Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Kwani wameshafunga? Lawama za nini? Kama ni kuwahamasisha tu wananchi watafute hivyo vitambulisho kwa kutambua uvuvi wao na umuhimu wa kuwatambua wananchi kitaifa ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo unamaanisha Mkuu wa Nchi alikuwa anatuongopea pale aliposema tarehe 20/01/2020 mwisho wa kusajili line za Simu?!
 
Pongezi zetu ziwafikie viongozi wa kiserikali kwa Maamuzi ya kuwatambua watanzania wote kupitia utoaji wa vitambulisho vya Taifa.

Mbali na yote kuna tangazo lililotolewa kuwa ifikapo tarehe 20/01/2020 simu(laini) ambazo zitakuwa bado hazijasajiliwa kwa mfumo wa alama za vidole zitazimwa.

Hakika mpango wa serikali ni mzuri lakini wananchi wengi hatujapata namba zetu za NIDA hivyo tutahukumiwa kwa kosa ambalo sio letu. Baadhi ya Wananchi kila kukicha tunafuatilia namba zetu kupitia mifumo iliyotolewa hadi kwenye ofisi za NIDA lakini zinaibuka sababu mbalimbali ikiwemo kutakiwa kurudia na tunafanya Kama maelekezo yanavotolewa, Je tunastahili kuadhibiwa?

OMBI
kwakuwa serikali ni moja na taasisi zote zinazohuska ziko chini ya serikali hiyohiyo niombe taasisi hizi ziwasiliane na pale mtakapojiridhisha kuwa wote waliojiandikisha kabla ya tarehe 20/01/2020 namba zao (NIN) zimeishakamilika na kuwekwa mtandaoni hapo ndo mzime laini ambazo hazijakamilisha usajili.

"Mungu ibariki Tanzania,"



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe hujitambui na wala huwajui Viongozi wako jinsi walivyo wakurupukaji! Mfano Mkoa wa Kigoma walisajiliwa na NIDA tangu mwaka jana.Wiki iliyo pita ndo wameanza kutoa namba za NIDA na kwa baadhi ya Watu wachache! Wenye makosa hapo ni Wananchi au ni wenye Mamlaka?!
 
Sisi tupo huku vijijini na tumesajili line zetu kwa namba za NIDA. Poleni sana wazee wa ' HIYO PESA TUMA KWENYE NAMBA HII' Tafuteni kazi zingine za kufanya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa wale wenye wasiwasi na vijana wanaopita mitaani kuwasajilia laini zaidi ya moja unaweza kwenda Mtandao husika ukaomba wakuonyeshe laini zako zote zilizotumia kitambulisho chako ambazo huzitambui wanazicancel nimeona Hayo ktk Mtandao WA airtel
Hili ni jambo zuri sana .
 
WhatsApp kinachotumika ni internet namba yako utambulisho tu ndio maana unaona mtu yupo Ulaya ila anatumia utambulisho wa namba yake ya voda au tigo utashindwa kuiupdate kwa sababu namba za kuverify wanakutumia kwenye namba ya utambulisho
Asante kwa ufafanuzi mzuri.
 
Achana nae huyo mkuu! Ni limbukeni tu,anahisi kupata kitambulisho cha NIDA ndo kuyapatia maisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi tupo huku vijijini na tumesajili line zetu kwa namba za NIDA. Poleni sana wazee wa ' HIYO PESA TUMA KWENYE NAMBA HII' Tafuteni kazi zingine za kufanya

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya ni majibu ya akili za nzi kucheza na uchafu. Angekuwa na akili angetengeneza asali. Nchi inahitaji muda zaidi kujisajili. Line zikizimwa kesho wanyonge wengi wataumia. Mm nimeshasajili ila najua kwa muda uliowekwa ni ngumu nchi zima kuwa imesajili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…