Kocha wa Simba, Didier Gomes inawezekana kutokuwa sehemu ya benchi la Ufundi katika mechi za CAF

Kocha wa Simba, Didier Gomes inawezekana kutokuwa sehemu ya benchi la Ufundi katika mechi za CAF

Dr Restart

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
4,949
Reaction score
24,046
Shirikisho la Soka barani Africa (CAF) limetoa orodha ya makocha ambao hawatoruhusiwa kuwa sehemu ya benchi la ufundi katika timu zao kwa kukosa vigezo vya leseni ya CAF A na UEFA PRO.

Didier ambaye ana diploma ya UEFA A, hajakidhi vigezo vilivyowekwa kwa kocha Mkuu kuwa na leseni ya CAF A ama UEFA PRO.

Katika maelezo yaliyotolewa na CAF, kocha Mkuu anapaswa kuwa na leseni tajwa hapo juu huku kocha Msaidizi akipaswa kuwa na CAF B.

Kocha ambaye hatokidhi vigezo tajwa hatoruhusiwa kuwa sehemu ya benchi la ufundi wakati wa mechi za Ligi ya Mabingwa na kombe la Shirikisho.

Hatua hii imefikiwa na CAF ili kuleta thamani na ubora katika michuano hiyo. Hii ni ili kuleta maendeleo katika soka la Africa kwa kuhakikisha kuwa vilabu vinafunzwa na makocha wenye viwango toshelezi katika madaraja ya juu.

Pamoja na kocha Didier, makocha wa klabu za APR, KMKM, El Mereikh na wengine hawatoruhusiwa kuwa sehemu ya benchi la ufundi katika mechi tajwa.

Simba huenda ikawakosa kocha Mkuu na kocha Msaidizi kwa kuwa kocha msaidizi Ndg Selemani Matola ana lesenu ya CAF C ambayo haikidhi vigezo vya kuwa kocha msaidizi.

Simba wana kazi ya ziada ya kufanya.

Naipenda Simba Mshabiki wa Damu.

Pia, soma=> Simba: Kocha Gomez anasoma online course, tuna imani hadi mchezo wetu unachezwa atakuwa ameshamaliza masomo
 
Ungeleta na link tukaenda kujisomea wenyewe hilo moja

Pili kaama ni kweli basi CAF sio timamu ni wakurupukaji, vitu kama hivi sheria iinawekwa kwa msimu ujao ama miwili mbele na sio watu wameshapeleka majina na kila kitu, nyinyi ndio mnakurupuka, ndio maana napata ukakasi wa hii habari yako, sasa simba sasa hv ndio wafanyaje, wafukuze kocha, na kwanini wamepokea majina yao?
 
Ungeleta na link tukaenda kujisomea wenyewe hilo moja

Pili kaama ni kweli basi CAF sio timamu ni wakurupukaji, vitu kama hivi sheria iinawekwa kwa msimu ujao ama miwili mbele na sio watu wameshapeleka majina na kila kitu, nyinyi ndio mnakurupuka, ndio maana napata ukakasi wa hii habari yako, sasa simba sasa hv ndio wafanyaje, wafukuze kocha, na kwanini wamepokea majina yao?
Kama CAF tulikuwa tunataka kulipotezea hili swala la kuwa na Coaches ambazo hawana elimu ya kutosha kukaa kwenye mabenchi kwenye CAF champions league

Ila tumesema hapana hawatakaa kwenye mabenchi wakati timu zikicheza, vinginevyo wakaongeza elimu yao

Hatuhitaji makocha wa kubahatisha katika kufanya mambo yao
 
Ungeleta na link tukaenda kujisomea wenyewe hilo moja

Pili kaama ni kweli basi CAF sio timamu ni wakurupukaji, vitu kama hivi sheria iinawekwa kwa msimu ujao ama miwili mbele na sio watu wameshapeleka majina na kila kitu, nyinyi ndio mnakurupuka, ndio maana napata ukakasi wa hii habari yako, sasa simba sasa hv ndio wafanyaje, wafukuze kocha, na kwanini wamepokea majina yao?
Kwani wewe unajua ilo tangazo lamitoka lini au mwaka gani?? Inawezekana sheria ilitungwa hata miaka mi3 nyuma ila utekelezaji unatakiwa kuanza msimu huu. Kama mikia wenyewe hawajisomei sheria mpya zinapotungwa,unataka CAF wawasaidie nini hapo.
 
Makolosenge FC humu yako busy na akina djuma shaaban, mayele na aucho lakini hayajui kocha wao ni QT ndo maana analipwa mil 1 Tu Kwa mwezi. Mwamed ni tapeli sn kafukuza makocha wenye CV kubwa ili alete kocha WA academy za watoto wadogo hata kamshahara kawe kadogo.
Makolosenge yote humu ni majingamajinga Tu mambumbu
 
Ungeleta na link tukaenda kujisomea wenyewe hilo moja

Pili kaama ni kweli basi CAF sio timamu ni wakurupukaji, vitu kama hivi sheria iinawekwa kwa msimu ujao ama miwili mbele na sio watu wameshapeleka majina na kila kitu, nyinyi ndio mnakurupuka, ndio maana napata ukakasi wa hii habari yako, sasa simba sasa hv ndio wafanyaje, wafukuze kocha, na kwanini wamepokea majina yao?
Soma hapa, kisha angalia hiyo misimu ilivyotaja na ndipo utapata jibu ikiwa CAF ni wakurupukaji au ni akina Da' Barbara ndio wakurupukaji. Vile vile kwenye hii link utaona barua ya CAF kwenda TFF ya Kenya baada Gor Mahia na wenyewe msimu uliopita kuwa na kocha aliye-pass QT tu kama Gormez na eti wakadhani ana haki na hiyo QT yake

Maendeleo hayana chama, wala ushabiki! SAY "NO" TO JANJA JANJA YA WENYE QT KWENYE AFRICAN SOCCER!!
 
Back
Top Bottom