Kuanguka chooni/bafuni na kufa, kuna uhusiano gani?

Kuanguka chooni/bafuni na kufa, kuna uhusiano gani?

hii habari ya Majn nimesoma usiku huu Yarabbi mbona nimeogopa.uwiiiiiii Naomba Mungu nilinde navtimbwi vya viumbe vsivyoonekana
 
Jamani, kitaalam kuanguka na kupoteza fahamu ama kupata kiharusi haihusiani na mahali gani mtu amedondoka,, inategemea ni namna gani damu imevuja kwenyw ubongo, ama wengine moyo husimama , sasa hili laweza mpata mtu mpirani wakati anacheza,wakti anafanya mapenzi, wakti anaoga, wakti amelala fofofoo, hakuna jini wala pepo ktk ugonjwa
 
Tatizo ni masturbation...hawa wazee hufanya huo mchezo bafuni au chooni...kwavile nguvu za kujizuia zinakuwa zimewaishia huishia kuangukia kichwa...
 
Majini ni viumbe kam bindamu walioumbwa kbal ya binadamu wanaishi kama

tunavyoishi sisi. Wako Majini wazuri na Majini Mabaya kama tulivyo sisi Binadamu tupo binadamu wazuri na wapo

binadamu wabaya tunawaita ni Mashetani wa kibinadamu ukiwa wewe ni muuwaji basi wewe ni shetani wa kibindamu,na pia wapo majini wa kishetani .Shetani ni yule muovu hata binadamu akiwa ni muovu tunamwita ni shetani

mkuu. Kuna Viumbe aliowaumba Mungu sisi binadamu hatuwezi kuwaona kwa macho yetu kam hao majini na malaika ukiwa unaamıni kuna viumbe wanaoitwa malaika basi itakuwa ni rahisi pia kuamini kuwa kuna viumbe wanaoitwa Majini.


SHEITANI MTU NI NANI?




Sheitanimtu anaweza kuwa jamaa yako, ndugu yako, rafiki yako au wewe mwenyewe. Sheitanimtu ni kila anayeweza kumpoteza mtu akatenda jambo ovu kama vile kuiba, kuzini, kunywa pombe, kuvuta bangi na kutumia madawa ya kulevya au kukupandikiza chuki baina yako na mwengine.


Sheitanimtu kila siku unatembea naye, unakula naye lakini huwezi kumgundua kwa urahisi wakati wote unapokuwa nae hujifanya anaushari, busara na hekima upande wako kiasi kwamba wewe mwenyewe humpenda na kumwamini kwa kumuamini na kumthamini kwako basi anajenga katika akili yako mizizi ya tabia na mwenendo wake na hivyo kukufanya uwe miongoni mwa tawi lake.


Ewe ndugu yangu sheitanimtu hafanyi mambo yake kwa siri bali hufanya kwa uwazi ili wewe uyaone na uweze kushawishika. Anaweza kunywa pombe mbele yako kutumia madawa ya kulevya, kuvuta bangi na anaweza kukusimulia jambo lolote kama uzinzi n.k vitendo na masimulizi hayo yote ni kukuvuta wewe kutoka tabia nzuri kukupeleka katika tabia mbaya.


Rafiki yangu mpendwa huyo sheitanimtu yuko tayari kutumia hata gharama ilimradi tu akupoteze. Anaweza kununua vitu vya gharama ili akupe wewe akitaka uwe tu pamoja naye katika maovu. Hapa siyo kwa jinsi yako tu, msichana anaweza kugharamiwa na mvulana au mvulana anaweza kugharamiwa na msichana kwa ajili ya kufanya uovu. Jambo hili ewe ndugu yangu ni hatari sana kwani wewe unajua fedha ni fedheha.


Ewe ndugu yangu, wewe unaakili timamu na unajua ukweli wa mambo unajua yenye manufaa na hasara katika maisha ya kila siku. Kutokana na akili uliyokuwa nayo huna budi kuwa makini na kutafakari wakati unapopewa ushauri na huyo ambaye unasema rafiki yako. Tafadhali sana usipende kusema “ndiyo” au “hapana” bila kufikiria faida au madhara ya hiyo NDIO AU HAPANA yako.


Bila shaka wewe unapenda kuisha kwa amani na furaha karibu kila siku kwa hiyo huna budi kuwa makini katika ,maisha yako. Umakini ambao ninakuambia ni “KUFIKIRI KABLA YA KUTENDA” suala hili la kufikiri kabla ya kutenda litakufanya uweze kugundua mbinu na ujanja anaotumia huyo sheitanimtu na hivyo kujiepusha naye mimi sipendi kuona wewe rafiki yangu ukiwa katika huzuni na majuto ndio maana nina kupa mwanga katika maisha yako.


Ndugu yangu, sheitanimtu katika maisha yako ujitahidi kamuogopa kama ukoma jiepushe nae na asikuzoe nakukutawala katika akili yako na kukufanya wewe kuwa mtu usiyekuwa na kauli ya kusema HAPANA katika kila jambo la uovu.


Wewe ni rafiki na ni ndugu yangu, ninakupa mwanga huu kwa manufaa yako mwenyewe na sio kwa manufaa yangu. Nijukumu lako kutumia akili na hekima alizo kupa Mungu ili uweze kuepukana na sheitanimtu, nawe utaifanya akili yako ifanye kazi kama inavyo takiwa. Kama ulikwisha potenzwa siyo ukate tamaa bali tumia muda huu kujuta na kujirekebisha mara moja.






Mkuu,
Umeandika maelezo mengi sana,lakini ngoja nikuulize swali moja tu,
Shetani maana yake nini?
 
Mtakuja ku wauwa watu nyie ,shauri zenu

huyu jamaa na bibi yake wana logic ila hawajajua sayansi behind that. kama mtu ndizi ina sukari nyingi sana na madini ya potasium. mtu akianguka ghafla posibly sukari imeshuka au pressure imeshuka. kuongeza sukari kutamuamusha mgonjwa ikiwa sukari ilishuka na kupandisha pressure unahitaji maji ya kutosha au adrenaline. lakini pia potassium inausaidia moyo kupump haraka na hivyo kuongeza cardiac output na hatimaye pressure kupanda. Nb. hapa cmanishi mtu akianguka basi umlishe ndizi la hasha ila nimejaribu kuelezea ndizi ina vitu gani mhimu kwa pressure na sukari ya mwili.
naomba kuwasilisha.
 
Unapokuwa na shinikizo la damu au ugonjwa ya moyo, unaweza kupata matatizo pale unaponyanyuka kutoka chooni, kwenye kiti, au hata kitandani.

Matatizo mengi yanayowapata watu vyooni hayatokani na mashetani au kulogwa. Yanatokana na shinikizo la damu au magonjwa ya moyo. Mtu mwenye shinikizo la damu au magonjwa ya moyo hatakiwi kuchuchumaa na kusisimama ghafla. Vilevile hatakiwi kutoka kitandani au kusimama kutoka kwenye ghafla.
 
Acheni kwanza kuingiza imani za kishirikina;

Kuna wakati nilimsikiliza dakatari mmoja wa magonjwa ya moyo, na alilielezea hili (ilikuwa siku nyingi kidogo) kwamba inawatokea sana wale wenye matatizo ya presha, magonjwa ya moyo. Kubwa ni kwamba, inaweza kuwa ni kutokana na mstuko wa moyo/presha pale ambapo nguvu kubwa inatumika kusukuma "gogo" na hivyo kuchangia mstuko kwenye mishipa inayopeleka damu kwenye moyo.

Kuna maelezo zaidi kuhusu hili ila kumbukumbu imenipita kidogo. Labda tuwaite wataalamu wetu kwanza (wa tiba za kisasa) kabla ya kuingia kwenye majini.

CC: Riwa, Mupirocin

​Kwanini hali kama hiyo itokee chooni tu na si kwengineko na wengi wanaoanguka huko hufa, Mungu ndiye ajuaye.
 
hata wakichunguza hao ma-profesa wenu hawawezi kuona kitu huko chooni. Kuna shetani mbaya kila anaye anguka mwisho wake anapatwa na ugonjwa wa kupooza stroke na asipojishughulikia kujitibia basi mwisho wa huo ugonjwa aliopata ni kifo tu hakuna kitu kingine zaidi ya hicho kifo tujihadhari tunapokwenda chooni.
inamana haipo kisayansi ya darasani,ipo sayansi ya kiswahili
 
Unajua co wote watembeao brbrn n wzm watanzania ha2na kawaida ya kufanya chek up ya afya ze2 ndomana v2 kama hvyo vnashrkshwa na uchaw ila mnaamn co wote wangkao choon wameligwa mengne n maradh2
 
inamana haipo kisayansi ya darasani,ipo sayansi ya kiswahili
Haipo Kisayansi ya darasani hiyo ipo Sayansi ya kiafrika kuna mambo mengine huwezi kupata kwenye Shule za kizungu unapata Kwenye Shule za kienyeji tu.Hakuna hata Professor yoyote yule anayejuwa hayo mambo ya Sayansi ya Kiafrika.
 
Hata vitabu vya dini vinakubali kuna majini na shetani. ila tunawahususha vibaya na maisha yetu. watu wanatelezaga tu bafuni kwa kuwa kuna sabuni na hupelekea kujigonga vichwa kuvuja damu nyiingi ana kupasua mishipa ya fahamu. hakuna uchawi bafuni. amkeni

Well sayed Mkuu !!
Hakuna Uchawi kwani watelezapo,
Kuanguka na kubamiza Vichwa wanapata HEAD INJURY - na hii ni sababu tosha ya Vifo hivyo !!
 
Acheni kwanza kuingiza imani za kishirikina;

Kuna wakati nilimsikiliza dakatari mmoja wa magonjwa ya moyo, na alilielezea hili (ilikuwa siku nyingi kidogo) kwamba inawatokea sana wale wenye matatizo ya presha, magonjwa ya moyo. Kubwa ni kwamba, inaweza kuwa ni kutokana na mstuko wa moyo/presha pale ambapo nguvu kubwa inatumika kusukuma "gogo" na hivyo kuchangia mstuko kwenye mishipa inayopeleka damu kwenye moyo.

Kuna maelezo zaidi kuhusu hili ila kumbukumbu imenipita kidogo. Labda tuwaite wataalamu wetu kwanza (wa tiba za kisasa) kabla ya kuingia kwenye majini.

CC: Riwa, Mupirocin

Kama tatizo ni mishipa inaponzwa na kusukuma gogo, je vipi kuhusu wale wanafunzi wa shule ambao huwa wanaanguka kwa pamoja wanapokwenda chooni. je utasema wanafunzi wote wnapressure au choo kina mapepo.
naomba majibu tafadhali
 
Hakuna mashetani wala Majini. Hio mi naona inakuwa ni Pressure kali inayoendana na paralysis. hata mtu akipatwa na kiharusi midomo hupinda na either mkono au mguu au vyote hupooza.

vipi kuhusu wanafunzi wanaoanguka na kuzimia kwa pamoja wanapokwenda kwa vyoo vya shule.
prove my ignorance
 
Una jua vitu vingine ni vya ajabu sana kwanin chooni kila cku na tucckie chumban, jmn uchawi upo
 
Back
Top Bottom