#COVID19 Kudhibiti maambukizi ya COVID-19: Wasafiri kutoka Tanzania wapigwa marufuku kuingia Uingereza

#COVID19 Kudhibiti maambukizi ya COVID-19: Wasafiri kutoka Tanzania wapigwa marufuku kuingia Uingereza

Kwenye utawala huu au ujao?!!

Utawala huu mtu Unaweza kufanya uamuzi wa kiofisi kesho yake ukafukuzwa kazi au ukaambiwa nyumba yako ipo kwenye hifadhi ya chemchem hivyo Ni ya kubomoa au hata ukashtakiwa kwa uhujumu uchumi.
nenda bank ukajionee,sio siasa zenu za majitaka mnazoimbiwa majukwaani na twitter kila siku.
 
Mimi nafikiri wamefanya vyema maana serikali pamoja na mambo yote haikupaswa kupuuzia swala la chanjo.... tulipaswa kuweka msimamo juu ya chanjo wala sio jambo baya...
kwani wao UK si wamechanja mkuu!

hawaiamini chanjo ama?

unaona sasa bussness imegeukia kwenye chanjo,hawataki takwimu tena!!!!
 
nenda bank ukajionee,sio siasa zenu za majitaka mnazoimbiwa majukwaani na twitter kila siku.
Unafikiri hatujui na hatuoni? Au kwa vile tumekaa kimya?

Chombo Cha habar tu chenyewe kuandika habari Ni tabu ije iwe eti mtu uchukue uamuz wa peke yako? Unapigwa ya uhujumu uchum na huko mahakaman nako unakutana na maelekezo yalishatolewa kutoka juu.
 
kwani wao UK si wamechanja mkuu!!!
hawaiamini chanjo ama??
unaona sasa bussness imegeukia kwenye chanjo,hawataki takwimu tena!!!!
Vyote vinatakiwa mzee...chanjo na takwimu..

fuateni utaratibu wa kisayansi unaokubalika kidunia na ambao unatumiwa hata kwa magonjwa mengine yote Kama ukimwi,. Ndui, nk, acheni ushindani usio na mantiki na ambao hata hamuuwezi hata tone kwanza. Kwani mkitoa takwimu Kuna shida gan na mkichanjwa Kuna shida gani? Mnakataa chanjo ya Corona lakin mnaomba chanjo ya ukimwi!!! Kwani mbona chanjo nyingine mnapokea why only Corona???!!!
 
Issue siyo Coronavirus tena, ni variant ya Coronavirus.
Sasa hiyo variant yupo south africa na kwa watani zetu, lakini tumekuwa singled out among all southern African countries , hapa ndio tatizo lilipo.
Cha msingi ni mtu kuchekiwa hapa na ulifika huko kutenganishwa kwa hizo wiki 2
 
Lakini hii sirikali yetu inachekesha sana, ni kweli maambukizi ya korona sio makubwa nchini...kuna ubaya gani wa kutoa data za hao wagonjwa?!.
Chukua tahadhari bila kushurutishwa. Uhai ni mali yako siyo mali ya serikali.
 
Hahaa kwahiyo kazi yetu ni kusubiri wengine wagundue dawa, sisi tunafanya jitihada gani hata za kuzuia kusambaa kwa ugonjwa kwani hata barakoa tu rais haonyeshi mfano wa kuvaa au maombi yanatosha.
Wewe umekatazwa kuvaa barakoa?

Ni kama kipindi kile mnapiga kelele eti mbona rais hasemi tukae lockdown,? Yani eti unasubiri rais akwambie ukae lockdown?,!

Wewe kama unaona hizo ndio njia za kuzuia corona si ufanye kwako na famikia yako?
 
bahati mbaya wamekutana na watu wanaofikiri kabla ya kufata mkumbo.

cha kushangaza utakuta kati ya walii 10 wanaoshuka viwanja vya ndege 5 wanatoka UK,jiulize wanakujaje nchi hatari kwa afya zao??

nakumbuka hata US kipindi inatangaza raia wake warejee ubarozi ili iwarudishe nyumbani,hakutokea hata mtu mmoja maana nyumbani hali ilikuwa inatisha.

Kuna yule wa twiter kutoka kutoa siri za selikali na sasa kageukia kuaminisha umma kwamba tz kuna corona na inaua maelefu ya watu kila siku.

Sasa kasahau hata mambo yote ya icc
 
Kwa hiyo lumumba mnataka kushindana na UK? Mnafikiri hao Ni ACT? Siyo kila Vita Ni ya kupigana, nyingine unaziepuka hata kwa kutumia style ya mbuni...unafukia kichwa mchangani kiwiliwili nje unajifanya hujui.

Wee hao watu wapo wanaangalia namna gani ya kuhamishia makazi yao mwezini wewe hata matundu ya choo mashulen bado halafu eti uvimbishane nao msuli!!!!
Ngoja kwanza wapige pin afta pin akili zitakaa sawa tu.
Siku zote huwa nasema chadema mnajidharau sana sijui kwanini,

Hao wazungu ni Mungu? Si ni binadamu kama wewe? Sasa hii kuwatetemekea unayoonesha hapa wakija kwenye familia yako na kutaka wawale kigabo wote utakataa kweli?
 
mtasubiri sanaa.
Maisha ya mtanzania NI CORONA TOSHA.
wewe Kama una matatizo yako ya kiafya chukua tahadhari.
Mitano mingine [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Siku zote huwa nasema chadema mnajidharau sana sijui kwanini,

Hao wazungu ni Mungu? Si ni binadamu kama wewe? Sasa hii kuwatetemekea unayoonesha hapa wakija kwenye familia yako na kutaka wawale kigabo wote utakataa kweli?
Ahahaaaa hasira haisadii Mkuu.

Hivi Ma CCM mlivokuwa mnaibaka demokrasia hamkujua Kuwa in every action there is equal and opposite reaction?!!! Tulia hivo hivo mzee fimbo zaidi zinakuja.
 
1. UK haijazuia "watanzania" kuingia nchini mwao. Wamezuia WAGENI wanaotoka au waliopitia Tanzania ndani ya siku 10 kabla ya tarehe 22 Januari 2021. Raia wao na raia wenye haki za makazi UK wataruhusiwa ila kwa masharti ya kujitenga kwa siku 10. Hivyo hata kama ni raia wa nchi nyingine unaishi Tanzania au umepitia, na haukidhi vigezo vya uraia na haki za makazi, hautaruhusiwa kuingia.

2. Uingereza wana haki na wajibu wa kulinda wananchi wao na kutanguliza maslahi ya nchi yao. Ikiwa wamefanya utafiti wao na kuona kuwa WAGENI kutoka "Tanzania" wanaleta madhara, wanayo haki ya kujilinda.

Hata hivyo, bado kuna shaka hii hatua imechukuliwa kisiasa zaidi kuliko kiutaalam.
Mosi, je ugonjwa na 'variant' mpya ya COVID 19 inaangalia uraia? Ikiwa kama wanaoruhusiwa kuingia wanaweza kujidhibiti au kudhibitiwa ili wasiambukize wengine, kwa nini kusiwe na utaratibu utakaochuja wanaoweza kufuata njia hizo hizo?

Pili, ikiwa mashirika ya ndege yanalazimisha vipimo vya ugonjwa wa Korona kabla ya kusafiri, ina maana hawaviamini vipimo hivyo na hivyo kuvifanya batili? Kuna haja gani ya kufanya vipimo vya USD100 na bado vinaonekana havina tija?

Nota Bene: mtazamo huu hauainishi kama msimamo au hatua za Tanzania kukabiliana na magonjwa ya Korona ni sahihi au la.
 
Hizi propaganda zako ulizianza tangu mwaka jana.ukapiga na ramli zako za lock down ukaangukia pua.
Choko choko nyingine zimeanza naona umerudi upya.
Nikwambie tu maisha yetu ya mtanzania NI CORONA TOSHA.
Huo ugonjwa utawasumbua wanaoukumbatia Ila sisi tumeamua kuishi maisha YETU.
Kumbe hata watu ambao hizi tanzia zinazopelekea nyuzi hizi nao wanaishi?

Ama kweli stajaabu ya Mussa!
 
Mabeberu Hayatupendi
Ndiyo Ukweli Wenyewe
Nasema Uongo Ndugu Zangu
😀😁😂🤣😃😄😅😅😃😃🤣
 
Rasmi nasimama na rais wangu, mabeberu hawafai na wanatumia corona kutaka kututawala.. Rais endelea na msimamo nakuunga mkono na katika maeneo nitakayokuwa naelezea jinsi ambavyo mabeberu hawafai.
Kama Wana Nia ya kututawala kupitia magonjwa kwani ugonjwa Ni korona tu? Ni ugonjwa upi ambao sisi tuna uwezo wa kuushughulikia bila wao kwa maana ya Kinga, dawa, tafiti nk? Taja hata mmoja tu ambao hatuwategemei wao.
 
Back
Top Bottom