Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

jk ndiye amiri jeshi mkuu huenda shimbo amefanya hivyo kwa maelekezo ya boss wake.
 
Nimeona hawa majamaa wanatupiga mkwara kuelekea uchaguzi sasa naomba kupatiwa CV ya meja jenerali Abdulhaman Shimbo
 
shimbo asileta mambo yake ya ushoga hapa pumbavu zake..ujinga wake huko huko na bosi wake mwamunyange mrembua macho...Rais wanayemtaka hapiti na ni mgonjwa wasitulazimishe kuchagua maiti iliyo hai...Dr.Slaaa goo gooo goo!!!
 
yaaani JK chupi inambana sasa kila akipiga hesabu haziendi ...jeshi lenyewe la kutisha watu liko wapi walevi wa komoni tupu..kutwa tuko nao kwenye supu za makongoro pale Mary land ,,,
 
Hivi CCM na vibaraka vyake(Polisi,Jeshi na Usalama wa Taifa) wanataka kuipeleka wapi Tanzania??????????????

Tamko la mjeshi Shimbo kwa wadhifa wa Mnadhimu wa Jeshi umeniacha hoi. Ni dhahiri kabisa Shimbo ametumwa na Amiri Jeshi mkuu wa sasa anayemaliza muda wake ambaye ni mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM!Shimbo hajakurupuka,ametumwa tena si na Kikwete tu baali na uongozi wa Ngazi za juu kabisa wa CCM.

Nachelea kusema kuwa wimbo wa Tanzania ni nchi ya Amani,Upendo na Mshikamano unaenda kufutwa kwenye vitabu vya historia ya nchi hii. Hakuna Amani tena, Hakuna Upendo tena. Hakuna Mshikamano tena. Viti hivi ameondoka navyo Baba yetu kipenzi, Baba wa Taifa Letu marehemu Julius Kambarage Nyerere.(Mungu ailaze roho yake pema peponi). Na ndiyo maana kabla ya kifo chake alisema tutamkumbuka sana na tutamlilia sana. Amani imemalizwa na Chama cha Majambazi-CCM). No more love,no more peace no more solidarity. Tanzania is doomed! Finished!
Ukisoma katika ya mistari ni dhahiri kabisa kuwa CCM WAMEKUBALI KUSHINDWA MAPEMA HATA KABLA YA UCHAGUZI. Nitaeleza.

Baada ya CCM kuona hali ya hewa imebadilika na kusoma alama za nyakati kwa Uchaguzi Mkuu 2010 wamejua kabisa kuwa mwaka huu lazima CCM watapigwa mwereka vibaya na vyama vya upinzani vikiongozwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA).

Hii hali ni wazi na dhahiri kabisa kwa kila mtu na CCM wanajua hivo. Kwa hiyo CCM wanachofanya sasa hivi ni kujaribu kutumia mbinu za kila namna kuanzia kwenye kuchakachua matokeo,kuiba kura,kutumia vyombo vya usalama ikiwamo Polisi, Mashushu,JWTZ na viongozi wa kada mbalimbali wakiwemo wakurugenzi wa Wilaya na Mikoa.

Mbinu zote za CCM za kuiba na kuchakachua matokeo ya kura zimegundulika mapema sana. Kwa hiyo CCM wameamua sasa kutumia Jeshi la Wananchi ili kuwatisha Watz na hasa WAPIGA KURA.

Tangu nchi yetu hii ipate uhuru toka enzi za mwalimu sikusikia JWTZ wanazungumzia Uchaguzi Mkuu, hii ni kwa mara ya Kwanza Jeshi la Wananchi Tanzania kujiingiza kwenye maswala ya Uchaguzi Mkuu.

KWANINI JWTZ MWAKA HUU?
Imeonekana kwamba Polisi hawataweza kuuthibiti umma wa Watanzania wenye hasira siku ya uchaguzi kama matokeo ya Uchaguzi yatachakachuliwa. Chaguzi zote zilizopita CCM ri hii kuna upinzani mkali na Watz wameshapata mwamko wa kisiasa kwa hiyo si rahisi kuwarubuni. Kwa hiyo CCM wameamua kuandaa JWTZ ili iwasaidie kupitisha matokeo yao.

Hii inadhihirisha kwamba MATOKEO YA CCM TAYARI YALISHAANDALIWA KWA HIYO KINACHAFANYIKA HAPA NI KUTAFUTA MBINU ZA KUHALALISHA MATOKEO HAYO YA KUPIKA AU KUCHAKACHUA.

OMBI: Naomba jumuia za kimataifa na nchi rafiki wa Tanzania zenye kuitakia amani nchi hii waanze kufuatilia Uchaguzi Mkuu wa Tanzania kwa karibu sana. Mimi naamini kuna Waangalizi wa kimataifa(Election Observers) ambao huteuliwa aidha na jumuia za kimataifa kuja kuangalia uchaguzi unavofanyika.

Natoa ombi hili kwa masikitiko makubwa kwani nahisi kuwa safari hii kuna hatari ya kupatwa na ayale yaliyotokea Z'bara mwaka 2005 na hasa kile kilichotokea kwa jirani zetu Kenya!!!!Hali hii inaanza kuwa tete sana hasa baada ya JWTZ kuanza kuingilia mambo ya Uchaguzi. Kama ndugu zangu mna jamaa zenu nje ya nchi hii nzeni kujiandaa kuwa wakimbizi baada ya 31/10/2010.

Kama CCM watashindwa basi hii nchi haitakalika. CCM wako tayari kumwaga damu za Watanzania ili watawale nchi hii. Kila mmoja ni shahidi ya kile kilichotokea pale Zanzibar mwaka 2005 tena. God forbid!
 

Heshima kwako August,

Mkuu wangu Lt Gen A Shimbo alikuwa msaidizi wa waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa enzi za msomali A kinana.
aisee! na Mwamunyange akiwa kama CDF anakuwa na kilaza kama huyu nae anashindwa ku-discipline? au nae sio kwa merit? ingawa namuona ni kama kwa merit, basi amfuate Amiri Geshi mkuu na kumueleza anakkoipeleka nchi siko? nasikia Kiaro/Msuguri aliwahi mfanyia Alhaji Ali Hassan Mwinyi. na pia waelewe hili tatizo halipo juu juu tu wasipoangalia hizi kambi za Jeshi zitakuwa kama Somalia
maana kuna wanaopinga haya yanayo tamkwa na Shombo, na kuna wale bila kuelewa watamtetea Shombo
 
Dr Slaa amshukia Shimbo wa JWTZ
MGOMBEA wa urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Willibrod Slaa amesema kitendo cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuingilia siasa kwa vitisho ni kielelezo kingine kwamba serikali inafanya jitihada za kuhujumu uchaguzi kukinusuru Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Akihutubia umati wa wananchi waliofika kumsikiliza, Dk. Slaa alitoa siku kwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema kuwakamata watu wote waliotishia kumwaga damu dani ya siku saba
Hata hivyo alimtaka Shimbo kuwaomba radhi watanzania kwa vitisho alivyotoa katika kipindi hicho cha siku saba huku akijinasibu kuwa kuna uwezekano wa yeye kupita bila bingamizi kama serikali ya CCM itaendelea na vitisho kama hivyo
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo katika viwanja vya Mdete Wilayani Njombe akiwa katika mwendelezo wa kampeni zake katika Mkoa wa Iringa.
Dk. Slaa alisema kitendo cha Luteni Jenerali Shimbo hakupashwa kutoa kauli kama hiyo kwa kuwa ni vitisho kwa watanzania hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi na kwamba kauli kama hiyo ilipaswaitolewe na IGP Mwema kwa maana ya kushughulikia watu wanaotaka kuvunja amani ya nchi.
“Tunalitaka jeshi la Ulinzi na Polisi kuwakamata wale wote waliotoa kauli ya kutaka kumwaga damu…kama halitafanya hivyo, tujue ni propaganda chafu za Kikwete na vyombo vyake vya usalama za kuiba kura na kutaka kuvunja amani.
Alisema yeye kama Dk. Slaa asingependa kuwa rais wa Tanzania kwa watanzania kumwaga damu lakini anatambua kuwa kauli kamahizo ni mbinu za CCM za kutaka kuchakachua matokeo ya katika uchaguzi mkuu.
Dk. Slaa alisema atahakikisha watanzania hawadanganyiki na kauli za viongozi mbalimbali wakiwemo wale wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao wamekuwa wakitumika kisiasa kutaka kuisaidia CCM ambayo inaonekana kushindwa kwa kutoa kauli za vitisho na nyaraka mbalimbali za kutaka kusaidiwa.
“nataka kumwambia Bwana Shimbo kama hajui Siasa atuachie mwenyewe nay eye arudi kambini kuendelea na kazi yake badala ya kutumika kutoa vitisho kwa watanzani ambao wamechoka kubebwa katika malori kwenda katika mikutano ya CCM….lakini hii ni dalili kuwa mgombea urais wa CCM na chama chake wameona hali ni mbaya kwao”

Hata hivyo alisema kwa hofu za mgombea wa CCM Kikwete kwa kutumia vyombo vya dola kutisaha ni sawa na kuonyesha kushindwa kabla ya dakika 90 na kumtaka afanye kampeni za kunadi sera badala ya kutumia vyombo vya dola kumfanyia kampeni za kutisha watanzania ambao kwa sasa hawapotayari kudanganywa na vitisho vya CCM

Aidha alimtaka aliyekuwa naibu spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania na mbunge wa jimbo la Njombe kusini Anne Makinda kuacha kuendelea kuwatisha wananchi wa jimbo hilo na kudanganya umma kuwa yeye ni mbunge wa kupita bila kupingwa na kuwa hiki ni kipindi chake cha mwisho na kama mwaka 2015
 
Sina uhakika lakini huenda ni mmojawapo waliofanikisha lile dili la meremeta.
 
Ukiona hivyo ujue wameshaona kuna sehemu lazima kuiba kura , sasa wanataka ku-justify nguvu watazotumia kama kukiwa na upinzani toka kwa wananchi. Mwenye akili anauweza ona hili mapema. Ama kweli mafisadi wana nguvu!
 
Mitumishi ya umma hapa kwetu mingine ni mijinga. Nililiona hilo li Shimbo linakenua kenua mijimeno kwenye TV, wala halijui madhara ya kutumika na mafisadi. Ni lini jeshi likajibu tuhuma za kisiasa? pambafu kweli!
 
Nimeona hawa majamaa wanatupiga mkwara kuelekea uchaguzi sasa naomba kupatiwa CV ya meja jenerali Abdulhaman Shimbo
Atakua kilaza tu, Ila Mkewe nilisikia alikua ni mwanamke wa pili kuwa na strong PhD ya sc & Eng, Barani Africa coz Kabinti ka huyu jamaa
Nilishawahi...:tonguez:. sijui zilikua ni story...
 
Atakua kilaza tu, Ila Mkewe nilisikia alikua ni mwanamke wa pili kuwa na strong PhD ya sc & Eng, Barani Africa coz Kabinti ka huyu jamaa
Nilishawahi...:tonguez:. sijui zilikua ni story...
Ila kale kabinti kalikua ni ka Kristu but somebody shimbo na mzee wake ni mjeda, kitambo kidogo. sasa sijui ndo huyu...
 
SHIMBO HIZI NDOSHUGHULI ZAKO ZA KUSIMAMIA



Miaka 44 ya JWTZ
JWTZ limepata mafanikio lukuki
o Kwa kulinda mipaka, watu na mali
o Kusaidia Ukombozi wa Afrika
o Kushiriki katika Ulinzi wa amani
o Uokoaji wakati wa maafa
Kila ifikapo Septemba Mosi ya mwaka, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) huadhimisha sikukuu ya kuanzishwa kwake miaka 44 iliyopita yaani Septemba Mosi 1964.
Kuanzishwa kwa jeshi hilo la kizalendo, ambalo jukumu lake la msingi ni ulinzi wa mipaka ya nchi, watu na mali zao pamoja na rasilimali za taifa ndiko kumeifikisha Tanzania hapa ilipo likiwa ni taifa la kupigiwa mfano kwa amani, usalama na utulivu.
JWTZ lilianzishwa mwaka 1964 baada ya maasi ya jeshi la Tanganyika yaani Tanganyika Rifles (TR) ambalo lilirithiwa kutoka kwa wakoloni na kuasi miaka minne tu tangu Tanganyika (Tanzania Bara) ipate uhuru wake.
Maasi hayo ambayo yalitokea wakati taifa likiwa bado changa, yalileta mashaka, hofu na wasiwasi mkubwa hasa katika jiji la Dar es Salaam.
Sababu za maasi ya vikosi vya TR zilikuwa nyingi ikiwemo kuboreshewa mishahara na marupurupu pia makamanda wa Kiafrika kupewa hadhi sawa na makamanda wa Kizungu.
Itakumbukwa kuwa baada ya Tanganyika kupata uhuru wake Disemba 9,1961, vikosi vya King's African Rifles (KAR) vilibadilishwa jina na kuwa vikosi vya ulinzi wa Tanganyika yaani Tanganyika Rifles (TR), lakini sheria, kanuni na taratibu za uongozi zilibaki zile zile za wakati wa ukoloni.
Aidha, makamanda wake wote akiwemo Mkuu wa Majeshi alibakia yule yule wa KAR yaani Brigedia Jenerali Sholto Douglass huku makamanda wa kizungu wakiwa wameshikilia nyadhifa mbalimbali za juu jeshini.
Kutokana na hali hiyo, wanajeshi wazalendo hawakuna na namna ya kuwasilisha matakwa yao ya kutaka mabadiliko kwa uongozi wa kitaifa na kuamua kuasi Aprili 19,1964.
Maasi hayo yalianzia katika kikosi cha Colito (Lugalo) Dar es Salaam na kuungwa mkono na vikosi vya Kalewa (Mirambo) Tabora na Godar (Nachingwea) hali iliyoleta hofu, mashaka na kuwafanya watu kukimbia ovyo.
Maasi hayo ya kukataa kunyanyaswa na makamnda wa kizungu yaliyodumu kwa siku kadhaa na kuzimwa na kikosi cha makomandoo kutoka Uingereza cha Royal Marine Comandoes hali inayoweza kutafsiriwa kama Waingereza walikuja kuokoa wenzao.
Baadaye makamanada hao walirejeshwa kwao huku kikosi kutoka Nigeria kilipewa jukumu la kufundisha jeshi jipya ambalo lilipewa jina la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).


Kuundwa kwa JWTZ

Itakumbukwa kuwa siku chache baada ya maasi hayo, Tanganyika na Zazibar ziliungana aprili 26,1964 na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao ni muungano wa pekee barani Afrika.
Kutokana na muungano huo, vijana wapatao 1000 waliandikishwa kutoka bara na visiwani wakiwemo vijana kutoka chama cha Tanganyika African Union (TANU) cha Tanzania bara, vijana kutoka chama cha Afro Shiraz Party (ASP) kutoka Zanzibar na kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Vijana 30 kati ya hao walikuwa wanawake sawa na asilimia 30 ya wanajeshi wapya.
Mafunzo ya awali ya 'kuwanoa" askari wapya yalifanyika chini ya makamanda kutoka Nigeria na kuhitimu rasmi Septemba Mosi 1964 na kula kiapo cha utii na uaminifu mbele ya Amiri Jeshi Mkuu wa kwanza, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Tangu hapo JWTZ likaanza kuandika historia mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo ukombozi wa bara la Afrika, ushindi wa vita ya Kagera, nidhamu na utiifu, uokoaji wakati wa majanga, ulinzi wa amani na hivi karibuni ukombozi wa kisiwa cha Anjouan.
Ukombozi wa Afrika
Baada ya kuhitimu mafunzo hayo, jeshi hilo lilianza kazi ya ulinzi wa nchi lilikiwa pia na jukumu la kusaidia ukombozi Kusini mwa Afrika ikiwemo Msumbiji, Afrika Kusini, Angola, Namibia, Zimbabwe na nchi nyingine kwa kutoa mafunzo ya kijeshi kwa wapigania uhuru wa nchi hizo.

Tanzania ilianzisha makambi katika sehemu mbalimbali nchini kwa ajili ya kuwafundishia ikiwemo Kongwa Dodoma, Mgagao Kilolo Iringa, Farm 17 Nachingwea, Masonya Tunduru, Shelala Lindi, Kidogozero Pwani, Pongwe Msungura Msata Pwani, Mkuyu Tanga, Matekwe Songea likuyu sekamaganga Namtumbo Ruvuma na nyinginezo
Aidha, Wapiganaji walifunzwa nchini waliongeza vuguvugu la ukombozi katika nchi zao kwa kuanzisha mapigano yaliyozikomboa nchi hizo kutoka katika minyororo ya ukoloni na ubaguzi wa rangi na kufanikisha nchi zote kujikomboa hadi kufikia mwaka 1975.


Jeshi la Kujenga taifa JKT

Mapema mwaka 1963 lilianzishwa Jeshi la Kujenga Taifa hapa nchini kwa lengo la kuwalea vijana kwa kuwafundisha umoja na uzalendo, kuwafundisha mbinu za uzalishaji mali na mafunzo ya ulinzi.
Kuanzia mwaka 1964 JWT ilisaidia pia kutoa mafunzo ya kijeshi kwa vijana wa JKT kazi ambayo inaendelea hadi sasa.
Mgambo
Jukumu jingine la JWTZ ilikuwa ni kuwashirikisha wananchi katika ulinzi wa taifa kwa kufundisha jeshi la mgambo. Jukumu hilo ambalo lilipata muitikio mkubwa lilifanyika katika mikoa yote na watu kwa maelfu walipata mafunzo hayo.
Matunda ya kazi hiyo yalionekana mwaka 1978 pale majeshi ya Iddi Amini wa Uganda yalipovamia na kuchukua eneo la Kaskazini la mto Kagera mwaka 1978 na jeshi la Mgambo kushirikiana na JWTZ katika kutoa "Dozi" kwa majeshi ya adui.
Kwa kuwashirikisha Mgambo, Tanzania ilionesha kwa vitendo kuwa kweli jukumu la ulinzi ni wa nchi ni la wananchi wote.
Vita vya Kagera
Kama ilivyoelezwa awali, mtihani wa kwanza wa JWTZ ulikuwa mwaka 1978 pale vikosi vya Dikteta Idd Amini vilipovamia na kuteka Kaskazini ya mto Kagera na kutangaza kuwa eneo hilo ni lao.
Kutokana na uchokozi huo, Amiri jeshi Mkuu wa kwanza Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alitangaza vita dhidi ya jeshi la uvamizi na kuwahakikishia wananchi kuwa, "Tanzania kupitia JWTZ ilikuwa na nia ya kumpiga, sababu ya kumpiga na uwezo wa kumpiga Iddi Amini na vikosi vyake.
Baada ya hapo Tanzania iliingia vitani Novemba mwaka 1978 na kwa kipindi kifupi majeshi ya Amini kwanza yalitolewa katika eneo la Kagera baada ya kipigo na hatimaye kazi ya kumuondoa Amini ilifanyika ndani ya nchi yake.
Mashujaa wa vita hivyo walirejea nchini na kupokelewa rasmi na amiri Jeshi Mkuu wa kwanza Hayati Julius nyerere katika eneo la Bunazi julai 25, 1979 siku ambayo sasa ni sikukuu ya mashujaa.
Kwa kuyashinda majeshi ya Nduli Amini JWTZ iliandika historia nyingine ya kuwa makini katika ulinzi wa nchi kwa kutekeleza jukumu lake la msingi la kulinda nchi, mipaka yake, watu na mali zao.
Kusaidia Msumbiji
Pamoja na majukumu yake ya msingi ya kulinda nchi JWTZ pia ilishiriki katika kusaidia ulinzi wa nchi nyingine za Kiafrika kwa mfano kuanzia mwaka 1976 nchi ya Msumbiji ilipambana na waasi wa Renamo ambao walitishia uhuru wa taifa hilo.
Katika harakati hiyo, wanajeshi wa Tanzania zaidi ya 101 walipoteza maisha yao na kuzikwa katika majimbo mbalimbali ya Tete, Manica, Qulimani. Mabaki ya miili ya wahanga hao zilizikwa upya katika eneo la Naliendele Mtwara Septemba Mosi, 2004.


Ulinzi wa amani

Jeshi la Ulinzi laWananchi wa Tanzania (JWTZ) pia limeshiriki katika ulinzi wa amani duniani mara ya kwanza mwaka 1993-95 nchini Liberia na hatimaye nchi hiyo kufanya uchaguzi wa kidemokrasia.
Aidha kuanzia mwaka 2007 wanajeshi wa JWTZ wameshiriki kama sehemu ya majeshi ya kulinda amani nchini Lebanon. Kazi ambayo inafanyika kwa kwa ufanisi mkubwa.
Ukombozi wa Anjouan Comoro
Vilevile Tanzania iliweka historia mwaka huu Machi 25, 2008 pake vikosi vya Tanzania vilipoongoza majeshi ya Afrika katika kukikomboa kisiwa cha anjouan. Katika vita hivyo vya kisayansi, majeshi ya AU yalipenya hadi ndani nya kisiwa na kuzingira maeneo yote mhimu.
Tendo hilo la kijasiri liliyaacha mataifa mengine yakiwa midomo wazi kwa mshangao kwani kwa kawaida silaha kubwa ikiwemo mizinga, ndege na hupiga kwanza kabla ya vikosi vya miguu kukamata eneo husika. Hiyo iliwezekana kwa Tanzania kutumia Makomando wake kuzingira eneo bila kutumia silaha kubwa.
Kutokana na ujasiri huo, JWTZ iliandika historia ya kupata ushindi bila kuua wala kuharibu mali za wananchi jambo ambalo ni nadra sana kutokea katika vita.
Aidha ujasiri wa JWTZ na Tanzania ni wa kihistoria tangu wakati wa mababu ambao waliosimama kidete kutetea heshima ya taifa letu na kupigana kiume dhidi ya wakoloni wa Kijerumani.
Mashujaa hao ni pamoja na Chifu Mkwawa wa Wahehe, Abushiri wa Pangani, Kinjeketile Ngwale wa Kilwa na wote wote waliojitoa muhanga kulinda heshima na utu wa Mtanzania.
Tunapoadhimisha siku hii tutambue, kuthamini na kuenzi mchango unaotolewa na JWTZ na kuwapa moyo maafisa na wapiganaji kuendelea kulinda mafanikio yetu ambayo yanaifanya Tanzania kuwa nchi ya kujivunia kwa kuwa na amani na utulivu ukilinganisha na nchi nyingi barani Afrika na sehemu nyingine duniani.
Sikukuu ya kuanzishwa kwa JWTZ inatoa funzo kuwa amani, usalama na utulivu uliopo unapaswa kulindwa na kudumishwa kwa faida ya vizazi vijavyo ili nao waje washerehekee kama tufanyavyo sisi.




miaka2.png
miaka3.png
miaka6.png
miaka5.png
 
Wanaandaa mazingira ya kuiba kura na kujiapisha one day after. Jeshi kazi yake kulinda mipaka. mambo ya ndani kwani wizara haipo!? Shimbo mnajimu tu!! Aibu kuwa na askari aliyetekwa na siasa. askari ni mwamuzi wa mwisho wa haki. Mwl.Nyerere aliunda jeshi la wananchi na sio jeshi la chama. Lakini Dr.Slaa ataunda jeshi upya maana mwaka huu sio tofauti na tulivyopata uhuru toka kwa wadhalimu kama walivyo ccm.


Hii sawa
 
Makamba alishasema kila kitu ni chao, Mahakama, Jeshi, Bunge n.k - sasa msishangae matamko kama haya na ndiyo bado chakachua inakuja tukae mkao wa kula.

Nani atakuwa radhi kuachia madaraka kirahisi, kiti amekikalia mwenyewe then ainuke akikabidhi? wakuu tuna safari ndefu - nawapa tahadhali tu kuwa kazi ndiyo kwanza inakaribia inaanza.
 
Gentlemen why dont you see the whole scenario from a fair distance.
It is obvious that the contest in this years election will be too close to call, alarm bells are ringing.
Hence the need to sound the peace bugler, come what may.
Wakuu lets wait for 31st October 2010
 
Kuna wale wanaonufaika na MEREMETA,so si ajabu kusikia maneno kama haya,almost kila idara ya serikali iko corupt na hata jeshi la wananchi kama lile la polisi corruption imeota mizizi. Ni mbinu na mikakati ya ccm ambayo ni well calculated na haijaanza leo....Tumeshuhudia wanajeshi wastaafu wakipewa ukuu wa mkoa na mgodi wa madini uliotekwa na mafisadi "MEREMETA" Kuhakikisha kwamba jeshi lina husika, huu ni mwavuli wa "Siri ya jeshi" wa mafisadi(plus wanajeshi mafisadi)kama Pinda alivyopindisha ukweli!

Jeshi haliwezi kutoa tamko based on harakati za uchaguzi wa kidemokrasi kwa kuwatisha wanasiasa wasipinge matokeo kama wana ushahidi kuwa haki imepindishwa....Ni heri wangesema matokeo yapingwe kwa amani ie kama ikigundulika rigging ilitake place,basi maamuzi stahiki ya kubatilisha matokeo hayo yachukue mkondo wake...Aliyemtuma huyo mjeshi pamoja na mjeshi mwenyewe wamechemsha....Wanawatisha wananchi,hilo tayari ni kosa na linaweza kutumika against chama tawala.Jeshi kusema wananchi wasipinge matokeo hata kama si ya halali ina maana gani?
 
Sasa hivi: Mlimani TV inaonesha watu wakilaani tamko la JWTZ.
 
Tunaenda mbele Luteni jenerali shimbo ni kada wa CCM , alikuwa mkuu wa mkoa wa Arusha kabla ya cheo alicho nacho sasa. Kuwa mkuu wa mkoa lazima uwe mwanan ccm. Sasa anatetea fadhila aliyopewa na sio msimamo wa jeshi kuwa upande wa ccm. Mbona anagombana na chadema wakati CCM ndio wenye jeshi la green card?
 
shimbo asileta mambo yake ya ushoga hapa pumbavu zake..ujinga wake huko huko na bosi wake mwamunyange mrembua macho...Rais wanayemtaka hapiti na ni mgonjwa wasitulazimishe kuchagua maiti iliyo hai...Dr.Slaaa goo gooo goo!!!

yaaani JK chupi inambana sasa kila akipiga hesabu haziendi ...jeshi lenyewe la kutisha watu liko wapi walevi wa komoni tupu..kutwa tuko nao kwenye supu za makongoro pale Mary land ,,,
UH!!!!
mazee punguza munkari tumkome nyani giladi.
tumia lugha nyepesi kwani mara nyingi tukituna tutapasuka mwishoni.
tuwatekenye mpaka wacheke halafu washangae tunamwapisha Slaa kuwa next residaa
 
Back
Top Bottom