Kubali au kataa lakini page ya Mange Kimambi ya instagram ndio talk of the town kwa sasa

Kubali au kataa lakini page ya Mange Kimambi ya instagram ndio talk of the town kwa sasa

Matusi mazito kwa rais had itv
Sio rais tu; yaani ye yeyote yule ili mradi hakubaliani nae! Mie ingawaje sio CCM na wala sina mahaba na chama chenyewe katu siwezi kumwagia mtu matusi eti kisa amehamia CCM! Alivyo mtu wa ajabu, anachofanya yeye ndicho sahii zaidi! Miaka miwili iliyopita alikuwa CCM na kazi yake kubwa ilikuwa kutukana upinzani na kuwashabikia CCM!
 
Hiyo kitu ipo dunia ipi? Sijawahi nenda nje ya JF tangu nijiunge. Kabla ya hapo ni BBC, CNN na SKY news.
 
Mwanaume ambaye ana app ya Instagram sijui huwa namuonaje!It's more girlishly hiyo app
Sio kosa lako ni kipaji cha ushamba ulionacho, kwa vile hujui hata kutumia hiyo insta baki hivyohivyo. Ukiwa insta inategemeana unamfollow nani ndio umbea unapoanzia. Kama sie wapenzi wa mpira ni sehemu bora kupata update mbali mbali na siasa Mange yuko vizuri kutujuza yanayojiri kuliko hata jf humu kuna mengine hayaruhusiwi siku hizi.
 
Sio rais tu; yaani ye yeyote yule ili mradi hakubaliani nae! Mie ingawaje sio CCM na wala sina mahaba na chama chenyewe katu siwezi kumwagia mtu matusi eti kisa amehamia CCM! Alivyo mtu wa ajabu, anachofanya yeye ndicho sahii zaidi! Miaka miwili iliyopita alikuwa CCM na kazi yake kubwa ilikuwa kutukana upinzani na kuwashabikia CCM!
Nashangaa upinzani wanao msupport. Alimtukana lowasa na upinzani mpaka basi.
Leo hii wanampigia vigelegele
 
Nashangaa upinzani wanao msupport. Alimtukana lowasa na upinzani mpaka basi.
Leo hii wanampigia vigelegele
Alimkosea adabu sana mzee wa watu! And it's a matter of time ipo cku atawageukia wao wenyewe manake akili zake zinamtosha peke yake.
 
Alimkosea adabu sana mzee wa watu! And it's a matter of time ipo cku atawageukia wao wenyewe manake akili zake zinamtosha peke yake.
Mwezi mchanga yule. Anajiona Google wakati Google nayo kuna muda inashindwa kutambua neno
 
Mwezi mchanga yule. Anajiona Google wakati Google nayo kuna muda inashindwa kutambua neno
Ndo vile tena wafuasi wake ni kama wafuasi wa kanisa na msikiti! Hakuna kuhoji... ni kupiga makofi tu kila atakachosema! Kama hukipendi; kaa kimya!

Kwa akina sie ambao huwa tunahoji hadi Maandiko; ni ngumu kweli kweli kuwa Followers wake!
 
Salaaam wanajamvi.

Kwa wale watumiaji wenzangu wa mtandao wa kijamii wa instagram wengi wenu mtakuwa mmemfollow mwanadada machachari anaeweza kuikosoa serikali bila woga:- Mange Kimambi. Imefikia mahali sasa watumiaji wa insta wengi niliongea nao wanasema wakilog in wanaingia kusoma posts za mange kimambi tu kisha wanalog out. Yaani kiufupi page ya huyu mwanadada aishie marekani inatembelewa mara nyingi sana. I presume inaweza ikawa most visited page kutoka audience/followers wa kitanzania.
Mange amekuwa akijikita sana kutetea wananchi, kukosoa serikali, kuwachamba wabaya wake wanaomchokoza, kupigania freedom of speech n.k.

Swali: Je haujawahi kuingia instagram na moja kwa moja ukasearch page ya huyu dada na uliposoma posts zake ukaridhika then ukalog out? Admit it .....
Mm nimmoja wao mkuu siwezi pitisha siku bila kusoma post za mange
 
Kwa kweli najisikia aibu kuingia page za mastaa uchwara wa bongo,lakini kwa Mange nilishindwa kujizuia.

Masha pamoja na uanasheria wake anamtumia Mange issue za kupost
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji3] [emoji23] [emoji23] umejuaje mkuu??
 
Mwanaume ambaye ana app ya Instagram sijui huwa namuonaje!It's more girlishly hiyo app
Kwakweli I declare kuwa hata Mimi huwa ninaona walakini kwa dume kuwa insta
 
Naamini sote Tumeanza Mwezi Wa December wenye shamrashamshara za kipekee, nikiwa bado niko Arusha nikimalizia kazi, nimeona nirudi tena kwenu kwa salamu za December.

Kwanza nataka CHADEMA na Afisa Habari wenu mnayemheshimu Mange Kimambi mtambue kuwa watoto 1,300 wa Kibiti mnaotangaza kuwa wamepotea na kutaka kuwaaminisha Watanzania kuwa wamekufa sio kweli, Kamanda Simon Sirro anasema alitajiwa idadi hiyo kuwa ni ya watoto watoro wa shule (Absentees).

Na kwa kuwa Afisa Habari wenu anayetumiwa na Wazungu kuivuruga Tanzania na nyie kwa Unyumbu wenu mnamtukuza hajui tatizo la utoro Tanzania basi mmedandia hoja na kuanza kushutumu kuwa wameuawa na Serikali imenyamazisha vyombo vya habari visiripoti .

CHADEMA mchukueni Mange Kimambi wenu mpelekeni wilaya zote za Tanzania akajionee tatizo la utoro.

Mwambie Afisa Habari wenu anayefanya kazi kutokea Marekani kuwa kuna wilaya za Tanzania utoro umefikia hadi wanafunzi 7,000 .

Mwambieni wanaoripotiwa kuwa watoro wengine wamehama shule bila kutoa taarifa shuleni ama mamlaka za Serikali.

Mwambie wengine wanaolewa na kutoroka shule, mwambieni wengine wanaacha kusoma na kwenda kwenye uzalishaji mali na familia .

Na hii sio mara ya kwanza, ilikuwa inaokotwa miili ufukwe wa bahari Dar es Salaam. Afisa Habari wa CHADEMA Mange Kimambi akaanza kutangaza wananchi wanaua, na Viongozi wakuu wa CHADEMA wakadandia lakini mpaka leo hawajaonesha ni ndugu wa nani waliuawa kwa idadi ile.

Nataka kuwatahadharisha Watanzania dhidi ya uchochezi unaofanywa na Mange Kimambi.

Wazungu ni wataalamu sana wa kutengeneza akina Mange Kimambi ili waivuruge nchi. Wanatumia mitandao ya kijamii hivi hivi na wanashabikiwa na wananchi.

Tunayoyaona leo Libya yalianza hivi, Wazungu waliwatumia akina Mange Kimambi wakagombanisha watu na Serikali, wakawatengeneza vijana ili wamuue Ghadafi na walifanikiwa wakamuua Ghadafi.

Leo Libya imevurugika, haikaliki na wananchi wa Libya wamekuwa watumwa wanauzwa kama bidhaa. Wanadhalilishwa, na wanauawa kama kuku, Libya neema haipo tena. Libya imekuwa jehanamu .

Ni hayahaya yalifanyika Syria leo Syria ni balaa. Ni hayahaya yalifanyika Iraq. Yanayotokea Iraq wote tunayaona.

Najua Watanzania wanaakili timamu na wanauwezo wa kutambua upuuzi wa CHADEMA na Mange Kimambi wao ambaye baada ya Watanzania kuwaadhibu kwenye kura za udiwani juzi amejaribu kuhamasisha watu waanze kupambana na Serikali eti wameibiwa kura lakini amekwama.

Mimi naomba Watanzania tukiangalie Chama cha CHADEMA . Tuwaangalie viongozi wake, tuwapime wanaitakia nini nchi hii. Hivi chama Serious kinaweza kufika mahali kinamtukuza mgonjwa wa akili kama Mange Kimambi? Yaani Mwenyekiti Freeman Mbowe anamtaja kabisa kwenye hotuba yake na kumshukuru Mange Kimambi? Anayoyaposti Mange Kimambi yanafaa kwenye nchi ya wastaarabu kama Tanzania? Halafu ndio hawa wanataka wapewe nchi.

Tuonane Machame this Xmass .

Ngariba Mkuu
Arusha, Tanzania
01/12/2017
 
Kwa uandishi huu hata uteuzi wa uafisa mtendaji wa kijiji hupati.
Alafu watetea ujinga siku hizi mmepewa kisogo kwenye teuzi hadi pale wapinzani tuliowanunua wapate nyadhifa.
Wakati mwingine ukirudi hapa uje na takwimu sio kupiga kelele. Umeongelea suala la utoro, ni vyema ungetupa DATA kidogo za rate na trend ya utoro ya huko Kibiti.
 
Back
Top Bottom