Kuanzia mwaka 2030 Dkt. Nchimbi ataishi maisha ya kipweke angali kijana kama ilivyo kwa Obama, Sumaye na Vuai Nahodha

Kuanzia mwaka 2030 Dkt. Nchimbi ataishi maisha ya kipweke angali kijana kama ilivyo kwa Obama, Sumaye na Vuai Nahodha

Nasisitiza hiyo 1971 ni umri aliotutajia yeye. Cheti cha kuzaliwa hajatuonyesha.
Cheti kinaweza kuonesha alizaliwa mwaka huo lakini uhalisia inaweza kuwa tofauti.
Mfumo wetu wa kupata cheti Cha kuzaliwa unatoa mwanya kuongopa tarehe ya kuzaliwa. Hasa waliozaliwa 1980's kurudi nyuma.
 
Kutokuonesha cheti cha kuzaliwa haimaanishi kuwa hajazaliwa 1971.

This is a logical non sequitur fallacy.

Weka ushahidi kwamba hajazaliwa 1971.
Ushahidi ni cheti cha kuzaliwa, na cheti hajaonyesha. Hivyo hiyo 1971 ni tarehe aliyotuambia. Unakwama wapi mzee, wenzako wanagusa na kuachia, ww unashupaza shingo!
 
Ushahidi ni cheti cha kuzaliwa, na cheti hajaonyesha. Hivyo hiyo 1971 ni tarehe aliyotuambia. Unakwama wapi mzee, wenzako wanagusa na kuachia, ww unashupaza shingo!
Hata cheti cha kuzaliwa kwani hawezi kuchonga cha uongo akakuonesha kazaliwa 1971 wakati hajazaliwa 1971?

Na mtu asipokuwa na cheti cha kuzaliwa maana yake hawezi juwa kazaliwa 1971?

Mbona unakuwa mjinga hivyo?
 
Gusa achia mzee.
Umetoa madai ambayo huna ushahidi nayo.

Umekuwa kama Donald Trump aliposema Obama hakuzaliwa USA, kwa sababu hajaonesha cheti chake cha kuzaliwa.

Logical non sequitur fallacy.

Kama hajazaliwa 1971, kazaliwa mwaka gani?

Maana usije hapa kudai hajazaliwa kabisa pia.

Nchimbi kasoma Oysterbay Primary kuna watu wamesoma naye wanamjua kutoka shule ya msingi, tunaweza kuwaita hapa watuambie madarasa waliyosoma walisoma watu wa kuzaliwa miaka gani.
 
umepotosha gentleman,
miongoni mwa ma VP waliokua maraisi ni pamoja na Dr Alli Mohamed Shein, lakini pia Dr Samia Suluhu Hassan.

Ni muhimu kua makini unapotaka kupotosha wadau wa JF, japo maelezo mengine ni ya msingi na yana mantiki muhimu sana 🐒
Tunaongelea uRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Shein alikuwa Rais Zanzibar.
Kama Nagufuli asingekufa Samia asingekuwa Rais katu
 
Cheti kinaweza kuonesha alizaliwa mwaka huo lakini uhalisia inaweza kuwa tofauti.
Mfumo wetu wa kupata cheti Cha kuzaliwa unatoa mwanya kuongopa tarehe ya kuzaliwa. Hasa waliozaliwa 1980's kurudi nyuma.
Uko sahihi mimi nimepunguza miaka minne
 
Wengi tu wamepunguza.
Cheti cha kuzaliwa na NIDA vinaonesha umri huo uliopunguzwa.
Mimi nilikuwa smart Nida,Passport,keseni na cheti cha kuzaliwa viko sawa,siku nikifa historia fupi ya marehenu sijui itakuwaje.watasoma umri fake au halisi?watajijua kwanza ntakuwa sisikii
 
Nchimbi atakuwa Rais.Nchimbi akiumua jambo huwa hashindwi labda afe.Si unaona 2015 kambi yao ilikatwa ila si unaona alivyorudi.This time hatofanya makosa.
Na wote walikatwa akina sophia simba ila yeye akawa barozi. Jamaa kweli hapotei
 
umepotosha gentleman,
miongoni mwa ma VP waliokua maraisi ni pamoja na Dr Alli Mohamed Shein, lakini pia Dr Samia Suluhu Hassan.

Ni muhimu kua makini unapotaka kupotosha wadau wa JF, japo maelezo mengine ni ya msingi na yana mantiki muhimu sana 🐒
Dr Ali Mohamed Shein alikua Rais wa wapi? Yani kiongozi wa Mkoa anaitwa Rais ? Anyway tukubaliane Alikua Rais mbona tukisena Zanzibar ni nchi mnataka kutufunga?
 
Hii ni problem of induction logical fallacy.

Unasema Tanzania haijawahi jutoa rais ambaye amewahi kuwa PM au VP wakati rais wa sasa aliwahi kuwa VP.

Na kwa nini unafikiri kuwa kama Tanzania haijawahi juwa na rais aliyekuwa PM, basi itakuwa hivyo siku zote?

Mbona Tanzania ilikuwa haijawahi kuwa na rais mwanamke na sasa hivi imekuwa na rais mwanamke?

Kila kitu kina mwanzo.

Umeweka induction logical fallacy kwamba kama kwenye nyumba yako glasi haijawahi kuvunjika, basi haiwezi kuvunjika. That is wrong logic.
Hivi Kiranga wewe chuo kikuu ulisomea taaluma gani ? Japo unaonekana huwa unapenda kusoma vitabu hata vilivyo nje ya taaluma yako.

Ningependa kujua haya mambo ya logical fallacy au logical non sequitur yako katika taaluma gani !!!
 
kwa watawala wa afrika vyeo si kwa ajili ya kuwatumikia wananchi ila ni ulaji tu..kwa ishu yako mtoa mada na kwa sheria zetu za mafao ya viongozi hata akishika cheo kwa mwaka tu inamtosha vizuri tu sababu ataendelea kulipwa vile vile yaani 80% ya mshahara wa aliye madarakani na mkewe akilipwa 60 % wa aliye madarakani kwahiyo mke na mume wanalamba jumla 140 % ya mshahara na marupurupu sawa au pungufu kidogo na aliye kwenye madaraka ofisini..so mleta thread hawa jamaa hawana upweke wala dhiki yoyote kwani lengo lao la kuvuna vinono limetimia
 
Kwani watu wote waliozaliwa 1971 wana vyeti vya kuzaliwa?

Wewe umetoa madai, wewe ndiye mwenye wajibu wa kutoa ushahidi wa kuthibitisha hayo madai.

Thibitisha hajazaliwa 1971.

Ulitakiwa kuja hapa kuonesha hiki hapa cheti cha kuzaliwa.

Ulitakiwa kuja hapa kutupa ushahidi kwamba hakuzaliwa 1971.

Hujafanya hilo. Unatuonesha kuwa wewe mwenyewe huna ushahidi, unamtaka Nchimbi atie ushahidi.

Weka ushahidi wa kutetea tuhuma yako.
Umetema madini matupu.
Aoneshe ushahidi kama Gwajiboy alivyokuja na vyeti vya Bashite kututhibitishia.
 
Back
Top Bottom