Kodi mpya za miamala: Mahakama iweke zuio la haraka

Kodi mpya za miamala: Mahakama iweke zuio la haraka

Lorenzo Samike

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2021
Posts
1,187
Reaction score
1,914
Huu uharamia wa kodi mpya za miamala ya simu unapaswa kusimama.

Wanasheria wetu mtusaidie hili. Hakuna kitu kinachoitwa sijui "kodi ya uzalendo" — Lazima Mahakama iweke ZUIO la hizi kodi za kitapeli.

Hauwezi ukakata kodi mara tatu kwenye muamala mmoja. Huo ni uhuni na wizi.

Hizi ndizo kodi za dhulma tulizokuwa tunazisema.

Badala ya kudhibiti madini na bandari pamoja na vitega uchumi vingine vikubwa, mmewaachia wazungu wanajichotea tu, halafu mnatengeneza vijikodi vya ajabu ajabu mnamtwika mwananchi mara tatu tatu?

HAPANA, Double taxation ni uhuni na dhuluma ambayo inapaswa kusimama.

Msituletee mambo ya kuupiga mwingi hapa. Kodi za kitapeli ni mwiko.

Wanasheria fanyeni kazi yenu, na tutaipima mahakama kama bado inajitambua kupitia hili.
 
Yani wewe jamaa una akili Sana.Nashangaa Yani watu tupo kama wendawazimu hata kesi tu mahakamani tumeshindwa kufungua hivi Watanzania tuna akili kweli?Tunaumizwa tunakaa kama makondoo.

Nimeamini serikali ya Tanzania haipo kwa ajili ya kuwainua Wananchi wake .Wlichikifanya ni zaidi ya uhuni.
 
Yani wewe jamaa una akili Sana.Nashangaa Yani watu tupo kama wendawazimu hata kesi tu mahakamani tumeshindwa kufungua hivi Watanzania tuna akili kweli?Tunaumizwa tunakaa kama makondoo . Nimeamini serikali ya Tanzania haipo kwa ajili ya kuwainua Wananchi wake .Wlichikifanya ni zaidi ya uhuni.
Kafungue kesi mjomba. Mimi tayari nalipa kodi ya uzalendo ikajenge barabara kijijini kwetu malinyi niuze mpunga wangu kwa uarahisi.
 
Fungua kesi sasa wewe uliye na ushahidi unawatuma wanasheria bure tu
 
Ngoja tuhamasishe mgomo kwa siku moja ili tuone. Je? yale malipo ya serikali ambazo tunayolipa kwa njia ya M-Pesa nayo yanakatiwa kodi?
 
Huu uharamia wa kodi mpya za miamala ya simu unapaswa kusimama.

Wanasheria wetu mtusaidie hili. Hakuna kitu kinachoitwa sijui "kodi ya uzalendo" — Lazima Mahakama iweke ZUIO la hizi kodi za kitapeli.

Hauwezi ukakata kodi mara tatu kwenye muamala mmoja. Huo ni uhuni na wizi.

Hizi ndizo kodi za dhulma tulizokuwa tunazisema.

Badala ya kudhibiti madini na bandari pamoja na vitega uchumi vingine vikubwa, mmewaachia wazungu wanajichotea tu, halafu mnatengeneza vijikodi vya ajabu ajabu mnamtwika mwananchi mara tatu tatu?

HAPANA, Double taxation ni uhuni na dhuluma ambayo inapaswa kusimama.

Msituletee mambo ya kuupiga mwingi hapa. Kodi za kitapeli ni mwiko.

Wanasheria fanyeni kazi yenu, na tutaipima mahakama kama bado inajitambua kupitia hili.

E0NhMwdXIAAW0HL (1).jpeg
 
Wananchi ndio wanaojua nani anafaa nani afai huyu msingida mda mrefu Sana ameambiwa afai ye kamkumbatia ngoja amuharibie ataelewa akiwa kachelewa.Hiki ni kirusi kitamfitinisha Sana wananchi shauri yake.
 
Kiukweli kama wanasheria wote nchi nzima hakuna hata aliyefungua case mpaka sasa kupinga huu uharamia, basi tupo nchi ya ajabu sana inayoenda enda tu watu wamekaa, hii na kwa hali ilivo mtaani ni kutaka kuwalaza watu njaa

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
Wanasheria wanasimamia kesi. sisi wananchi ndo tunatakiwa kuwaambia kufungua kesi.
 
Tanzania ni nchi ya kijinga sn ndio maana viongozo wetu wanasema na kufanya mambo ya hovyo wanavyotaka......

Badala ya kuingia barabarani kudai hali unaongea na mahakama?? 🙄🙄
 
Back
Top Bottom