Kubeba majeruhi kwenye gari za wazi (Pickup) badala ya gari za wagonjwa (ambulance) kwenye tukio la kuanguka ghorofa K/Koo ni sahihi?

Kwani wakikwambia Jehanamu unahisi ni wapi?.
Watanzania tunaishi Jehanamu, hatuishi kwenye nchi inayojali watu wake.
Tupo kwenye nchi ya Mazombi...
Kwani watanzania hata kuishi wanaishi sasa?

Hiyo nchi iko corrupted,ni rushwa kila sehemu.

Mambo ya aibu sana.
 
Lengo ni kuokoa uhai wa binadamu hizo ambulance kama zimechelewa haisababishi majeruhi kuchelewa hospitali.

Hata mjamzito anaweza kujifungulia kwenye gari wakati anawahi labour.

Acha siaasa na kuona kila kitu ni kosa.
 
Ambulance zilikuwepo, nimeziona nyingi tu, it's just Ambulance moja inapakia magonjwa mmoja, ili upakie Maiti na majeruhi zaidi ya 40 unahitaji ambulance zaidi ya 40, kuliko ukae tusubirie Ambulance ije iondoke irudi unajiongeza.

Mfano hii

View: https://www.instagram.com/eastafricaradio/reel/DCboojVpfVF/
 
Kuna mganga mkuu, mkuu wa wilaya , mkurugenzi, mkuu wa Mkoa halafu eti dereva akatae kutoa ambulance ? Sasa hiyo ni nchi au Utopolo. Haiwezekani dereva kuwa na hayo mamlaka. Lawama zote Kwa viongozi.
Hao uliwataja sio madereva wa ambulance, madereva wa ambulance zile gari wamepewa zao wao ndio wanaamua wabebe mgonjwa gani kumpeleka wapi kwa hio hawajaamua kwenda kubeba wagonjwa hapo
 
Uhuni
 
Hao mnawaita viongozi ni wanyama hasa....dunia haina huruma..
 
Kama mkuu wao aliyewateua anaruhusu hivyo vyombo vya Usalama kuteka na kuua raia unahisi atawajali wakiangukiwa na ghorofa?
 
Hakuna kitu KIBAYA Mkuu kama Tabia inayoshamiri ya kukatisha tamaa kila Jambo jema. Watu wameshinda Kariakoo wakifanya uokoaji toka Asubuhi. Ndugu yangu hujaona mazingira halisi, hujashiriki kusaidia, ajabu unakosoa kilichotumika kuwawahisha Hospitali. Kama hakukuwa na Ambulance karibu, wangeachwa pembeni wapoteze maisha eti kwasababu inasubiriwa ambulance? Au Prof Janabi baada ya kufika angeagiza zoezi lisitishwe mpaka ambulance zifike? Mbona wapo majeruhi ambao nimeshuhudia wakipakiwa kwny Ambulance kueahishwa Hospitali na sio wote wamepakiwa kwny Pick up. Hivi unajua NEGATIVITY ni Ugonjwa?
 
Ishu ya majeruhi hata kama kuna baiskeli unapakiza.
Bongo yenyewe hii uanze kukaa ufuatize ambulance hivi si unatafuta uokote maiti badala ya majeruhi!?
 
Ni sahihi kabisa. Kama sisi raia tumelala na tunashangalia fedha za magoli ya mpira basi ni haki tuvune tulichopanda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…