Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Nimeipenda sana hii, thanx for reminding gen shimbo. Aliniboa juzi hadi nilitamani Idd Amini Dada afufuke ili awasaidie hawa jamaa zetu wa ami kuondoa vitambi manake wanakaa tu wanakula mishahara bure, ndo maana wanajiingiza ktk siasa. Mwenzao museven kawapeleka hadi somalia wakapate uzoefu wa kukabiliana na Al shabaab wkt sisi hata maghaidi wa meli wanatushinda. Turudishie ushiriki wa mgambo kwa lazima kama zamani ili muwe bize kdg nyie akina shimbo...
 
Maoni yangu mimi, Tanzania inataka kuongozwa kijeshi naona. Sababu ya kusema ni kuwa asilimia kubwa ya wakuu wa mikoa ni wanajeshi, pili wakuu wa wilaya wengi nao ni wanajeshi, tatu naona JWTZ kuanza kutoa vitisho ni dalili tosha za kutaka kuanza kutengeneza njia jeshi la wananchi kuchukua nchi hata kama hakuna vurugu zozote za kutishia amani. Tusubiri tuone mwisho wake itakuwaje!!!
 
Na wana usongo wa kupiga mtu mda mrefu hawajaenda vita.
Wangelikuwa busy na yanayowahusu hilo tamko hata wasingelitoa mi naona wanakula good time tuu mjini.
Kuna haja ya kuwakeep busy kwa kuwapeleka Darfur,Somali
 
JWTZ Lilianzishwa tarehe 01 Septemba, 1964 likiwa na lengo la kulinda uhuru, na mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. JWTZ lina majukumu yafuatayo:
  1. Kutoa msaada unaohitajika kwa mamlaka za Serikali katika hali ya hatari na maafa yatokanayo na nguvu za asili.

Napenda kujua nguvu za asili ni zipi???

  1. Kusaidia uwezo wa mamlaka ya Serikali katika kudhibiti ghasia au vurugu ndani ya nchi.

Sasa kama Police wakishindwa kuzui vurugu wao JWTZ ndio waje sasa kwenye kile kikoa cha kutoa tahadhali kwanini police hawa kuwa ndio wakwanza kuliongelea ??inamaana wameyajua mapungufu ya police hata vurugu hazijaaanza au wamejua kuwa police hawana skills za kuzuia vurugu?

JWTZ walikuwa wapi wakati ule wa uchaguzi mdogo Tarime????? kule kulikuwa na vurugu kubwa sana ambayo police kweli walionyesha upungufu wa skills katika kutuliza vurugu na wao ndio wakawa waanzilishi wa vurugu kwanini nasema hayo kama mkutano haukuwa wa halali kwani police hawakuchukua evidence za mkutano mpaka mwisho na kesho yake wangewafungulia mashitaka hao viongozi wa chadema walio andaa mkutano bila kibali maarumu. matokeo yake police wakawatawanyisha watu kwa mabomu ya machozi hapo ni wazi police hawakutumiambinu yoyote ya kutuliza vurugu bali kuiongeza vurugu na kuumiza raia.

ndilo hili sasa JWTZ wanataka kutuletea hapa sasa tena wao wanakuja na mbinu mpya ati kuna dalili za kumwagika damu jamani ivi mwajua kumwagika damu inamaaana kuan makundi ya watu yako tayari kuivamia serikali na sio uchaguzi.

mtu akiniambia vurugu kweli nakubali zaweza kuwepo kwani tulijionea kule tarime lakini police ndio wasababisha kuwepo hiyo hali lakini kama vyombo vya usalama wakijifunza jinsi ya kucontrol hii hali wanaweza tena kwa amani na utulivu bila shida asilimia kubwa ya watanzania ni wapenda amani sasa sielewi JWTZ wamefanay lini hiyo research yao kuwa kuna kumwagika damu???

Do we have political terrorism in this Country?? au? Nilisha sema hapo nyuma kipindi hiki cha uchaguzi viongozi wengi wajaribu kuchunga midomo yao na sio kuropoka tuuu waonekane kwa runinga kipindi hiki ni kigumu sana its like neutral zone to the new beginning sasa tusipokuwa makini na hawa viongozi wa ngazi za juu tena kama usalama wa taifa na kuropoka ovyo badala ya kuwaelezea wananchi kuwa wawe watulivu wakati wa kupiga kura na kupokea matokeo na hakutokuwa na matatizo, wao wameisha wajaza wananchi kuwa tayari kuna hari ya hatari ooh kuna dalili ya damu kumwagika huu ni ukosefu wa skills za kijeshi.
 
Atawajibika tu siku moja mbele ya mahakama za uhalifu wa kivita za Uholanzi pindi mambo yatakapokuja kuharibika wakati na baada ya uchaguzi. Nasema hivyo kwa sababu jenerali Shimbo amekwisha buku nafasi na hivyo kuhesabiwa tayari na jumuiya ya kimataifa kwa kujihusisha kwake na vitisho dhidi ya kondoo wa kitanzania katika kipindi hiki. Jenerali Shimbo ajue kuwa Watanzania ndio mashahidi wa kwanza ikiwa kweli kuna vurugu ama viashiria vya vurugu vyenye kiwango cha kuvuka uwezo wa Polisi kiasi cha kuhitaji Intervention ya kijeshi. Pia Shimbo ufahamu kuwa jumuiya za kimataifa zilizo ndani na nje ya Tanzania zinafuatilia mwenendo mzima wa mambo hapa nyumbani. Ukidhani unaweza kuwatisha na kuwalaghai kwa hofu Watanzania, huna uwezo wa kuitisha jumuiya ya kimatafa, na wala huwezi kuilaghai kihivyo. Miamba kama wewe na wenzio wote wenye nia moja na wewe wanaendelea kunyea ndoo magerezani huku heshima zao na ubabe wao vikibaki kuwa historia yenye kukinaisha. Ushauri kwako: Fanya mambo yako ya kijeshi yaliyo ya msingi na ustaafu kwa heshima. Vitisho havijawahi kujenga dola ya heshima na ustaarabu wakati wowote wala mahali popote.
 
Good leaders are those who are proactice!!! You do not wait for problem to happen in order to tackle it!
 
Nguvu za asili nadhani watakuwa wanamaanisha natural calamities kama walivyofanya kule kilosa wakati wa mafuriko
 
Dk. Slaa ashangaa majeshi
• Awapa siku saba kuwakamata wachochezi

na Mwandishi wetu


amka2.gif

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema kitendo cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kuingilia siasa kwa vitisho ni kielelezo kingine kuwa serikali inafanya jitihada za kuhujumu uchaguzi na kukinusuru Chama Cha Mapinduzi (CCM), kabla ya upigaji kura Oktoba 31, mwaka huu.
Akihutubia umati wa wananchi waliofurika kumsikiliza mjini hapa jana, Dk. Slaa alitoa siku saba kwa Mnadhimu Mkuu wa jeshi hilo, Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema, kuwakamata watu wote waliotishia kumwaga damu ndani ya siku hizo.
Hata hivyo alimtaka Luteni Jenerali Shimbo kuwaomba radhi Watanzania kwa vitisho alivyotoa katika kipindi hicho cha siku saba, huku akijinasibu kuwa kuna uwezekano wa yeye kupita bila pingamizi kama serikali ya CCM itaendelea na vitisho kama hivyo.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo katika viwanja vya Mdete, wilayani Njombe, akiwa katika mwendelezo wa kampeni zake katika Mkoa wa Iringa.
Dk. Slaa alisema Luteni Jenerali Shimbo hakupaswa kutoa kauli kama hiyo, kwa kuwa ni vitisho kwa Watanzania, hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi, na kwamba kauli kama hiyo ilipaswa itolewe na IGP Mwema, kwa maana ya kushughulikia watu wanaotaka kuvunja amani ya nchi.
“Tunaitaka JWTZ na Polisi kuwakamata wale wote waliotoa kauli ya kutaka kumwaga damu…kama haitafanya hivyo, tujue ni propaganda chafu za Kikwete na vyombo vyake vya usalama za kuiba kura na kutaka kuvunja amani,” alisema.
Alisema yeye kama Dk. Slaa asingependa kuwa rais wa Tanzania kwa Watanzania kumwaga damu, lakini anatambua kauli kama hizo ni mbinu za CCM za kutaka kuchakachua matokeo ya Uchaguzi Mkuu.
Dk. Slaa alisema atahakikisha Watanzania hawadanganyiki na kauli za viongozi mbalimbali, wakiwamo wale wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao wamekuwa wakitumika kisiasa kutaka kuisaidia CCM, ambayo inaonekana kushindwa, kwa kutoa kauli za vitisho na nyaraka mbalimbali za kutaka kusaidiwa.
“Nataka kumwambia Shimbo, kama hajui siasa atuachie wenyewe, yeye arudi kambini kuendelea na kazi yake, badala ya kutumika kutoa vitisho kwa Watanzania ambao wamechoka kubebwa katika malori kwenda katika mikutano ya CCM….lakini hii ni dalili kuwa mgombea urais wa CCM na chama chake wameona hali ni mbaya kwao,” alisema Dk. Slaa.
Hata hivyo, alisema hofu za mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete, kutumia vyombo vya dola kutisha, ni sawa na kuonyesha kushindwa kabla ya dakika 90, na kumtaka afanye kampeni za kunadi sera badala ya kutumia dola kumfanyia kampeni.
Alimtaka aliyekuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Njombe Kusini, Anne Makinda, kuacha kuendelea kuwatisha wananchi wa jimbo hilo na kudanganya umma kuwa yeye ni mbunge wa kupita bila kupingwa.
Alisema hiki ni kipindi chake cha mwisho na kama mwaka 2015, atafanya hivyo atakuwa tayari kuacha urais na kwenda kugombea kwenye jimbo hilo.
Kwa upande wake, Meneja Kampeni kitaifa wa CHADEMA, Profesa Mwesiga Baregu, alisema ameshangazwa na kauli hiyo ya Mnadhimu Mkuu Shimbo kuwataka wananchi wakubaliane na matokeo yatakayopatikana katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Baregu alisema tamko hilo liliashiria kuwepo kwa hali ya hatari, kitu ambacho kinaonyesha kuwatia hofu wananchi, ambapo hadi sasa haijaeleweka kwanini wafikie hatua hiyo.
“Tumeshangazwa na tamko hilo ambalo linaonyesha limezingirwa na hali ya hatari na hadi sasa hatujaelewa kwa nini wafikie hatua hiyo,” alisema Prof. Baregu. Alisema katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, haikupaswa kutolewa kwa tamko kama hilo, kwa kuwa linaonyesha kutaka kujenga mazingira ya kuufanya uchaguzi kutokuwa wa haki. “Isije ikawa wanaandaa mazingira ya kufuta au kuahirisha uchaguzi kwa kuzidiwa na CHADEMA,” alisema Profesa Baregu.
 
Nimeshindwa kumtofautisha Luteni Jenerali Shimbo na Mama Salma, Hongera JK
 
Hivi msemaji wa JWTZ ni nani? Mkuu wa Majeshi, Mnadhimu au nani?
 
Mitanzania bwana, je kama Shimbo anamaanisha hata JK akishindwa akubali matokeo? Hapo itakuwa sawa? Au bado mtabwatuka?
 
Ibara ya 38 (2) (a) inasema bunge likivunjwa kiti cha rais kiko wazi. Na ile ya 42 (3) (a) inasema Rais aliyepo madarakani atakoma kuwa Rais mara yule mteule atakapoapishwa! Je, kutumia kati ya hivi si kuvunja katiba? Au katiba ndio imevunjika vunjika yenyewe? JK aseme anatumia kifungu kipi kati ya hivi? Kumtumia mshikaji wake Lt. Gen. Shimbo kuwatisha wananchi ni kutumia si kutumia kifungu cha 38 (2) (a)?
 
Hivi unavyo waambia wagombea wapinge matokeo kwa ustaarabu una maanisha wagombea wepi? Yaani ngazi ipi? Ya Urais? Ubunge? Udiwani? Au wote? Kwa taarifa yako yale ya Urais hayachunguzwi kwa mujibu wa katiba ibara ya 41 (7)! Kama umekwisha kubadilisha kifungu hicho cha katiba tafadhari tutaarifa kiuwazi zaidi!

Pia unafikiri hao wanajeshi hawana ndugu zao ambao wako kwenye lindi la umaskini? Kwanza wewe mwenyewe una ndugu na jamaa walio kwenye lindi la umaskini.
 
Chief of Staff, Lt. Gen. Abdulaman Shimbo has amended the contitution of the United Republic of Tanzania of 1977 as amended in 2005. Now we have that of 1977 amended in 2010 under TPDF Chief of Staff, Lt. Gen. Shimbo! Lt. Gen. Shimbo has changed section 41 (7) to read that presidential election results shall peacefully and in a civilised manner be challenged in the court of law.

Though this is undemocratic way of amending our constitution but gives a way to real democracy and rule of law. Lt. Gen. Shimbo got all the blessings from Commander in Chief, President JK through Chief of Defence Forces, General Davis Mwamnyange to do that. Let us take advantage of this ignorance of our mother law!!
 
Sababu ni:
Dr. Slaa kutangaza kipindi cha lala salama kwa kuanza kufyatua makombora yake ambayo mengine yanaelekea TPDF!
 
Ibara ya 38 (2) (a) inasema bunge likivunjwa kiti cha rais kiko wazi. Na ile ya 42 (3) (a) inasema Rais aliyepo madarakani atakoma kuwa Rais mara yule mteule atakapoapishwa! Je, kutumia kati ya hivi si kuvunja katiba? Au katiba ndio imevunjika vunjika yenyewe? JK aseme anatumia kifungu kipi kati ya hivi? Kumtumia mshikaji wake Lt. Gen. Shimbo kuwatisha wananchi ni kutumia si kutumia kifungu cha 38 (2) (a)?

Wakuu,mnajua Lt Gen bosi wake ni mkuu wa majeshi ambaye bosi wake ni Amiri jeshi mkuu, kwahiyo Lt Gn ametoa maelekezo ya mkuu wake wa kazi ambaye yupo nje ya ofisi kwa kampeni.
Aaaa! Mwanamayu kwani ni mara moja au mbili! umesahau amesaini sheria ya uchaguzi iliyochomekwa vipengele na Jaji Werema, in other words haikutungwa na bunge,sasa hiyo si kuvunja katiba.
 
1. Kupanda daladal bure?
2. Kuwa na maduka makubwa ya vyakula na vifaa kama mafriji kwa bei ndogo?
3. Kukopeshwa magari?
4. Wenye vyeo vya juu kupewa guu la ng'ombe kila siku?
5. bia, sigara bei cheee
 
Chief of Staff, Lt. Gen. Abdulaman Shimbo has amended the contitution of the United Republic of Tanzania of 1977 as amended in 2005. Now we have that of 1977 amended in 2010 under TPDF Chief of Staff, Lt. Gen. Shimbo! Lt. Gen. Shimbo has changed section 41 (7) to read that presidential election results shall peacefully and in a civilised manner be challenged in the court of law.

This is a great observation, from the analytical perspective, but as the Chief of Staff is a presidential appointee, nothing will come of it.

Do we really believe that OURS is a REAL DEMOCRACY?
 
Back
Top Bottom