Kuchapwa watoto kiasi hiki ni sawa?

Kuchapwa watoto kiasi hiki ni sawa?

MUFTI MKUU amelaani kitendo hicho cha kikatili, your mental faculties need to be examined by Psychologists
Sasa Muft si kasema ili isionekane anaunga mkono, lakini hamna kichapo hapo ni jambo limekuzwa tu
 
Huo ni utumwa au ni mbinu zilizotumiwa na watawala yaani wakoloni kumazimisha watu waishi vile watavyo wao.
Muhimu na la msingi, ni kufuatilia kila nyendo ya mtoto na kumpangia ratiba yenye kumjenga. Ukimuacha mtoto ajilee au alelewe na ulimwengu, utapiga uue
Yes Exactly. Wanasemaga Unakuwa benet na mwanao na hata kwenye kumrudi ww ndo utajua kiwango kitakachokuwa ni Fair(size yake) kwake.
 
Uzi umeibua hoja mchanganyiko, zenye hisia, ila ni muhimu kufahamu kuwa Kuna Sheria zinasimamia mambo ya utoaji wa adhabu, Kuna mdau huko juu alishazigusia, Sheria ya Kanuni za Adhabu (Penal Code), Sheria ya Mtoto (Law of the Child Act) na zingine..
Pamoja na hisia zote, tunapaswa kucheza humo kwenye Sheria,
Adhabu haikatazwi popote pale, ila iwe inawiana na uwezo wa mtoto kuhimili, na pia isitoke nje ya lengo la adhabu, ambalo ni...kurekebisha tabia.
Kama adhabu Iko nje ya uwezo wa kuhimili, hayo ni mateso, ambayo humletea madhara muhanga, ikiwemo ya kimwili na kisaikolojia, (unatibu tatizo A unafungua matatizo B na C ambayo hayatatibiwa) wapo waliopoteza maisha kutokana na adhabu kutozingatia uwezo wa kuhimili, wako watoto wamepata Ulemavu, wapo watoto wamechomwa moto mikono, na mambo mengine ambayo ukiyaangalia unabaini hayakuwa na lengo la kurekebisha tabia, bali kuondoa hasira za mzazi/mlezi/mtoa adhabu, au kulipiza kisasi kwa mtoa adhabu, kwa vile naye alipita kwenye mateso kama hayo (vicious circle of violence) na ambae mara nyingi huja kujutia baadae.. kama huyu mwalimu.
kwa kulinda afya ya muadabiwa na muadabishaji, ni vyema kuwe na kiasi kwenye kila tunalofanya, kinyume na hapo ndo kama haya yanatokea, Sheria zipo na Kuna watu zimewaharibia maisha.
Kila jambo huwa ni la kawaida, na unaweza kuwa na mifano mingi ya jambo kama hilo kufanyika pasipo kuleta madhara, lakini siku madhara yakitokea kwako..ni wewe against The Law
 
Sasa Muft si kasema ili isionekane anaunga mkono, lakini hamna kichapo hapo ni jambo limekuzwa tu
Hilo ni dhahiri na limefanyika kwa nia ovu kabisa:
1. Kufitinisha Imani ya watu (Waislam) na Serikali yao kuanzia Ngazi ya Mtaa/kitongoji au Shehia hadi kwa Mufti ; Polisi hadi kwa Waziri. Tukumbuke "Mdomo uliiponza shingo"
2. Kuzua Taharuki baina ya kituo cha mafunzo (Madrasa) na Jamii inayokizunguka e.g. Msikiti, Mtaa n.k.
3. Kuamsha hisia za chuki dhidi ya mwl. na Jamii ya mahali hapo ikiwa ni pamoja na wazazi wa mtoto aliyeadhibiwa.
4. Kuchochea kuwepo kwa mtafaruku ndani ya Uongozi wa Kituo hicho i.e. waalimu na mwl. Kiongozi, wanafunzi na waalimu wao na baina ya wanafunzi wao kwa wao......Kwa mantiki hiyo tusishangae baadaye tukasikia watoto wanagomea adhabu, watoto wanawapiga mawe waalimu wao n.k. na kero nyinginezo
 
Uzi umeibua hoja mchanganyiko, zenye hisia, ila ni muhimu kufahamu kuwa Kuna Sheria zinasimamia mambo ya utoaji wa adhabu, Kuna mdau huko juu alishazigusia, Sheria ya Kanuni za Adhabu (Penal Code), Sheria ya Mtoto (Law of the Child Act) na zingine..
Pamoja na hisia zote, tunapaswa kucheza humo kwenye Sheria,
Adhabu haikatazwi popote pale, ila iwe inawiana na uwezo wa mtoto kuhimili, na pia isitoke nje ya lengo la adhabu, ambalo ni...kurekebisha tabia.
Kama adhabu Iko nje ya uwezo wa kuhimili, hayo ni mateso, ambayo humletea madhara muhanga, ikiwemo ya kimwili na kisaikolojia, (unatibu tatizo A unafungua matatizo B na C ambayo hayatatibiwa) wapo waliopoteza maisha kutokana na adhabu kutozingatia uwezo wa kuhimili, wako watoto wamepata Ulemavu, wapo watoto wamechomwa moto mikono, na mambo mengine ambayo ukiyaangalia unabaini hayakuwa na lengo la kurekebisha tabia, bali kuondoa hasira za mzazi/mlezi/mtoa adhabu, au kulipiza kisasi kwa mtoa adhabu, kwa vile naye alipita kwenye mateso kama hayo (vicious circle of violence) na ambae mara nyingi huja kujutia baadae.. kama huyu mwalimu.
kwa kulinda afya ya muadabiwa na muadabishaji, ni vyema kuwe na kiasi kwenye kila tunalofanya, kinyume na hapo ndo kama haya yanatokea, Sheria zipo na Kuna watu zimewaharibia maisha.
Kila jambo huwa ni la kawaida, na unaweza kuwa na mifano mingi ya jambo kama hilo kufanyika pasipo kuleta madhara, lakini siku madhara yakitokea kwako..ni wewe against The Law
Adhabu haikatazwi popote pale ila iwe inawiana na uwezo wa kuhimili na isitoke nje ya lengo la adhabu.:BanHammer::BanHammer::HYPERCLAPHD:
 
Nimeshindwa hata kuelezea, naomba kufahamu kama ni sawa jaman,. Kuna mtoto mdogo hapo nimemuonea huruma sana.

Lakini serikal imekataza kuchapa watoto wawapo mashule, sasa swali, hapo ni wanaruhusiwa kuchapwa namna hiyo? Hakuna adhabu nyingine kwani ya kuwafanya wasirudie kosa?

Nawasilisha.
Cc: Doroth Gwajima

Pia soma
- Mwalimu wa Madrasa apandishwa Kizimbani kwa tuhuma za kuwachapa fimbo (Ukatili) wanafunzi wa madrasa

View attachment 3242079Hakuna watu waliopotea njia kama waislam
 
Ila mbona sie tukiwa primary na sekondari tumechapwa sana, hapo ni cha mtoto.
Mnataka kuniambia kwamba siku hizi hakuna shule inayochapa viboko?
Miaka ya 90's na 2000's mwanzoni kulikuwa na fimbo za hatari. Sitaki kukumbuka
 
Sasa acha kurefer kwamba eti sijui kitabu cha dini kilisema hivi ama vile, hivyo vitabu vimeandikwa kwa maslahi ya walioviandika..
Ila cha ajabu (out of point) Mawaziri wetu na Makatibu wakuu(Watunga Sera Tz) hawapeleki bungeni Muswada wa kuboresha mafao ya kustaafu kana kwamba wao hawatokaa wastaafu.
 
Miaka ya 90's na 2000's mwanzoni kulikuwa na fimbo za hatari. Sitaki kukumbuka
Tumechapwa sana bakora aisee na ilikuwa ni jambo la lawaida hata nyumbani huendi kusema. Na nyumbani penyewe mama kanitandika sana bakora. Kila unapoenda ni mwendo wa bakora tu kasoro kanisani.
Sasa nashangaa huyo ustaadhi kuwaadhibu watoto kwenye shule ya dini.
 
Tumechapwa sana bakora aisee na ilikuwa ni jambo la lawaida hata nyumbani huendi kusema. Na nyumbani penyewe mama kanitandika sana bakora. Kila unapoenda ni mwendo wa bakora tu kasoro kanisani.
Sasa nashangaa huyo ustaadhi kuwaadhibu watoto kwenye shule ya dini.
Kizazi kibabadirika kila baada ya "miongo" kadhaa ndo maana shule za leo mpaka hesabu wanaletewa multiple choices.
 
Hayo maadili mbona pia yanavuniwa na watu wazima wa kale kabisa. Kwani umefanya uchambuzi wa wavunja maadili ukaona huko hawako watu wa kale? Mbona kibao
Kipigo alichotoa sio sahihi lakini jamii yenyewe ndio mfumo wake wa maisha , ulishawahi kushuhudia askari polisi wakijaribu kuzuia maandamano tena mengine ya amani? Jamii zetu wa Afrika zimejengeka kwenye mifumo ya matendo maovu yanazuiwa kwa adhabu kali kuanzia ngazi ya familia mpaka mifumo ya serikali ndio maana baadhi ya wazazi wanajaribu kumfundisha kwa mfumo huohuo mtoto kwamba kuna vitu ukifanya utakutana na madhara makubwa kwa mfano mtoto akiiba mzazi atamkanya kwa viboko maana jamii itamchoma moto au serikali itamfunga jela miaka 30 … ili tuondoke huku ondoeni utaratibu wa viboko mashuleni, ondoeni adhabu ya kifo vifungo visizidi maika 20 kama Norway la sivyo tutakua tunaziba huku kule pako wazi
 
Kizazi kibabadirika kila baada ya "miongo" kadhaa ndo maana shule za leo mpaka hesabu wanaletewa multiple choices.
Kuna siku nimeenda shuleni kwa mwanangu kuonana na mwalimu kutokana na ukorofi wa mtoto.
Nikamwambia mwalimu akirudia tena mchape, mwalimu akasema hawaruhusiwi kuwachapa na camera zimewekwa kila darasa.
Nikajisemea moyoni yaani mimi ningekuwa mwalimu ningefukuzwa kazi mchana kweupeee, watoto wadogo class 3 na 4 walivyo sio watulivu ningeachaje kuwachapa
 
sasa wewe kama sio muislam inakuwaje unageuka kuwa msemaji wa mambo ya kiislam? wakati mashehe wameshatoa waraka kulaani kitendo cha ustaadhi huyo? au ule waraka haukuusikia.
Mimi cjatoa msimamo wa kubarik wa la kulaan zaid ya kusema hyo ni tasisi ya kidg na labda ina miongoz yake na kama yupo kinyume achukuliwe hatua hvyo. Kuna sehemu nimesema yupo saw au ayupo sawa specifical kwakutumia muongoz wa dini ?
 
Mihemko ya mitandaoni ni ya kipumbavu kabisa....
Fimbo za kawaida kabisa hizoo...

🚮🚮
 
  • Thanks
Reactions: I M
Nimeshindwa hata kuelezea, naomba kufahamu kama ni sawa jaman,. Kuna mtoto mdogo hapo nimemuonea huruma sana.

Lakini serikal imekataza kuchapa watoto wawapo mashule, sasa swali, hapo ni wanaruhusiwa kuchapwa namna hiyo? Hakuna adhabu nyingine kwani ya kuwafanya wasirudie kosa?

Nawasilisha.
Cc: Doroth Gwajima

Pia soma
- Mwalimu wa Madrasa apandishwa Kizimbani kwa tuhuma za kuwachapa fimbo (Ukatili) wanafunzi wa madrasa

View attachment 3242079
Huyu Mwl kazidisha idadi ya fimbo kisheria ila nia yake ni njema kuliko aliyechukua video na kuzambaza.

Video ya adhabu ila watu wanaonyesha chuki za kidini.
 
sio sawa ila sisi tumechapwa viboko chini ya unyayo na mapaja na maisha yaliend miaka kumi ijayo tanzania vijana wa kiume 30% watakuwa mashoga tayari trust me miaka 20 ijayo 70% watoto wa kiume watakuwa addicted na ushoga na na 90% ya wanawake watakuwa ma feminist
 
Inaweza
Huyu Mwl kazidisha idadi ya fimbo kisheria ila nia yake ni njema kuliko aliyechukua video na kuzambaza.

Video ya adhabu ila watu wanaonyesha chuki za kidini.
Inaweza kuwa Nia yake njema,ila iwe fundisho kwa wenye Nia ya kupania kupiga watoto ovyo!
 
Back
Top Bottom