Kodi mbili kwenye muamala mmoja! Tuseme hapana

Kodi mbili kwenye muamala mmoja! Tuseme hapana

Makato mapya ya Miamala ya fedha katika Simu yanatisha, vipi Muamala mmoja ukatwe kodi mara mbili?

Tuanze pia kuonesha UZALENDO kwenye kukata KODI ya Uzalendo kwenye marupurupu yote wanayolipwa wabunge wetu ambayo kwa sasa hawakatwi chochote

Mfikishieni ujumbe huu Waziri Mwigulu malipo yapo juu sana. Uzalendo huoneshwa kwa mtu kujitoa yeye mwenyewe bila kulazimishwa.
Bado gharama za kutuma na kupokea ni hatari sn
 
Jamani serikali haipendi kuwafanyieni hivi ila hakuna namna maana mwendazake alikufa na baadhi ya passwords za akiba ya taifa

Wote si mnajua namna kifo kilivyomvaa ghafla,hakupata hata nafasi ya kuwambia wanawe mayanga construction sio ya Kitwanga ni mali yao
 
Sisi tunahenyeshwa ili kumaintain maisha ya gharama ya wengine.
Tunapowaambia ulazima wa kuongea lugha moja kama taifa mnaleta uCCM kila mahali. Wananchi hatuwezi kupata haki kwa kuwa na Bunge la vigelegele.
 
Safari zitaongezeka, laki makato yake ni zaidi ya 9,500 kutuma na kutolea hapo nauli ya kuifuata ukute haizidi elfu 5 aisee naifuata
 
Tunarudishwa nyuma kwa kasi ya "Bolt"
Vibanda vya uwakala wa mobile money kifo cha mende hivyo ajira nazo kupitia mitandao ya simu zitapungua.

Kodi hii ya kizalendo lipeni nyie wabunge, sisi huku tulikuwa tukituma 15,000/= mpokeaji alipata 13,000/= ila sasa mmetuletea utopolo huu mna tupa shida bhana.Pia mmetukandamizia kodi kwenye mafuta shame on you Madelu with your rotten government.

Kwenye mda wa maongezi mmetubana (airtel case study) na huku nako mnakuja hivi aisee nyinyi ni MUMIYANI na WAUAJI.
 
Wacha tuoneshane makali kwanza, In Dr Shika's voice
 
Serikali inataka kuwafanya Wananchi muache uvivu....Wewe kama unatuma pesa ndani ya eneo hilohilo kwa nini utumie mtandao?.

Tumieni fursa muanzishe huduma fasta za bodaboda...milioni moja inakimbizwa kwa Muhusika unalipa elfu moja, au mbili, au tatu hata tano kuliko kupoteza elfu ishirini.
 
Kweli anaupiga mwingi,,
Wese kutoka shs 2 mbaka shs 100 kwa lita 1
 
Makato mapya ya Miamala ya fedha katika Simu yanatisha, vipi Muamala mmoja ukatwe kodi mara mbili?

Tuanze pia kuonesha UZALENDO kwenye kukata KODI ya Uzalendo kwenye marupurupu yote wanayolipwa wabunge wetu ambayo kwa sasa hawakatwi chochote

Mfikishieni ujumbe huu Waziri Mwigulu malipo yapo juu sana. Uzalendo huoneshwa kwa mtu kujitoa yeye mwenyewe bila kulazimishwa.
Nashangaa marekebisho yamefanyika haraka wakati kipindi cha kurudisha gharama za vifurushi walikua wazito kufanya
 
Mama awe makini na hawa watendaji wake kina mwigulu wameamua kumuharibia kwa wananchi Ili achukue, kumbuka mwigulu anautamani uraisi,njia pekee ya kumuharibia mama ni kama hivi Ili achukuwe na wananchi.Hakuna nchi yeyeto duniani yenye tozo kama hizi.
Tulimwambia hawa jiwe toxin awamkubali watamhurabia.
Anashindwa vipi kusuka watu wake,hili kundi litamuharibia shauri yake

IMG-20210715-WA0000.jpg
 
Muu shida sio kulipa na kujenga nchi jiulize je hiyo kodi itafika sehemu sahihi au itaishia mifukoni mwa watu?
 
Makato mapya ya Miamala ya fedha katika Simu yanatisha, vipi Muamala mmoja ukatwe kodi mara mbili?

Tuanze pia kuonesha UZALENDO kwenye kukata KODI ya Uzalendo kwenye marupurupu yote wanayolipwa wabunge wetu ambayo kwa sasa hawakatwi chochote

Mfikishieni ujumbe huu Waziri Mwigulu malipo yapo juu sana. Uzalendo huoneshwa kwa mtu kujitoa yeye mwenyewe bila kulazimishwa.
Useme Hapana na Nani? Sisi kwenye Chama chetu tumeridhia.
 
Makato mapya ya Miamala ya fedha katika Simu yanatisha, vipi Muamala mmoja ukatwe kodi mara mbili?

Tuanze pia kuonesha UZALENDO kwenye kukata KODI ya Uzalendo kwenye marupurupu yote wanayolipwa wabunge wetu ambayo kwa sasa hawakatwi chochote

Mfikishieni ujumbe huu Waziri Mwigulu malipo yapo juu sana. Uzalendo huoneshwa kwa mtu kujitoa yeye mwenyewe bila kulazimishwa.
Kaamua kumuhujumu mama Ili achukuwe na wananchi.
 
Back
Top Bottom