mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 20,925
- 51,688
Kuna vyeo vya kisiasa ukishavifikia huwezi tena kusonga mbele,inakuwa ndio climax ya mafanikio yako.
Tanzania haijawahi kuto Rais ambaye amewahi kuwa PM au VP,imeonekana kama ndio kautaratibu wakubwa wamejiwekea.
Pia soma - CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025
Fredrick Sumaye alikuwa Waziri mkuu akiwa na miaka 45, alistaafu akiwa na miaka 55 mwaka 2005, kwa miaka 20 iliyopita anatapatapa tu anashika hiki kinakataa anashika hiki wapi, sababu alitoka madarakani akiwa kijana sana, na siasa ukizizoea kuacha ngumu, kwa rank aliyofikia ya kuwa PM huwezi kugombea Ubunge, ni kujishusha, japo Warioba aliwahi kujaribu hiyo akaishia kujidhalilisha. Sumaye ametapatapa sana, mara ajiunge upinzani, mara akasome degree Havard, degree yake imekuwa ni urembo tu haijasaidia taifa
Shamsi Vuai Nahodha alikuwa waziri kiongozi Zanzibar akiwa na miaka 38 mwaka 2000, aliachia mwaka 2010 akiwa na miaka 48, kijana kabisa, tangu muda huo hakuna cheo cha juu kinachomfaa, anaishi kiupweke sana.
Obama nae ni hivyo hivyo, alitoka madarakani akiwan na umri mdogo kabisa.
Raha ya hivi vyeo vya juu, uvipate ukiwa na miaka 55-60, ili ukiachia na nguvu zinakuwa zimeisha vinginevyo utapewa vyeo vya kuwa mkuu wa vyuo vikuu tu ili hali mwili na akili bado viko active
Dkt Nchimbi atatoka akiwa na 59, ni dhairi hawezi kuwa Rais wa Tanzania, siasa zilivyo tamu kurudi kijijini na miaka 59 ni mtihani
Tanzania haijawahi kuto Rais ambaye amewahi kuwa PM au VP,imeonekana kama ndio kautaratibu wakubwa wamejiwekea.
Pia soma - CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025
Fredrick Sumaye alikuwa Waziri mkuu akiwa na miaka 45, alistaafu akiwa na miaka 55 mwaka 2005, kwa miaka 20 iliyopita anatapatapa tu anashika hiki kinakataa anashika hiki wapi, sababu alitoka madarakani akiwa kijana sana, na siasa ukizizoea kuacha ngumu, kwa rank aliyofikia ya kuwa PM huwezi kugombea Ubunge, ni kujishusha, japo Warioba aliwahi kujaribu hiyo akaishia kujidhalilisha. Sumaye ametapatapa sana, mara ajiunge upinzani, mara akasome degree Havard, degree yake imekuwa ni urembo tu haijasaidia taifa
Shamsi Vuai Nahodha alikuwa waziri kiongozi Zanzibar akiwa na miaka 38 mwaka 2000, aliachia mwaka 2010 akiwa na miaka 48, kijana kabisa, tangu muda huo hakuna cheo cha juu kinachomfaa, anaishi kiupweke sana.
Obama nae ni hivyo hivyo, alitoka madarakani akiwan na umri mdogo kabisa.
Raha ya hivi vyeo vya juu, uvipate ukiwa na miaka 55-60, ili ukiachia na nguvu zinakuwa zimeisha vinginevyo utapewa vyeo vya kuwa mkuu wa vyuo vikuu tu ili hali mwili na akili bado viko active
Dkt Nchimbi atatoka akiwa na 59, ni dhairi hawezi kuwa Rais wa Tanzania, siasa zilivyo tamu kurudi kijijini na miaka 59 ni mtihani