Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Hawa ndio wameshakigawa chama. Upande mmoja kuna kundi linalomuunga mkono Zitto likiongozwa na Msafiri Mtemelwa lenye makada kama Kafulila, Danda na wenyeviti wa zamani wa mikoa. Upande mwingine kuna wanaompinga asiwe mwenyekiti, kundi hili yuko Dr Slaa, Profesa Baregu, Mnyika, Tundu Lissu, Benson Kigaila na viongozi wa wilaya

Serayamajimbo
 
Hawa ndio wameshakigawa chama. Upande mmoja kuna kundi linalomuunga mkono Zitto likiongozwa na Msafiri Mtemelwa lenye makada kama Kafulila, Danda na wenyeviti wa zamani wa mikoa. Upande mwingine kuna wanaompinga asiwe mwenyekiti, kundi hili yuko Dr Slaa, Profesa Baregu, Mnyika, Tundu Lissu, Benson Kigaila na viongozi wa wilaya

Serayamajimbo

hapo kuna kazi kubwa. hawa wasiomtaka wanamtaka nani? Mbowe?😕
no we need a new chairman.

Mbowe akiondoka mie nitachukua kadi ya chadema
 
Habari tulizozipata hivi punde kutoka vyanzo vya ndani kabisa vya CHADEMA zimetupasha kuwa Dr. Wilbroad Peter Slaa amechukua fomu ya kugombea kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA.

Habari hii imekuja muda mfupi baada ya ile iliyomhusu Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA bara Mhe. Zitto Zuberi Kabwe kuchukua fomu na kuiwasilisha akiwa amenuia kikamilifu kuukwaa uenyekiti wa chama hicho kinachokua kwa kasi kubwa.

Hadi sasa Dr. Slaa ndiye Katibu Mkuu wa CHADEMA. Uchaguzi wa viongozi wa Taifa wa CHADEMA unatarajiwa kufanyika katika mkutano mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika katikati ya mwezi ujao
 
Wakiwa makini huu utakuwa msingi mzuri wa Demokrasia, lakini wakichemsha yatakuwa yale yale ya NCCR_mageuzi ya Kina, Mrema, Marando, Maguto etc.
 
Slaa angefaa sana kuwa candidate wa CHADEMA ktk Uraisi wa nchi!

Slaa akiwa raisi wa nchi hii..Tanzania ingebadilika kuwa nchi nzuri zaidi kwa haraka!!

Vipi Mbowe hapendi tena uenyekiti??
 
Last edited:
hapo kuna kazi kubwa. hawa wasiomtaka wanamtaka nani? Mbowe?😕
no we need a new chairman.

Mbowe akiondoka mie nitachukua kadi ya chadema


Mkuu ni Mwenyekiti Mbowe tu ndio anakufanya usichukue kadi ya Chadema?Au kuna zaidi ya hilo? Nadhani Chadema ni kubwa/Pana zaidi ya Mbowe....Mbowe ni mwanachama tu kama walivyo wanachama wengine....Usiogope kujiunga na Chadema kwa sababu ya Mwanachama mmoja...Chadema ni chama inachoongozwa na Kanuni......Jali zaidi Katiba na kanuni za chama hicho na sio kuangalia mwanachama mmoja mmoja!
 
Slaa angefaa sana kuwa canditate wa CHADEMA ktk Uraisi wa nchi!

Slaa akiwa raisi wa nchi hii..Tanzania ingebadilika kuwa nchi nzuri zaidi kwa haraka!!

Vipi Mbowe hapendi tena uenyekiti??

Nimesikia Freeman anampisha mwingine katika nafasi hiyo ya Uongozi wa juu wa Chama,yeye anajikita zaidi katika kuutafuta Ubunge,anataka kuongeza nguvu za Upinzani Bungeni.

Kwa mtazamo wake ameona hatoweza kuwa Mwenyekiti na Mbunge kwa wakati mmoja,Lakini kwa mara ya kwanza Chadema wanaweza kuwa na Mwenyekiti wa Chama ambaye pia ni Mbunge kama ilivyo kwa UDP...Moja ya mikakati ya Chadema ni kuongeza Wabunge wengi wa Majimbo (Wabunge wa kuchaguliwa)
 
Hii ni sawa tu ndio demokrasia. Ingekuwa vizuri kama Mh Zitto akajikita kwenye ukatibu mkuu,, ili nguvu iwe kubwa zaidi.

Hilo la Mbowe kugombea ubunge naona ni uamuzi wa busara pia.

wana JF wangapi wanagombea kwa tiketi ya Chadema? manake wa CCM tumeshawasikia
 
Hili ndio tatizo la CHADEMA , nafikiri tayali Sultani CCM ameshapandikiza watu wake na sasa wapo katika kuhitimisha kukisambaratisha Chama hiki, afu CCM kwa vyama kama hivi vidogo vidogo inakuwa haina haraka wala hawafanyizii kama kule kwenye chama cha wababe CUF ambako CCM imegonga mwamba na sasa inaendeshwa puta.

Kitu kimoja napenda mkielewe kuwa katika Chadema kuna mambo ambayo wakuu wake wanashirikiana na wafuasi wa baadhi ya wakuu wa Sultani CCM ,katika maslahi ya kibiashara hapo ndio ukaona hiki chama huwa kinalega lega na kufikia hata wakati wanaungana na wateja wenzao wa CCM katika kufuatilia baadhi ya mambo ambayo yanawagusa kimaslahi.

Mkiambiwa Chadema sio Chama kinachoweza kumkomboa Mtanzania mnapanda peresha ,na kama mnataka ushahidi mnauona hapa JF ,siku hizi makada wa Chadema wamekuwa kama kuku waliotiwa kwenye gunia lililoloweshwa maji ,wamekaa kimya na kuduwaa wakingojea hatima ya uchaguzi wa chama chao uliojaa mizengwe na migawanyiko ,tatizo ninaloliona ni kuwa ndani ya CHADEMA hakuna security inayoweza kuwang'amua mamluki ambao wamejikita ndani ya chama kwa muda mrefu unaweza kuwafanisha na wale askari maalum wa kutunga na kuwaua watu maalum ndani ya vita au kwa jina la kijeshi wanaitwa snippers ,hawa snippers wa CCM wamejikita ndani ya vyama vya siasa vya upinzani na wametulia kikweli inataka mbinu za hali ya juu katika kuona mienendo yao. Tumeona kwenye uchaguzi wa CUF ni jinsi gani snippers wa CCM waliondolewa kwa kupigwa na chini wakiachwa wakipiga makelele,hawa snippers wa CCM wanaweza ukawaona ni viongozi imara kabisa ndani ya chama chako ambao wapo mstari wa mbele kila siku ,lakini shabaha yao ni kukivuruga chama na wakati muafaka wauonao ni mzuri ni huu wa uchagusi ndani ya Chama ,hapa ndipo wanapojaribu kucheza.

Nawatakia uchaguzi wenye utulivu ambao utajenga maelelwano ya kweli na vyama vingine vya upinzani kuliko huu umoja unaowaonyesha CHADEMA kama ndumila kuwili.
 
Kama tetesi hizi na zile za zito zina msingi wowote wa kuaminiwa, kwa nini wote wagombee uenyekiti? nadhani ingefaa mmojawapo katika hao wawili angegombea ukatibu mkuu, au wote wanataka kuwa wenye kauli ya mwisho? hata hivyo ni maamuzi yao na haki yao ya kidemokrasia, lakini ni vyema wakafikiria mbali.
 
Mungu wangu ibakishe salama walau Chadema, najuwa CCM wamekaa mkao wakula kuotea "machafuko" ndani ya Chadema. Tuwaombeeni Chadema wafanye mkutano wa kupanga safu zao kwa amani na utulivu na kukiimarisha chama chao. Kama habari hizo ni za kweli nawatakia chadema uchaguzi mwema na wapite salama katika jaribio hili la kimageuzi.
 
Hawa hawana itifaki na inaonyesha wanamatatizo makubwa sana ,yaani kuwepo kote kwa muda mrefu wakiwa viongozi wakuu ,wanaonyesha dalili za kuwa na matatizo ya ndani kabisa ,ninavyoamini ikiwa nyote ni wananchama wa chama kimoja na mmetoka mbali katika kukiendeleza chama chenu basi lazima mtakuwa na mashirikiano (strategy) za karibu kabisa na kuweza kumpanga Mwenyekiti ,ikiwa tu aliekuwepo atakumbwa na mauti au atasema basi, kupeleka watu wazito wawili katika kugombea nafasi ya juu ya Chama ni kuonyesha kuwa au ni kukigawa chama ,inaonyesha waChadema hawana maelewano ,nilivyotaraji labda angetokea mtu mwengine kabisa zaidi ya wale heads kutaka kugombea nafasi hiyo na sio vinara walio juu ,huko ni kukosa muelekeo na hapa Chadema watakuwa wamechemsha au labda iwe ni mbinu ya kutaka kuwadanganya waTz kuwa ndani ya Chama chao kuna demo na sio demokrasi.

Ilikuwa ni lazima awepo kiongozi katika top 10 wa Chadema ambae angeweza kuchukua nafasi ya kugombea pindipo Mwenyekiti aliekuwepo ameamua kubwaga manyanga ,na itakuwa wenyewe wawe wanalijua hilo na wawe wanamjua kwani ni jambo la kuridhiana kabisa katika harakati za kuendesha Chama kikuu na sio mnatokea kama mnaonekana mnanyang'anyia ,ni kukigawa Chama ,na hapo ikitokea kufikia kupigiwa kura na kuibuka mmoja kumshinda mwenziwe kwa kura kidogo basi mambo hayatakuwa mazuri & they will never be the same again ,ingawa watataka ionekane machoni mwa WaTz kuwa mambo ni kawaida na ndio demokrasia ilivyo ,ni sawa lakini not in that way at all and spesho in Tz.
 
Nafasi ya Katibu Mkuu haigombewi, nadhali anateuliwa na Kamati tendaji au kamati kuu.
Kama busara zitafanya kazi, Dr. Slaa awe M/kiti, Zitto Katibu Mkuu, Lwakatare Naibu M/kiti bara.
 
Mwiba, CUF imekukaa sana kichwani, sidhani kama CHADEMA wanaweza kudesa chochote toka katika ukiritimba wa uongozi wa CUF
 
Mwiba,
mkuu wangu hata sielewi unazungumza kitu gani.. Nani kasema mwenyekiti wa chama cha Chadema hana msaidizi wake kwani lini Chadema imefuta kiti cha makamu mwenyekiti. Ikiwa mwenyekiti ataondoka ghafla makamu atashika wadhifa wa mwenyekiti na pia sii lazima mfumo wa Uongozi wa CCM ndio unatumiwa na Chadema au chama chochote kingine, Yawezekana kabisa mwenyekiti wa Chadema hatagombea kiti cha Urais..au rais wa nchi kutokuwa mwenyekiti wa chama.
Inaonyesha wazi kuwa Dr.Slaa kuchukua form imewakuna kichizi....Na bado list ni kubwa..
 
Hawa hawana itifaki na inaonyesha wanamatatizo makubwa sana ,yaani kuwepo kote kwa muda mrefu wakiwa viongozi wakuu ,wanaonyesha dalili za kuwa na matatizo ya ndani kabisa ,ninavyoamini ikiwa nyote ni wananchama wa chama kimoja na mmetoka mbali katika kukiendeleza chama chenu basi lazima mtakuwa na mashirikiano (strategy) za karibu kabisa na kuweza kumpanga Mwenyekiti ,ikiwa tu aliekuwepo atakumbwa na mauti au atasema basi, kupeleka watu wazito wawili katika kugombea nafasi ya juu ya Chama ni kuonyesha kuwa au ni kukigawa chama ,inaonyesha waChadema hawana maelewano ,nilivyotaraji labda angetokea mtu mwengine kabisa zaidi ya wale heads kutaka kugombea nafasi hiyo na sio vinara walio juu ,huko ni kukosa muelekeo na hapa Chadema watakuwa wamechemsha au labda iwe ni mbinu ya kutaka kuwadanganya waTz kuwa ndani ya Chama chao kuna demo na sio demokrasi.

Ilikuwa ni lazima awepo kiongozi katika top 10 wa Chadema ambae angeweza kuchukua nafasi ya kugombea pindipo Mwenyekiti aliekuwepo ameamua kubwaga manyanga ,na itakuwa wenyewe wawe wanalijua hilo na wawe wanamjua kwani ni jambo la kuridhiana kabisa katika harakati za kuendesha Chama kikuu na sio mnatokea kama mnaonekana mnanyang'anyia ,ni kukigawa Chama ,na hapo ikitokea kufikia kupigiwa kura na kuibuka mmoja kumshinda mwenziwe kwa kura kidogo basi mambo hayatakuwa mazuri & they will never be the same again ,ingawa watataka ionekane machoni mwa WaTz kuwa mambo ni kawaida na ndio demokrasia ilivyo ,ni sawa lakini not in that way at all and spesho in Tz.

Ndugu yangu na rafiki yangu wa muda mrefu Mwiba (unayechoma), hatutaki kabisa kuiga siasa za CCM za itifaki isiyo na tija. Kama wote muna nia njema hakuna ubaya wote kufanya siasa za kweli na hilo likifanyika kwa dhati. Sioni ubaya wowote hata kama Mbowe naye akigombea na Slaa na Zitto na Mnyika naye achukue fomu. Hiyo ni habari njema kabisa. Si vyema ikawa kama ya Profesa Safari na Profesa Lipumba, ambao hawakuwa na maelewano bali Prof Safari alikwenda akiwa na ajenda ya kupambana kwa nia mbaya na Mwenyekiti wake na ndio maana alikuwa akitoa maneno mabaya hata kabla ya kuchukua fomu. Lakini kwa Chadema hadi sasa hakuna maneno mabaya kati ya viongozi hayo (ukiacha mambo ya chini chini ambayo hayana maana). Ikiwa watafanikiwa kuingia katika uchaguzi wote na wakashindana na atakayeshinda akakumbatiwa na walioshindwa na kuunda sekretarieti inayowaingiza walioshindwa. Tumechoka na U-CCM wa zidumu fikra za Mwenyekiti.

Naamini/Naomba iwe/ni vyema ikawa kwamba Mbowe na makamanda wake wameingia na gia kubwa ya kutwaa madaraka 2010 maana inawezekana njia ikawa nyeupe lakini wakiteleza tu, tujue kama Taifa TUMEKWISHA na tusahau kabisa kupata nafasi kama hii.

"Huu ni mwaka wa UHURU."
 
Mungu wangu ibakishe salama walau Chadema, najuwa CCM wamekaa mkao wakula kuotea "machafuko" ndani ya Chadema. Tuwaombeeni Chadema wafanye mkutano wa kupanga safu zao kwa amani na utulivu na kukiimarisha chama chao. Kama habari hizo ni za kweli nawatakia chadema uchaguzi mwema na wapite salama katika jaribio hili la kimageuzi.

Najua kwa sasa ni ndoto lakini inawezekana kwa Chadema na CUF wakashirikiana kuunda timu ya kampeni kwa Chadema kupambana bara na CUF Zanzibar na Pemba kwa ajili ya kupigania uhury wa Tanzania 2010. Hakuna sababu yoyote ya maana na sababu nyingi ni za kijinga (samahani wahusika) na za kibinafsi zaidi na sitosita kusema za KIFISADI za kuzuia vyama hivi kuungana kama ilivyokuwa mwaka 2000. Wananchi/wapiga kura wanataka kusikia hilo na si matakwa ya viongozi. Tembeeni musikilize watu na si kuwahutubia mutaona watu wanataka nini. Tembeeni si kusemana wenyewe kwa wenyewe bali kutumia nafasi zilizopo mikoani kujenga upinzani wa dhati. Mutakuwa wajinga (samahani tena) kuendelea kusubiri mkono udondoke (toka CCM) kama fisi mukirejea maneno ya Nyerere kwamba upinzani wa kweli utatoka CCM, huko ni kudumaa na kujidumaza kwamba "SISI HATUWEZI".... Kwanini hamuwezi? Nakumbuka mwaka 2000 tulikuwa na Lipumba mkoani Kagera, alitangaza Baraza lake la Mawaziri na Mbowe alitajwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Pale alikuwa na UHAKIKA wa ushindi kabla ya "KIZUNGUMKUTI" kutokea. Sijui IBILISI GANI AMEWAKUTA. INAUMA SANA MJOMBA.......!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom