Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
wakubwa..
vyombo kadhaa vya habari leo vimeripoti uchukuaji wa fomu kwa bwana zitto zuberi kabwe kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA..
katika hili tunapaswa tumpongeze sana zitto kwani ataweza kukomesha malalamiko kadhaa yaliyokuwa yanawakabili wanachama wa CHADEMA ambayo MBOWE aliyashindwa..
ila chakushangaza ndugu zangu eti MBOWE KASUSA anataka kupita bila kupingwa...
Hivi ndugu wadau mnadhani kweli MBOWE ataweza kupambana na ZITTO?..SIO KWAMBA AJITOE TU ASIGOMBEE ILI ASIUMBULIWE NA DAMU CHANGA?
 
Anatakiwa akubali demokrasia ichukue mkondo wake, awaachie kina Zitto na Dr. Slaa sasa. Yeye akitaka akagombee ubunge. Bado anayo nafasi ya kutoa mchango kwa Taifa letu.
 
Zitto
Muachie uenyekiti Slaa.Wewe subiri upitishwe kuwa katibu.Msianze fujo halafu mkaiparaganyisha chadema
 
wakubwa..
vyombo kadhaa vya habari leo vimeripoti uchukuaji wa fomu kwa bwana zitto zuberi kabwe kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA..
katika hili tunapaswa tumpongeze sana zitto kwani ataweza kukomesha malalamiko kadhaa yaliyokuwa yanawakabili wanachama wa CHADEMA ambayo MBOWE aliyashindwa..
ila chakushangaza ndugu zangu eti MBOWE KASUSA anataka kupita bila kupingwa...
Hivi ndugu wadau mnadhani kweli MBOWE ataweza kupambana na ZITTO?..SIO KWAMBA AJITOE TU ASIGOMBEE ILI ASIUMBULIWE NA DAMU CHANGA?


Yeye akisusa wenzie wala! go! go! Zitto
 
wakubwa..
vyombo kadhaa vya habari leo vimeripoti uchukuaji wa fomu kwa bwana zitto zuberi kabwe kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA..
katika hili tunapaswa tumpongeze sana zitto kwani ataweza kukomesha malalamiko kadhaa yaliyokuwa yanawakabili wanachama wa CHADEMA ambayo MBOWE aliyashindwa..
ila chakushangaza ndugu zangu eti MBOWE KASUSA anataka kupita bila kupingwa...
Hivi ndugu wadau mnadhani kweli MBOWE ataweza kupambana na ZITTO?..SIO KWAMBA AJITOE TU ASIGOMBEE ILI ASIUMBULIWE NA DAMU CHANGA?

Nani kasema Mbowe kasusa???
 
wakubwa..
vyombo kadhaa vya habari leo vimeripoti uchukuaji wa fomu kwa bwana zitto zuberi kabwe kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA..
katika hili tunapaswa tumpongeze sana zitto kwani ataweza kukomesha malalamiko kadhaa yaliyokuwa yanawakabili wanachama wa CHADEMA ambayo MBOWE aliyashindwa..
ila chakushangaza ndugu zangu eti MBOWE KASUSA anataka kupita bila kupingwa...
Hivi ndugu wadau mnadhani kweli MBOWE ataweza kupambana na ZITTO?..SIO KWAMBA AJITOE TU ASIGOMBEE ILI ASIUMBULIWE NA DAMU CHANGA?

Hii manda imejadiliwa vya kutosha ndani ya jukwaa hili. Ila kinachoonekana ni kuwa ulitaka tu kuleta ushankupe hapa, haswa kwa hiyo niliyo highlight red. Hayo rejea yake umeipata wapi? kwani mtiririko mzima wa tukio hili taarifa ni tofauti na ya kwako! Kila kitu 0 ila kimoja tu ndio 1, kulikoni?
 
Join Date: Tue Aug 2009
Posts: 1
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts

wakubwa..
vyombo kadhaa vya habari leo vimeripoti uchukuaji wa fomu kwa bwana zitto zuberi kabwe kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA..
katika hili tunapaswa tumpongeze sana zitto kwani ataweza kukomesha malalamiko kadhaa yaliyokuwa yanawakabili wanachama wa CHADEMA ambayo MBOWE aliyashindwa..
ila chakushangaza ndugu zangu eti MBOWE KASUSA anataka kupita bila kupingwa...
Hivi ndugu wadau mnadhani kweli MBOWE ataweza kupambana na ZITTO?..SIO KWAMBA AJITOE TU ASIGOMBEE ILI ASIUMBULIWE NA DAMU CHANGA?

Ado karibu jamvini. Ila wasi wasi wangu ni kuwa itachukua muda kidogo kujua kuwa hapa si mahali pa "Breaking news" zisizo kuwa na source. Ninajua 2010 inakaribia there is a lot of kamati za ushindi ila ni lazima mtu ajue kuwa kila kitu kitakuwa questioned so think before you erupt with post without clarification
 
ndio..MBOWE anajidai kususa eti anataka kubembelezwa ili agombee as if he is the only politician


Ado, Karibu sana... Hata mie nilikuja na vijungu vyangu na vitetesi kibao!!! Badae nikagundua hapa ni great thinkers, kama una uhakika toa ushahidi, la sivyo... Kakojoe ulale
 
AUSTIN BEYADI, 29th August 2009

DEPUTY Secretary General of Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mr Zitto Kabwe, has called for peaceful and clean campaign that would not divide the party at a time when elections are around the corner.

Mr Kabwe who will stand against Chadema's incumbent Chairman, Freeman Mbowe, said in Dar es Salaam yesterday that the timing of the election scheduled for next month, was a litmus test for his party as the country gears up for the general election.

"My joining the race for chairmanship is a sign of Chadema's political maturity. After the elections we'll have to bury our differences and focus on building and strengthening the party," he said.

He also dismissed as baseless claims that he had been 'planted' by the ruling party so as to weaken solidarity within his party.

He said that his decision to vie for the top leadership did not come from other political party leaders but was a decision made after pleas from upcountry leaders.

Rubbishing speculations that he was not capable of leading the party since he was still very young, Mr Kabwe said that he has managed to lead the Parliamentary Parastatal Organisation Accounts Committee (POAC), whose accumulated capital for all parastatal organizations was more than 5 trillion/- , adding that Chadema's income was 72m/- only.

Mr Kabwe (32) said that he had no interest whatsoever to contest as president under the Party ticket, during the forthcoming elections.

He said that the party's current and previous leaders have done a tremendous job to move the party from the least popular party to the second strongest party after CCM and his intention was to make the party number one.

"We must forge ahead with a new vision of strengthening our unity because Chadema has already proved that it is capable of taking over the country and I am just the man for that job," he said.

Mr Kabwe said that in the coming general elections there will be a lot of youth who will be voting for the first time and they will be eager to vote for their fellow youth.

He called upon various people and contestants who are campaigning for the post to avoid dirty campaigns because such campaigns will only benefit the ruling party.

Last week Mr Kabwe, who is also the Kigoma North MP, caused a stir when he declared that he had decided to wrest the leadership of Chadema from Mr Mbowe to restore unity in the party, with the possibility of playing a bigger role in national politics.


Source: Daily News
 
Zito amejitoa unconditionally kwenye kinyang'anyiro baada ya kukutana na wazee wa chama.
 
Habari ni kwamba Zitto amekutana na wazee wa chama jioni la leo na amekubali kujitoa kukinusuru chama kuwa na makundi.
 
Zito amejitoa unconditionally kwenye kinyang'anyiro baada ya kukutana na wazee wa chama.


Mimi ndio maana nasema kamwe sitokuja upinzani.

WAPINZANI WA CCM WANAHUBIRI KILE WASICHOTENDA.

Sick and tired of these cheap politicians!!!

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!
 
Mimi ndio maana nasema kamwe sitokuja upinzani.

WAPINZANI WA CCM WANAHUBIRI KILE WASICHOTENDA.

Sick and tired of these cheap politicians!!!

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!

Zitto amejitoa ?Acheni utani bwana kuna ukweli kwenye hili ?
 
Mimi ndio maana nasema kamwe sitokuja upinzani.

WAPINZANI WA CCM WANAHUBIRI KILE WASICHOTENDA.

Sick and tired of these cheap politicians!!!

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!

By the way huhitajiki kabisa baki huko huko kwa mafisadi wenu!
 
By the way huhitajiki kabisa baki huko huko kwa mafisadi wenu!

Masa;

Teh teh teh unaanza sasa moto ukianza utaona jiko ni too hot for you to stay!!!.

Mbona humwambii Mfadhili wako Mwakyembe aende CHADEMA?, unajua wazi wazee watamshauri amwachie Mbowe. Kile ni chama cha wale wazee ni chama cha watu binafsi!!

Najua utapinga kwa sababu nimesema mimi lakini ukweli unao MOYONI kaka.

Walichofanya hao wazee ni KUUWA DEMOKRASIA NDUGU YANGU
 
Zitto sasa ataka nafasi ya mwenyekiti agombee Dk Slaa

Na Fred Azzah

MOTO wa Uchaguzi wa nafasi ya uenyekiti wa Chama cha Demokarsia na Maendeleo (Chadema), bado unazidi kuwaka baada ya Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kukataa mapendekezo ya wazee wa yeye kuwa Katibu Mkuu ili kumpisha Mbowe na badala yake kutoa masharti mapya ya kujitoa.

Habari zilizopatikana jana kutoka makao makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam zinaeleza wazee walieleza kuwa mgawanyiko uliotokana na vigogo hao wa Chadema, Zitto na Mbowe kuchukua fomu kuwania uenyekiti ni hatari kwa uhai wa chama.

Walisema ili kukinusuru chama hicho walipendekeza Katibu Mkuu wa sasa, Dk Willibrod Slaa agombee nafasi ya Makamu Mwenyekiti na Zitto awe Katibu Mkuu wa chama ili kumwachia Mbowe kusimama kugombea uenyekiti.

Kikao hicho kilianza saa 4:00 asubuhi na kumalizika kikishirikisha Mwasisi wa Chama hicho, Edwin Mtei, Mwenyekiti mstaafu, Bob Makani, Victor Kimesera, Phillemon Ndesamburo, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Wilibrod Slaa na Mbunge wa Viti Maalumu wa chama hicho, Halima Mdee.

Ziito ndiye alianza kuingia katika kikao hicho saa 9:00 alasiri huku Mbowe akingia baadaye saa 11:00 jioni.

Pia inaelezwa kuwa moja ya ajenda kubwa ya kikao hicho ilikuwa ni kujaribu kukinusuru chama kwa kumtaka Zitto akubali kuondoa jina lake katika kinyang'anyiro hicho ili kumpisha Mbowe aweze kugombea ili kulinda hadhi ya chama.

Hata hivyo, taarifa za ndani zinaeleza kuwa Zitto alikataa pendekezo hilo na kuwaleza wazee hao kuwa yupo tayari kujitoa iwapo Mbowe na yeye atajitoa kugombea nafasi hiyo ili ichukuliwe na Dk Slaa kwa lengo la kuleta umoja ndani ya chama hicho.

Inaelezwa kwamba Zitto alipinga mapendekezo ya wazee kwa madai kuwa kama Mbowe ataendelea kugombea nafasi ya uenyekiti wakati amekuwa akimchafu kuwa ni fisadi, umoja katika chama hicho hautakuwapo.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinasema kwamba Zitto alipendekeza badala yake wote wawili—yeye na Mbowe, wajitoe katika kinyang’anyiro ili kukinusuru chama kugawanyika na nafasi hiyo ichukuliwe na Dk Slaa ambaye alikuwa katibu wa kikao hicho cha wazee.

Vyanzo vyetu vya uhakika vinasema Zitto aliwaeleza wazee hao kuwa yupo tayari kutokuwa na cheo lakini chama kibaki salama.

Hata hivyo, wazee waliamua kuwapa muda wa kujadili mapendekjezo ya wazee Dk Slaa, Mbowe na Zitto leo saa 3:00 asubuhi kabla ya kikao cha kamati kuu hakijaanza. Mkutano huo ulimazika saa 12:45 jioni.

Zitto alipotakiwa kutoa ufafanuzi wake alikataa na badala yake akataka aulizwe Slaa ambaye alikuwa katibu wa kikao hicho cha wazee.

Msimamo huo wa Zitto unatokana na kikao cha awali alichokaa na viongozi wa kambi yake kwenye Hoteli ya Tamali iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano huo wapambe wake walimtaka Zitto kukataa wazo la kumpisha Mbowe kwa kuwa ni haki yake ya kikatiba kugombea nafasi hiyo.

Katika kikao hicho kilichoelezwa kuwa ni cha kuweka mikakati ya kuendesha kampeni wafuasi wake hao walisisitiza kuwa hawatakubali mgombea wao ajitoe.

Mwandishi wa gazeti hili ambaye alikuwapo katika hoteli hiyo alishuhudia Zitto akiingia saa 5:00 asubuhi katika hoteli hiyo na kwenda kukaa pamoja na baadhi ya viongozi wa chama hicho.

"Mwandishi tunaomba utupishe tunataka kuzungumza mambo yetu," alimwambia mmoja wa viongozi hao wa chama hicho ambaye awali walikuwa wamekaa pamoja kabla ya Zitto kuingia hotelini hapo.

Kikao hicho kilichokuwa na watu watano, akiwamo, Afisa Uhusiano wa Chama hicho, David Kafulila na Msafiri Mtemelwa kilifanyika nje ya vyumba vya hoteli hiyo.

Hata hivyo, baada ya kikao hicho, mmoja wa watu hao walimdokeza Mwandishi wetu kuwa Zitto hatakubali wazo la kumpisha Mbowe kugombea nafasi ya mwenyekiti katika kikao cha baraza la wazee kilichokuwa kikifanyika makao makuu ya chama hicho na kwamba walikuwa wanaendelea na kampeni za mwisho kwa wajumbe wa mkutano mkuu ambao wameanza kuingia jijini Dar es Salaam.

Wakati juhudi za wazee hao zikiendelea, habari za ndani ya Chadema zinaeleza kuwa Zitto anaendelea na kampeni zake na hadi sasa anaungwa mkono na mikoa 15 na Zanzibar na kwamba ana nguvu kubwa iwapo jina lake litapitishwa kugombea nafasi hiyo. Leo Kamati Kuu ya chama hicho inakaa na kesho uchaguzi wa baraza la vijana na wazee.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom