Kodi ya majengo kuanza kukatwa kwenye Luku kuanzia Agosti 20, 2021. Je, Serikali imekosa Dira, mbinu zimewaishia?

Naomba kujibu

1. Serikali imeondoa mfumo wa zamani sababu ulikuwa rahisi watu kukwepa kulipa na ngumu kukamatwa. Hivyo serikali ilikuwa inapoteza sana mapato.
Umejibu upumbavu sana, hivi unazijua nyumba za kupanga wewe?
 
Ungeuliza Mwigulu na viongozi wanaolipiwa umeme wao na serikali watalipiaje maghorofa yao wanayopangisha kwa dola?
 
Ndio inaitwa for more dreams and financial stability
 
Daah ifike mahali watuhurumie mbona hivi lakini
 
Ukinunua Umeme sasa hivi unalipa Kodi nne:

1. VAT asilimia 18

2. Ewura Asimilia 3

3. REA asilima 1

4. Kodi ya Jengo (Tsh 1000- Tsh 5000)
 
nadhani wanataka kufanya mabadiliko katika kodi za jengo kwa kuongeza malipo ya umeme hii inawezekanaje? inamaanisha bili itakuwa kubwa kufidia kodi ya jengo?
... inashangaza hao TRA wanarudi mbio mbio wakati walishajitoa kwenye masuala ya kodi za majengo na kuwaachia halmashauri kwa kisingizo "ukusanyaji wake ni gharama kuliko kiasi kinachopatikana". Baada ya kutozwa kupitia bili za umeme wamerudi mbio kwa sababu watazichota kirahisi kutoka Tanesco (kwa "kushirikiana na Tanesco"); sina hakika kama WATAVUKA MALENGO kama enzi zile. Hii inaonesha ubunifu nchi hii ni SIFURI.
 
 
Umesomeka
 
Serikali yenyewe inatudharau wananchi kwa sababu hatuwezi kupinga chochote wale Wezi wa bungeni watakachoamua.
"Nyie viongozi wekeni Kodi mnazojisikia maana mnaongoza kondoo"
 
Sio sifa Mkuu,kodi ya 12000 kwa mwaka Kwa raia anayejitambua ni kitu gani?Tulipe Kodi ili tupate haki ya kulalamika tunapoona hakuna maendelo
Basi warudishe na Kodi ya kichwa kwani sh 4000 kwa mwaka Ni kitu gani kwa raia anayejitambua.
 
Ujinga mtupu ulioujibu hapa,!
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Namba ya jengo?

Unachekesha wewe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…