Kuelekea Mpambano wa Watani wa Jadi 'TPL' Simba SC dhidi ya Yanga SC, Tayari ameshafungwa

Kuelekea Mpambano wa Watani wa Jadi 'TPL' Simba SC dhidi ya Yanga SC, Tayari ameshafungwa

Kuelekea pambano la kukata na shoka Jumamosi Februari 16, 2019 la watani wa Jadi (Kariakoo Derby) katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Tanzania 'TPL' Simba SC Mnyama, Wekundu wa Msimbazi dhidi ya Yanga SC Vijana wa Jangwani, ni kama kusema tayari Yanga ameshafungwa, yaani wamekwishapoteza mchezo huo wa TPL.

Wa kimataifa Original Simba SC Taifa Kubwa


Ni kutokana na ubora wa kikosi cha Simba SC, na thamani yake pamoja na safu hatari ya ushambuliaji ikiongozwa na Streika Matata uwanjani Meddie Kagere MK 14, akiunda Muunganiko wa Emmanuel Okwi, John Bocco na kiungo mshambuliaji ambaye anaudambwi mwingi mpaka anakuwa Kero uwanjani Cleoutus Chota Chama 'Triple C'

Mwana Kulitaka Mwana Kulipewa

Kocha Patrick Aussems baada ya ushindi dhidi ya Al Ahly SC katika Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) amesema umewaongezea morali Vijana wake kabla ya kuwavaa Vijana wa Yanga akiweka wazi mipango ya kumaliza kazi ya kuwasambaratisha watani hao mapema kabisa.

Simba iliitambia Al Ahly ya Misri kwa kuifunga bao 1-0 na kurudia ilichokifanya timu hiyo katika michuano ya CAFCL miaka 33 iliyopita katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Kwa muktadha huo 'ikiwa mwarabu amefungwa basi Vijana wa Jangwani watatepeta kama mate ya mlevi, Simba imechapwa Klabu bora inatakuwa Vijana wa Jangwani bhana' na hasa ukizingatia Septemba 30 ilikuwa tia tia maji mwana ukome kufuata wakubwa. Ushindi ndo lengo letu la kwanza iwe Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) au Tanzania Premier League TPL..

Tukutane National Stadium kwa MCHINA kama unaweza kuzuia kipigo cha kufedhehesha.View attachment 1022213View attachment 1022214View attachment 1022215

Sent using Jamii Forums mobile app
.
IMG-20190213-WA0012.jpeg


Jr[emoji769]
 
Sijawahi kuwa Yanga na sitakuwa milele. Ila nasemea uhalisia Simba iko overrated sana.
Simba iliyo ingia kwenye timu bora 16 barani Africa! kwa kumtoa Mbabane swallows (alikula 8) na Nkana! Simba hipo kwenye kundi gumu ila ana point 6, akimfunga Vita hapa nyumbani anaingia robo fainali. Sasa hapo inakuwaje over rated. Chama, Okwi, Kagere wote wanahitajika na timu kubwa ila Simba inapambana kuwatuliza. Ata Man city na kikosi chake kipana Burnley wanaeza mtoa nishai huo ni mpira. Ila hii Simba hiko vizuri mkuu, kuwa na amani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiungo kufunga Mara kwa Mara ni added value kama Casamillo..Msimu wa 2016-2017 Tambwe alifunga double digits..msimu uliopita alikuwa injury.. Amerudi tena..unafikiri kwa nini Amunike anampa nafasi.Feisal kuliko Mkude?ameona bright future kwake
Mkude ni defensive midfielder na anafanya vzr kwa namba hiyo, Feisal akipangwa kama defensive midfielder hua anatapata shida sana na analazimika kukata muda mwingi. Huwez kumlinganisha mkude na Feisal katika kuisaidia defence ila kama Feisal akicheza kama attacking ndio anacheza vzr. Ndio maana nilikwambia viungo wana vigezo vya vya kupima kutokana na nafasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
DOOOH. Wacha yangu yawe macho na masikio tu maana kwenye huu uzi nitayaona mengi hasa kutoka kwa Watani zangu hali ya kuwa hata mpira haujachezwa bado. Teh

Haya Mujitahidi Mujae Uwanjani basi msiishie hapa.

"DAIMA MBELE NYUMA MWIKO"
Mtani vipi ushapata tikiti kesho tuonane?
 
Back
Top Bottom