Klabu ya Polisi waingia mkataba wa milioni 50 na kanisa kuiombea timu

Klabu ya Polisi waingia mkataba wa milioni 50 na kanisa kuiombea timu

View attachment 2377563
Uongozi wa Klabu ya Polisi Tanzania umeingia mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya Sh 50 Milioni na Kanisa la Kingdom Embassy (HPCC) la jijini Dar es Salaam ambao ni maalumu kwa ajili ya kupatiwa maji ya kunywa, fedha na maombi timu inapocheza popote kuhakikisha kwamba wanafanya vizuri zaidi.

Nabii Clear Malisa kutoka Kanisa hilo alisema; “Tutakuwa pia tukijitahidi kuiombea timu yetu kwani maombi ni muhimu ili iweze kufanya vizuri kwenye Ligi.”
Mpira wetu kivyetu vyetu

Bado waganga kuanza kudhamini klabu za ligi kuu
 
Mbona kwenye biblia wanasema mazoezi ya mwili yana faida kiafya.
1 Tim. 4:8
Kwa hiyo kucheza mpira hauwezi ikawa dhambi
Kwan mazoezi ni mpira tu?
Hapo mazoezi ni kama kukimbia, kuruka kamba nk.

Kama ishu ni hiyo Timotheo basi hata wachepukaji wanaweza kusema huwa wanafanya mazoezi kifuani.
 
Kwan mazoezi ni mpira tu?
Hapo mazoezi ni kama kukimbia, kuruka kamba nk.

Kama ishu ni hiyo Timotheo basi hata wachepukaji wanaweza kusema huwa wanafanya mazoezi kifuani.
Kuchepuka kamwe hayawezi kuwa mazoezi mkuu


Tubaki kwenye mada; Polisi Tanzania wanatafuta pesa kwa njia zote
 
Polisi ndio anayelipwa...nahisi kuna sehemu watakuwa wanawatangaza kama sio bango uwanjani polisi awapo uwanja wake wa nyumbani basi itakuwa kwenye sehemu ya jezi zao wanazotumia uwanjani
Umeeleza vizuri. Ni kama Simba na Emirates Aluminium
 
Mimi naona huo mkataba ni kwa ajili ya kununulia maji ya kunywa. Hayo mambo mengine ni mbwembwe tu.

Na pia jambo hili ni aibu kubwa kwa makampuni lukuki ya maji nchini kushindwa kudhamini vilabu vya ligi kuu, kwa lengo la kujitangaza. Na badala yake makanisa yanatumia udhaifu wai, kujitangaza!

Mkataba wa milioni 50 kwa kampuni ya maji ni wa kawaida kabisa.
 
Huu ni udini wa waziwazi na inafaa upigwe vita. Michezo na dini wapi na wapi?
Hilo Kanisa limetumia tu fursa kama taasisi. Hivyo hakuna udini hapo. Mikataba kama hii ilitakiwa ifanywe na makampuni, na taasisi mbalimbali za serikali kwa lengo la kujitangaza!

Kwa bahati mbaya makampuni na taasisi hizo, yako busy kujitangaza/kutangaza ishu zao kupitia wasanii wa bongo fleva, bongo muvi na baadhi ya watu.
 
Acheni uchochezi
1007912708.jpg
 
View attachment 2377563
Uongozi wa Klabu ya Polisi Tanzania umeingia mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya Sh 50 Milioni na Kanisa la Kingdom Embassy (HPCC) la jijini Dar es Salaam ambao ni maalumu kwa ajili ya kupatiwa maji ya kunywa, fedha na maombi timu inapocheza popote kuhakikisha kwamba wanafanya vizuri zaidi.

Nabii Clear Malisa kutoka Kanisa hilo alisema; “Tutakuwa pia tukijitahidi kuiombea timu yetu kwani maombi ni muhimu ili iweze kufanya vizuri kwenye Ligi.”
Hahaha[emoji23]
 
Back
Top Bottom