Kuelekea kuadhimisha miaka 10 ya ndoa

Kuelekea kuadhimisha miaka 10 ya ndoa

Hongera mkuu, inaonekana mda wa uchumba uliutumia vizuri katika kuchunguzana.
Asikudanganye mtu hakuna cha kuchunguzana wala nini, ukimchunguza sana binadamu utakuta madhaifu kama 100 na ushee, na kila ukichunguza utabaini mengi zaidi, na kila achunguzae sana haoi, mwisho wake huishia kula tunda kimasihara na kutokomea. Kama huamini fuatilia hili kwenye jamii zetu utabaini ukweli.
 
Habari wadau, nikiwa nipo mbioni kuelekea kuadhimisha miaka 10 ya ndoa yangu leo hii nimeona nitoe ujumbe mfupi tu kwa wanaume kama mimi maana watoto wa kiume kwao sio rahisi kuiweza ndoa.

1. Ndoa ni sawa na gereza ambalo tofauti iliyopo kwa gereza la kawaida ni kwamba gereza la ndoa mfungwa huchagua mfungwa wenziwe wa kuishi nae gerezani.

2. Ndoa ni kipimo cha akili kwa maana wenye akili pekee ndio watakaoiweza ndoa kwani wasio na akili mapema sana huamua kujitoa.

3. Ndoa ni kipimo cha uvumilivu, hapa sasa kila mmoja na uwezo wake kwenye kuvumilia mambo yaliyomo ndoani, kuna uvumilivu kwa mambo na aina tofauti. Na wasio wavumilivu huishia ugomvi usiokwisha ikiwemo kupigana na mwisho wa siku kuishindwa ndoa.

4. Lakini pia ndoa ni kipimo cha utu, hapa sasa nataka niweke bayana baadhi ya mambo. Kuoa sio kwa ajili ya kupata watoto tu kwani hata watu wasio na ndoa wanao uwezo wa kupata watoto, isipokuwa utofauti uliopo watoto wanaolelewa na wazazi wao wakiwa ndoani hadi kufikia kuwa wakubwa huwa na makuzi mazuri sana.

Hasa ikichangiwa na wazazi wakiwa ni washika dini ipasavyo na hapa ndio pale ambapo utofauti wa mtoto aliyelelewa na wazazi wake na mtoto aliyelelewa na mzazi mmoja huonekana. Wazazi huweza kusaidiana majukumu mbali mbali ya kimalezi na kadhalika hiyo yote ni katika kuhakikisha watoto wao wanawalea katika misingi iliyo bora, huo ndio utu.

Kuwa na ndoa ni kitu ambacho kila mwanaadamu hutamani kuwa nacho isipokuwa baadhi ya matatizo, makuzi, nyendo na baadhi ya tabia ndio ambazo hupelekea baadhi yetu kuzishindwa ndoa. Kitendo cha kukosa utu ni kama vile kumuachia mwanamke mtoto alee peke yake, au mtoto kulelewa na mama mwengine asiye mama yake wa kumzaa, kitendo ambacho aidha kitapandikiza chuki kwa mtoto dhidi ya baba yake au mama yake.

Mwisho kabisa napenda niseme "Ndoa ni kwa wanaume na sio watoto wa kiume"

Ahsante.
Unasherekea miaka 10 ya kugongewa bila kujua?😂

Hakuna mke wa mtu aliewahi nikataa otherwise wako Ni mbovu
 
Unasherekea miaka 10 ya kugongewa bila kujua?😂

Hakuna mke wa mtu aliewahi nikataa otherwise wako Ni mbovu
Hata akiwa mbovu ni sawa tu ilimradi maisha yanakwenda. Then unagonga wa wenzio basi nakutahadharisha tu jiunge na team kataa ndoa. Maana uchungu wa kugongewa hauwezi kukukwepa endapo utaoa. Malipo ni hapa hapa duniani.
 
Habari wadau, nikiwa nipo mbioni kuelekea kuadhimisha miaka 10 ya ndoa yangu leo hii nimeona nitoe ujumbe mfupi tu kwa wanaume kama mimi maana watoto wa kiume kwao sio rahisi kuiweza ndoa.

1. Ndoa ni sawa na gereza ambalo tofauti iliyopo kwa gereza la kawaida ni kwamba gereza la ndoa mfungwa huchagua mfungwa wenziwe wa kuishi nae gerezani.

2. Ndoa ni kipimo cha akili kwa maana wenye akili pekee ndio watakaoiweza ndoa kwani wasio na akili mapema sana huamua kujitoa.

3. Ndoa ni kipimo cha uvumilivu, hapa sasa kila mmoja na uwezo wake kwenye kuvumilia mambo yaliyomo ndoani, kuna uvumilivu kwa mambo na aina tofauti. Na wasio wavumilivu huishia ugomvi usiokwisha ikiwemo kupigana na mwisho wa siku kuishindwa ndoa.

4. Lakini pia ndoa ni kipimo cha utu, hapa sasa nataka niweke bayana baadhi ya mambo. Kuoa sio kwa ajili ya kupata watoto tu kwani hata watu wasio na ndoa wanao uwezo wa kupata watoto, isipokuwa utofauti uliopo watoto wanaolelewa na wazazi wao wakiwa ndoani hadi kufikia kuwa wakubwa huwa na makuzi mazuri sana.

Hasa ikichangiwa na wazazi wakiwa ni washika dini ipasavyo na hapa ndio pale ambapo utofauti wa mtoto aliyelelewa na wazazi wake na mtoto aliyelelewa na mzazi mmoja huonekana. Wazazi huweza kusaidiana majukumu mbali mbali ya kimalezi na kadhalika hiyo yote ni katika kuhakikisha watoto wao wanawalea katika misingi iliyo bora, huo ndio utu.

Kuwa na ndoa ni kitu ambacho kila mwanaadamu hutamani kuwa nacho isipokuwa baadhi ya matatizo, makuzi, nyendo na baadhi ya tabia ndio ambazo hupelekea baadhi yetu kuzishindwa ndoa. Kitendo cha kukosa utu ni kama vile kumuachia mwanamke mtoto alee peke yake, au mtoto kulelewa na mama mwengine asiye mama yake wa kumzaa, kitendo ambacho aidha kitapandikiza chuki kwa mtoto dhidi ya baba yake au mama yake.

Mwisho kabisa napenda niseme "Ndoa ni kwa wanaume na sio watoto wa kiume"

Ahsante.
Hatukatai kuishi kinyumba baina ya mwanamke na mwanaume, hatukai watoto kulelewa kimaadili wakiwa chini ya uangalizi wa wazazi wote wawili, hatukatai mahusiano yana kupanda na kushuka ivyo kuvumiliana na kusameheana ni muhimu. Tunachokataa ni ule mkataba mnaotakiwa kuusaini kwa sababu vifungu vyake vinamkandamiza mwanaume pale ndoa inapovunjika.
 
Inamaana huelewi kuwa wewe mwenyewe ni athari ya kizazi cha mababu zako, au hujui kama mababu zako walizaliwa na hata wao pia walikuwa na mababu zao hadi kufikia wewe!
Sasa mimi inanisaidia nini hiyo ya mababu zangu kuwa na mababu zao
 
Hatukatai kuishi kinyumba baina ya mwanamke na mwanaume, hatukai watoto kulelewa kimaadili wakiwa chini ya uangalizi wa wazazi wote wawili, hatukatai mahusiano yana kupanda na kushuka ivyo kuvumiliana na kusameheana ni muhimu. Tunachokataa ni ule mkataba mnaotakiwa kuusaini kwa sababu vifungu vyake vinamkandamiza mwanaume pale ndoa inapovunjika.
Umesomeka na kueleweka barabara.
 
Mwaka ujao,natimiza miaka 10 ya ndoa,ndoa ni nzuri,familia ni nzuri,kila napoamka asubuhi nawaona watoto wangu wanavyonifurahia,naporudi nyumbani wanavyonikimbilia na kunikumbatia,nahisi faraja,Upendo,amani najawa na tumaini katika maisha🙏
 
Back
Top Bottom