Kodi mpya ya Majengo kupitia LUKU inatakiwa kulipwa na Mmiliki wa Jengo na sio Wapangaji wa Jengo

Kodi mpya ya Majengo kupitia LUKU inatakiwa kulipwa na Mmiliki wa Jengo na sio Wapangaji wa Jengo

Na kuna nyumba nyngne wananunua umeme mara moja kwa miez miwili mpaka mitatu,,,je hapo itakuaje?
Ile miezi yote ambayo mtu hajanunua, atakutana nayo kwenye ule mwezi atakaonunua. Kwa mfano sasahivi kodi hii imeanza kukatwa mwezi huu wa 8, lakini wanakata hata kodi ya mwezi wa 7. Mtu akinunua sasahivi anakatwa 2,000/=, kama hata huu mwezi wa 8 hatanunua kwa sababu alinunua umeme wa kutosha say mwezi wa 7, akaja kununua mwezi wa 9 huko, atakatwa miezi mitatu, 7, 8 na 9.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu kuna mahali nina ofisi naona wanakata 5000 kila mwezi na sio nyumba ya ghorofa...hii ikoje.
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa kodi ya majengo kwa njia ya ununuzi wa umeme ambayo itaanza kutumika Agosti 20, 2021 inatakiwa kulipwa na wamiliki wa majengo na sio wapangaji kwenye majengo hayo.

Hayo yameelezwa na Lazaro Lucas katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambapo ameongeza kuwa kwa sasa kuna changamoto wa kutofautisha mnunuzi wa umeme kama ni mwenye nyumba au mpangaji, hivyo kwa mwanzoni mpangaji anaweza kukatwa kodi hiyo kimakosa.

“Hiyo kodi inapaswa kulipwa na mwenye jengo lakini kwa mwanzo kumekuwepo na changamoto ya kujua ni yupi mwenye jengo ni yupi mpangaji kwa hiyo mwanzoni [mpangaji] unaweza ukapata ‘bill’… mwenye jengo afike ofisini aseme nyumba zangu ni moja, mbili, tatu, ili wenye zile mita ziondolewe,” amesema Lucas.

Lucas ameongeza kuwa mwenye jengo anaweza kulipia kodi ya nyumba za wapangaji taslimu shilingi 12,000 kwa kila nyumba ya kawaida kwa mwaka na namba za mita za wapangaji zitaondolewa kwenye mfumo, au kodi hiyo itahamishiwa kwenye mita yake.

Aidha, TRA imesema kuwa endapo mwenye jengo hatowasilisha taarifa za wapangaji TRA, wapangaji wanaweza kupeleka malalamiko yao kwamba wanatozwa kodi ya jengo kimakosa.

Viwango hivyo kwa sasa ni shilingi 12,000 kwa kila jengo la kawaida ndani ya kiwanja kutoka shilingi 10,000 iliyokuwa ikitozwa awali, na shilingi 60,000 kwa kila sakafu ya ghorofa kutoka 50,000. Hata hivyo kwa upande wa halmashauri za wilaya na miji midogo nyumba za ghorofa bila kujali idadi ya sakafu zitatozwa shilingi 60,000.

Kwa utaratibu huo kila mnunuzi wa umeme atakatwa shilingi 1,000 kwa mwezi kwa nyumba ya kawaida na shilingi 5,000 kwa mwezi kwa kila sakafu ya ghorofa. Kwa wanaotumia mita za ankara watalipa kodi hiyo kwa pamoja katika Ankara zao za mwezi.
Huu ni upigaji kama upigaji mwingine tu, haiwezekan property tax ifyonzeshwe kwenye bili ya umeme,huko vijijini wanaumia zaidi,au rea ilipelekwe Ili hata nyumba za udongo zilipe Kodi kupitia bili? Eti waende Tra, vijijini Kuna matawi ya Tra?
 
Back
Top Bottom