe kuwepo, haya swali la mwanzo wa bidamu. Ni lazima kwanza wewe uwepo. Kwa hiyo mwanzo wa binadamu ni uwepo wa binadamu.
 
Kama ulivyosema ni Imani. Haina basis ya scientific proof

Ndo mana Imani ziko nyingi,kila mtu ana uhuru wa kuamini anachotaka.Ila hawezi kuki parade kama fact kwasababu akijathibitishwa kisayansi
Sayansi sio nyenzo madhubuti ya kuhakiki mambo,aghalabu hufeli,sayansi ni ujuzi wa kibinaadamu tu
 
Kama ulivyosema ni Imani. Haina basis ya scientific proof

Ndo mana Imani ziko nyingi,kila mtu ana uhuru wa kuamini anachotaka.Ila hawezi kuki parade kama fact kwasababu akijathibitishwa kisayansi
Kuna wanasayansi makundi mawili, wanasayansi wakubwa kabis lakini wanaamin haya tunayojadili na kundi lingine haliamini.
Mfano:Raymond Damadian mvumbuzi wa MRI Scanner na bado analikuwa anaimani nzuri tu ya yasiyoonekana kama sisi uchwara huku.
Unazungumziaje hilo mkuu.
 
Mkuu mitale na midimu ubarikiwe kwa mada murua pia napenda utoaji majibu wako kuna watu wamekosoa kwa jazba ila umewajibu kwa busara sana kwa hilo nikupongeze sana

Kwanza nieleze msimamo wangu kuwa naamini mtu akifa anaenda kusubiri sehemu whether paradiso yaani sehem ya mustarehe akisubiri hukumu ya Mungu ama aende kuzimu yaani kwenye mateso ya shetani akisubiri hukumu ya mwisho

Ila nimesoma hapo unasema unaamini mtu akifa analala tu kaburini anasubiri hukumu je una maana mtenda dhambi na mtenda wema wote watasubiri tu kaburini mpaka hukumu??

Je wale wafu aliowafufua Yesu wakapaa naye kwenda JUU kutoka kuzimu walikwenda kusubiria wapi hukumu tofauti na WAOVU waliobaki kuzimu kama Biblia inavyosema kuwa kuzimu itatema wote waliokufa ili wakahukumiwe

Natanguliz shukrani kwa majibu yako
 
Mimi naamini kuwa, kufa ni hali ya moyo kushindwa kusukuma damu. Hivyo hufanya viungo vyote kushindwa kufanya kazi yake na kupelekea milango ya fahamu kushindwa kutoa taarifa.

Ndio maana ili ujue mtu kafa, lazima uangalie mapigo ya moyo

Na mtu akisha kufa, haendi popote, huo ndo unakua mwisho wake
Utazika mtu akiwa hai
 
Kifo fumbo ambalo ni kutokuwa na majibu ya haraka sahihi na kwa sababu hawa jamaa hawarudi na hata kama wakirudi hatuwaamini.

1:Wahindu (hinduism)
Hakuna cha mbingu wala jehanam, Mtu akifa anarudi kwenye maisha haya kama kitu au kiumbe kingine.

2:Uislam
Quran 45:26. Sema: Mwenyezi Mungu anakuhuisheni, kisha anakufisheni, kisha anakukusanyeni Siku ya Kiyama isiyo na shaka. Lakini watu wengi hawajui.
hapa inaonekena Hata ufeje, mwili utakusanywa na kutakiwa kusimama mbele ya hukumu. wataalam wanaweza kutupa maarifa zaidi.

3:Wabudha
Hawa wanaamini Ukifa mwili utaoza lkn akili/mind itaendelea kuwepo. Na pia kuna kuzaliwa upya baada ya kifo.

4:Wayahudi/Judaism
Nafsi inaishi milele, mwili ni kama kasha ambalo limeazimwa roho likifa linaoza roho inaendelea kula maisha.pamoja na hili wanamaelezo ya ziada.

5:Wakristo
Hapa wamegawanyika makundi mawili.
wale wanaoamini Mtu akifa roho yake haifi, inaenda kula raha mbinguni, au kama ni ovu inateswa motoni. Pia wapo wanaoamini na mimi nikiwemo mtu akifa ni kaubirini analala usingizi mzuri wa mauti kusubiri hukumu ya haki siku ya kiyama. haendi popote.

6:Mababu zetu na Wababe wakiafrika wanasemaje.
Kifo sio mwisho wa maisha, bali ni mwendelezo wa maisha kwa mfumo tofauti ambao hauna mwili. Kwa baadhi ya mila Kifo ni sherehe maana jamaa anakuwa amehamishiwa katika maisha mengine ambayo ni bora zaidi.

8:Wanasayansi na wasiamini Mungu na Miungu
Hapa nao wanamaoni mengi, ila athiest na mwanasayansi nguli aliyefariki majuzi Stephen Hawking anasema Ubongo ni kama Kompyuta kuna wakati Unachoka unaacha kufanya kazi na kufa. Hakuna chochote mtu akifa, zaidi hakuna cha mbingu wala kiyama wala moto. Hizo ni hadithi za watu Wanaoogopa giza.



vipi wewe unaamini lipi.

Nami kama Atheists, naamini kuwa kuwa ukifa imetoka na hatuna tofauti kama anapokufa kuku au kiumbe chochote chenye pumzi. Kinachotuchanganya ni conscience or consciousness. Naamini hakuna moto au kiama au maisha ya milele. Ni mawazo ya kijinga kuwa kuwa ukifa kuna kufufuka, wala makaburi kufumka. Maisha ni haya, yakiisha, BASI. So what we need, is to be kind, generous, sympathetic, giving smiles to people, loving people, forgiving without any revenge, enjoying life without annoying any one, making your god to be the one you are close to (person). Mengine yote ni kudanganyana na kuibiana tu bila huruma. All revival churches are characterized with theft, except the normal churches which are for peace, harmony, justice and love, living as humans.
 
Nipo na mababu na wababe wakiafrika,kufa ni mabadiliko ya binadamu kutoka aina moja ya maisha kuelekea aina nyingine ya maisha.Tukichimbachimba sana tunaipata mizimu.
 
Uchaguzi bora kabisa katkati ya dunia ya mashaka na kizungumkuti wakifa bila kuwa na tumaini ambalo Mungu ametuletea sisi viumbe wake anaotupenda kupitia Yesu Kristo.
mkuu unanikumbusha ya chief songea eti mpokeeni kwanza bwana yesu kabla hamjanyongwa.akawaona wangese akanyongwa akajiendea zake mizimuni huko yupo mpaka leo.
 
Mkuu mitale na midimu ubarikiwe kwa mada murua pia napenda utoaji majibu wako kuna watu wamekosoa kwa jazba ila umewajibu kwa busara sana kwa hilo nikupongeze sana

Kwanza nieleze msimamo wangu kuwa naamini mtu akifa anaenda kusubiri sehemu whether paradiso yaani sehem ya mustarehe akisubiri hukumu ya Mungu ama aende kuzimu yaani kwenye mateso ya shetani akisubiri hukumu ya mwisho

Ila nimesoma hapo unasema unaamini mtu akifa analala tu kaburini anasubiri hukumu je una maana mtenda dhambi na mtenda wema wote watasubiri tu kaburini mpaka hukumu??

Je wale wafu aliowafufua Yesu wakapaa naye kwenda JUU kutoka kuzimu walikwenda kusubiria wapi hukumu tofauti na WAOVU waliobaki kuzimu kama Biblia inavyosema kuwa kuzimu itatema wote waliokufa ili wakahukumiwe

Natanguliz shukrani kwa majibu yako
mkuu
Huoni kuwagawa makundi mawili kabla ya hukumu ni kuwahukumu tayari?

mkuu huoni ukisema wanakwenda kustarehe na kupata suruba sehemu isiyofahamika huoni kuwa wanakuwa hawajafa ila wamebadili state tu?

Mkuu Huoni imani hiyo inaonyesha Mungu ni Katili anatoa double Punishment, kipindi kabla ya Hukumu na baada ya hukumu?

####
Ndio, Watenda Dhambi na waovu wamelala mavumbini kusubiri hukumu ya haki. Naona hilo ndilo tumaini la waandishi wa Bibilia karibu wote.'' hatutawatangulia waliolala mavumbini'' Paulo.
Lazaro alipofufuliwa na Yesu, Yesu alimtoa kaburini, na aliagiza jiwe litoke, ili akifufuka kutoka humo kaburini asishindwe kitoka, na alipotoka hakulalamika Yesu amemkatisha raha ya huko paradiso na kumfufua aje duniani kuugua mafua, kula kwa jasho, etc..


Kuzimu kuwa imani yangu ni kaburini tu. Ndio maana hata hao watu walitokea makaburini. Naamini pia walienda Mbingu moja kwa Moja sio kona nyingine Yoyote. Na naamini hao walikuwa limbuko tu (first fruit) kuonyesha kuwa Huyu mliyemuua ndiye anayefufua na atafufua wafu wote wema siku ya MAVUNO HALISI (kuja kwake mara ya pili).

Kuhusu hukumu, Hilo dai shetani atalidai sio sisi maana yeye ndiye mshtaki wetu kwa Baba. Ila sitegemei adai watu kwenda mbinguni kabla ya MaVUNO, maana eliya alienda, Henoko Alienda, na Musa japo alilala Malaika alitumwa kuja kumfufua na Shetani alileta madai lkn yalikuwa uongo, na Musa akachukuliwa kwenda mbinguni kama walivyochukuliwa wale sample wakati wa Yesu. Na Bibilia haijasema watakatifu wote, wala haijataja majina ila inaonekana walifahamika kwa waliowatokea hivyo kuna uwezekano ni wale tu waliokufa kipindi Yesu Yuko hai ambao ndugu zao walikuwa bado wako hai.

ubarikiwe mkuu, huu uzi ulikuwa umefukiwa mavumbini nimekutana nao na kuona sikutendea haki hoja yako.
 
Back
Top Bottom