Naomba nianze kwa kuwapa pole waumini ambao walibarikiwa na mchungaji kimaro!
Kazi ya kitume ni kama mvua, inanyesha kwa wakati wake na kupisha kwa muda ili shughuli zingine zifanyike, mpate muda wa kupanda, kuvuna, na hata kuezeka panapovuja.
Yamkini mvua ya mahubiri ya mchungaji kimaro ilipendwa na wengi, ili stawisha imani za watu wengi, ili punguza joto kali la mizigo.
LAKINI Tusisahau mvua za namna hii kwa upande mwingine zina majanga yasiyoonekana bayana!
Yamkini kupitia mvua hii watu walizibua mitaro yao, yamkini mvua hii ilileta limonia,yamkini kuna mahali palivuja sana.
Hivyo mambo kama hayo huwezi kuyaelewea kama ukiitazama mvua kwa lengo la masika!
Mchungaji ELIONA KIMARO ANAWEZA KUWA NA SHIDA GANI?
Mimi siyo kiongozi wala muumini wa KKKT! Mimi bado natafta kanisa zuri hata humu jf niliwahi kuuliza kanisa gani zuri ili nikajiunge.
Hivyo Kwa uzoefu wangu na elimu yangu ndogo ya kuchunguza matukio kama haya ikiwemo migogoro ya kiimani, kijamii, mauaji, siasa na uchumi n.k
Naweza kusema mchungaji ELIONA KIMARO Ana sifa zifuatazo
Lakini kwasababu kanisa lina hitaji uponyaji wa kiroho, kimwili na kiuchumi! Ni lazima VIONGOZI wake wafanye hivyo walivyofanya! Kumuhamisha kwasababu za ndani za kiuchumi! HAWAJAKURUPUKA
Hata viongozi wanaweza kuwa wanampenda sana ELIONA KIMARO Lakini haina budi kupisha eneo hilo linalohitaji usimamizi bora wa kiroho, kimwili na kiuchumi kwa mstakabali wa kanisa zima!
Ikiwapendeza viongozi wanaweza kumrudisha lakini awe chini ya usimamizi wa mchungaji mwingine!
Lakini kwa kutambua nguvu aliyonayo kimaro kuwa chini ya mtu palepale Kijitonyama ni changamoto!
Huenda viongozi wameona ni bora sasa akatumike na kwingine.
Kama lengo lingekuwa moja tu kuinjilisha huenda wangemuacha.
Lakini kwasababu linahitaji kukua zaidi kiroho na kiuchumi, ndiyo maana VIONGOZI WAMEFIKIA UAMUZI HUU.
Endeeleeni kusubiri taarifa ya KKKT lakini nauhakika haiwezi kuwa mbali na maoni yangu.
Wewe unampenda kimaro, Viongozi wanampenda kimaro lakini tusisaha Kanisa la KKKT ni kubwa kuliko Kimaro.
Tuliokaribu naye tumsihi asiwaone wabaya viongozi, alipokee hili kwa wema na akatumike popote atakapopangiwa.
Asikuruouke KUHAMA au KIANZISHA KANISA ATAPOTEA, Atambue kwamba mbio zake ni kama samaki baharini,
Kimaro anaonekana kupiga mbizi za kuvutia akiwa ndani ya KKKT, akitoka inje ATAPOTEA!
KKKT ni bahari inayomfanya a-shine!
Asithubutu kutoka Bali atii mamlaka yake ilivyoamua!
Mapadri wa kikatoliki huhamishwa, wachungaji KKKT huhamishwa, Kimaro asione ajabu kuhamishwa.
Yesu alihubiri Galilaya, Yerusalem, Kapenaumu hata kirindini kwa wavuvi kanisa!
Kwanini KIMARO ang'ang'ane pale pale kijitonyama na sio kwingine? HAMJIULIZI HILO?
JF ukweli na uwazi.
Kazi ya kitume ni kama mvua, inanyesha kwa wakati wake na kupisha kwa muda ili shughuli zingine zifanyike, mpate muda wa kupanda, kuvuna, na hata kuezeka panapovuja.
Yamkini mvua ya mahubiri ya mchungaji kimaro ilipendwa na wengi, ili stawisha imani za watu wengi, ili punguza joto kali la mizigo.
LAKINI Tusisahau mvua za namna hii kwa upande mwingine zina majanga yasiyoonekana bayana!
Yamkini kupitia mvua hii watu walizibua mitaro yao, yamkini mvua hii ilileta limonia,yamkini kuna mahali palivuja sana.
Hivyo mambo kama hayo huwezi kuyaelewea kama ukiitazama mvua kwa lengo la masika!
Mchungaji ELIONA KIMARO ANAWEZA KUWA NA SHIDA GANI?
Mimi siyo kiongozi wala muumini wa KKKT! Mimi bado natafta kanisa zuri hata humu jf niliwahi kuuliza kanisa gani zuri ili nikajiunge.
Hivyo Kwa uzoefu wangu na elimu yangu ndogo ya kuchunguza matukio kama haya ikiwemo migogoro ya kiimani, kijamii, mauaji, siasa na uchumi n.k
Naweza kusema mchungaji ELIONA KIMARO Ana sifa zifuatazo
- Mchungaji kimaro analijua andiko analolihubiri
- Mchungaji kimaro anawajua waumini anaowahubiri na shida zao
- Mchungaji kimaro anaijua vyema jamii anayo ihubiri
- Mchungaji kimaro hayumbishwi hasa pale anapokuwa kapanga jambo lake!
- Mchungaji kimaro siyo msimamizi mzuri wa rasilimali na fedha za kanisa ( fedha ni rahisi kupotea mikononi mwake)
- Mchungaji kimaro kwa kutambua karama yake anaitumia kuficha madhaifu mengine hasa kwenye matumizi ya fedha!
- Kuna uwezekano mkubwa wa wa kuonywa lakini kwa kiburi cha kupendwa na waumini aliamini hagusiki!
- Kwa karama yake ya kichungaji alipogundua viongozi wakuu wake wana jambo naye! Alianzisha semina nyingi za mafunzo ili atakapoitwa WAUMINI Waone kama kuna shida!
Lakini kwasababu kanisa lina hitaji uponyaji wa kiroho, kimwili na kiuchumi! Ni lazima VIONGOZI wake wafanye hivyo walivyofanya! Kumuhamisha kwasababu za ndani za kiuchumi! HAWAJAKURUPUKA
Hata viongozi wanaweza kuwa wanampenda sana ELIONA KIMARO Lakini haina budi kupisha eneo hilo linalohitaji usimamizi bora wa kiroho, kimwili na kiuchumi kwa mstakabali wa kanisa zima!
Ikiwapendeza viongozi wanaweza kumrudisha lakini awe chini ya usimamizi wa mchungaji mwingine!
Lakini kwa kutambua nguvu aliyonayo kimaro kuwa chini ya mtu palepale Kijitonyama ni changamoto!
Huenda viongozi wameona ni bora sasa akatumike na kwingine.
Kama lengo lingekuwa moja tu kuinjilisha huenda wangemuacha.
Lakini kwasababu linahitaji kukua zaidi kiroho na kiuchumi, ndiyo maana VIONGOZI WAMEFIKIA UAMUZI HUU.
Endeeleeni kusubiri taarifa ya KKKT lakini nauhakika haiwezi kuwa mbali na maoni yangu.
Wewe unampenda kimaro, Viongozi wanampenda kimaro lakini tusisaha Kanisa la KKKT ni kubwa kuliko Kimaro.
Tuliokaribu naye tumsihi asiwaone wabaya viongozi, alipokee hili kwa wema na akatumike popote atakapopangiwa.
Asikuruouke KUHAMA au KIANZISHA KANISA ATAPOTEA, Atambue kwamba mbio zake ni kama samaki baharini,
Kimaro anaonekana kupiga mbizi za kuvutia akiwa ndani ya KKKT, akitoka inje ATAPOTEA!
KKKT ni bahari inayomfanya a-shine!
Asithubutu kutoka Bali atii mamlaka yake ilivyoamua!
Mapadri wa kikatoliki huhamishwa, wachungaji KKKT huhamishwa, Kimaro asione ajabu kuhamishwa.
Yesu alihubiri Galilaya, Yerusalem, Kapenaumu hata kirindini kwa wavuvi kanisa!
Kwanini KIMARO ang'ang'ane pale pale kijitonyama na sio kwingine? HAMJIULIZI HILO?
JF ukweli na uwazi.