Kuanzisha Shule ya Msingi na Sekondari: Utaratibu wa Kiserikali, Ushauri, Changamoto na Faida

Kuanzisha Shule ya Msingi na Sekondari: Utaratibu wa Kiserikali, Ushauri, Changamoto na Faida

Pia epuka ku share na mtu usiemjua, licha ya kukupiga ulichonacho kuna hatari ya kutofautiana kimaamuzi ktk kuiongoza na kuisimamia shule mliyoanzisha
 
Kaka, kwanini usifungue english m. school, kwani sekondari kwa sasa hazilipi kutokana na utitili wa shule za kata, ila kwa uhitaji wa sasa ni hiyo english medium school. huo nimtazamo wangu na kutokana na uzoefu wangu wa kufundisha.
 
Nawaomba ndugu zangu SAYAYA, NAPENDA na HITLER, kabla ya ku-comment maoni yenu nitangulize shukurani zangu kwenu kwa kunipa moyo/maoni mazuri ya kufanya haya mambo ya ujenzi wa shule yangu. Asanteni sana na mungu awabariki katika kazi zenu mnazofanya.

Kwa ujumla naendelea vizuri na heka heka za ujenzi wa mradi wangu huu. Isipokuwa watu wa wilayani ndio changamoto ya sasa hivi inayonisumbua kwani zile ramani lazima wazipitishe wao ndio ujenzi uendelee vinginevyo mtu unaweza ukajianzia tu kujenga lakini athari yake wanapokuja kukagua watatoa madai mengi ya kukosewa either ramani au hata ujenzi wenyewe, kwa hiyo navuta subira vibali vyote vitick ndio nianze rasmi ujenzi.

Kingine ni mwanJF amenishauri kwamba nipange/nifungue English medium, ni sawa lakini kuna changamoto moja ya 'INITIAL COST' ni kubwa katika shule za msingi ukilinganisha na sekondary. Kwa mfano, sekondary unaweza kuanza na wanafunzi wa kujitegemea kwa madarasa ya QT,FIII na FIV (Tuition) kwanza kabla ya wale wa kawaida (school). Hii ndiyo inayopelekea niegemee zaidi kupanga nifungue sekondari. Kwa shule za msingi, kwanza inahitajika madarasa na walimu wengi kidogo kwa hiyo mtaji mkubwa. Pia watoto wa msingi ni delicate kulinganisha na sekondari.

Suala jingine la ku-share ni zuri, ila tangu naanza kuwa na hii ndoto nilipania na kumuomba mungu kwamba nijitahidi kufungua shule itakayo kuwa ya familia yangu. Ndio maana hata ninavyoendelea najikongoja sana katika kufanikisha huu mradi.

Vinginevyo wanaJF nawatakia kila la heri katika kazi zenu, na nitaendelea kuwaletea maendeleo ya kinachoendelea, mungu awabariki sana.
 
Hongera kwa uthubutu. Nakushauri uanze tu kama kituo cha mitihani ya Necta kwa private candidates kwa sababu hiyo 8m haitoshi kabisa. Shule sio kufundisha tu ina mambo mengi sana. Jipe muda jipange. 8m haitoshi. Anza na hao PC
 
Asante diranqhe. Nitajitahidi, ila umesema shule ina mambo mengi, yapi hayo? Ukitoa gharama za uendeshaji (yaani mishahara ya walimu na walinzi max. 3)
 
Asante diranqhe. Nitajitahidi, ila umesema shule ina mambo mengi, yapi hayo? Ukitoa gharama za uendeshaji (yaani mishahara ya walimu na walinzi max. 3)

Nina ndoto kama zako za kuanzisha shule, nimejitahidi kutembelea shule nyingi za binafsi, mashirika ya dini, ngo,na za serikali. Kote huko nilikuwa/ninaendelea kuokoteza vionjo mbalimbali ili nikifika ktk implementation ya ndoto zangu nisilazimike kutoa rushwa au kuingia gharama kubwa kwa mambo yanayoepukika mapema.

Anza na chekechea kwenye hicho kiwanja chako. Ila usijenge shule ktk kiwanja hicho, ni kidogo mno. Chekechea pia inataka vibali na usajiri. Ukipata usajiri wa chekechea, unatumia kibali cha chekechea kuombea shule yako ya msingi na baadae sekondari. Kuna raha kubwa kuwa na wanafunzi unaowajua vizuri tangu wakiwa wadogo. Baadae unaomba A level na hatimaye chuo kikuu au chuo cha kati.

Hiyo pesa, nenda nje ya mji, tafuta eneo kubwa kabisa zuri, liombee kwa Mungu wako. Anza kujenga shule yako hapo kwa kuanza na mazingira kama huna hela, wakati ktk kiwanja chako cha sasa kuna kituo cha chekechea. Utakapoulizwa maabara, utajenga wapi, utakapotakiwa kuwa na uwanja wa michezo utaweka wapi, nyumba ya matron/patron utajenga wapi, vyoo vyako utajenga wapi,arena itakaa wapi. Je, hati ya kiwanja unayo?

Muda ni mchache, ningechangia mengi.

Usiache kutimiza ndoto yako,maana yatoka kwa Mungu.
 
Asante sana MALILA;

Kwa ujumla nilishapata kama heka 6 nje kidogo ya pale niliponunua heka 1. Kwenye heka moja ni kijijini kabisa ambapo watoto watakuja na kurudi nyumbani kwa miguu (kwa kuanzia).Ninachotakiwa sasa ni kujenga darasa moja ambalo litakuwa multi-purpose kwa chekechea, msingi au hata secondary.

Sina uhakika kama hii 8m itatosha kwa darasa hili,maana ninayo kamili. Ninatakiwa kupiga mahesabu kabla ya kuanza ujenzi naogopa kuishia katikati,natamani dara likamilike chekechea ya watoto 70 ianze. Halafu nianze kujipanga kuongeza darasa jingine.
 
Kwa wenye ndoto za kuwa na shule. Please anzia hapa. Sio lazima uanze kujenga shule na kujitanagaza unajenga shule. Jenga vyumba viwili vya ukubwa wa madarasa andikisha watoto wa nursery school waanze kusoma.Then fuatilia usajili wa nursery school ambao hauchukui mda mrefu. Then kupitia hao watoto wa nursery utapata uzoef wa kuendesha shule for one to two years.

Ndani ya hiyo miaka weka tuition ya jioni ya wanafunzi wa msingi na secondari kuendeleza kipato na kukuza kituo.Maana kwa mda huo itakuwq nursery na tuition center. Ukishajipanga ndo uanze kufuatilia taratibu za usajili ujitahidi kiwafuata right people kuwauliza taratibu za usajili. Hasa hawa wanaomiliki shule watakusaidia. Ukipata majibu ya kukatisha tamaa kwa mmoja jaribu kwingine.Hii ni kwa eng medium pri and primary school.

Mimi nasimamia shule amabayo boss wangu alianza hivyo na sasa hivi ndo tupo kwenye hatua za mwesho za uasajili ila tuna hadi darasa la pili wanasomea kule nursery. Cha msingi ni elimu bora ambayo itamfanya mzazi akutangazie shule.

Kwa secondary sina uzoef sana japo tuna mpango wa kujenga. Kama kipato chako ni cha chini anziaha tuition Centre ambayo haihitaji hata kuwa na kabali cha kuendesha. Naomba niishie hapa kwa hiki kidogo mnaotaka kuanzisha shule mtajifuza kitu.
 
Kwa wenye ndoto za kuwa na shule. Please anzia hapa. Sio lazima uanze kujenga shule na kujitanagaza unajenga shule. Jenga vyumba viwili vya ukubwa wa madarasa andikisha watoto wa nursery school waanze kusoma.Then fuatilia usajili wa nursery school ambao hauchukui mda mrefu. Then kupitia hao watoto wa nursery utapata uzoef wa kuendesha shule for one to two years.

Ndani ya hiyo miaka weka tuition ya jioni ya wanafunzi wa msingi na secondari kuendeleza kipato na kukuza kituo.Maana kwa mda huo itakuwq nursery na tuition center. Ukishajipanga ndo uanze kufuatilia taratibu za usajili ujitahidi kiwafuata right people kuwauliza taratibu za usajili. Hasa hawa wanaomiliki shule watakusaidia. Ukipata majibu ya kukatisha tamaa kwa mmoja jaribu kwingine.Hii ni kwa eng medium pri and primary school.

Mimi nasimamia shule amabayo boss wangu alianza hivyo na sasa hivi ndo tupo kwenye hatua za mwesho za uasajili ila tuna hadi darasa la pili wanasomea kule nursery. Cha msingi ni elimu bora ambayo itamfanya mzazi akutangazie shule.

Kwa secondary sina uzoef sana japo tuna mpango wa kujenga. Kama kipato chako ni cha chini anziaha tuition Centre ambayo haihitaji hata kuwa na kabali cha kuendesha. Naomba niishie hapa kwa hiki kidogo mnaotaka kuanzisha shule mtajifuza kitu.




Thanks Quote Reply

Select for moderation Edit History Ban
Wewe umemaliza kitu.. asipofuata huu ushauri atakuwa na lake jambo. 8m ni kidogo sana kwa shule ya sekondari. Kama angekuwa na angalau 100m ningesema asonge mbele.
 
Asante sana MALILA;
Kwa ujumla nilishapata kama heka 6 nje kidogo ya pale niliponunua heka 1. Kwenye heka moja ni kijijini kabisa ambapo watoto watakuja na kurudi nyumbani kwa miguu (kwa kuanzia).Ninachotakiwa sasa ni kujenga darasa moja ambalo litakuwa multi-purpose kwa chekechea, msingi au hata secondary. Sina uhakika kama hii 8m itatosha kwa darasa hili,maana ninayo kamili. Ninatakiwa kupiga mahesabu kabla ya kuanza ujenzi naogopa kuishia katikati,natamani dara likamilike chekechea ya watoto 70 ianze. Halafu nianze kujipanga kuongeza darasa jingine.

Ungeweza kusema exactly location ulipo ingesaidia kukupa idea zingine za ujenzi...
 
Ungeweza kusema exactly location ulipo ingesaidia kukupa idea zingine za ujenzi...

Eneo lipo Misugusugu-Kibaha kijijini kabisa ambapo pana watu wa kutosha na nilivyo wachunguza wana pata shida ya kuwapeleka mbali watoto wao kupata elimu ya chekechea.
 
Nina ndoto kama zako za kuanzisha shule,nimejitahidi kutembelea shule nyingi za binafsi, mashirika ya dini, ngo,na za serikali. Kote huko nilikuwa/ninaendelea kuokoteza vionjo mbali mbali ili nikifika ktk implementation ya ndoto zangu nisilazimike kutoa rushwa au kuingia gharama kubwa kwa mambo yanayoepukika mapema.

Anza na chekechea kwenye hicho kiwanja chako. Ila usijenge shule ktk kiwanja hicho, ni kidogo mno. Chekechea pia inataka vibali na usajiri. Ukipata usajiri wa chekechea, unatumia kibali cha chekechea kuombea shule yako ya msingi na baadae sekondari. Kuna raha kubwa kuwa na wanafunzi unaowajua vizuri tangu wakiwa wadogo. Baadae unaomba A level na hatimaye chuo kikuu au chuo cha kati.

Hiyo pesa, nenda nje ya mji, tafuta eneo kubwa kabisa zuri, liombee kwa Mungu wako. Anza kujenga shule yako hapo kwa kuanza na mazingira kama huna hela, wakati ktk kiwanja chako cha sasa kuna kituo cha chekechea. Utakapoulizwa maabara, utajenga wapi, utakapotakiwa kuwa na uwanja wa michezo utaweka wapi, nyumba ya matron/patron utajenga wapi, vyoo vyako utajenga wapi,arena itakaa wapi.Je hati ya kiwanja unayo?

Muda ni mchache, ningechangia mengi.

Usiache kutimiza ndoto yako,maana yatoka kwa Mungu.

Mkuu nafikiri masharti ya kufungua shule ni lazima uwe na EKA 10 na yenye hati yaani title deed
 
Kuwa na eneo kubwa ni vizuri.

Ni kweli eneo kubwa linafaa, lakini kwa kuanzia heka 1.5 inatosha kwa chekechea na Tuition. Mambo yakiwa mazuri nitahamia ktk eneo jingine ambalo liko nje kabisa ya kijiji(bado pako pori) ambapo nina heka za kutosha tu.
 
Wakuu nimedunduliza dunduliza mpaka nilipofikia nina kamtaji kidogo sasa nataka nifungue shule ya sekondari.

Kwa yeyote anayefahamu anipe dondoo muhimu kuhusu hii biashara, mchanganuo kiujumla kuhusu taratibu za usajili, namna ya kupata faida kupitia biashara hii nk.
 
Mkuu hiyo pesa mbona ndogo snaa bado. .
hujanunua kiwanja. .
Ujenzi bado hapo
Vitabuu , walimu ..
badoo sana. .
 
Mkuu hiyo pesa mbona ndogo snaa bado. .
hujanunua kiwanja. .
Ujenzi bado hapo
Vitabuu , walimu ..
badoo sana. .
Nina eneo kubwa lipo msanga

Vitu vingine hivyo ndio bado.

Ila niikuwa nataka nianze hata na madarasa manne.
 
Kwanini usijenge gest mtu wangu watu wawe wanabinayana utapiga hela sana mkuu jenga gest
 
Back
Top Bottom