Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Hili ndio tatizo la CHADEMA , nafikiri tayali Sultani CCM ameshapandikiza watu wake na sasa wapo katika kuhitimisha kukisambaratisha Chama hiki, afu CCM kwa vyama kama hivi vidogo vidogo inakuwa haina haraka wala hawafanyizii kama kule kwenye chama cha wababe CUF ambako CCM imegonga mwamba na sasa inaendeshwa puta.

Kitu kimoja napenda mkielewe kuwa katika Chadema kuna mambo ambayo wakuu wake wanashirikiana na wafuasi wa baadhi ya wakuu wa Sultani CCM ,katika maslahi ya kibiashara hapo ndio ukaona hiki chama huwa kinalega lega na kufikia hata wakati wanaungana na wateja wenzao wa CCM katika kufuatilia baadhi ya mambo ambayo yanawagusa kimaslahi.

Mkiambiwa Chadema sio Chama kinachoweza kumkomboa Mtanzania mnapanda peresha ,na kama mnataka ushahidi mnauona hapa JF ,siku hizi makada wa Chadema wamekuwa kama kuku waliotiwa kwenye gunia lililoloweshwa maji ,wamekaa kimya na kuduwaa wakingojea hatima ya uchaguzi wa chama chao uliojaa mizengwe na migawanyiko ,tatizo ninaloliona ni kuwa ndani ya CHADEMA hakuna security inayoweza kuwang'amua mamluki ambao wamejikita ndani ya chama kwa muda mrefu unaweza kuwafanisha na wale askari maalum wa kutunga na kuwaua watu maalum ndani ya vita au kwa jina la kijeshi wanaitwa snippers ,hawa snippers wa CCM wamejikita ndani ya vyama vya siasa vya upinzani na wametulia kikweli inataka mbinu za hali ya juu katika kuona mienendo yao. Tumeona kwenye uchaguzi wa CUF ni jinsi gani snippers wa CCM waliondolewa kwa kupigwa na chini wakiachwa wakipiga makelele,hawa snippers wa CCM wanaweza ukawaona ni viongozi imara kabisa ndani ya chama chako ambao wapo mstari wa mbele kila siku ,lakini shabaha yao ni kukivuruga chama na wakati muafaka wauonao ni mzuri ni huu wa uchagusi ndani ya Chama ,hapa ndipo wanapojaribu kucheza.

Nawatakia uchaguzi wenye utulivu ambao utajenga maelelwano ya kweli na vyama vingine vya upinzani kuliko huu umoja unaowaonyesha CHADEMA kama ndumila kuwili.

Huyu naye......na dua la kuku kamwe haliwapati mwewe, wataendelea kukudonowa hadi ubaki mifupa...

omarilyas
 
Mwiba, CUF imekukaa sana kichwani, sidhani kama CHADEMA wanaweza kudesa chochote toka katika ukiritimba wa uongozi wa CUF
Kibunango, rangi ya kijani inakuuuma kweli,umeivaa hasa, hee!!
......Inaonyesha wazi kuwa Dr.Slaa kuchukua form imewakuna kichizi....Na bado list ni kubwa..
Mkandara ww utagombea nafasi gani, nlikuwa sijuwi kama ww chadema ati!!
 
Mwiba,
mkuu wangu hata sielewi unazungumza kitu gani.. Nani kasema mwenyekiti wa chama cha Chadema hana msaidizi wake kwani lini Chadema imefuta kiti cha makamu mwenyekiti. Ikiwa mwenyekiti ataondoka ghafla makamu atashika wadhifa wa mwenyekiti na pia sii lazima mfumo wa Uongozi wa CCM ndio unatumiwa na Chadema au chama chochote kingine, Yawezekana kabisa mwenyekiti wa Chadema hatagombea kiti cha Urais..au rais wa nchi kutokuwa mwenyekiti wa chama.
Inaonyesha wazi kuwa Dr.Slaa kuchukua form imewakuna kichizi....Na bado list ni kubwa..


Mimi nafikiri hujamwelewa mwiba ana maanisha nini,hasa kwa siasa za tz.
 
Najua kwa sasa ni ndoto lakini inawezekana kwa Chadema na CUF wakashirikiana kuunda timu ya kampeni kwa Chadema kupambana bara na CUF Zanzibar na Pemba kwa ajili ya kupigania uhury wa Tanzania 2010. Hakuna sababu yoyote ya maana na sababu nyingi ni za kijinga (samahani wahusika) na za kibinafsi zaidi na sitosita kusema za KIFISADI za kuzuia vyama hivi kuungana kama ilivyokuwa mwaka 2000. Wananchi/wapiga kura wanataka kusikia hilo na si matakwa ya viongozi. Tembeeni musikilize watu na si kuwahutubia mutaona watu wanataka nini. Tembeeni si kusemana wenyewe kwa wenyewe bali kutumia nafasi zilizopo mikoani kujenga upinzani wa dhati. Mutakuwa wajinga (samahani tena) kuendelea kusubiri mkono udondoke (toka CCM) kama fisi mukirejea maneno ya Nyerere kwamba upinzani wa kweli utatoka CCM, huko ni kudumaa na kujidumaza kwamba "SISI HATUWEZI".... Kwanini hamuwezi? Nakumbuka mwaka 2000 tulikuwa na Lipumba mkoani Kagera, alitangaza Baraza lake la Mawaziri na Mbowe alitajwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Pale alikuwa na UHAKIKA wa ushindi kabla ya "KIZUNGUMKUTI" kutokea. Sijui IBILISI GANI AMEWAKUTA. INAUMA SANA MJOMBA.......!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Upo sahihi Mkuu, tatizo nia ya dhati ya viongozi wetu wa kisiasa.
 
Najua kwa sasa ni ndoto lakini inawezekana kwa Chadema na CUF wakashirikiana kuunda timu ya kampeni kwa Chadema kupambana bara na CUF Zanzibar na Pemba kwa ajili ya kupigania uhury wa Tanzania 2010. Hakuna sababu yoyote ya maana na sababu nyingi ni za kijinga (samahani wahusika) na za kibinafsi zaidi na sitosita kusema za KIFISADI za kuzuia vyama hivi kuungana kama ilivyokuwa mwaka 2000. Wananchi/wapiga kura wanataka kusikia hilo na si matakwa ya viongozi. Tembeeni musikilize watu na si kuwahutubia mutaona watu wanataka nini. Tembeeni si kusemana wenyewe kwa wenyewe bali kutumia nafasi zilizopo mikoani kujenga upinzani wa dhati. Mutakuwa wajinga (samahani tena) kuendelea kusubiri mkono udondoke (toka CCM) kama fisi mukirejea maneno ya Nyerere kwamba upinzani wa kweli utatoka CCM, huko ni kudumaa na kujidumaza kwamba "SISI HATUWEZI".... Kwanini hamuwezi? Nakumbuka mwaka 2000 tulikuwa na Lipumba mkoani Kagera, alitangaza Baraza lake la Mawaziri na Mbowe alitajwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Pale alikuwa na UHAKIKA wa ushindi kabla ya "KIZUNGUMKUTI" kutokea. Sijui IBILISI GANI AMEWAKUTA. INAUMA SANA MJOMBA.......!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

theory na practical ni vitu viwili vilivyo na mtazamo unaoelekeana lakini ktk uhalisia ni vitu viwili tofauti.
 
Hakuna cha theory bwana Mkapa, hilo linawezekana na liliwezekana 2000.
 
Huyu naye......na dua la kuku kamwe haliwapati mwewe, wataendelea kukudonowa hadi ubaki mifupa...

omarilyas

Kama Omar, pamoja na kwamba Mwiba ana lake jambo kuhusu Chadema, na ndio maana mara nyingi huwa natofautiana naye lakini bado kuna eneo ambalo hoja yake ina nguvu. Hoja yake ina nguvu katika kuhakikisha vyama vyote vya upinzani (ikiwamo Chadema na CUF) ni lazima viwe na mtandao mkali wa kiintelijensia kukabiliana na mbinu za chama tawala.

Hili naamini linahitaji gharama na muda lakini zaidi utashi, ari na kujituma. Mwiba anaweza kuwa ana watu anawalenga, lakini la msingi ni vyema kila chama kikatafuta ushauri wa kitaalamu katika kung'amua kila aina ya mbinu chafu. Wapo watu wenye uwezo na ambao wanaweza kuifanya kazi hiyo bureee!

Lakini pia si vyama vya siasa pekee, hata JF na media nao wawe macho.
 
Yaani Mkapa(fisadi papa No.6) ni jina kubwa.
Umezipata wapi fikra hizi za "ki-halmashauri kuu ya taifa CCM?"

Teh teh teh mumeambiwa mumuache ni mtaafu huyo hahahahah.....asiguswe!
 
kama hawachezi drama ngoja mheshimiwa utakumbuka maneno ya mwiba

Sorry MkamaP kukuita Mkapa>>> Tukirudi kwenye mada maneno yako yana uzito mkubwa, lakini nilishasema hakuna theory kwa kuwa inawezekana na hata wakivurunda pia si theory ni wameamua tu hakuna bahati mbaya hapo
 
Yaani Mkapa(fisadi papa No.6) ni jina kubwa.
Umezipata wapi fikra hizi za "ki-halmashauri kuu ya taifa CCM?"

Mtakuwa hamlitendi jina haki,maana kabla ya mwaka 1995 aliyejulikana sana mkapa ni benki no 3 wa yanga Keneth Mkapa, sasa sijui ninyi mna mrefer nani?
 
Sorry MkamaP kukuita Mkapa>>> Tukirudi kwenye mada maneno yako yana uzito mkubwa, lakini nilishasema hakuna theory kwa kuwa inawezekana na hata wakivurunda pia si theory ni wameamua tu hakuna bahati mbaya hapo

wenye mapendo na Taifa hili ni wachache (wenda wasiwepo kabisa)wengi wanakwenda kwa mi target yao wenyewe wanayoijuwa.
 
Mtakuwa hamlitendi jina haki,maana kabla ya mwaka 1995 aliyejulikana sana mkapa ni benki no 3 wa yanga Keneth Mkapa, sasa sijui ninyi mna mrefer nani?

Yeah Mzee wa Lupaso alikuwa hajulikani sana kabla ya 1995, wengi walikuwa wanamjua Keneth Mkapa wa Yanga....lakini baada ya 2005 ameonyesha uhalisia wake wa ufisadi.
 
CCM inawakuna sana mwaka huu Eeeh!
.......saaaaana tu manake mikwaju mtu na maisha bora nayo....!!!!???
Mtakuwa hamlitendi jina haki,maana kabla ya mwaka 1995 aliyejulikana sana mkapa ni benki no 3 wa yanga Keneth Mkapa, sasa sijui ninyi mna mrefer nani?
Mkapa halitendei haki jina lake mwenyewe badala ya kuji-defend na tuhumu za ufisadi zinazochafua jina lake, yeye kashika kuchochea Sitta an'ngolewe eti anaruhusu wabunge kumtaja taja tuuuuuuuu wakati Chama kimeshaliagiza bunge(Pinda's statement in Parliament) limwache apumzike afaidi ngawira za walalahoi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom