Kodi mbili kwenye muamala mmoja! Tuseme hapana

SISI NI WAZEE WA KULALAMIKA KWENYE MITANDAO IMEISHA HIYO
kabisa na usishangae leo watu washasahau wakaanza kujadili Rolls Royce ya Diamond. Hilo ndilo tunallijua wa TZ. Kushadadia topic mtandaoni kutoka na upepo tu sio kwa kutaka suluhisho au kuwajibisha mtu.
Na hii inawapa nguvu watawala kufanya watakavyo wakijua fika watatafuta kiki nyingine lililopo kwenye mjadala likasahaulika.
 
Hawa watu watavuruga sana biashara ya pesa kwa mitandao. Hata kile walichokuwa wakipata hawatapata tena....!
Kama ni demu unampa ten ya matumizi hebu cheki ataambulia ngapi.
Yaani mie hela yangu huwa inaniumaje.
Kwanza ndo Mana huwa sipendi kazi za kutunziwa hela za uzeeni.
Yaani tunamalizana mbona wazee wangu hawakutunziwaga hela na wanaishi bana.maisha tunatishana na wakati Nikola ndizi mbili na maji Safi naishi.
 
Kutoa 100,000 ilikua 3600 sasa hivi 6,100
Kutoa 200,000 ilikua 5300 sasa hivi 8,240
Kutoa 300,000 ilikua 6500 sasa hivi 10,000
Kutoa 400000 ilikua 7000 sasa hivi 11,100
Kutoa 500,000 ilikua 7500 sasa hivi 12,700
Kutoa 600,000 ilikua 8000 sasa hivi 13,900
Kutoa 700,000 ilikua 8000 sasa hivi 15,100
Kutoa 800,000 ilikua 8000 sasa hivi 15,520
Kutoa 900,000 ilikua 8000 sasa hivi 16,900
Kutoa 1,000,000 ilikua 8000 sasa hivi 17,400
Kutoa 3,000,000 ilikua 10000 sasa hivi 20,000


Hiyo list ni ya MAKATO YA ZAMANI NA YA SASA .NA APO NI KUTOA KWA WAKALA.

BADO KUTUMA 😭😭
 
Ule ni wizi kabisa unataunziwa unapata bila interest wao washazunguzia
 
Hamna kodi mara mbili bwashee, mwamala mmoja una tozo (kama cost of service) na kodi ya serikali.
Tufanye mengine tuiache serikali ikusanye kodi
 
Leo tunaona Giza mbeleni naimani tutaona ukungu.
 
Ndio akili za Watanzania...ukiwashirikisha jambo la kumuangusha Mwenzao muitikio ni mkubwa, kumbe inachagizwa tu na roho mbaya.
Zile jitihada tungekua tunazitumia kwenye mambo kama haya walau hali isingekua mbaya namna hii. Wanasiasa wengi si upinzani si watawala wapo kimaslahi binafsi zaidi.
 
Umelala yoooo! Baba umelala yoooo!
 
Tulia ww .. mama anaupiga mwingi sana [emoji1787][emoji1787]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…