Hoja yako hujaiweka vizuri,mbona huwazi kwamba kati ya 53% ya line zilizosajiliwa kuna wengi waliosajilia ndugu na jamaa waliokosa vitambulisho ama wao wenyewe kusajili line zaidi ya moja?Mtu mmoja anamiliki line tatu mpaka nne na wengine mpaka sita kwa hiyo huenda hao wanaomiliki line nyingi wameamua kuzipunguza japo hii haiondoi ukweli kuwa wananchi wananyanyaswa kwa vile NIDA wameshindwa kazi yao
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa taarifa za tcra wamiliki wa simu Ni 21m line hai Ni 46m Ina maana kila mwenye simu alikuwa na line zaidi ya moja na 26m zimesha huishwa kwa vidole, kwa lugha nyingine Kuna mgomo baridi kila mtu kaamua kusajiri line moja na kutupa nyingine.Huu ni mtizamo wangu ambao nauleta kama tahadhari kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) juu tukio la kionevu ambalo Watanzania wanalipigia kelele lakini mamlaka zinatumia ubabe kulitekeleza.
Kwa mujibu wa TCRA, kesho kutwa ndio hatma ya line takribani milioni 20 za Watanzania kuwa hewani kwa kile kinachodaiwa kutokuwa na usajili wa alama za vidole.
Kwa mujibu wa TCRA mpaka juzi ni 53% tu ya line za simu kati ya line zote ndizo zilizosajiliwa kwa alama za vidole hivyo kitakwimu ni kama nusu ya watumiaji wa simu line zao zitafungwa mpaka watakapokamilisha taratibu.
Ningependa niwakumbushe chama changu pendwa CCM kwamba idadi ya watu ambao haijasajili line za simu kama wataamua kulipiza kisasi kwenye uchaguzi ujao kwa uonevu wakuzifunga line zao ni dhahiri uchaguzi utakuwa mgumu.
Nawakumbusha uchaguzi mkuu 2015 idadi ya watu waliojiandikisha kupiga kura ni 23,253,982 na idadi ya waliojitokeza kupiga kura kote bara na visiwani ni watu milioni 15.6.
Watu watakaofungiwa line za simu kwa makadirio ni takribani watu milioni 20, hivi hamuoni kwamba hili ni hatari hasa kwa mwaka wa uchaguzi kama huu?
CCM tambueni hili zoezi Watanzania mnaowatetea (wanyonge) ambao ndio wapiga kura ndio wahanga wakubwa kwani wengi wapo vijijini ambapo hizi huduma hazipo.
Watu wamepoteza muda wao tangu awali zoezi hili lilipoasisiwa mwaka 2014 wamehangaika na vitambulisho hivi pasipo mafanikio, wapo ambao wamediriki hata kuuza mifugo kama kuku ili kupata nauli za kwenda wilayani (NIDA) ili tu walau kupata hizo namba za NIDA lakini mpaka leo hawajazipata.
Hii dhana kwamba wananchi walipuuza hili zoezi mwanzoni sio kweli kwani sisi ndio wananchi, wapo wengi wamejitokeza mwanzoni kabisa 2014 lakini hawajapata vitambulisho, watu wamerudia tena na tena lakini hawa NIDA ni tatizo.
Tusijiamini eti tu kwasababu ya miradi kama Stiglers, ununuzi wa ndege. Hii idadi ya watu wanaoenda kuonewa tarehe 20 kwa uzembe wa NIDA inaweza kabisa ikawa tatizo uchaguzi ujao.
Watanzania hawakatai kujisajili ila ni vema wakawekewa mazingira wezeshi ili wajisajili.
SMS sent & delivered
Hapana huduma za kifedha linabadilika pia, linakuwa jina la mwenye kitambulishoKwenye huduma za kifedha litabaki jina lile lile la zamani, ni changamoto zaidi maana laini itakuwa sio yako wala huyo uliyemsajilia sio yake. Omba usipate tatizo kwenye huduma za kifedha
Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kuvuta ungaWasiongeze inatosha kwanza tunasumbuka, wasiokuwa na vitambulisho wengi Ni chadema
Sent using Jamii Forums mobile app
Utawala wa ccm ndiyo utawala unaowaumiza kasakologia Raia wakeWatukatie tu
Nchi zingine za Afrika, zinapambana kuingiza pesa kupitia subscribers wao wanatupunguza. Wasubiri October tutawaonyesha uchungu wetu
Hii naona imefanyiwakazi mapema sana ujumbe wa simu umeingia ingawa wengine tulishachukua vitambulisho vya NIDA miaka sasa.Kwa NIDA nashauri watume majina na namba za wananchi ambao wameshajaza form na hawajapata namba zao ili mitandao ya simu (MNO) wasiwafungie kwa sababu hawana hatia.
Kwani wameshafunga? Lawama za nini? Kama ni kuwahamasisha tu wananchi watafute hivyo vitambulisho kwa kutambua uvuvi wao na umuhimu wa kuwatambua wananchi kitaifa ?Tatizo ni NIDA adhabu anapewa Mwananchi! Serikali inayo endesha mambo kwa kukurupuka utadhani Taifa hili ni changa limeanzishwa miaka ya hivi karibuni!
Na ukiona mtawala anakomalia sheria flani ipite jua kuna jambo mbele,mim siamini kama ni ishu ya uharifu tu.Kwa serikali hii inavyopenda kupika data usishangae ukaambiwa mapato yameongezeka baada ya watu kusajili laini zao kwa alama za vidole...kivipi basi muulize polepole
Sent using Jamii Forums mobile app
Umeongea kama uko kijiweni. Inamaana kazi ya namba ya kitambulisho ni kusajili laini pekee? Waliochukua vitambulisho kabla ya zoezi la usajiri na kuondoka nchini, waliofariki, wasiotumia simu, hawa mtalazimisha wawe wamesajili line za simu?Naona mnadanganyana hahahaha mlikuwa wapi siku zote? NIDA kuna shida lakini watanzania tuna shida zaidi,,,,, kuna namba nyingi sana zimeshatoka lakini hadi leo hazijasajiliwa ,,,,,,,,
Wenyewe wala hawaangaiki na usajiri sijui line zao hazitofungwa au Magu kalenga hapo ili awabebe
washatoa taarifa amna kumsajilia mtu laini kwa namba yako....ukibainika ni faini 5m au miezi sita jela
Sent using Jamii Forums mobile app