Korea yanunua ardhi "kwa mkopo" Tanzania, Serikali yasita kuthibitisha

Korea yanunua ardhi "kwa mkopo" Tanzania, Serikali yasita kuthibitisha

dsm
inaonekana wazazi wako walikuwa na uwezo wa kukupeleka nje kusoma, mimi naongelea wa TZ ambao wazazi wao hawakuwa na uwezo wa kuwasomesha.



kutokana na wazazi wako kuwa na uwezo wa kukusomesha nje inamaanisha walikuwa ni watu wazito + ukijumlisha na chuki ulizokuwa nazo dhidi ya nyerere = najiuliza sijui wazazi wako waligombana nini na nyerere!!!!

basi kama hutaki UDSM nakupa TAZARA

Tazara, sijui hata kama Tanzania tulitowa senti tano yetu kuijenga. Labda wewe unafaham. Lakini naomba kaitazame hali ilivyozorota halafu ndio utajuwa, kama tuliitolea fedha yetu au la. Kama kweli tumeitolea fedha basi tu mapunguwani kwa kupoteza fedha nyingi halafu tunashindwa kukiendesha kitu tulichokigharamikia.
 
Wana JF,

tujadili namna ambavyo uwekezaji katika kilimo, uwe wa ndani au wa nje, unavyoweza kufanywa ili kuinua uchumi wa Taifa hili, linaloagiza mchele toka Pakistani,juisi toka Uarabuni, na toothpick toka Uchina.

Naona taa za barabarani na Nyerere vinachukua mkondo taratiibu, huku ardhi ikiendelea kuwepo bila kulimwa, na maji yakiingia baharini pasi na kutumika.

Mijadala yetu inatoa taswira ya viongozi wajao...tukitoa pumba, tutakuwa viongozi vilaza, tukijadili kwa umahiri, na kutoa mawazo mbadala, tutakuwa viongozi tutakaoleta mapinduzi...

Hapa nakuunga mkono mia kwa mia, na hawa wa Korea tutaona jinsi ardhi hiyo hiyo inayotushinda sisi kulima na ku-export mazao yawe ghafi au yameshasindikwa watakavyofanya. Na naomba waje na tupate fursa ya kujifunza kwa vitendo. Tusikae domo kaya tu.
 
Mkuu Semilong hawalioni hilo! Nyerere alikuwa ni jabari bwana kamwe hawezi kulinganishwa na akina Mwinyi, Mkapa wala Kikwete. Chini ya uongozi wake Tanzania iliweza kufanya mengi sana pamoja na kupigwa vita sana na nchi za magharibi ukilinganisha na yaliyofanywa na Mwinyi, Mkapa na Kikwere combined. Leo hii Wasomi wa Kitanzania wanaofanya kazi katika nchi mbali mbali duniani wanatokana na sera za Mwalimu. Kama binadamu na Kiongozi Mwalimu hakuwa perfect alifanya makosa yake na hata yeye mwenyewe alilisema hilo lakini makosa yake ni madogo sana ukilinganisha na mazuri mengi aliyoyafanya alipokuwa madarakani. Mwacheni Mwalimu apumzike kwa amani~RIP Mwalimu.

Mosi, nakushangaaa kwa kuona kupigwa ''vita sana na nchi za magharibi'' kuwa ni sifa.

Pili, unaemataja hapo juu ni Mwinyi huyu anaesemekana kuwa ni ''ambaye aliongoza serikali ya awamu ya pili iliyoruhusu mabadiliko makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi kiasi cha kupewa jina la Mzee Ruksa" Au unaongelea Mwinyi yupi?

Tatu, nakubaliana nawe kwa hili "Mwalimu hakuwa perfect alifanya makosa yake''

Nne, sikubaliani na wewe katika hili "makosa yake ni madogo sana ukilinganisha na mazuri mengi aliyoyafanya alipokuwa madarakani" nijuavyo mimi ni kuwa alikuwa na makosa mengi tena makubwa kuliko Rais wa Awamu yeyote Tanzania. From experience, na namshukuru Allah, kuniwezesha kuziona awamu zote nne zilizoshika madaraka Tanzania na kabla ya kuwa Tanzania, nilikuwepo wakati wa Nyerere toka alivyokuwa waziri mkuu mpaka alivyong'atuka, hadi hii leo (Alhamdullillah). Sijaona, ''mazuri'' yaliyopita ''mabaya'' aliyoyafanya Nyerere kuwashinda viongozi waliokuja baada yake, never. Kweli, tumwacheni awepo apapendapo kumuweka Mungu, na aliyochuma akiwa hai, alipwe kwa kipimo chake, huko aliko, bila kuzidishiwa wala kupunguziwa.
 
dsm
inaonekana wazazi wako walikuwa na uwezo wa kukupeleka nje kusoma, mimi naongelea wa TZ ambao wazazi wao hawakuwa na uwezo wa kuwasomesha.



kutokana na wazazi wako kuwa na uwezo wa kukusomesha nje inamaanisha walikuwa ni watu wazito + ukijumlisha na chuki ulizokuwa nazo dhidi ya nyerere = najiuliza sijui wazazi wako waligombana nini na nyerere!!!!

basi kama hutaki UDSM nakupa TAZARA

Wazazi wangu walikuwa na uwezo wa kula na kulala bila matatizo na wakiishi Kariakoo na waliweza kweli kunipeleka nje kwenda kusoma, namshukuru Allah kwa hilo, wala halina ubishi.

Hawakuwa wazito kama utakavyo + sina chuki na Nyerere kama Nyerere binafsi bali nnachuki ya kutokuwa kiongozi makini na kutuharibia nchi yetu. Nashangaa sana kuona watu wengine humu, nadhani wengi wao wakati wake, ya ama hawakuwepo au walikuwa bado vikinda, wanampa sifa ambazo hakuwa nazo.

Wazazi wangu hawakuwa na ugomvi na Nyerere, na by the way, ofisi ya kwanza ya TANU na kabla ya hapo TAA iko ubavuni wa iliyokuwa nyumbani kwetu hapo Mtaa wa Lumumba. Na wazee wangu wakijuana sana na Nyerere, kabla na baada ya kuukwaa ukuu. Kama kuna sifa yoyote inayobidi nimpe, ni kuwa, mara kwa mara (kila apatapo nafasi), alipokuwa akija ofisi ya TANU alikuwa akipita pale kwetu kuwasalimia wazee japo dakika mbili tatu, hilo moja lake nilijuwalo.
 
Ha ha ha ha naona umefilisika kimawazo! Kuna haja gani basi ya kuwa na mahakama Tanzania kama haziwezi kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa!? Si bora tu wazifunge na kuwapunguzia gharama walipa kodi kwa kujua kwamba mahakama hizo zimeshindwa kazi na wahalifu wote ndani ya nchi yetu wakashtakiwe kwenye mahakama za kimataifa. Jumamosi njema 🙂

Ni wewe ambae huziamini si mimi.
 
Labda ni wewe huijui historia ya Dar Es Salaam. Ukiacha sehemu zilizojulikana kama Uzunguni ama Uhindini, sehemu kubwa ya iliyojulikana kama Uswahilini wakati nchi inapata uhuru mwaka 1961, Ilala, Magomeni, Mwananyamala na kwingineko zilisheheni nyumba za makuti na hazikuwa na barabara za lami.

Mwaka mmoja tu baada ya nchi yetu kupata uhuru, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lilianzishwa ili kusaidia upatikanaji wa nyumba bora za makazi, hasa mijini. Baada tu ya Shirika kuanzishwa, Serikali ilikuwa inatoa ruzuku kwa Shirika ili kuliwezesha kujenga nyumba nyingi kadri ilivyowezekana. Kwa kutumia ruzuku hiyo, Shirika liliweza kuondoa nyumba za makuti (slum clearance), hasa jijini Dar es Salaam na kujenga nyumba za saruji na kuezekwa kwa mabati.

Hivyo ndivyo zilivyojengwa nyumba za Ilala, Magomeni, Mwananyamala. Ujenzi kama huo ulienea pia kwenye miji yote ya mikoa na wilaya nchini. Ni wakati huo huo wa "operation makuti" barabara zote katika sehemu hizo (Ilala, Magomeni na Mwananyamala) ziliwekewa lami. Kabla ya hapo sura ya jiji la Dar es Salama na hasa zile sehemu za uswahilini hazikuwa tofauti na yale mabanda tunayoyashuhudia hadi leo sehemu nyingi za mkoa wa pwani.

Unajuwa mwaka mmoja baada ya Uhuru bajeti ilikuwa ikitoka wapi? au unajisemea tu? na mpaka hii leo zaidi ya asilimia 30 ya bajeti unajuwa inatoka wapi?
 
Huyu Dar Es Salaam ama ni mtoto mdogo mtukutu au ni limbukeni asiyejua lolote kuhusu historia ya Tanzania. Lakini lazima atambue kuwa humu tupo ambao hatukusimuliwa, tuliyashuhudia kwa macho yetu. Kuna wakati iliyojulikana kana Magomeni Makuti haikuwa na nyumba hata moja ya bati. Mwaka 1964, barabara karibu zote za Magomeni Mapipa zilikuwa za lami tupu na nakumbuka tulivyojivunia mitaa ile kama ya Idrissa, Uweje na kahoteli ketu ka Butiama. Naomba huyu anayejiita Dar es Salaam mumwelewe kama alivyo - ni limbukeni.

Labda huo msikiti uliokuta ulikuwepo kabla, nenda kauone alijengwa baada ya kufa Nyerere halafu uulize umejengwa na nani? halafu njoo ubishane.
 
Huyu Dar Es Salaam ama ni mtoto mdogo mtukutu au ni limbukeni asiyejua lolote kuhusu historia ya Tanzania. Lakini lazima atambue kuwa humu tupo ambao hatukusimuliwa, tuliyashuhudia kwa macho yetu. Kuna wakati iliyojulikana kana Magomeni Makuti haikuwa na nyumba hata moja ya bati. Mwaka 1964, barabara karibu zote za Magomeni Mapipa zilikuwa za lami tupu na nakumbuka tulivyojivunia mitaa ile kama ya Idrissa, Uweje na kahoteli ketu ka Butiama. Naomba huyu anayejiita Dar es Salaam mumwelewe kama alivyo - ni limbukeni.

Tazama huyu mwingine, kuezekwa nyumba bati anaona ni maendeleo, wakati wa mkoloni alikuwa akijenga nyumba za mabati kwa ajili ya kukaa manamba, na maofisa walikuwa na nyumba za vigae.

Sisi, tuliopo pwani tulikuwa tukiezeka kwa makuti, tusiwe kama manamba wanaowekwa nyumba za full suit, juu bati pembeni bati.

Na raha yake nyumba za makuti ni kuwa, hazina joto. Na mpaka hii leo ukiona mahoteli ya kifahari Mengi tu Tanzania, ambayo si ya ghorofa yanaezekwa kwa makuti. Its simple, cheap comfort. Usifikiri kuezeka mabati ndio kuendelea. Katazame nchi zilizoendelea uone kama wanaezeka kwa bati. Sasa limbukeni wewe au mimi aonae kuwa nyumba ya bati ni maendeleo?

"Thatching is the craft of building a [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Roof"]roof[/ame] with dry vegetation such as [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Straw"]straw[/ame], [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Phragmites"]water reed[/ame], [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Cyperaceae"]sedge[/ame], [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Juncus"]rushes[/ame] and [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Calluna"]heather[/ame], layering the vegetation so as to shed water away from the inner roof. It is a very old roofing method and has been used in both tropical and temperate climates. Thatch is still employed by builders in developing countries, usually with low-cost, local vegetation. By contrast in some developed countries it is now the choice of well-to-do people who want their home to have a rustic look."

source:[ame]http://en.wikipedia.org/wiki/Thatching[/ame]
 
Mbona mashamba ya Nafco wameuziwa wakenya na ngano yote inakwenda huko, mbona hamlalamiki? Watanzania wengi tu walijitokeza kuomba mashamba ya ngano Katesh lakini hakuna hata mmoja aliye pata, wakenya wakamwaga kitu kidogo sasa mashamba ni yao.
 
mkuu Dar Es Salaam una hoja nzito sana!
kwa uzoefu wangu mdogo sidhani kama nastahili ku-argue na wewe
 
Kuna mahakama za Rushwa za kimataifa kama za Tanzania huziamini, unangoja nini?

Nina shaka na hiyo shule unayodai ulipelekwa na wazazi wako! Kuna mahakama gani ya rushwa ya kimataifa? Nitajie moja tu ambayo ipo kwa ajili ya kusikiliza kesi za rushwa. Msipende kudai usomi halafu maandishi yenu yakawashushua!

Amandla.....
 
Last edited:
Baada ya kuona taarifa za Korea Kusini kutaka kuhodhi eneo kubwa la ardhi nchini Tanzania kwa ajili ya kuendesha kilimo kukidhi mahitaji ya matumbo ya raia wake, nime-search online kwa dakika kumi nimegundua madudu ya kumwaga!

Viongozi kuanzia aliyeko Ikulu mpaka mwenyekiti wa kijiji wanafumbia macho dhuluma ya ardhi kwa wananchi masikini wasioweza kuchanganua faida na hasara za kuachia wageni kutoka nje ya Tanzania kukwapua ardhi yetu ( land grabbing) - ukoloni umerudi kwa lugha tofauti.

Ukweli ni kwamba, we have been too lenient kwa mkuu wa nchi Jakaya Kikwete, kiasi kwamba haoni sababu ya kuzuia huu uozo chini ya utawala wake. Kikwete kama rais ana jukumu la kulinda maslahi ya usalama wa taifa la Tanzania, na ardhi pamoja na nishati ni maswala yaliyo juu katika kusimamia usalama wa nchi.

Kwanini kiongozi huyu anashindwa kupiga marufuku hii dhuluma? Anaweza kutumia madaraka yake kutoa agizo la rais au kwa kutunga sheria mpya katika bunge kudhibiti umiliki wa ardhi kwa wageni? Kuwa rais ni kazi ngumu, hiki ni kipimo, si kila anayeomba anaweza kuongoza. Na kuongoza siyo kufungua miradi na kuhudhuria harusi na misiba, au kwenda UN kuhutubia. Leadership ya nchi kitu kingine kabisa.

Rais anaona fahari kufunga barabara zinazozunguka Ikulu yake, lakini haoni sababu ya kudhibiti ardhi ya wananchi anaowaongozwa isiporwe na mabepari wa kigeni.

Tayari tunafahamu kuna makampuni kadhaa ya kigeni yameshanunua au yako mbioni kununua kiasi kikubwa cha ardhi ya kilimo - ni serikali ndiyo inawakaribisha kwa kisingizio cha uwekezaji. Hawa wageni hawawezi kuja kisha wakaanza kujipimia land. Tutakuja kulaumiana baadaye, lakini bora tuyaseme tupate ufumbuzi sasa.

Hapa chini naorodhesha links za baadhi ya madudu yanayofanywa kwenye ardhi yetu na hakuna anayekemea. Land grabbing business ventures are taking place Tanzania, it's real. We got to act now, we can't stand by and just watch, tuseme ardhi yetu is not for sale kwa wageni. Haiozi, tuiache mpaka watanzania watakapopata mtaji na maarifa ya kuitumia wenyewe - waliotangulia wangeiuza kwa wageni sisi tungekuwa wapi?

Huenda si habari mpya, lakini inaonyesha msimamo wa serikali ni uza uza uza!!!!



Dhuluma ya ardhi Tanzania

Swedish neo-colonialism or Tanzania's savior?


Hawa ndiyo SEKAB wenyewe, wanaomba ardhi bure Rufiji


Tanzania Govt On Spot Over Biofuel Production


Sun Biofuels Tanzania Ltd

Tatizo letu wengi hatujui maana ya neno ukoloni hivi jamamani tunaweza pata mtu akazungumzia defination ya ukoloni in very simple language labda watu wataelewa.

Watu wanadhania ukoloni ni bendera ya mkoloni ipepee kila mahali, wengine wanadhania ni magwanda na makofia ya PC na DC na au office attendant kuitwa messenger, wengine wanadhania ni kodi ya kichwa na baiskeli, lakini majority hawajui hii concept ya ukoloni.

Naomba mdau mmoja atueleze maana ya ukoloni
 
It took Nyerere 30 Years ku haribu kila kinachofanya kazi Tanzania. It may ta ke a long time kuirudisha kama ilivyokuwa na it will take longer kuiboresha kwani waswahili hunena ''kubomoa ni rahisi lakini kujenga...).

Hayo ya Nyerere na Idi Amin, wala usiyalete, sio mahala pake hapa. Kwako Idi Amin ni Nduli kwanguu ni Shujaa aliechangiwa na nchi zinazoongozwa na wakiristo kumuondoa madarakani kwa kuwa ni muIslam. Usitake tubadili mada, naomba ya Idi Amin humu tusiyalete tuyatafutie thread nyingine ikibidi.

Kiswahili, kilikuwepo kabla ya Nyerere kikiongewa si tu, Tanganyika bali mpaka Kongo na kwingineko kwingi. Ukitaka kujuwa waliekieneza kiswahili, rejea historia na utazame wapi kiswahili kimetoka na ilikuwaje kikafika kilikofika.

Niambie, Tanzania tulikuwa na Nyerere miaka 30, tumepigana vita ngapi na niambie miaka 30 kabla ya Nyerere tumepigana vita ngapi na miaka 30 baada ya Nyerere tumepigana vita ngapi?

Ukipata jibu za statiscs hizo utaelewa alikuwa ni kiongozi aina gani.

Well, nnachojifunza hapo ni kwamba uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana ukilinganishwa na wa Nyerere. Au ni hii pia unakataa?
 
Mbona mashamba ya Nafco wameuziwa wakenya na ngano yote inakwenda huko, mbona hamlalamiki? Watanzania wengi tu walijitokeza kuomba mashamba ya ngano Katesh lakini hakuna hata mmoja aliye pata, wakenya wakamwaga kitu kidogo sasa mashamba ni yao.

Nadhani tuanze kuangalia ni jinsi gani tunareposses hayo mashamba kupewa wakenya mashamba hayo isiwe sababu ya sisi kuendelea kutoa mashamba kwa wakorea, waarabu na watu wengine wasio na ardhi wanaokuja kutunyang'anya sisi.

Kama walipewa kwa kutoa kitu kidogo basi hii ni sababu tosha ya kutengua mkataba uliofunikwa na rushwa. Kinachofuata ni kutoa taarifa PCCB ili wafuatilie kama wanavyofanya kwenye kesi ya Liyumba wakishindwa basi tuchukue hatua nyingine za kulazimisha upelelezi uendelee.
 
Tatizo letu wengi hatujui maana ya neno ukoloni hivi jamamani tunaweza pata mtu akazungumzia defination ya ukoloni in very simple language labda watu wataelewa.

Watu wanadhania ukoloni ni bendera ya mkoloni ipepee kila mahali, wengine wanadhania ni magwanda na makofia ya PC na DC na au office attendant kuitwa messenger, wengine wanadhania ni kodi ya kichwa na baiskeli, lakini majority hawajui hii concept ya ukoloni.

Naomba mdau mmoja atueleze maana ya ukoloni


ukoloni kama mfumo wa kueneza himaya na kulinda maslahi unakuja na sura tofauti, nchi moja yenye nguvu kiuchumi na kisiasa kuinyonya nchi masikini

zamani ilikuwa mkoloni anaitawala nchi nyingine katika kila nyanja, lakini enzi hizo zilishapita. kwasasa ukoloni umejikita kukomba maliasili za nchi kama Tanzania.

Tanzania ni mfano mzuri jinsi ukoloni wa kisasa unavyotumika kuwanyonya masikini, viongozi wetu wanabisha hilo - akili zao zimelewa moshi wa madaraka na fedha.

tukumbuke kuwa hata wakati wa kupigania uhuru miaka 50 na 60, wapo waafrika waliwaunga mkono na kushirikiana na wazungu kuwakandamiza waafrika.

nadhani ushamsikia Kikwete akisema bila wawekezaji wa kigeni Tanzania haiwezi kuendelea. maana yake ni kwamba yuko radhi awafungulie milango wachukue kila wanachokitaka, kuliko kulinda maliasili zetu. angalia madini yanavyochotwa, angalia ardhi inavyouzwa, vitalu vya uwindaji wanagawiana waarabu.
 
Prime Minister Pinda should come clean on this, atwambie anajua nini kuhusu huu mradi.Na yeye alipokua Korea walizungumza nini na hao wenyeji wake kuhusu swala la ardhi. Vinginevyo hii kitu ni swala muda tu, watakuja watafanya wanavyotaka na tutanyamaza.
 
Back
Top Bottom