Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

kama unataka kujua jukumu la nani subilia saa 11:59 na lingine kwani ungekua una issu na hicho kitambulisho binafsi usingekifuatilia tuache siasi fuatilia kitambulisho kuna mambo mengi ya ukiwa na hicho kitambulisho.
 
Mara simu fake sijui iliishia wapi, tukapata hasara, ivi kweli raia mimi ntajuaje hii ni fake au sio, kwanini Serikali kupitia TBS isizuie zisiingie, kiukweli Serikali ndo inarudisha nyuma Maendeleo ya wananchi
Kipind niliumia Sana nilikuwa na mkebe mmoja matata Sana ulitoka UK babu Cha kushangaaa nikaambiwa fake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Mtaani wanapita vijana wamachinga na maspika yao, wanatangaza "tunasajili laini kwa alama za vidole". Wanachomoa vimtambo vyao, wanakuomba kitambulisho wanakusajili. Ni nani anaweza kupreserve integrity ya zoezi?

Hivi watu wenye ajenda zao wakiwapa hawa vijana pesa na wakisajili kwa fingerprints za watu wengine zoezi hili umakini wake utakuwaje?

2. Mtandao mmoja mtu anaweza kuwa na laini hadi 5

Je mtu mmoja mwenye kitambulisho akisajili laini kadhaa na kugawa nyingine kwa ndugu, jamaa na marafiki itakuwaje?

3. Huko vijijini ndani ndani kabisa hao wanaosajili kwa alama za vidole capacity yao ya kufika huko ndanindani ikoje?

MY TAKE:
Hii nchi ni nchi ya watu masikini sana, kinachosikitisha ni kwamba pale kunapoanza kutokea mwangaza fulani hivi wa sekta fulani kuanza kuchomoza na kushine ili baadae iwe nguzo muhimu ya kiuchumi na kijamii, huwa zinatokea forces fulani kutoka kwa serikali ileile kuanza kuweka regulation ngumungumu zinazorudisha mafanikio ya wananchi nyuma. Kwa mfano:

a) Wananchi walikuwa wameshapiga hatua kubwa kweli kwenye kumiliki TV, kiufupi nyumba za wananchi wengi vijijini na mijini walishaanza kuona TV kama sehemu ya utamaduni wao. Cha ajabu serikali ikaja na mambo ya kuhama Kutoka Analojia kuja Dijitali, na kusababisha kuleta watu wa ving'amuzi kitu kilichopekekea gharama za kumiliki TV kuwa juu, na matokeo yake nyumba nyingi nchini leo hii TV ni anasa!. Watu leo hii imefikia hafua kuangalia Taarifa za habari Bar, au kuangalia mpira wa ligi yao wenyewe kwenye mabanda ya mpira!
Kiufupi base ya wananchi wamiliki TV, imeshrink mno

b) Leo tena baada ya mafanikio ya wananchi mamilioni kwa mamilioni kumiliki laini za simu, serikali ile ile yenye kawaida ya kuvuruga baada ya mambo kuanza kuonekana kukaa kwenye msitari inakuja na reguation juu ya regulation, leo inataka watu wajisajili kwa vitambulisho vya NIDA plus fingerprints, wakati inajua ipasavyo kuwa capacity ya kuprovide vitambulisho hivyo kwa kasi ni ndogo lakini pia uwezo wa kusajili hizo alama za vidole kwa kasi ya kutosha hadi kucover huko vijijini ni mdogo!
Matokeo ya hili zoezi la usajili wa laini ni ama watu wengi watacheat kwa kutokuwa na usajili sahihi au kupelekea upunguaji wa umiliki wa laini za simu, matokeo yake wamiliki simu watapungua kama ilivyotokea kwenye zoezi la TV
Ongeza mambo ya blogs na TV mitandaoni
 
Kwanza maisha ni magumu, halafu wewe unaongeza ugumu kwa kufunga laini za simu.

Wapiga kura wako, wengi wapo vijijini na hawajawahi kupata namba za NIDA. Octoba wanaenda kukuchinjia baharini (au una plan B ya kushinda?)

Unaenda kuvunja mahusiano ya watu, kuzuia miamala yote ya fedha na kujenga chuki kati yako na wananchi.

Ulitakiwa kuwawajibisha viongozi wa NIDA wala si wananchi. Nyota yako inazidi kufifia. Kwanini kila unachogusa kinafeli?

Je, mbona mnakomalia namba, tutaishia kupata namba tu bila vitambulisho?

Tarehe 20 ni usiku huu, lets wait and see if mzee wa font fed atafanya yake.

.....UPDATES....

Serikali ya Tanzania imesema itatumia hekima kuwasaidia wananchi walioshindwa kusajili laini za simu kwa sababu ya kukosa kitambulisho cha Taifa na namba licha ya kuanza mchakato wa kupata kitambulisho hicho.

Imesema wananchi hao taarifa zao zipo katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), huenda wamekosa kitambulisho au namba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.

Hayo yameelezwa leo Jumapili Januari 19, 2020 na naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye katika mkutano wa ndani wa CCM mkoani Kigoma.

"Serikali itaona jinsi ya kutumia hekima kwa wananchi ambao taarifa zao zipo katika ofisi za Nida kuona namna ya kufanya lakini kwa wengine ambao hawajajaza fomu laini zao zitazimwa,” amesema Nditiye.

Amesema ambao laini zao zitazimwa ni wale waliosajili laini chache na kuacha nyingine licha ya kuwa na kitambulisho hicho.

Amebainisha kuwa usajili wa laini za simu ni endelevu licha ya baadhi ya wananchi kupuuza.


....
Binafsi sijamuelewa kuhusu aina ya laini zitakazofungiwa.
 
Niwaulizeni nyie mnalalamikia NIDA TCRA hivi NIDA wanamiaka ngapi toka waanze kutoa vitambulisho.TCRA nao wana muda gani toka waanze kutuhimiza tukasajili line zetu.

Wasilaumiwe makosa ni yetu wananchi kila jambo tunadharau ata mombo ya msingi tunaleta dharau mie nimejiandikisha miezi ya nyuma huko na famila yangu baada ya muda mchache tumchuka namba.au toka miaka yote mlikua amjafikisha miaka 18 sasa ndio mmefikisha hiyo miaka.

Acheni lawama kwanza TCRA wametuvumia sana Chekini mnavyopanga mafoleni mtasema mnasubiria Mwendo Kasi Kimara.WAZIME LINE MSAJILI ZINGINE MLIYATAKA WENYEWE
Watakaokosa mapato si wao wafunge hata wakifunga sio mwisho wa kuwasiliana
 
kagombe,
Muda mwingine tumia kichwa kilichoko juu ya mabega kufikiri na sio kilichoko chini ya kitovu, watu wamejiandikisha mwaka 2013 hadileo hawajapata, waziri kaenda ruvuma kamkuta afisa wa nida anavitambulidho elfu 14 kavikalia hajavigawa, halafu unaleta janaba hapa
Huyu jamaa nadhani hatumii hata hicho kichwa cha chini kufikiri. .

RIP Dkt. Didas Masaburi
 
Ukiwasikiliza viongozi wetu, wote wanasema usajili wa line utaondoa uhalifu wa kimtandao na kusaidia usalama...
Sijawahi kuona popote usajili wa line za simu kuwa ni hakikisho la usalama!
NIDA na kitambulisho chao wanasaidia vipi usalama?
Kwani fingerprint inashindikana vipi kuwa recorded kupitia namba ya simu bila kitambulisho cha NIDA?
Kwa Watanzania wasiokuwa na simu wao hili zoezi haliwahusu? Kama haliwahusu uhakikisho wa usalama utakuaje ikiwa mhalifu hana namba ya simu anayomiliki? Nani alishauri usajili wa line ya simu kwa kitambulisho cha NIDA kuwa ni njia sahihi ya kuzuia uhalifu?
Lengo la vitambulisho vya Taifa ni kwa ajili ya kuzuia uhalifu?
Kwa nini vitambulisho vya Taifa vihusishwe na matumizi ya mawasiliano ya Watanzania?
Serikali ikizima line za watu baada ya January 20 itakuwa na uhakika wa kuzuia uhalifu wa kimtandao?
Nchi gani imefanikiwa katika hilo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawawezi kuupeleka ndugu. Ndiyo uchawi wenyewe waliurithi kutoka kwa mchawi mkuu kale kazee. Na wao wanauendeleza. Nia yao ni ovu sana..kufanya wadanganyika waendelee kuwa makondoo.
Mungu ni mkubwa, itafikia kipindi utaondolewa.
 
Niwaulizeni nyie mnalalamikia NIDA TCRA hivi NIDA wanamiaka ngapi toka waanze kutoa vitambulisho.TCRA nao wana muda gani toka waanze kutuhimiza tukasajili line zetu.

Wasilaumiwe makosa ni yetu wananchi kila jambo tunadharau ata mombo ya msingi tunaleta dharau mie nimejiandikisha miezi ya nyuma huko na famila yangu baada ya muda mchache tumchuka namba.au toka miaka yote mlikua amjafikisha miaka 18 sasa ndio mmefikisha hiyo miaka.

Acheni lawama kwanza TCRA wametuvumia sana Chekini mnavyopanga mafoleni mtasema mnasubiria Mwendo Kasi Kimara.WAZIME LINE MSAJILI ZINGINE MLIYATAKA WENYEWE
Ndg nadhani wewe unaishi mjini huangalii hawa watu wa vijijini
Kosa la nida kutowafuta watu vijijini wengi wao huko hawajui hata maana ya vitambulisho, ingekua vizuri kurudia rudia kuwafuata huko,sio kama hivi walipita mara 1 na kuwasahau na bado waliojiandikisha hawajapata Namba toka 2017 vip wasirudi kurekebisha kama walikosea baadhi yao!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa nadhani hatumii hata hicho kichwa cha chini kufikiri. .

RIP Dkt. Didas Masaburi
Kichwa cha chini kazi yake ukuongeza familia tu.Kichwa cha juu kazi yake kusoma ramani ya pesa sasa nyie mnawaza tofauti huku mnatupigia kelele mara NIDA OR TCRA wewe toa 2013 mpaka leo ujapata kitambulisho huo ni uzembe wako tu.mnalalamika ktk keybord futilieni vitambulisho 11:59pm
 
Ndg nadhani wewe unaishi mjini huangalii hawa watu wa vijijini
Kosa la nida kutowafuta watu vijijini wengi wao huko hawajui hata maana ya vitambulisho, ingekua vizuri kurudia rudia kuwafuata huko,sio kama hivi walipita mara 1 na kuwasahau na bado waliojiandikisha hawajapata Namba toka 2017 vip wasirudi kurekebisha kama walikosea baadhi yao!!

Sent using Jamii Forums mobile app
mkuu mie niko kijijini tena shambani kabisa ila walivyokuja tu nikachukua familia yangu yote tukaenda tukaambiwa baada ya mwezi na mmoja na nusu namba zitakua tayari.kweli baada ya huo muda nikaanza kufuatilia nikazipata
 
Back
Top Bottom