Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,505
- 4,427
Amani iwe nanyi,
Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema, amani, upendo, umoja na mshikamano kwa taifa letu. Ni mengi makuu Mungu ametenda maishani mwetu kustahili shukrani kuu. Pia, nakipongeza CCM kwa kudumisha utamaduni wa kuandaa chaguzi za kidemokrasia. Demokrasia ndio sifa kuu ya uwepo, ueneaji na ukuaji wa siasa za CCM.
Zikiwa zimebaki siku mbili kufanyika mkutano mkuu wa 10 wa CCM ,natumaini viongozi imara na wenye ushawishi watapatika. Nakipongeza chama kwa kufanikisha uchaguzi wa jumuiya ngazi ya taifa. Kilichonifurahisha jumuiya zote wamepatikana watu licha ya waliokuwepo kugombea kutetea nafasi zao lakini hawakufanikiwa.Hii ni ishara kwamba watu wenye ushawishi ndio wanahitajika.
Katika Uzi wangu wenye'title' CCM ni chama kikubwa lakini kimekosa viongozi wenye ushawishi nimejaribu kuonesha ni faida zipi watu hao wataweza kusaidia kuimarisha chama.
Tunapoelekea mkutano huo mkuu kama ilivyo mikutano mikuu ya jumuiya lengo lake ni uchaguzi na kutoa malengo ya chama. Ni matumaini yangu uchaguzi mkuu utatuletea watu safi na wenye ushawishi kwa nafasi zisizokuwa na kugombea.
Kama chuma cha mabadilko ya uongozi ndani ya jumuiya na chama na kuangusha baadhi ya miamba ,natamani kuona mabadiliko hayo yakifanyika pia ndani ya uongozi wa chama taifa .
Kwa nini natamani kuona mabadiliko?
Natamani kuona mabadilko ya uongozi ndani ya Chama kwa sababu ni kipindi ambacho zitaibuka na kuibuliwa hoja nyingi na wapinzani bila watu wenye uwezo wa kujenga hoja na ushawishi Chama kinaweza kupitia kipindi kigumu uchaguzi mkuu wa 2025.
Natamani kuona watu wapya ili kurekebisha makosa na kuziba mashimo yaliachwa na watangulizi wao.
Watu wenye ushawishi wa hoja watakisaidia chama kuvuka hususani kipindi hiki cha maridhiano.
Siku za nyuma niliwahi kuandika juu ya mtu anayeitwa Thobias Mwilapwa kupitia Uzi huu Thobias Mwilapwa apewe Ukatibu Mkuu wa CCM kwa uwezo wa ziada alionao ,mpaka sasa bado nina imani na uwezo alionao kwa nafasi hiyo
Nakitakia CCM mkutano mkuu mwema
Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema, amani, upendo, umoja na mshikamano kwa taifa letu. Ni mengi makuu Mungu ametenda maishani mwetu kustahili shukrani kuu. Pia, nakipongeza CCM kwa kudumisha utamaduni wa kuandaa chaguzi za kidemokrasia. Demokrasia ndio sifa kuu ya uwepo, ueneaji na ukuaji wa siasa za CCM.
Zikiwa zimebaki siku mbili kufanyika mkutano mkuu wa 10 wa CCM ,natumaini viongozi imara na wenye ushawishi watapatika. Nakipongeza chama kwa kufanikisha uchaguzi wa jumuiya ngazi ya taifa. Kilichonifurahisha jumuiya zote wamepatikana watu licha ya waliokuwepo kugombea kutetea nafasi zao lakini hawakufanikiwa.Hii ni ishara kwamba watu wenye ushawishi ndio wanahitajika.
Katika Uzi wangu wenye'title' CCM ni chama kikubwa lakini kimekosa viongozi wenye ushawishi nimejaribu kuonesha ni faida zipi watu hao wataweza kusaidia kuimarisha chama.
Tunapoelekea mkutano huo mkuu kama ilivyo mikutano mikuu ya jumuiya lengo lake ni uchaguzi na kutoa malengo ya chama. Ni matumaini yangu uchaguzi mkuu utatuletea watu safi na wenye ushawishi kwa nafasi zisizokuwa na kugombea.
Kama chuma cha mabadilko ya uongozi ndani ya jumuiya na chama na kuangusha baadhi ya miamba ,natamani kuona mabadiliko hayo yakifanyika pia ndani ya uongozi wa chama taifa .
Kwa nini natamani kuona mabadiliko?
Natamani kuona mabadilko ya uongozi ndani ya Chama kwa sababu ni kipindi ambacho zitaibuka na kuibuliwa hoja nyingi na wapinzani bila watu wenye uwezo wa kujenga hoja na ushawishi Chama kinaweza kupitia kipindi kigumu uchaguzi mkuu wa 2025.
Natamani kuona watu wapya ili kurekebisha makosa na kuziba mashimo yaliachwa na watangulizi wao.
Watu wenye ushawishi wa hoja watakisaidia chama kuvuka hususani kipindi hiki cha maridhiano.
Siku za nyuma niliwahi kuandika juu ya mtu anayeitwa Thobias Mwilapwa kupitia Uzi huu Thobias Mwilapwa apewe Ukatibu Mkuu wa CCM kwa uwezo wa ziada alionao ,mpaka sasa bado nina imani na uwezo alionao kwa nafasi hiyo
Nakitakia CCM mkutano mkuu mwema