Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Hawa hawana itifaki na inaonyesha wanamatatizo makubwa sana ,yaani kuwepo kote kwa muda mrefu wakiwa viongozi wakuu ,wanaonyesha dalili za kuwa na matatizo ya ndani kabisa ,ninavyoamini ikiwa nyote ni wananchama wa chama kimoja na mmetoka mbali katika kukiendeleza chama chenu basi lazima mtakuwa na mashirikiano (strategy) za karibu kabisa na kuweza kumpanga Mwenyekiti ,ikiwa tu aliekuwepo atakumbwa na mauti au atasema basi, kupeleka watu wazito wawili katika kugombea nafasi ya juu ya Chama ni kuonyesha kuwa au ni kukigawa chama ,inaonyesha waChadema hawana maelewano ,nilivyotaraji labda angetokea mtu mwengine kabisa zaidi ya wale heads kutaka kugombea nafasi hiyo na sio vinara walio juu ,huko ni kukosa muelekeo na hapa Chadema watakuwa wamechemsha au labda iwe ni mbinu ya kutaka kuwadanganya waTz kuwa ndani ya Chama chao kuna demo na sio demokrasi.

Ilikuwa ni lazima awepo kiongozi katika top 10 wa Chadema ambae angeweza kuchukua nafasi ya kugombea pindipo Mwenyekiti aliekuwepo ameamua kubwaga manyanga ,na itakuwa wenyewe wawe wanalijua hilo na wawe wanamjua kwani ni jambo la kuridhiana kabisa katika harakati za kuendesha Chama kikuu na sio mnatokea kama mnaonekana mnanyang'anyia ,ni kukigawa Chama ,na hapo ikitokea kufikia kupigiwa kura na kuibuka mmoja kumshinda mwenziwe kwa kura kidogo basi mambo hayatakuwa mazuri & they will never be the same again ,ingawa watataka ionekane machoni mwa WaTz kuwa mambo ni kawaida na ndio demokrasia ilivyo ,ni sawa lakini not in that way at all and spesho in Tz.


Mkuu Mwiba, mtazamo wako wa maana ya Demokrasia umenishangaza kweli..!!
 
Naomba hizi ziunganishwe na ile ya Zitto. Lakini wote wawili, Zitto na Slaa ni member wa JF na ni vyema wakawa makini zaidi. Humu JF wanaweza kupata wasaa huo. Nadhani hakuna ubaya kwa wote kuwania kama hawatatuvurugia chama chetu. Kwa kweli kama ukisikia amani kuchafuka ni kama Chadema itachafuka, hapo mambo yatawaka na hapatakalika na wananchi wataanza kuchukua sheria mkononi. Hapa ndipo kazi za UWT zinatakiwa kuonekana na si kulinda MAFISADI. Usalama wa Taifa ni pamoja na kuwa na mahali ambapo angalao wananchi watakuwa na matumaini ya haki zao kutetewa lakini ukiua njia za kupumulia patalipuka
 
Kama ni kweli, basi hongera sana Chadema na Dr. Slaa, siamini kwamba atakuwa amekurupuka na kubeba fomu, watakuwa wameongea na kuelewana hii inatia moyo sana, na Freeman ni lazima anziwe sana kwa mchango wake usio na kipimo kwa upinzani nchini.

- Freeman aliichukua Chadema butu na kuipatia meno, sasa ni zamu ya wengine kuipatia makucha, yeye amesema anaenda kwenye ubunge, hakijaharibika kitu hapo, saafi sana!

- Mimi ninamsubiria Rais wangu Dr. Slaa, ili tuone hawa mafisadi tutafika nao wapi, maana ninamuaminia sana na hilo la kuwafunua na kuwaacha wazi mafisadi, tatizo letu bongo sasa hivi ni mafisadi kwanza, tukiwaweza hayo majibu ya matatizo mengine yote yatajipanga yenyewe!

Bravo Dr. Slaa.

Respect
.

Field Marshall Es
 
Zitto na Dr. Slaa ni membaz hapa, hivyo wanaweza kudondosha ukweli kama wamechukuwa fomu au la.
 
Margreth
user_offline.gif

Margreth has no status.
Senior Member
red_left.png
red.png
red_right.png
green_left.png
green.png
green_right.png
Join Date: Thu May 2009
Posts: 74
Thanks: 0
Thanked 23 Times in 17 Posts
Rep Power: 21
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif



icon1.gif
Re: Zitto kugombea Uenyekiti CHADEMA
Basi wasifanya uchaguzi kama ndo hivi, Zitto atatumiwa na MAFISADI hajakomaa kumbuka sakata la DOWANS


Ama kweli hii ndiyo JF. Sina hakika hapa mtu alitumia muda ku-type kwa kutumia vidole kwenye keyboard. Siku hizi kuna software za ku-type kile unachoongea; nina wasiwasi hii software ilitumika hapa akasahau ku-edit.......
 
Wakuu tukumbuke kuwa Chadema sio Zitto na Slaa tu, japokuwa wao ni wanachama muhimu wa chama hicho. Kuchukua fomu ni jambo muhimu lakini waliomuhimu zaidi na wale watakaopiga kura.
Kama Freeman hagombei anataka kwenda Kugombea ubunge ni jambo la maana sana. Amejitahidi kutoa leadership nzuri kwa chama katika kuipindi chake cha uongozi, hatukusikia ufisadi wa significant migogoro kama ilivyo kwenye baadhi ya vyama vya upinzani.
 
Habari tulizozipata hivi punde kutoka vyanzo vya ndani kabisa vya CHADEMA zimetupasha kuwa Dr. Wilbroad Peter Slaa amechukua fomu ya kugombea kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA.

Habari hii imekuja muda mfupi baada ya ile iliyomhusu Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA bara Mhe. Zitto Zuberi Kabwe kuchukua fomu na kuiwasilisha akiwa amenuia kikamilifu kuukwaa uenyekiti wa chama hicho kinachokua kwa kasi kubwa.

Hadi sasa Dr. Slaa ndiye Katibu Mkuu wa CHADEMA. Uchaguzi wa viongozi wa Taifa wa CHADEMA unatarajiwa kufanyika katika mkutano mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika katikati ya mwezi ujao

DR. Slaa for the Presidency!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hawawezi kumpa MUISLAM dont fool yourself.

Itawaudhi lakini ndio ukweli wenyewe huo, haya njooni na jazba zenu sasa

Nenda kwenye hoja,acha udini wewe,toka lini mwislamu akanywa bia?Zitto anakunywa
 
yap.....!!!
All the best Chadema in your way to general election let it be free and fair so that CCM,never get anything to say about because there are there to get somewhere to talk about....
Big up M M. Mwanakijiji and others.
2po pamoja......
 
Zitto alichemka sana katika suala la Dowans.ni mapema sana kumkabidhi mikoba ya kukiongoza chama hasa tukizingatia umri na kuyumba yumba katika masula muhimu ya kitaifa.

Bwana Zitto pia alikuwa kioja katika suala la EAC alitofautiana na asilimia kubwa ya watanzania waliokataa kuharakishwa uundwaji wa shirikisho la Afrika mashariki.Kumpatia majukumu makubwa ni sawa na kumwangamiza kisiasa.Bwana mdogo bado anatakiwa kujifunza ili aweze kuja kuwa kiongozi bora.

Bwana Zitto alishatutangazia kwamba hatatetea kiti cha ubunge lakini baadae akabadili mawazo.Kwa maoni yangu nadhani huko ni kukosa msimamo na inaonyesha dogo ni mwanasiasa asiyekuwa na msimamo hii dosari kubwa sana kwa mtu tuanyetaka aje akiongoze chama.

Kwa maoni yangu nadhani Zitto anatakiwa abakie na nafasi yake ya ubunge tu,hafai kabisa kuongoza chama makini.

Namuunga mkono Ngongo,

SEMA UKWELI DAIMA. Tumpe muda Mh. Zitto angalau 2015 ndo achukue fomu kugombea. Lakini kwa wakati huu ni mgumu sana kwa MAFISADI kutumiwa. Fikiria Mh. Mbatia na NCCR yake yuko wapi, kaishia kabisa na chama chake yote hii ni MAFISADI. Angalia Mh. Lipumba anatikiswa haswa, Maoni yangu ni kuwa Mh. Zitto agombee nafasi nyingine lakini ya U/kiti asubiri kwanza.
 
Mtanzania ya RA na kigazeti kingine kina jina jipya wanasema Mh Zitto kachukua na kurudisha fomu za kugombea Uenyekiti CHADEMA. Nadhani haya ndio MABADILIKO tunayoyasubiri baadhi yetu.
 
Democracy at work in CHADEMA............. chama hakitavunjika, kitamaliza uchaguzi kikiwa imara kabisa. tukumbatie demokrasia na tusiihofu.

...................................
 
Hii ni Demokrasia ambayo kwa kweli inabidi vyama vingine viige mfano,sio ndani ya CCM tayari viongozi wa juu wameshapiga marufuku mwanachama mwingine yeyote kumpinga JK mwakani ktk Urais.Hii ndiyo tofauti kati ya CCM na Chama mbadala CHADEMA.

Hata hivyo,nawaomba WANACHADEMA kuwa makini sana na huu uchaguzi kwani CCM wanajua wamebanwa kila kona na CHADEMA na matatizo yao yote ya tuhuma za ufisadi ni presha ya CHADEMA,so wanajua hata next year ktk general elections kutakua na kazi kama CHADEMA itaendelea kuwa imara.Kwa hiyo watajaribu kufanya kila njia kutumia hiifursa vizuri kupata njia za kuwarahisishia kazi mwakani kwani CHADEMA ndio tataizo na kikwazo kikubwa kwao kuelekea uchaguzi mku,so you have to be very carefully.Soon nami nitarudi nyumbani kuchochea Demokrasia ili tusaidiane kuijenga nchi yetu.Kila la heri CHADEMA.

By the way,Ndugu Zitto huijasema au kuwaweka wanajamvi sawa kama kweli umechukua fomu.Tafadhali hebu toa tamko ili tusiendelee kuamini roumours!

MUNGU IBARIKI CHADEMA,MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
To be experienced means being wise enough to avoid mistakes you made in the past.

If we wait until we do all the mistakes so that we can learn from them, we will take eternity. Learning from our mistakes and mostly from others mistakes would be more prudent
 
Democracy at work in CHADEMA............. chama hakitavunjika, kitamaliza uchaguzi kikiwa imara kabisa. tukumbatie demokrasia na tusiihofu.

...................................

Bravoo Mh. Zito, busara itumike hata pale mtakapotofautiana. It is clear watu wenye upeo mkubwa kutofautiana ni kawaida lakini hawaparanganyiki
 
Kwa nini GT unatutakia mabaya? Dr. Slaa ni nguzo imara Chadema na amekiimarisha chama wakati wa ukatibu wake. Akifuata misimamo ya Chadema, Dr Slaa ameimarisha demokrasia Tanzania kwa michango yake Bungeni na nje ya Bunge.

Mungu ampe afya njema, aendelee kukiongoza Chama katika nafasi yoyote Mkutano Mkuu ujao utakayampa. Tunamhitaji.

Kilasara

Ni kwa nini unaumiza kichwa? huyo unayemjibu ni wale wale wanaotaka tuangamie sisi na kizazi chetu , tuendelee kumuomba mwenyezi Mungu ampe Dr. Slaa afya njema ili aweze kututetea sisi watanzania Masikini.
 
Uchaguzi Chadema Kindumbwendumbwe Mbeya

Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Mbeya umeshindwa kufanyika baada ya kuzuka vurugu zilizosababishwa na wanachama na wagombea waliokuwa wakipinga kukiukwa kwa taratibu.

Dalili za kukwama kwa uchaguzi huo zilianza kujitokeza jana saa tatu asubuhi, ambapo wajumbe walipinga kauli ya Katibu anayemaliza muda wake, Ipyana Seme, ambaye aliwataka wajumbe waliojipeleka katika uchaguzi huo kuondoka.

Kauli hiyo ilipokewa kwa hisia tofauti na wajumbe ambao walipinga kuondolewa kwa wenzao wa wilaya za Mbozi na Ileje na baada ya kuona kelele zinazidi huku wajumbe wakimzonga, Seme aliondoka na gari na kurudi na askari Polisi.

Hatua hiyo ilitokana na kauli yake ya kuzuia wajumbe hao kwa madai kuwa hawajafanya uchaguzi katika wilaya zao, hivyo si wajumbe halali na hawana sifa za kushiriki mkutano huo, jambo ambalo lilipingwa na wajumbe wengine.

Katika uchaguzi huo, waliokuwa wanagombea uenyekiti ni Sambwee Shitambala ambaye aliwania ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Mbeya Vijijini na George Mtasha wakati ukatibu ulikuwa ukiwaniwa na Seme na Eddo Mkata.

Kutokana na vurugu na kutoelewana, Msimamizi wa Uchaguzi huo, Ally Chitanda wa makao makuu ya Chadema, alitangaza kuahirishwa kwa uchaguzi huo saa mbili usiku kwa alichodai ni maagizo kutoka makao makuu kutokana na vurugu hizo.

Aidha, Chitanda alisema matokeo mengine ya watu waliochaguliwa kushika nafasi za Mwenyekiti wa Baraza la Vijana, Wanawake na Wazee, yatabaki kama yalivyo na nafasi za viongozi wa juu zitajazwa siku nyingine itakayotangazwa.

Akizungumzia kuahirishwa kwa uchaguzi huo, Shitambala alisema kanuni kadhaa za uchaguzi zilikiukwa ikiwamo ya kutokuwapo muhtasari wa kikao kilichopita na usajili wa wajumbe wa mkutano mkuu.

“Hamuwezi kuwa kwenye mkutano na watu wanaanza kusema na yule ni mjumbe, Katibu tunamwambia alete muhtasari haleti, hatuwezi kufanya uchaguzi bila kufuata taratibu.

“Katika uchaguzi hatuhitaji kuchaguliwa kwa kelele za mashabiki, hata kama walikuwapo mashabiki wangu, mimi sijali sana kuhusu kushinda, kwa sababu hakuna mishahara ila tunagombea ili kusaidia kuleta maendeleo, mimi nina kazi yangu na nimeajiri watu,” alisema.

Mwenyekiti anayemaliza muda wake, Mtasha alisema kuahirishwa kwa mkutano wa uchaguzi huo kunatokana na vurugu ambazo zilitokea baina ya wajumbe ambao wanamuunga mkono yeye na wa mpinzani wake.

Mtasha alidai kuwa yeye alikuwa anaungwa mkono na wajumbe wa wilaya tano za Mbarali, Ileje, Rungwe, Mbozi na Chunya. Akizungumzia vurugu hizo, aliyekuwa mgombea ubunge Mbeya Vijijini kwa tiketi ya CUF na baadaye kujiunga Chadema, Daud Mponzi, alisema uchaguzi huo ni wa kwanza kufanyika ndani hivyo ni jambo la kawaida kutoelewana.

Hata hivyo, alishauri kuwa ni vizuri wagombea wakakaa na kushauriana juu ya namna ya kuendesha uchaguzi huo badala ya kufanya vurugu ambazo hazina maslahi kwa mtu yeyote yule. Mjini Sumbawanga, Mbunge wa Mpanda Kati, Said Arfi, aliibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu wa chama hicho mkoa na kuwa Mwenyekiti.

Akitangaza matokeo hayo, Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi huo, Martin Juju, kutoka makao makuu ya chama hicho, alisema wanachama wa Chadema wanapaswa kutambua kuwa wamechaguliwa kwa lengo la kukikuza chama hicho na si kufurahia nyadhifa walizopata.

Alisema hivi karibuni utafanyika uchaguzi wa serikali za mitaa, wao kama viongozi wana wajibu wa kuhakikisha Chadema inaibuka na ushindi mkubwa, ili pia iwape nafasi wakati wa uchaguzi mkuu na kuwapa ushindi wa kishindo katika ubunge ambao wameuwekea mikakati ya kutosha na kutwaa majimbo mengi nchini. Katika uchaguzi huo, Juju alimtangaza Arfi aliyepata kura 38 na kumshinda Menrad Suwi aliyepata kura 10 kati ya 48 zilizopigwa na wajumbe wa mkutano huo.

Alisema Ozem Chapita alipata kura 43 na kuwa Katibu huku mpinzani wake Charles Ndonde akipata kura 4 kati ya 47 zilizopigwa. Juju alimtangaza Katibu Mwenezi kuwa ni John Matongo aliyepata kura zote 47 zilizopigwa kutokana na mpinzani wake Suwi kujitoa dakika za mwisho.

Mjini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa alisema chama hicho kimesimamisha uchaguzi wa wagombea wa mikoa ya Mbeya na Mara baada ya kupata malalamiko juu ya wagombea. Alisema wagombea wa mikoa hiyo, walisimamishwa na Kamati Kuu ya chama hicho, kutokana na malalamiko ya wajumbe, kuwa hawakuwa halali na kwa mujibu wa taratibu za Katiba imebidi kuchukuliwa hatua hiyo.

“Mbeya na Mara jana tulisimamisha uchaguzi wao, yamekuwapo malalamiko ya msingi juu ya wagombea hao, hivyo tutaendelea kusimamia haki,” alisema Dk. Slaa.

Aliongeza kuwa chama kiko makini na hawataruhusu kufanyika kwa hila, wala aina yoyote ya ufisadi katika kipindi cha uchaguzi wa viongozi wa chama hicho. Kuhusu hali inavyoendelea ya uchaguzi, alisema wanaendelea vyema na taratibu za kawaida za kurudisha fomu kwa ngazi ya Taifa kutokana na jana kuwa siku ya mwisho kurudisha.

“Nimeshapokea fomu nyingi, ingawa siwezi kukutajia nani na nani waliorudisha hadi hapo kamati ya kuchambua itakapofanya kazi yake Agosti 29,” alisema Dk. Slaa.

Aliongeza kuwa ngazi zinazogombewa na ambazo amepokea fomu za wagombea ni pamoja na ngazi ya uenyekiti, makamu mwenyekiti kwa Tanzania Bara na Visiwani, kiongozi wa vijana, wanawake na wazee. Mkutano mkuu wa Chadema, unatarajiwa kufanyika Septemba 3 hadi 4 ambapo utatanguliwa na wa Kamati Kuu na mabaraza matatu ya chama.

SOURCE: Habari Leo (25/08/2009)

Nawaombea wapenda demokrasia wezangu CHADEMA wafanye uchaguzi kwa hali ya usalama na amani; kuanzia hizi chaguzi za ngazi ya chini hadi ule Uchaguzi Mkuu.

All the best CHADEMA
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom