Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Wenzangu wengi wameshachangia kuhusu kilichotokea jana cha mwanajeshi anayetwa Shimbo kuwatisha wananchi. Nimejaribu kufikiri kwa undani kwa nini iwe sasa? Ninavyojua mimi jeshi la wananchi linatakiwa liingilie mambo ya ndani pale ambapo situation itakuwa desperate kwamba hata polisi wameshindwa kufanya kazi. Hali kama hii hatujaifikia, kwa maana ya kwanza wamedharilisha jeshi la polisi kwamba limeshindwa kazi. Pili wamekiuka maadili ya kazi yao ambao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi. Kikubwa zaidi nilichogundua ni kwamba kuna mpango ambao ni coordinated na baadhi ya vyombovya habari. Kwa mfano wakati ITV inatangaza habari hiyo liweka picha za wanajeshi wakiwakamata raia wakiwa wameinua miono juu!. Kwa hiyo huu ni mpango zaidi ya wanajeshi.Cha msingi hawa wanajeshi watambue kwamba raia w sasa hivi hawatishwi hovyo tunataka haki mambo ya kuleta amani kwa mtutu hatutaki na kwa hiyo tamko lao halikuwa na ulazima zadi ya wao kutumika kama papet wa CCM jambo linaloshusha heshima ya jeshi.Navishauri vyama vya ushindani kuufahamisha umoja wa Africa (AU), Umoja wa mataifa (UN) NA nchi wafadhili wafahamu mambo yanayoendelea behind the scene as a preemptive move.Namalizi kusema kwamba wanajeshi wamerukia yasiyoahusu kwa sasa.
 
Wenzangu wengi wameshachangia kuhusu kilichotokea jana cha mwanajeshi anayetwa Shimbo kuwatisha wananchi. Nimejaribu kufikiri kwa undani kwa nini iwe sasa? Ninavyojua mimi jeshi la wananchi linatakiwa liingilie mambo ya ndani pale ambapo situation itakuwa desperate kwamba hata polisi wameshindwa kufanya kazi. Hali kama hii hatujaifikia, kwa maana ya kwanza wamedharilisha jeshi la polisi kwamba limeshindwa kazi. Pili wamekiuka maadili ya kazi yao ambao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi. Kikubwa zaidi nilichogundua ni kwamba kuna mpango ambao ni coordinated na baadhi ya vyombo vya habari. Kwa mfano wakati ITV inatangaza habari hiyo liweka picha za wanajeshi wakiwakamata raia wakiwa wameinua miono juu!. Kwa hiyo huu ni mpango zaidi ya wanajeshi.Cha msingi hawa wanajeshi watambue kwamba raia wa sasa hivi hawatishwi hovyo tunataka haki mambo ya kuleta amani kwa mtutu hatutaki na kwa hiyo tamko lao halikuwa na ulazima zadi ya wao kutumika kama papet wa CCM jambo linaloshusha hadhi na heshima ya jeshi.Navishauri vyama vya ushindani kuufahamisha umoja wa Africa (AU), Umoja wa mataifa (UN) na nchi wafadhili wafahamu mambo yanayoendelea behind the scene as a preemptive move. Jumuiya ya kimataifa ifahamishwe kwamba there is a premeditated intention of influencing the outcome of electionNamalizi kusema kwamba wanajeshi wamerukia yasiyowahusu kwa sasa.
 
[FONT=Arial, sans-serif]Hii nimeipata sasa hivi
[/FONT]
Vyombo vya ulinzi na usalama nchini Tanzania vimewataka viongozi wa vyama vya siasa nchini kukubali matokeo ya uchaguzi mkuu yatakayotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi NEC na kutothubutu kupinga matokeo hayo na kusababisha vurugu.

Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Luteni Jenerali Abdurahmani Shimbo ametoa tamko hilo leo Jijini Dar-Es-Salaam kufuatia kuwepo kwa taarifa za vyama vya kisiasa kujiandaa kukataa matokeo yatakayotangazwa na tume ya uchaguzi.

Luteni Jenerali Shimbo amesema vyombo vya usalama vimejipanga kukabiliana na hali yoyote ya vurugu ambayo itajitokeza na kuwaonya watu kutoshiriki katika vurugu zozote baada ya kutangazwa matokeo.

Duh huyo jamaa mbona anaanza kuingilia kazi za polisi wakati hazimhusu au IGP ameshindwa kazi....awaambie NEC wasifanye uchakachuaji kama hataki watu wakatae matokeo
 
Wenzangu wengi wameshachangia kuhusu kilichotokea jana cha mwanajeshi anayetwa Shimbo kuwatisha wananchi. Nimejaribu kufikiri kwa undani kwa nini iwe sasa? Ninavyojua mimi jeshi la wananchi linatakiwa liingilie mambo ya ndani pale ambapo situation itakuwa desperate kwamba hata polisi wameshindwa kufanya kazi. Hali kama hii hatujaifikia, kwa maana ya kwanza wamedharilisha jeshi la polisi kwamba limeshindwa kazi. Pili wamekiuka maadili ya kazi yao ambao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi. Kikubwa zaidi nilichogundua ni kwamba kuna mpango ambao ni coordinated na baadhi ya vyombo vya habari. Kwa mfano wakati ITV inatangaza habari hiyo liweka picha za wanajeshi wakiwakamata raia wakiwa wameinua miono juu!. Kwa hiyo huu ni mpango zaidi ya wanajeshi.Cha msingi hawa wanajeshi watambue kwamba raia wa sasa hivi hawatishwi hovyo tunataka haki mambo ya kuleta amani kwa mtutu hatutaki na kwa hiyo tamko lao halikuwa na ulazima zadi ya wao kutumika kama papet wa CCM jambo linaloshusha hadhi na heshima ya jeshi.Navishauri vyama vya ushindani kuufahamisha umoja wa Africa (AU), Umoja wa mataifa (UN) na nchi wafadhili wafahamu mambo yanayoendelea behind the scene as a preemptive move. Jumuiya ya kimataifa ifahamishwe kwamba there is a premeditated intention of influencing the outcome of electionNamalizi kusema kwamba wanajeshi wamerukia yasiyowahusu kwa sasa.
Maoni yako ni mazuri sana broda, ila kuna threads nyingi zilizofunguliwa juu ya hii maneno, ungechangia kule!...just an advice!
 
Maoni yako ni mazuri sana broda, ila kuna threads nyingi zilizofunguliwa juu ya hii maneno, ungechangia kule!...just an advice!

Ni kweli, ndo nalalamiakia mambo anayofanya Malaria Sugu, post zinakuwa nyingi bila sababu. Sasa anajisifia juu ya ushauri ulioutoa kuhusu kugonga ignore, kwamba "Kugonga mtagonga sana..." Huu ni utoto.
 
wametumwa, kwanza wengi wao nao wanataabika vilevile .wachache ndio wanakula urefu wa kamba zao
 
Sio tu haikuwa lazima, ni ukiukwaji wa kila kitu. JWTZ linatakiwa kutulinda dhidi ya maadui wa nje ya mipaka - nukta.
 
Wanaandaa mazingira ya kuiba kura na kujiapisha one day after. Jeshi kazi yake kulinda mipaka. mambo ya ndani kwani wizara haipo!? Shimbo mnajimu tu!! Aibu kuwa na askari aliyetekwa na siasa. askari ni mwamuzi wa mwisho wa haki. Mwl.Nyerere aliunda jeshi la wananchi na sio jeshi la chama. Lakini Dr.Slaa ataunda jeshi upya maana mwaka huu sio tofauti na tulivyopata uhuru toka kwa wadhalimu kama walivyo ccm.
 
Njia pekee ya kuinusuru Tanzania na michezo ya rafu ambayo ni dhahiri sasa ni kukimbilia kwa Umoja wa Mataifa na Balozi marafiki kuwataka wakemea kinachoendelea sasa. Sioni ndani ya kauli za huyu Mnajimu(call him anything) chochote kinachotokana na yeye binafsi bali yeye amekuwa kinywa cha kinachozungumziwa. JK jana tu katika hotuba zake amewaambia wapiga kura wawakwepa wapinzani ambao wao alidai wanataka kumwaga damu. Haiwezekani kauli kama hizi (soma magazeti ya leo, 2 okttoba) zisiwe na uhusiano na hayo aliyoyatangaza (ametangaza sio ametoa maoni yake binafsi) Mnadhimu Mkuu wa Majeshi.

Tuanzie wapi!? Tuanzie wapi? Pengine ni Lipumba na Slaa ndio watatusaidia kuliweka hili wazi mbele ya wenzetu, sio swala la kupigania kutoka ndani, ni lazima twende the Hague, maskini JK anataka aishie huko??????
 
Kama wana nguvu si waende somalia wakatulize fujo? Ndo tuone kuchapo hasa, si kuwakwida watz wasokuwa na silaha eti kwakuwa wanampenda Slaa?
 
Mimi nadhani umefika wakati sasa wa Dr. Slaa kuendeleza focus ya agenda yake ya kampeni, naona sasa amekua anajibujibu tu na hiyo si lazima... akumbuke kwamba hizo hoja anzojibu ndio destructive to his focus.... UTAJIBU KILA HOJA KWELI?

Tupe sera na mipango ya kutuondolea uozo kama TRA, Bandari, reli, kilimo, elimu, afya, miundombinu, utendaji mbovu wa watumishi wa serikali, rushwa, mauaji, uchawi na ulinzi na usalama

ukishaanza kujibishana na jeshi la ulinzi, basi usitegemee kuwa amiri jeshi mkuu... WATCH OUT NOW!!!

Mkuu,

Kuna msemo mmoja wa Kiingereza ambao ntautafsiri kwa Kiswahili unaokwenda kama hivi: Uongo una tabia moja mbaya sana.Ukiachwa bila kukanushwa au kukumewa una tabia ya kujitambulisha kama ukweli.

Ni sawa kuwa DKT sLAA anatakiwa a-focus zaidi kwenye kampeni,na hicho ndicho kinachomzungusha sehemu mbalimbali za nchi yetu.Sasa unaposema akupe sera na mipango,una maana HAJAWAHI KUTOA SERA NA MIPANGO YA SERIKALI YA CHADEMA au?Maana katika kila mkutano anawaeleza wapiga kura kwanini wamchague yeye na wamtose Kikwete.Au Mkuu kuna unalotaka kuskia kutoka kwake na hajalisema?

Mgombea yoyote yule mwenye akili timamu hawezi kukaa kimya wakati wapiga kura wanatishwa na vyombo vya dola.Hizo sera na mipango atakazotoa zitamsaidia vipi kushinda iwapo vitisho kama vya huyo afande wa JWTZ vitapelekea baadhi ya watu kuamini kuwa Chadema ni chama cha fujo?

Kumbuka,kila hoja inapaswa kujibiwa kwa hoja na hilo ndilo analofanya Dkt Slaa.Na si kujibu hoja tu bali pia kueleza nini atawafanyia Watanzania.

With all due respect,nadhani lawama zako ni misguided.Yani kwa busara zako jeshi la ulinzi,au polisi,au usalama wa taifa wakitumika kwa maslahi ya mafisadi basi Slaa akae kimya kwa vile akisema lolote hatoweza kuwa Amiri Jeshi Mkuu?

Kweli safari ya ukombozi bado ni ndefu
 
Sikuwahi kuona popote pale duniani ambapo jeshi linatoa kauli dhidi ya Raia wakati Rais akiwa bado yupo madarakani. Mara nyingi jeshi linaposimama kuongea na raia huwa ni katika hali ya hatari kuwepo katika hali ya janga (tetemeko, mafuriko, moto nk). Au wakati Rais ameshapinduliwa au yupo mbioni kupinduliwa. Rais ndiye amiri jeshi mkuu wa majeshi yote, na mwanye mamlaka ya kutoa kauli yoyote ya JWTZ kwa wananchi ni ama waziri wa ulinzi au Rais na si mkuu wa majeshi wala kiongozi yeyote wa jeshi la Wananchi, except in the state of emergence or catastrophe.

Ni ajabu sana kuona mnadhimu mkuu wa jeshi la wananchi ndiye anayeongea na wananchi hii ni ajabu kubwa. Na inawezekana kwamba jeshi limegundua kwamba Rais aliyeko madarakani ni bushoke (mwanaume....). Hana uwezo wa kutoa kauli wala kukemea juu ya mambo yanayoihusu nchi. Hapa si tu jeshi limejidhalilisha, bali pia limevuka mipaka ya mamlaka yake na limemdharau na kumdhalilisha Rais wa nchi.
 
Hawa jamaa mbona wana jihami kiasi hiki? Kama wanauwezo wa kutuliza ghasia waambie waende Somalia wawatuliza al shababu ndo tuwakubali!
 
Hivi Jenerali Shombo alipata cheo kwa merit au ????

Heshima kwako August,

Mkuu wangu Lt Gen A Shimbo alikuwa msaidizi wa waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa enzi za msomali A kinana.
 
Mtu mzima hatishiwi nyau, hawa wametumwa tu na kuanza kuleta mkwara kuwa hata CCM wakiiba kura watu wasiseme au kuandamana, sisi tunasema HATUOGOPEEEEEEEEEEEE KISHA HATUDANAGANYIKIIIIIIIIIIII.
 
Dr Slaa atakuwa na kazi kubwa sana, hapo atakapochukua nchi, maana nchi nzima inahitaji kujengwa upya, maaana UWT, JWTZ, Police, Mhakama na idara zote za Tanzania zinahitaji kuvunjwa na kujengwa upya, idara zote zinahitaji watu wapya wasio na harufu yoyote ya kutumiwa au kulipa fadhira
 
Watanzania jamani msishabikie ujinga,leo mnaona majeshi yetu mabaya kwa kuwa mnaushabiki wa kisiasa,natakakuwaambia kama mnatka kujua nini maana ya kupotea kwa amani endeleeeni kuwashawishi watu kubeba mapanga na visu kudai udiwani na ubunge.nchi hii haiwezi kuangalia kaundi ka wachaga na wamasai wachache wanaotaka madaraka kwa nguvu kuipeleka kusiko takiwa ,mimi nazani muda umefika wote wanaotoa kauli kama za mbowe na slaa waakamatwe.
Nchi haitakombolewa na cowards kama wewe. Keep quite if ur such a coward.
 
Nadhani kwa hali kama hii wataweza tu kuwatisha wananchi!
 
Wenzangu wengi wameshachangia kuhusu kilichotokea jana cha mwanajeshi anayetwa Shimbo kuwatisha wananchi. Nimejaribu kufikiri kwa undani kwa nini iwe sasa? Ninavyojua mimi jeshi la wananchi linatakiwa liingilie mambo ya ndani pale ambapo situation itakuwa desperate kwamba hata polisi wameshindwa kufanya kazi. Hali kama hii hatujaifikia, kwa maana ya kwanza wamedharilisha jeshi la polisi kwamba limeshindwa kazi. Pili wamekiuka maadili ya kazi yao ambao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi. Kikubwa zaidi nilichogundua ni kwamba kuna mpango ambao ni coordinated na baadhi ya vyombo vya habari. Kwa mfano wakati ITV inatangaza habari hiyo liweka picha za wanajeshi wakiwakamata raia wakiwa wameinua miono juu!. Kwa hiyo huu ni mpango zaidi ya wanajeshi.Cha msingi hawa wanajeshi watambue kwamba raia wa sasa hivi hawatishwi hovyo tunataka haki mambo ya kuleta amani kwa mtutu hatutaki na kwa hiyo tamko lao halikuwa na ulazima zadi ya wao kutumika kama papet wa CCM jambo linaloshusha hadhi na heshima ya jeshi.Navishauri vyama vya ushindani kuufahamisha umoja wa Africa (AU), Umoja wa mataifa (UN) na nchi wafadhili wafahamu mambo yanayoendelea behind the scene as a preemptive move. Jumuiya ya kimataifa ifahamishwe kwamba there is a premeditated intention of influencing the outcome of electionNamalizi kusema kwamba wanajeshi wamerukia yasiyowahusu kwa sasa.

katika siku ambayo, nilipigwa bumbuwazi , kuhusu jeshi la wananchi ni jana.
 
Lakini katika nchi yenye demokrasia nzuri kama Tanzania, jeshi la ulinzi is supposed to be neutral kwa sababu ni jeshi la watanzania wote
 
Back
Top Bottom