Krismasi ya kwanza pasipo mvua ni ujumbe kwa mamlaka. Tuchukue tahadhari

Chuki ni kitu kibaya wewe kwako ndio hakuna mvua ila mikoani mvua zinanyesha kama zote. Yani ni baraka tele. Utabaki na chuki zako kwa serikali wenzanko tunasonga mbele. Pole sana
 
Ajabu sana kwanini watu wanakereka sana na maandiko,ila waambie hakuna uchawi watakavyo bisha!waliosema mvua imenyesha hongera kwa kumjibu mtoa mada.
 
Baraka zipo kama zote. Haki inatendeka na hakuna haja ya Mungu kulitesa taifa kwa uzembe wa watendaji ambao Mh Rais hakuwatuma. Nidhambi kutumia nia njema ya Mh Rais kuwaumiza watu. Nataka kuwaaambia hakuna mahali Rais ameahiza Raia awaye yeyote afanyiewe mabaya. Na kama ingekuwa kweli mamlaka zingesha react. Happy chriz Mass
 
Unaongelea nchi gani ww!? Huku dodoma tangu jana mvua imenyesha usiku kucha mpaka mida hii bado inanyesha.
 
Jana tarehe 24 Dec 2020 kunamtu nilikua naongea nae yupo Mwanza mjini,akanambia nisubiri kwanza mvua ikate ndo atakwenda nilipo muagiza.
Watu wa Mwanza town kama wapo humu watakuwa mashahidi.
 
Huku kwetu imenyesha usiku kucha na bado inaendelea kunyesha.
 
Mara nyingine tunapo post thread ni vema kusema tupo nchi gani ama mkoa upi. Kama weee ni sadist unayeombea mabaya tu yatokee ni vema pia ukapata taarifa sahihi kabla ya kuonesha matamanio yako maovu:

Kwa kitambo, siku ya leo ndo tumeshuhudia mvua ya kutosha hapa dodoma, mvua imekesha....... Endelea na fikra ovi zako
 
Mkuu huu utafiti wako mbona una kasoro nyingi japo sijasoma hadi mwisho.
Siku haijaisha tayari usha hitimisha hakutakuwa ma mvua.
Una uhakika sehem zote mvua haijanyesha leo?
Huku nilipo leo watu tumefurah kajua kametoka kidogo leo siku ichanganye ma pilau ya ive ndo mvua inyeshe manake kila siku imefululiza kwaiyo kutoka kwa jua leo huku kwetu ni baraka tele.
 
Mvua za baraka zinaendelea kunyesha mkoa wa Dodoma majira ya Christmas hata kuleta changamoto kwa wengi kwenda ibada. Nashangaa maelezo yako dmkali labda kama mko chini ya laana kwa kupinga sikukuu kubwa kuliko zote duniani na utawala halali uliowekwa na Mungu katika nchi yetu iliyobarikiwa tangu kuumbwa kwake.

Mimi nipo Dodoma ya Rais mcha Mungu, mhe.Dkt.John Magufuli na makuu ya nchi ya Tanzania na CCM ! Mvua ni kubwa tangu jana 24-12-2020 na hata leo tumeamka na mvua ya kutosha na wanyakaya wengi wamekimbilia kupanda mbegu mashambani baada ya baraka za mvua majira ya Christmas.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…