Kuanguka chooni/bafuni na kufa, kuna uhusiano gani?

Kuanguka chooni/bafuni na kufa, kuna uhusiano gani?

Jamani wana jf.Naamini humu ndani tupo tofauti tofauti na kila mmoja kajaliwa karama pekee na mola wetu.Kwa hivyo basi ujuaji wako ndo karama yako ya ufahamu wako..Sasa back to the topic ni kwamba ni kwamba rafki yangu kafiwa na shangazi yake,chanzo alianguka chooni wakati alipo enda kujisaidia..sasa baada ya kuanguka huyu marehem mama mdomo wake ulikaa upande akapelekwa Hospitali ya Temeke,akalazwa kwa matibabu.Baada ya wk mbili na nusu huyo Mama (marehemu sasa)akafariki.Sasa kinachonifanya niiwasilishe hii thread.,ni kuwa taarifa kama hizi kwangu mimi zishanishawishi niamini mtu akianguka chooni huku town basii huyo ni kifo tuu.Hebu basi wenye ufaham,ushuhuda kama huu na uelewa wa mambo kama haya au yanayohusiana na kuanguka chooni/bafuni baada ya hapo unaugua au kufa,basi tutiririke kuringana na ujuzi,uelewa na ufahamu tulio jaaliwa.Rest in Peace.Shangazi.

Hiyo ni presha kali wala hakuna kingine...moja ya dalili ya presha kali ni kupinda mdomo....fuatilia au oogle utaona...hakuna cha ushirikina wala mauza uza...presha ya namna hiyo inaweza kukutokea sehemu yoyote tu
 
Mkuu MziziMkavu ka unamwomba Mungu kabla ya kuingia na kutoka, kutanguliza miguu kuna husikaje?
Mungu hana masharti ya kihivyo, upande wowote yupo, kama kakubali ombi lako anavunja nira zote za mashart ya kutanguliza miguu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu.@KakaJambaz Hiyo kwa imani ya Dini ya Kiislam kila kitu kwa Dini ya kiislam kina masharti yake hata ukitaka kula kwa dini ya kiislam

unatakiwa utumie mkono wa kulia ukitaka kuvaa kiatu kwa dini ya Kiislam unatakiwa uvae kiatu cha mkono wa kulia ukitaka kulala kwa dini

ya Kiislam unatakiwa ulale ubavu wa kulia kila kitu kwa Dini ya kiislam kinanzia mkono wa kulia. Hata kumsalimia mtu unatakiwa umsalimie

kwa mkono wa kulia ndivyo tulivyo fundisha sisi Waislam Adabu ya kila kitu sijuwi wewe upo dini gani? na mnatumia Upande gani? Ukiwa

chooni wakati wa kuchamba unatumia mkono wa kushoto tu sasa wewe unatumia mkono gani?
 
Acheni kwanza kuingiza imani za kishirikina;

Kuna wakati nilimsikiliza dakatari mmoja wa magonjwa ya moyo, na alilielezea hili (ilikuwa siku nyingi kidogo) kwamba inawatokea sana wale wenye matatizo ya presha, magonjwa ya moyo. Kubwa ni kwamba, inaweza kuwa ni kutokana na mstuko wa moyo/presha pale ambapo nguvu kubwa inatumika kusukuma "gogo" na hivyo kuchangia mstuko kwenye mishipa inayopeleka damu kwenye moyo.

Kuna maelezo zaidi kuhusu hili ila kumbukumbu imenipita kidogo. Labda tuwaite wataalamu wetu kwanza (wa tiba za kisasa) kabla ya kuingia kwenye majini.

CC: Riwa, Mupirocin
 
Last edited by a moderator:
Hii issue iliondoa uhai mjomba wangu pia, alianguka uani na kupinda mdomo na mkono wa kulia kushindwa fanya kazi. Kwa miezi mitatu aliteseka sana baadae ndipo shida ikagundulika muhimbili kuwa kuna mshipa ulipasuka kichwani. Bahati mbaya ikawa too late!!!

Mdau muanzisha mada pamoja na mchangiaji, kuanguka huko kumesababishwa na stroke (au maradhi ya baridi kwa kiswahili). Ndiyo maana mdomo umekaa upande au au mkono au hata upande mmoja wa mwili huwa haufanyi kazi vizuri.

Hakuna uhusiano na kuanguka chooni, yaani angeanguka po pote tu pindi stroke inapopiga.
 
haya mambo yapo,ndio maana uswahilini mtu,akianguka chooni kwa wanaojua hapelekwi hospital anawahishwa kwa fundi(mganga)na hii nimeisha ishuhudia tmk,kuna mama nyumba ya jirani alianguka chooni,wakataka kumpeleka tmk hospital wakatokea wazee,wakadai endapo atapelekwa hospital na kuchomwa sindano tu,damu ikatoka hatapona tena,ndipo wakampeleka kwa fundi hata saa haikuisha mama wa wa2 mzima!!na akaendelea na maisha yake kama kawaida,na hili jambo bwana lipo kwani matukio ya watu kudondoka vyoo/bafuni na kufariki au kupooza upande wa mwili yapo mengi sana,hususani uswahilini kwenye vyoo vya ku share!!Hayo mambo ya kitaalam mala oho ameangukia modula oblangata,sizani kama ni ya kweli,utakuta mtu wala hajagonga kichwa chini ametanguliza mkono tu,anaondoka!
 
Kuanguka chooni kunatokana na kiharusi(stroke)ambapo mishipa ya damu hupasuka(cerebral vascular accident)na hii inatokana na kupanda kwa presha kupita kiasi....na hii inatokea kwa watu wenye matatizo ya pressure kubwa...inatokea pale mtu anapofanya vitu vinavopandisha pressure ghafla kama kujisaidia haja kubwa au wakati wa ejaculation kwa wanaume( ndio maana weng hufa wakifanya mapenz au bafuni wakipiga punyeto)..na hiyo kupooza kunatokea kwa sababu ubongo ndo unacontrol misuli yote ya mwili..mishipa ikipasuka inasababisha damu kuvuja na hivyo kusababisha mgandamizo kwenye ubongo na seli za ubongo kufa..hii inaweza ikasababisha kufa ghafla kama mishipa mikubwa imepasuka au baada ya mda kama damu inavuja taratibu!!kama mishipa midogo ndo imekuwa affected mtu anaweza akapona baada ya muda
 
duh kweli JF noma,mi sina cha kuchangia nakula pindi tu.Ila hizo kesi za watu kufa baada ya kuanguka bafuni/chooni hata mimi nazisikia sana,miaka mi3 iliyopita nilipokuwa nasoma UDOM kuna mwanachuo alifariki baada ya kuanguka bafuni
 
kuna siku niliingia bafu lenye tiles... wakati naoga nikakumbuka kitu Fulani ikabidi nianze piga nyeto.... balaa ilikuwa pale wazungu walipotaka kutoka... nilijikuta naishiwa nguvu halafu nikateleza, ebana nilijibamiza sakafuni asikwambie mtu.... lakini nipo mpka leo
 
Kuanguka chooni kunatokana na kiharusi(stroke)ambapo mishipa ya damu hupasuka(cerebral vascular accident)na hii inatokana na kupanda kwa presha kupita kiasi....na hii inatokea kwa watu wenye matatizo ya pressure kubwa...inatokea pale mtu anapofanya vitu vinavopandisha pressure ghafla kama kujisaidia haja kubwa au wakati wa ejaculation kwa wanaume( ndio maana weng hufa wakifanya mapenz au bafuni wakipiga punyeto)..na hiyo kupooza kunatokea kwa sababu ubongo ndo unacontrol misuli yote ya mwili..mishipa ikipasuka inasababisha damu kuvuja na hivyo kusababisha mgandamizo kwenye ubongo na seli za ubongo kufa..hii inaweza ikasababisha kufa ghafla kama mishipa mikubwa imepasuka au baada ya mda kama damu inavuja taratibu!!kama mishipa midogo ndo imekuwa affected mtu anaweza akapona baada ya muda

Thanks kwa majibu yanayoelekea kwenye sayansi.
Watu wengi wanaamini ushirikina/uchawi/majini na kuyahusisha na kuanguka chooni. Hizi imani ni janga kubwa.
Kuna watu pressure ikipanda huwa wanajisikia kuumwa kichwa na hujisikia joto fulani kiasi cha kutamani kwenda kuoga maji ya baridi. Atajimwagia maji ya baridi ambayo yatafanya ku-shrink kwa blood vessels muda ambao ni critical na mishipa inatakiwa itanuke. Hii hupelekea madhara kwenye moyo wenyewe au kwenye mishipa mingine ya damu kama ile ya kwenye ubongo. Next ni kupata heart attack (mishipa ya kwenye moyo imedhurika) au anapigwa stroke (mishipa ya kwenye ubongo imedhurika).
Vyote vitamuangusha huko huko bafuni au muda mfupi baada ya kutoka bafuni. Kama alikuwa anajikamua choo, pia hali ile ile yaweza kumtokea.

Hakuna cha mashetani wala majini wala wachawi.

Hivi hayo majini na mashetani ni vilaza hivyo mpaka wawe wanamngojea mtu bafuni au chooni????
 
Pia tunatakiwa..tukisha maliza haja ufanye utoke ..pia mambo ya kuimba chooni ni mabaya kabisa..kuna viumbe humo ndo makaazi yao..so unapomaliza toka..
duh, umenikumbusha mbali sana. Nakumbuka nikiwa mdogo nilipigwa marufuku kupiga miluzi au kuimba nikiwa chooni.

Anyway, kwa experience yangu, ambaye niliwahi kuanguka bafuni, nafikiri kuanguka kule huwa kunasababishwa wakati mwingine na sabuni. Kama unaoga kwenye bafu lenye tiles, halafu ukawa unatumia shampoo kwa mfano, huwa kuna tendency ya kusababisha utelezi, na kwa kuwa unakuwa umefumba macho ili kuzuia sabuni isiingie machoni, ukianza kuteleza na kuanguka, basi unaanguka kama kifurushi, huoni pa kujishika.

Mimi nilianguka hivyo, nikapoteza fahamu kwa kama dak tano hivi, halafu baadaye zikanirudia. Lakini habari ya mdomo kwenda upande na mkono kuvunjika or whatever, inategemeana na upande utakaoangukia. Maana kishindo kila cha uangukaji, kama unajibamiza ukutani basi ni lazima huo upande uparalaize, maana uwezekano wa kupasuka mishipa ya damu huo upande ulioangukia ni mkubwa sana. Kwa hakika likelihood ya kufa katika mazingira yale ni kubwa sana kwa kuwa unaweza kuangukia kisogo. Na sidhani kama ukiangukia kisogo unaweza kusalimika kwa namna yoyote ile.
 
Hii issue iliondoa uhai mjomba wangu pia, alianguka uani na kupinda mdomo na mkono wa kulia kushindwa fanya kazi. Kwa miezi mitatu aliteseka sana baadae ndipo shida ikagundulika muhimbili kuwa kuna mshipa ulipasuka kichwani. Bahati mbaya ikawa too late!!!

.........mjomba wako alipata stroke, hili tatizo lipo dunia yote,sema hawaanguki chooni kama bongo.
Na hapa bongo watu wengi naanguka chooni sababu ya mtindo wa vyoo vingi ni vya kuchuchumaa.

Ujue kuchuchumaa ni zoezi tosha, sasa utakuta mtu ana tatizo la high blood pressure, mtu kama huyu
akichuchumaa na kuinuka ghafla inaweza sababisha hypertension,hivyo mfupa unaweza pasuka na
kusababisha mtu kuanguka ghafla na kusababisha stroke.

Na ukipata stroke lazima mdomo upinde upande, hakuna ushirikina wala nini.
 
Mkuu.@KakaJambaz Hiyo kwa imani ya Dini ya Kiislam kila kitu kwa Dini ya kiislam kina masharti yake hata ukitaka kula kwa dini ya kiislam

unatakiwa utumie mkono wa kulia ukitaka kuvaa kiatu kwa dini ya Kiislam unatakiwa uvae kiatu cha mkono wa kulia ukitaka kulala kwa dini

ya Kiislam unatakiwa ulale ubavu wa kulia kila kitu kwa Dini ya kiislam kinanzia mkono wa kulia. Hata kumsalimia mtu unatakiwa umsalimie

kwa mkono wa kulia ndivyo tulivyo fundisha sisi Waislam Adabu ya kila kitu sijuwi wewe upo dini gani? na mnatumia Upande gani? Ukiwa

chooni wakati wa kuchamba unatumia mkono wa kushoto tu sasa wewe unatumia mkono gani?

'naaam,ukila kwa mkono wa kushoto unakula na shetani,ukila bila ya kusema BISMILLAH unakula na shetani na kwa kuongezea tu ni kwamba,unapoingia chooni ukasoma DUA na kutanguliza mguu wa kushoto basi hata kama kuna MAJINI na MASHEITWAAN mia hakuna hata mmoja atakayekuona mpaka unatoka'
 
Mmh mzizi mkavu umenitisha kwa kweli lol.. Mungu nilinde na maajabu ya dunia
Bibie.Diana Fares Majin na Mashetani yapo na yametajwa pia katika Biblia hebu soma hapa
Majini na Shetani, ni nini tofauti yake?

Math. 16: 22-23.

MASKANI ZA MAJINI. (WANAMOISHI)





Ndugu yangu msomaji umuhimu wa elimu hii ni kubwa sana, kwani Mwenyezi mungu ametupa tahadhari sana kuhusiana na Shetani kiumbe wake. Kwani yeye Mwenyezi mungu ndiye alie muumba na yeye mwenyezi Mungu ndiye alietupa habari kujikinga naye huyo Shetani. hivyo basi ni vyema kutambua baadhi ya sehemu ambazo anakaa au anaishi shetani.

Sehemu hizo nazitaja kama ifuatavyo:

MAJANGWANI- Ni sehemu ambayo hupenda sana kukaa Shetani au Jini, hivyo ni vyema kupita sehemu hiyo kwa dua (dhikri) maalum.

NYUMBA ZA BINADAMU- Pia hukaliwa na majini wa kishetani pia ni vizuri tukalifahamu hilo na kuishi maisha ambayo mwenyezi mungu anayaridhia.

MASHIMO YA TAKA TAKA- Ni moja katika sehemu za Shetani kukaa au kuishi, kwa hiyo ni muhimu sana kuchukua tahadhari.

MAPANGONI- Pia ni sehemu ya tahadhari kwani jini anaamini kwamba ni sehemu tulivu.

CHOONI- Ni sehemu ilio faragha pia ni sehemu ya hatari sana mara nyingi mtu akianguka chooni hupata madhara makubwa sana. hivyo ni vyema kuingia sehemu hii na dua maalum.

MITI MIKUBWA- Pia hupendelea kuishi au kukaa majini, miti hiyo ni kama vile mbuyu, msufi. N.K.

VISIMA- Hii ni sehemu ya muhimu sana kwa majini kukaa au kuishi katika maisha yao, pia ni muhimu sana kwa maisha ya binadam. Hivyo ni muhimu sana twende visimani tukiomba dua za ulinzi.

MITO- Pia ni sehemu muhimu sana kwa wanadamu alafu pia ni sehemu ambayo hupenda kuishi au kukaa majini. Hivyo ni muhimu kukumbuka dua wakati tupitapo au twendapo mtoni kwa shida ya muhimu.

MABWAWA- Ni sehemu ambayo hupenda sana kuishi au kukaa majini, tena na watoto wengi hupenda kuoga katika mabwawa. Kwa hiyo ni lazima tuyafahamu hayo.

BAHARINI AU MAZIWANI- Nayo ni sehemu ambayo wanaishi majini au mashetani. pia si sehemu ya kudharau, ni vizuri kulitambua hilo na kujikinga nalo kwa dua au maombi kutoka kwa Mwenyezi mungu.

MILIMANI- Ni sehemu muhimu kwa majini na hupenda sana kuishi au kukaa. Pia ni lazima kufata sheria zote ambazo kwa waislamu Mtume amefundisha pia kwa wakristo wanamaombi yao yakiwa kama kinga.

KATIKA MWILI WA BINADAMU- Shetani anaweza kuishi au kukaa katika mwili wa binadamu pasipo binadamu kugundua. Hii inatokea kama shetani huyo katumwa aje kwako na mtu fulani au kapenda mwenyewe kuingia katika mwili wako.

Ndugu yangu msomaji baada ya kutambua, kujua, kufahamu na kuelewa sehemu ambazo waishizo majini au mashetani basi ni lazima kuwa makini na kumuomba Mwenyezi Mungu atuepushie matatizo mbalimbali. Kila chenye kuumbwa huumbwa kwa makusudio ya mwenye kuumba na kila chenye kutengenezwa hutengenezwa kwa makusudio ya mwenye kutengeneza.

Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu. Au boonyeza hapa.Mzizi Mkavu






'heshima kwako mkuu long time kaka............upo'
Mkuu Mwanahip Nipo tu vipi wewe hali ya maisha huko uliko?
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: 1gb
Back
Top Bottom