Kuanguka chooni/bafuni na kufa, kuna uhusiano gani?

Kuanguka chooni/bafuni na kufa, kuna uhusiano gani?

Kwa waislam tunaamini kuwa huko chooni kuna wadudu wabaya saana (mashetan) na maumbo yao yapo tafauti ..mfano mtu akianguka chooni..utamuona mdomo wake ..umekuwa upande
.au mokono haifanyi kazi..alimradi hatokuwa sawaa tu..sasa hao wadudu wanakuwa sura zao kama hizo nolizozitaja..mdomo upande n.k. NDio maana mashekhe zetu kila siku anatwambia tusome dua malaum unapoingia chooni na unapotoka salaama ..ili dua hiyo ikukinge na ballaa hilo..


Mkuu naamini na elimu dunia umeipitia vizuri na una UPEO, jaribu kuchanganya na hiyo pia inaweza kusaidia. Hata mkuu wetu wa kaya aliwahi twambia, ''akili za kuambiwa changanya na zako'', nadhani alikua sahihi.
 
ukiona mtu kaanguka bafuni au chooni wahi umchane eneo lolote na wembe damu itoke kidogo, baada ya hapo mtoe kwa huduma ya kwanza.

kwa sisi wakristo hakuna haja ya kumchana popote, tunampa damu ya yesu.
 
  • Thanks
Reactions: 1gb
Jamani wana jf.Naamini humu ndani tupo tofauti tofauti na kila mmoja kajaliwa karama pekee na mola wetu.Kwa hivyo basi ujuaji wako ndo karama yako ya ufahamu wako..Sasa back to the topic ni kwamba ni kwamba rafki yangu kafiwa na shangazi yake,chanzo alianguka chooni wakati alipo enda kujisaidia..sasa baada ya kuanguka huyu marehem mama mdomo wake ulikaa upande akapelekwa Hospitali ya Temeke,akalazwa kwa matibabu.Baada ya wk mbili na nusu huyo Mama (marehemu sasa)akafariki.Sasa kinachonifanya niiwasilishe hii thread.,ni kuwa taarifa kama hizi kwangu mimi zishanishawishi niamini mtu akianguka chooni huku town basii huyo ni kifo tuu.Hebu basi wenye ufaham,ushuhuda kama huu na uelewa wa mambo kama haya au yanayohusiana na kuanguka chooni/bafuni baada ya hapo unaugua au kufa,basi tutiririke kuringana na ujuzi,uelewa na ufahamu tulio jaaliwa.Rest in Peace.Shangazi.

Matukio ya mtu kufariki ni ya aina nyingi. Mama alishaanguka chooni mara mbili na hajafa. Kuna watu wanakutwa wamekufa wakiwa wamepumzika sebuleni, wengine wamelala kitandani, wengine wakiwa wanasubiri usafiri kwenye kituo cha bus na wengine wakiwa wamelala guest house. Mimi nadhani ni imani tu rahisi ya kuhusisha masimulizi ya watu mbalimbali kuliko kudhani kama kuna uhusiano wowote. By the way, afadhali ya kusema kuna uhusiano kati ya kulewa sana gongo na kufariki maana kesi hizi nazo ni nyingi.
 
1gb
Kuanguka chooni itategemea utaitafsiri vipi, mfano kishirikina/kiimani/Kimila/ Kisayansi n.k.

Kishirikina watu huamini, mtu 'amemchawia' mwingine na hivyo kumuadhibu kwa njia hiyo.Hii ipo hadi leo katika jamii yetu.

Kiimani, wengine huamini ni aina ya adhabu kutokana na uovu mtu aliowahi kuufanya na hivyo Mungu kumuadhibu kwa nia hiyo. Au uwepo wa "Majini" kwa wenye kuamini hivyo.

Kisayansi, hali hii inaweza kutokea kwa watu wa aina nyingi lakini Mtu kudondoka Chooni (specifically), hutegemea Jinsia, umri, Kazi, aina ya ugonjwa n.k

Jinsia:
Wanaume- hasa kuanzia umri wa miaka ya 55 kuendelea, zaidi ikiwa kuanzia miaka 65 hadi 70 huwa na ongezeko la ukuaji wa tezi dume (Prostate), hii hufanya kugandamizwa kwa njia ya mkojo na hivyo wakati wa kujisaidia haja ndogo (kukojoa) hutumia nguvu nyingi 'Straining' na kusababisha kuongezeka kwa pressure tumboni ilihali kushuka ghafla kwa msukumo wa damu) na hivyo kuleta kizunguzungu na mtu kudondoka.(same scenario mtu akienda haja kubwa na ku-strain)

Wanawake- Kufikia umri wa miaka 55 na kuendelea(kwa wanawake) hasa ule muda ambao ukomo wa mzunguko/hedhi kukoma wanawake wengi hupatwa na tatizo hili, hasa kutokana na mifupa yako kutokuwa imara.

Pia wanawake wengi waliotunia vidonge vya uzazi wa mpango.

Kazi:
Pili aina ya kazi, wengi wa watu wenye kazi za kuinama...mfano kubeba mizigo, wapishi (hasa migahawa n.k), hupata shida ya pingili za uti wa mgongo, hii huweza kusababisha miguu kukosa nguvu, na mru awapo katika sehemu unayoteleza ni rahisi kuanguka na kuvunjika

Aina ya ugonjwa:
Magonjwa mfano Shinikizo kubwa la damu (Hypertension), na magonjwa mbali mbali ya kifua hutegemea sana uwiano mzuri wa msukumo wa damu na mgandamizo wa hewa, viashiria vya mgandamizo mkubwa (Baroreceptors ) mwilini hutambua endapo kunakuwa na shida hiyo.

Pili, magonjwa ya mifupa kwa aina zake hufanya miguu kutokuwa imara hivyo kazi za kuinama, kuchuchumaa kwa muda mrefu huweza kuwa katika hatari ya kudondoka na kuvunjika .

Hivyo basi the bottomline ni STRAINING activity yeyote yenye kusababisha kubadilika kwa pressure, pamoja na matatizo ya mifupa...na inakuwa chooni, kwa sababu tu ya slippery floor/tiles, straining wakati wa kujisaidia (haja kubwa na haja ndogo).
hippocratessocrates
Mkuu umenena vyema,mpaka nime ku pata vizuri.big up.Tumia ujuzi/maarifa yako kwa wanajamii
bila hiana utabarikiwa sana.GOD bless YOU
Make you great and so socrates.
 
Last edited by a moderator:
Duh mambo haya au imani hii ni kwa nchi zetu masikini au hata kwa akina OBAMA yapo?
 
Ama kweli "watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa" Wazungu wengi hasa Europe sasa hivi wengi hawaamini uwepo wa Mungu wala shetani! Ilianza hivi hivi kila kitu waliona kinatokea tu kama tunavyosema hapa mara Pressure,Stroke n.k hivyo kujiona hawahitaji msaada wa Mungu wala kumuabudu na makanisa ni matupu hivi sasa.

Yapo magonjwa kama hayo kwa wanadamu lakini shetani pia anatumia magonjwa kama hayo kutuangamiza huku tukikazana na vidonge na sindano tu bila maombi ya nguvu pia.

Shetani ni roho na anaweza kufanya lolote ili kuharibu maisha yako dakika yoyote.Matukio mengi ya kuanguka ghafla chooni yana mkono wa shetani ndio maana kesi nyingi za kuanguka chooni huwa ni kifo kama hujui kuliita jina la Yesu katika mazingira hayo au kuombewa.

Wandugu shetani sio mpaka ukutane na dudu kubwa usiku ni katika hali hizi hizi za kawaida kwa kutushawishi kufanya dhambi kupitia madhaifu yetu au kututesa kwa kila namna.Kama hujakutana na hali hizi na kuona jinsi maombi yanavyoweza kukutoa katika hali hiyo ni ngumu kuelewa zaidi ya kwenda kanisani tu kama ulivyofundishwa na wazazi wako bila kufanya bidii ya kumjua Mungu.
 
Samahani kaka nlikua naulizia kama umchane kidgo kivip na kwa nini unamchana kidogo?naomba utusaidie kwa majibu ili na sisi tuwasaidie na wengine.
Naomba kwa hilo
 
Shughuli zangu zina nilazimu kusafiri mara kwa mara, hivyo nimebahatika kuingia katika vyoo na mabafu ya aina tofauti tofauti, ukiwa unaingia mwanza mjini baada ya kuvuka reli kuna hoteli fulani ambayo tulifikia kipindi fulani, wenzetu waliotutangulia walituandikia barua pepe yenye kichwa cha habari "slippery floor" ikiwa na tafsiri sakafu inayoteleza barua pepe hiyo iliendelea kusema kwamba tafadhali mjihadhari na sakafu ya bafuni hapa hotelini kwani chini ina vigae ambavyo vikiingia maji wakati umevaa kandambili uwezekano wa kuanguka ni mkubwa..tafadhali chukua tahadhari kwani imenitokea mimi na watu wengine pia....kutokana na barua pepe hii ninaujasiri wa kusema sababu ya kwanza kwa watu kuanguka mabafuni/vyooni ni settings za choo au bafu kwa wale waliosakafia vyoo/mabafu yao hakikisha unasakafia choo/bafu lako vigae maalum kwa ajili ya vyoo/bafu mara nyingi huwa vina kashata kashata, tukija sababu ya watu wengi kufa au kuugua kiharusi na magonjwa mengi yanayosababishwa na kugongwa kuchwani "(troumour) sina uhakika na spelling...eneo la bafu/choo cha kawaida halimtoshi mwanadamu kulala ki marefu na mapana (yaani sio mraba) hivyo unapoanguka ni lazima kichwa kitagonga kwenye ukuta maeneo ya kisogono kwani mara nyingi tunaangukia mgongo, pia kichwa kinaweza kugonga sinki la kunawia mikono au hata toilet seat...hapo ni lazima ufe au upate na troumour bila uchawi wala ndumba
 
Hebu tupate basi uhusiano wa kwenda chooni/Bafuni na STROKE!!!!!!!

Binafsi nalifanyia kazi hilo mkuu ili tupate uhakika. Ni suala la kuvuta subira tutapata uhusiano uliopo.

Very good comment! I second you.

KUANGUKA CHOONI AU SEHEMU YOYOTE ILE UNAWEZWA KUPATWA NA UGONJWA WA KIHARUSI (STROKE)


KAMA kuna jambo au tatizo la kiafya linaloweza kubadilisha maisha ya mtu au hata kupoteza uhai wake haraka, ni ugonjwa wa Kiharusi (Stroke). Ugonjwa huu, ambao huwa ni matokeo ya matatizo ya kiafya ya muda mrefu, huweza kumtokea mtu bila kutarajia.

Lakini wataalamu wa masuala ya afya, hasa wanaoufahamu vizuri ugonjwa huu, wanatuambia kwamba kabla ya mtu kupatwa na kiharusi, huonesha dalili fulani, ambazo kama zikigundulika mapema na kushughulikiwa, anaweza kunusurika na athari zake.

Hebu soma kisa hiki; Wakiwa katika pikiniki, wakila, kunywa na kufurahi, Asha anajikwaa na kuanguka chini, wenzake wanashtuka na kumuuliza; “kulikoni, unaumwa?

Asha anajibu kuwa hana tatizo, bali viatu virefu alivyovaa, ambavyo hajavizoea, ndivyo vilivyomuangusha, anawatoa wasiwasi wenzake kuwa haumwi chochote. Asha anainuka, anajifuta na kuendelea na kufurahi na wenzake kama kawaida, ingawa usoni anaonekana hayuko sawa.

Wanamaliza pikiniki yao na saa 12 jioni ilipowadia kila mmoja alikuwa nyumbani kwake. Saa 3 baadaye, ndugu yake Asha anawapigia simu rafiki zake na kuwaambia kuwa Asha amekimbizwa hospitalini, baada ya kuanguka tena na saa moja iliyofuata, Asha alifariki dunia..! Kumbe Asha alipatwa na kiharusi tangu wakati ule akiwa pikiniki na wenzake.

Laiti wangebaini kuwa kule kuanguka kwake kulikuwa ni dalili ya kupatwa na kiharusi, wangemuwahisha hospitali na angepatiwa matibabu na pengine angepona. Wanaowahishwa hospitali, baadhi hupona kabisa na baadhi hunusurika kifo lakini hubaki katika hali mbaya, kama vile kupooza baadhi ya viungo au mdomo kwenda upande.

Wataalamu wa ugonjwa huu wanasema kuwa mgonjwa anapowahishwa hospitalini ndani ya muda wa saa 3 na kupewa matibabu yanayostahili huweza kupona kabisa.

UTAMJUAJE MGONJWA?

Wakati mwingine kuzijua dalili za kiharusi ni vigumu. Madaktari wanasema kuwa unaweza kumjua mtu anayenyemelewa na kiharusi kwa kumuuliza maswali matatu rahisi yafuatayo:

-Mwambie atabasamu – mtu mwenye tatizo hilo hawezi kufanya hivyo, akifanya atafanya kwa shida

-Mwambie azungumze na kusema sentesi fupi, kama vile; “hali yangu leo siyo nzuri” – bila shaka hataweza kusema, mdomo huwa mzito.

-Mwambie anyanyue juu mikono yake miwili – hatoweza kufanya hivyo.

Inaelezwa kuwa, iwapo ndugu, jirani au jamaa yako atafanya mambo hayo matatu kwa shida au akashindwa kufanya moja wapo, muwahishe haraka hospitali!

Njia nyingine ya kumgundua mtu mwenye kiharusi, ni kumuomba atoe ulimi nje – mara nyingi wenye kiharusi hushindwa kufanya hivyo na wakiweza, huweza kutoa ukiwa upande

UNAWEZAJE KUJIZUIA?


Hakuna njia nyingine unayoweza kujiepusha na ugonjwa huu isipokuwa kuzingatia ulaji sahihi wa vyakula. Watu wote ninaowajua mimi waliopoteza maisha au kuathirika kutokana na ugonjwa huu, historia yao ya ulaji vyakula haikuwa nzuri kabisa.

Ulaji sahihi ndiyo wimbo wa kila wiki katika makala haya. Tunaposema ulaji sahihi, tuna maana kuzingatia ile kanuni inayotutaka kula vyakula kutokana na umuhimu wake mwilini na si kwa sababu ni vitamu mdomoni. Kanuni hiyo inatutaka tule vyakula kwa wingi vitokanavyo na nafaka halisi.


Tunatakiwa tule kwa wingi matunda na mboga za majani kila siku, tunatakiwa tule kwa kiasi vyakula kama vile nyama nyekundu, maziwa, vyakula vya kukaanga n.k na tunatakiwa tule kiasi kidogosana cha sukari na bila kusahahu kunywa maji mengi kila siku, angalau lita moja.

Kushindwa kuzingatia kanuni hizo, ni kukaribisha matatizo mengi ya kiafya, ikiwemo ugonjwa huo hatari ambao unatuondoa kimya kimya tukiwa na umri mdogo.
 
Kuanguka chooni au bafuni na kufa si ushirikina bali ni science iliyojificha ambayo wengi hawajui hasa watanzania.
Kwanza kumbukeni vyumba vya choo na bafu ni vidogo sana kiramani uklinganisha na vyumba vya kawaida. Vyumba hivi most of the time vinakuwa na slippery ground. Na mara nyingi sana watu wanaokufa vyooni hasa ni kwenye vyoo vya kisasa hasa vile vya kukaa.
Sasa hivi vyoo/bafu watu wakiingia wanaoanguka mara nyingi huteleza na % kubwa wengi wao huangukia kisogo ambapo husababisha fuvu la kichwa kujibamiza kwenye ukuta au kwenye sink la choo hivyo husababisha fracture ya fuvu la kichwa na kutikisika kwa ubongo hivyo damu kuvujia kwenye ubongo na mara nyingi watu wa namna hii hufa pale pale. Wachache sana wanaofika hospital ambapo inategemea ameangukaje kama huyu ndugu wa mleta mada. Asilimia kubwa ya wanaokumbwa na mikasa hii ni wazee coz ya umri na kukosa balance. Lakini hata vijana baadhi hupatwa na shida hizi hasa wale wanaopenda kufanya mapenzi bafuni au choo ambapo wengine wao huanguka na pengine kuvunjika mifupa ilikaribu mishipa muhimu ya dam na kufa kwa kuvuja damu. Ukitaka kujua haya mambo waweza angalia kipindi cha 1000 ways to die on SONY MAX. kwa ufupi hii ndo medicine yangu na nimeshashuhudia nyingi sana baada ya post mortem. Mimi siku moja nilinusulika chooni niliteleza kidogo nianguke na choo cha kukaa yaani nisingepata balance nisingekuwepo Leo. Na siku nyingine nilikuwa nadeki nyumba ambayo nilikuwa nahamia sasa nikamwaga sabuni floor yote na maji nikavua viatu kuanza kutembea tu nilianguka vibaya kisogo kiligusa kidogo chini lakini coz ni mtu wa mazoezi yalinisaidia kuuinua kichwa na kutojigonga chini sana ila shingo iliniuma 2wks. Kwa hiyo hakuna majini this is a physiology of death behind falling in toilet or shower room.
 
kuanguka bafuni/chooni sio lazima ufe ila chamoto utakiona

VATICAN CITY - Pope John Paul II was hospitalized today after breaking his right thighbone in a

fall in his bathroom.

Vatican spokesman Joaquin Navarro said the 73-year-old pontiff's fall late yesterday was due to slipping, not due to losing consciousness or being ill.

Dk.Slaa aanguka bafuni

By Grace Chilongola

1st August 2010


headline_bullet.jpg
Avunjika mkono wa kushoto
headline_bullet.jpg
Amfagilia Dk. JK kwa amani



SlaaMkono%281%29.jpg

Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Dr Willibroad Slaa (kulia) akiwaelezea waandishi wa habari jinsi alivyoanguka na kuvunjika mkono.



Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, amevunjika mkono baada ya kuanguka akiwa bafuni Jijini Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, mgombea huyo wa urais ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chadema, alipata ajali hiyo kati ya saa 1:45 na saa 2:00 za usiku juzi baada ya kuteleza bafuni.
"Jana baada ya kutoka kwenye mkutano, akiwa hapa Nyumbani hoteli, alipata ajali baada ya kuteleza bafuni na kuangukia mkono wa kushoto ambao kwa mujibu wa madaktari, umevunjika." alisema Mbowe.
Alieleza kuwa, mgombea wake alipata huduma ya kwanza kwa Dk. Vicent Muada na baadaye alipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando na kusaidiwa na Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dk. Charles Majinge aliyemuunganisha na mtaalamu wa mifupa wa hospitali hiyo.
"Kweli nimevunjika mkono huu wa kushoto sehemu ya juu ya kiwiko." Alisema Dk. Slaa na kuongeza kwamba, juzi baada ya kuumia alipata hali mbaya lakini hadi jana alikuwa akijisikia nafuu.
Katika mkutano wake uliofanyika uwanja wa Furahisha Kirumba jijini hapa juzi, Slaa na viongozi wenzake wa Chadema walitumia muda mwingi kumshambulia Rais Jakaya Kikwete na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akitamba kwamba anataka kumung'oa Rais Kikwete Ikulu.
Pamoja na tambo na majigambo yake, Slaa alifagilia amani iliyopo nchini na kuipongeza serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kutokuwa na dini na ndiyo maana wananchi wake hawagombani kwa udini.
Toka alipotangazwa na chama chake kuwa mgombea urais, Dk. Slaa amekuwa akivuta umati wa wananchi katika mikutano yake ya kujitangaza.
 
Jamani wana jf,

Naamini humu ndani tupo tofauti tofauti na kila mmoja kajaliwa karama pekee na mola wetu.Kwa hivyo basi ujuaji wako ndo karama yako ya ufahamu wako.

Sasa back to the topic ni kwamba ni kwamba rafki yangu kafiwa na shangazi yake,chanzo alianguka chooni wakati alipo enda kujisaidia.

sasa baada ya kuanguka huyu marehem mama mdomo wake ulikaa upande akapelekwa Hospitali ya Temeke,akalazwa kwa matibabu.
Baada ya wk mbili na nusu huyo Mama (marehemu sasa)akafariki.

Sasa kinachonifanya niiwasilishe hii thread.,ni kuwa taarifa kama hizi kwangu mimi zishanishawishi niamini mtu akianguka chooni huku town basii huyo ni kifo tuu.

Hebu basi wenye ufaham,ushuhuda kama huu na uelewa wa mambo kama haya au yanayohusiana na kuanguka chooni/bafuni baada ya hapo unaugua au kufa,basi tutiririke kuringana na ujuzi,uelewa na ufahamu tulio jaaliwa.

Rest in Peace Shangazi.

Kitu kinachoweza kuwa na uhusiano wa kifo cha bafuni hasa kuliko chooni (kwa maoni yangu) ni kujimwagia maji baridi kwa mtu mwenye mshutuko wa moyo wakati anajisikia joto. Hii inaweza ikawa na reaction. Au kama ni chooni kama mtu anasukuma kwa nguvu kiasi cha kupungukiwa hela kwenye mapafu. Vinginevyo, sioni uhusiano. Au pengine ni kwa sababu siamini kama uchawi upo.
 
jamani wana jf,

naamini humu ndani tupo tofauti tofauti na kila mmoja kajaliwa karama pekee na mola wetu.kwa hivyo basi ujuaji wako ndo karama yako ya ufahamu wako.

Sasa back to the topic ni kwamba ni kwamba rafki yangu kafiwa na shangazi yake,chanzo alianguka chooni wakati alipo enda kujisaidia.

Sasa baada ya kuanguka huyu marehem mama mdomo wake ulikaa upande akapelekwa hospitali ya temeke,akalazwa kwa matibabu.
Baada ya wk mbili na nusu huyo mama (marehemu sasa)akafariki.

Sasa kinachonifanya niiwasilishe hii thread.,ni kuwa taarifa kama hizi kwangu mimi zishanishawishi niamini mtu akianguka chooni huku town basii huyo ni kifo tuu.

Hebu basi wenye ufaham,ushuhuda kama huu na uelewa wa mambo kama haya au yanayohusiana na kuanguka chooni/bafuni baada ya hapo unaugua au kufa,basi tutiririke kuringana na ujuzi,uelewa na ufahamu tulio jaaliwa.

Rest in peace shangazi.

hiyo ni ajali kama zingine
 
Wakuu hata mimi hili jambo nimelisikia mara kadhaa!
Binafsi nahisi sababu kuu 3 ukitoa ushirikina, nazo ni:
1. Wengi wetu vyooni/bafuni tunaweka tiles zinazoteleza,
2. Wengi wetu vyoo/bafu zetu ni vyumba vidogo ukiteleza huna jinsi ya kujitetea, unaishia kugonga kichwa ukutani na
3. Wengi wetu hatujui kusafisha vyoo/bafu zetu hivyo hubaki na sabuni zinazoteleza.
 
Back
Top Bottom