Kosa kubwa la Malecela wa NIMR: Rais kaona mbali athari za ZIKA

Kosa kubwa la Malecela wa NIMR: Rais kaona mbali athari za ZIKA

Suala ni kwamba hajaishirikisha Serikali ili kuipika taarifa na isingetangaza. Mi naona ni vema kujihami hasa kwa magonjwa mapya kumbukeni wenzetu walivyopata EBOLA madaktari wa Dunia nzima walienda kupiga kambi West Africa.
 
Haya nao TWAWEZA tafiti zao pia zipate baraka za serikali!! Hii ipo Tanzania tu
 
Zika na NIMR

Dk. Mwele Ntuli Malecela leo si Mkurugenzi tena wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR). Ikulu leo imemtangaza Profesa Yunus Mgaya kuwa mbadala wake.

Kwanini Mwele kaondolewa? Nimeulizwa hili swali na baadhi ya watu nami nikauliza hapa na pale ili kupata majibu. Na hili ndilo nililoambiwa.

Mosi, kwamba ugonjwa wa Zika upo Tanzania. Ugonjwa huu ulianzia Uganda na upo pia kwetu kwa muda mrefu. Ila upo katika hali iliyodhibitiwa, wataalamu wanaitwa Endemic. Si tatizo kubwa lakini upo.

Lakini Tanzania haina tatizo la ZIKA. Kwa jinsi tatizo la ugonjwa huo lilivyo kubwa, kabla halijatangazwa, kuna taratibu za kufuatwa ikiwamo kuhusisha Serikali na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Imefanyika hivi kwa sababu madhara ya kutangaza ugonjwa huo kwa taifa ni makubwa kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Tatizo ni kwamba tangazo la Mwele halikufuata hizo taratibu. Na zaidi, halikuzingatia athari ambazo zingejitokeza kwa yeye kutoa taarifa kama zile.

Kwenye Kiswahili, tofauti ya maneno Endemic na Epidemic ( ugonjwa uliodhibitiwa na uliolipuka) ni ndogo. Ukisema Zika ipo, magazeti yatasema ZIKA imeingia.

Sasa, labda, Rais mwingine, kwenye Serikali nyingine, angeweza ˊkupotezea` tu kauli ile ya Mwele. Lakini binti huyu wa mzee John Malecela hakuwa amesoma vema alama za nyakati.

Hivyo, kwa maana ya kosa, Mwele alikosea. Ishu ya ZIKA haikuwa ya kutangazwa na taasisi yake pekee bila kuhusisha serikali na wadau wengine.

Hivyo, hapa, tatizo si serikali kukataa taarifa ya kitaalamu. Ni kwamba mhusika amekiuka taratibu ambazo zimewekwa. Na huo ugonjwa haujaja sasa hivi. Upo siku nyingi ila umedhibitiwa.
pia utafiti wake ulikuwa ni wa awali tuu na haukuwa wa kufanya hitimisho kuwa nchini kuna Zika.
 
Sidhan atua alizochukuliwa ni stahili.
Ilipaswa watafute siku nyingine waweke Mambo sawa.

Sasa sipati picha ugonjwaa huu ukilipuka sijui huyo Pogba atasema nini?


Mbona hapo Uganda inatambulika ZIKA ipo lkn mnayosema sijui matatizo ya kiuchumi, kijamii hatuyaoni?

Tuache Ushamba!!
ulisikia watafiti wa uganda wamekurupuka kutangaza kwenye media
 
Hivi huyu....nae pia Anna kilango Malecele ni ndugu yake
 
Yeye katangaza tafiti ya kisayansi, na anatangazaga kila siku. Hivi mwananchi wa kawaida utataka kujua kuwa ugonjwa upo? au utataka kujua aliyesema ni nani? Kwangu ni bora nijue ugonjwa upo ili nichukue tahadhari, sio mnifiche kwa kigezo cha kuusubiria uwe epidemic ili mimi ndio niwe statistic
Ni kweli, tunapaswa kujua ili tuchukue tahadhali. Lakini tulipaswa kujua kwa namna ambayo haitaleta image mbaya kwa jamii ya kimataifa.. unadhani ni vizuri uwekewe vikwazo vya kusafiri kwenda nje kwa sababu inch imejulikana kuwa na zika? watalii wote kubadilisha route na kuikacha Tanzania? wawekezaji kuikacha tz kisa zika, wakati imekuwemo siku nyiiiiiiiiiingi na wala haijaleta madhara makubwa? kwa nini wasingetumia njia nzuri kuwaambia watanzania na sio kuleta sintofahamu kwa jumuiya za kimataifa?
 
Mnataka watu wafanye tafiti kisha wasiziseme? Kwa faida ya nani
 
Zika na NIMR

Dk. Mwele Ntuli Malecela leo si Mkurugenzi tena wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR). Ikulu leo imemtangaza Profesa Yunus Mgaya kuwa mbadala wake.

Kwanini Mwele kaondolewa? Nimeulizwa hili swali na baadhi ya watu nami nikauliza hapa na pale ili kupata majibu. Na hili ndilo nililoambiwa.

Mosi, kwamba ugonjwa wa Zika upo Tanzania. Ugonjwa huu ulianzia Uganda na upo pia kwetu kwa muda mrefu. Ila upo katika hali iliyodhibitiwa, wataalamu wanaitwa Endemic. Si tatizo kubwa lakini upo.

Lakini Tanzania haina tatizo la ZIKA. Kwa jinsi tatizo la ugonjwa huo lilivyo kubwa, kabla halijatangazwa, kuna taratibu za kufuatwa ikiwamo kuhusisha Serikali na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Imefanyika hivi kwa sababu madhara ya kutangaza ugonjwa huo kwa taifa ni makubwa kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Tatizo ni kwamba tangazo la Mwele halikufuata hizo taratibu. Na zaidi, halikuzingatia athari ambazo zingejitokeza kwa yeye kutoa taarifa kama zile.

Kwenye Kiswahili, tofauti ya maneno Endemic na Epidemic ( ugonjwa uliodhibitiwa na uliolipuka) ni ndogo. Ukisema Zika ipo, magazeti yatasema ZIKA imeingia.

Sasa, labda, Rais mwingine, kwenye Serikali nyingine, angeweza ˊkupotezea` tu kauli ile ya Mwele. Lakini binti huyu wa mzee John Malecela hakuwa amesoma vema alama za nyakati.

Hivyo, kwa maana ya kosa, Mwele alikosea. Ishu ya ZIKA haikuwa ya kutangazwa na taasisi yake pekee bila kuhusisha serikali na wadau wengine.

Hivyo, hapa, tatizo si serikali kukataa taarifa ya kitaalamu. Ni kwamba mhusika amekiuka taratibu ambazo zimewekwa. Na huo ugonjwa haujaja sasa hivi. Upo siku nyingi ila umedhibitiwa.
NIMR ni Taasisi ya wapi? Nani ni serikali? Yapi ni majukumu ya NIMR na yapi si majukumu yake Kwa mujibu wa Sheria?

"Think before you act"
 
Kuna tofauti kati ya kutangaza matokeo ya tafiti na kutangaza mlipuko wa ugonjwa.
Alichokifanya yule mama ametangaza matokeo ya utafiti ambao tahasisi yake imefanya....
Nilitegemea Waziri mwenye zamani aje kwa ufafanuzi kama huo mtoa mada ulioutoa...Kwanza wazili akitakiwa kuikubali tafiti then atueleze kuwa imezibitiwa /ipo kwa kiasi kidogo etc
 
wanapewa madaraka ya nini kama hawaruhusiwi kutoa tafiti zake? basi taasisi zote ziongozwe na kurugenzi ya ikulu.
Mbona na ww unakuwa mjinga kiasi hicho jamaa hapo katoa ufafanuzi mzuri kwamba kuna utaratibu unatakiwa kabla ya kutangaza tatizo kama hilo ikiwapo pamoja na kuijulisha serikali na WHO, watz mbona wengine uwezo wa kuelewa ni mdogo sana au unafurahi kuchangia bila hata kutafakari au ndiyo mlioajiriwa kukosoa kila kitu ? Very stupid
 
Mleta mada umepotosha pia.

Dr.Mwele Mallecela alitoa matokeo ya Utafiti uliofanywa na NIMR. Na utafiti ule ulikuwa unataka kujua Uhusiano wa watoto wanaozaliwa na vichwa vidogo hapa Tanzania na maambukizi ya Zika hapa Tanzania. Ambapo matokeo ya utafiti huo kuonyesha kuwa katika sampuli zaidi ya 500 zilizofanyiwa utafiti, Zaidi ya 15% walikuwa na Maambukizi ya Zika. Hitimisho la utafiti ule ni kuwa Homa ya Zika IPO(Endemic) hapa Tanzania na hivyo hatua zaidi zitapaswa kuchukuliwa.

Hakuna mahali popote ambapo Dr.Malecella alitamka kuwa kuna MLIPUKO(Epidemic) wa Zika hapa Tanzania.
 
Back
Top Bottom