Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Tabia iliyoanzishwa ndani ya CHADEMA ya jinsi ya kupambana na wasioafikiana na viongozi wa juu ndio inayokiyumbisha chama hivi sasa.

Ukiangalia hapa unaona wazi muendelezo wa yale yaliyokifika chama wakati wa mgogoro wa Wangwe vs Mbowe & Makao Makuu.

Kutamani madaraka ndani ya chama sasa imekuwa ni kifo cha mhusika kisiasa, sidhani kama hii ni tofauti sana na CCM.

Kwa nini CHADEMA isijitofautishe na CCM kuanzia kimfumo na hadi utendaji huku wakizingatia zaidi sheria na taratibu zilizokubalika?

Inasikitisha sana kuona DEMOKRASIA ndani ya CHADEMA iki-minywa hadharani kama ilivyo ndani ya CCM.
 
unajua unapokutana na sentiments kama hizi miongoni mwa wanachadema wanaopambana na zitto unaweza kuanza kujiuliza kama issue hapa ilikuwa ni kupingwa mbowe tu ama kuna mengine yamejificha.

Halafu zitto akimjibu mtu kama huyu mtamwita mdini, mbaguzi, mkabila....

Hivi hamuoni waathirika wa chuki za kidini na kikabila kama hawa?

Omarilyas
wasamehe wamechanganyikiwa hao vibaraka wa vikongwe vya chadema vilivyoyumia penseni zao vibaya.anataka kututoa kwenye mada mie nimeshamshtukia.hapa wanajitahidi kuuzima mjadala huu.
 
blank.gif
logo2.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
bullet1.gif
HABARI MPYA
bullet1.gif
LA JANA
bullet1.gif
MATANGAZO
bullet1.gif
BEI ZETU
bullet1.gif
WASILIANA NASI
bullet1.gif
TUMA HABARI
bullet1.gif
blank.gif
blank.gif
l_ban.jpg
banner.jpg
blank.gif
jumatano, 2 septemba 2009
Yaliyopita​
" 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 2009 2008 2007 2006
blank.gif

Pekua Tovuti​
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif
blank.gif

h.sep7.gif
master.gif

CHADEMA, kiberiti kimejaa
ban.tuendako.jpg


Absalom Kibanda

amka2.gif

ZITTO Zubeir Kabwe, amefanikiwa kumtikisa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe na chama hicho na kwa hakika bado anaendelea kukiweka roho joho wakati huu anapoendelea kujipanga kisiasa ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani.
Ni wazi kwamba mwangwi wa kishindo cha uamuzi wa Zitto kuamua kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya juu kabisa ya kimadaraka ndani ya chama hicho akikabiliana na Mbowe kabla hajafikia makubaliano na ushauri wa kamati ya wazee wa chama hicho bado unaendelea kukisika ndani na nje ya chama hicho.

Nikiwa miongoni mwa watu ambao tumekuwa tukiitakia mema CHADEMA na hata kuthamini kwa dhati mchango madhubuti wa viongozi wa chama hicho na wanachama wake katika kuimarisha mfumo wa ushindani wa vyama vingi tangu kuzaliwa kwake na hususan kuanzia mwaka 2005 walipomsimamisha Mbowe kuwa mgombea urais, nilipatwa na hofu kubwa kuhusu aina ya mabadiliko ya kiuongozi ambayo chama hicho kinaelekea kuyakamilisha wiki hii.
Si kwamba nilikuwa na hofu kwa kuwa nayaogopa mabadiliko ya kidemokrasia, bali kikubwa kilichokuwa kikinisumbua ni ukweli kwamba, chama hicho kilikuwa kikifanya mabadiliko wakati huu taifa linapojiandaa kwa ajili ya chaguzi kuu mbili, ule wa serikali za mitaa unaokuja siku chache zijazo na Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwakani.
Hofu yangu kuhusu hofu hii ya mabadiliko ambayo yangeweza kuwa ya hatari, ilizidi kuongezeka kila mara nilipokuwa nikiyasoma magazeti ama ya serikali au yale yanayomilikiwa moja kwa moja kwa njia za panya na mawakala au makada wa kimikakati wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Nilipoanza kusoma habari katika magazeti hayo na kuona namna yalivyokuwa yakishabikia kwa mapana na marefu mpasuko ndani ya CHADEMA mara moja kengele ya hatari ilionekana kuanza kugonga kichwani mwangu na mwangwi wake ukanisukuma kuandika makala yangu ya wiki iliyopita iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho; ‘Naliona anguko la Zitto Kabwe'.

Kama hiyo haitoshi, mazungumzo ya ana kwa ana na yale ya njia ya simu ambayo niliyafanya na vijana mbalimbali walio ndani ya CCM wakiwamo wale walio na ushawishi mkubwa katika Jumuiya ya Vijana ya chama hicho tawala (UVCCM) na wabunge na kuwasikia namna walivyokuwa wakiufuatilia kwa umakini mkubwa uchaguzi wa CHADEMA na takriban wote wakisisitiza haja ya kufanyika kwa mabadiliko ya kiuongozi, mara moja niliiona hatari ikija.

Ilipofika hatua ya Zitto kuchukua fomu, ghafla homa ya uchaguzi ndani ya CHADEMA ikazidi kupanda na takriban vijana (siyo wote) wa CCM ambao wamekuwa na mawasiliano ya kirafiki na mwanasiasa mwenzao kijana kwa muda mrefu, walichukua maamuzi ya kumuunga mkono kwa nguvu kubwa na wote wakarejesha hoja nyingi zilizokuwa zikionyesha udhaifu mkubwa wa viongozi takriban wote wa chama hicho.

Ilipofikia hatua hiyo, mara Mbowe, Dk. Willibrod Slaa, Mnyika, Halima Mdee, Grace Kiwelu, John Mnyika na viongozi wengine wote wa CHADEMA ukimuacha Zitto wakaanza kuonekana kuwa ni watu wasiofaa, wakionekana kuwa hivyo ndani ya chama hicho na nje.

Katika mnyumbuliko huo huo, ndani ya CHADEMA ghafla taswira ya Zitto mwenyewe ikaanza kujipambanua na hali ikazidi kuwa bayana aliporejea kutoka nchini Ujerumani alikokuwa amekwenda kwa shughuli maalum ya ushauri kwa rais wa nchi hiyo. Nguvu zake halisi zikaanza kubainika.

Kile ambacho awali kilionekana kuwa ni uamuzi wake wa kujaribu kutikisa tu kiberiti kikaanza kubadilika kwa haraka na mara Zitto akajitokeza na kuwa tishio la wazi kwa uenyekiti wa Mbowe na kwa hakika akaanza kuwa tishio la majaliwa ya kisiasa ya chama hicho na kambi nzima ya upinzani wakati huu akili za Watanzania wadadisi wa mambo wanapoangalia mustakabali mwema wa ushindani mkali wa kidemokrasia hapa nchini. Ni bahati tu kwamba kiberiti kingali kimejaa.

Kwa hakika tafsiri yangu ya haraka haraka ikanipa jibu moja tu tena la haraka kwamba, maamuzi hayo ya Zitto yalikuwa kwa makusudi kwa ujinga wa wapambe wake wa kushindwa kuona mambo kuwa ulikuwa ikilenga kumhakikishia Rais Jakaya Kikwete ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 80 alizokuwa amezipata mwaka 2005.

Ingawa baadhi ya watu wanaweza wakadhani mimi ni mwendawazimu ninapoliangalia tukio la Zitto kugombea uenyekiti wa CHADEMA wakati huu na kuwapo kwa jitihada za makusudi za kumsafishia Kikwete njia mwaka ujao, ukweli unabaki pale pale kwamba, makosa yoyote ya kisiasa yanayoweza kufanywa na viongozi waadilifu ndani ya vyama viwili vya CUF na CHADEMA wakati huu, yana nafasi kubwa ya kumhakikishia Rais wetu ahueni kubwa.

Ukiliacha hilo, mara moja nikakiona kitendo hicho cha Zitto mwanasiasa ambaye siku zote nimekuwa nikimuunga mkono anaposimamia na kupigania masuala ya msingi, cha kuamua kuutumia vibaya mwanya wa kidemokrasia wa kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA kuwa kilichokuwa kikilenga kwa kujua au kutojua, kupunguza makali na kasi ya chama hicho cha kushinda viti vingi katika chaguzi za serikali ya mitaa, udiwani na baadaye ubunge.

Nilipojiridhisha kwamba hayo yote yanaweza kutokea kwa sababu tu ya uamuzi wa Zitto kugombea uenyekiti na yakafuata hata kama atashinda au kushindwa katika mchuano huo, nikaona nitakuwa sikuitendea haki ndoto yangu ya siku zote ya kuona demokrasia ya vyama vingi inastawi katika nchi hii ambayo kwa takriban miaka 20 tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi CCM imeendelea kujivunia rekodi madhubuti dhidi ya upinzani.

Nilipoamua kuandika makala ya karipio na onyo dhidi ya Zitto katika safu hii, baadhi ya wasomaji wangu kwa makusudi au kwa kutojua wakakimbilia kuanza kunihukumu wengine wakisema najipendekeza kwa Mbowe ambaye ni mwajiri wangu, naganga njaa, nakandamiza demokrasia na wengine wakasema eti namzuia Zitto kutumia kipaji chake cha uongozi.

Ushawishi wote wa kundi hilo, ambao kwa kiwango kikubwa ulichagizwa na upotoshwaji mkubwa wa hoja yangu uliokuwa ikiratibiwa kwa karibu na vijana wa ndani wa CHADEMA waliokuwa wakimpigania Zitto na wale wa CCM na mawakala wao serikalini ulishindwa kulizuia Baraza la Wazee wa chama hicho, kumuacha kabla ya kumzuia kijana wao, kukiingiza chama chake na taifa katika balaa kwa kumsafishia Kikwete na chama chake mteremko. Ni jambo la kheri kwamba Zitto kwa dhati au kwa shingo upande aliliona hilo.

Kama alivyoandika Ansbert Ngurumo katika safu yake ya Maswali Magumu katika gazeti hili Jumapili iliyopita, Zitto na wapambe wake ambao nilifikia hatua ya kuwaita wajinga ambao waliamua kufumba macho na kuendelea kushangilia makosa ya kumruhusu Zitto kukimega chama ambacho siku zote amekuwa akionyesha kwa vitendo kubwa anakipenda kwa dhati wanapaswa kutulia na kutafakari kwa kina ni kitu gani hasa CCM na mawakala wake walikuwa wakikitafuta kutoka kwake hata ghafla kuanza kukiombea CHADEMA mema?

Kwa hakika unahitaji kuwa na akili za kuku za kusahau mapema ili kujidanganya kwamba, vijana ambao ni wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji au wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), wabunge, mawaziri na wanasiasa wengine serikalini wanaweza wakawa na mapenzi mema na CHADEMA hata kukiombea mema chama hicho wakati huu wakijua kuwa mwelekeo wa taifa ni Uchaguzi Mkuu ujao.
Hivi kweli wanasiasa katika vyama vya upinzani na Watanzania wengine hawajui kwamba, ndani ya vikao takriban vyote vya CCM na jumuiya zake, katika miezi na siku za hivi karibuni wamekuwa wakijadili namna wanavyoweza kushiriki katika kudhoofisha nguvu za CHADEMA kwa Tanzania Bara (baada ya kuidhoofisha CUF) na CUF kwa upande wa Zanzibar?

Hivi akina Mbowe, Slaa, Zitto, na wazee wa chama hicho wanaoongozwa na Mzee Edwin Mtei wamechukua hatua gani ili kuanzisha mchakato mahususi wa kufanya uchunguzi wa kina utakaowawezesha kubaini ni kwa kiwango gani nguvu za kifedha au za kiushawishi kutoka CCM na kwa mawakala wake zimefanikiwa kupenya akili za vijana na wazee wengi ndani ya chama hicho pasipo kujua au kwa kujua kiasi cha kujikuta wakiwa majeruhi wa kushabikia ujinga ambao kwa vyovyote vile matokeo yake yalikuwa yakiwachulia wao na chama chao anguko la kihistoria?

Maswali kama hayo tunapaswa kujiuliza hata sisi wana habari ambao kama ilivyokuwa kwa vigogo hao wa CHADEMA kwamba ni kwa kiasi gani kalamu zetu zimechochea au kudhoofisha jitihada mahususi ambazo ziko wazi na zinazolenga kukisambaratisha chama hicho cha upinzani ambacho hakuna shaka kimejipambanua kuwa chama shupavu katika miaka ya hivi karibuni?

Wakati sote tukitafuta majibu ya maswali hayo, tunao wajibu wa kutambua kwamba, pamoja na uamuzi wa Zitto kutangaza kujitoa katika kinyang'anyiro cha uenyekiti, ile sumu kali ambayo tayari imeshapenya mishipa ya uongozi ya chama hicho, haina budi kutafutiwa dawa mahususi ya kuipatia tiba ya haraka kwani tayari vijana wa kazi wa CCM na mawakala wao wameshatamba kwamba wameshakiachia vidonda vingi chama hicho ambavyo wanadai vitaendelea kukitesa hadi wakati wa chaguzi zijazo. Kwa sababu hiyo basi, ninaweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba, kile ambacho leo hii kinaendelea kuelezwa na kusisitizwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa ni demokrasia kandamizi ya ndani ya CHADEMA (eti kwa sababu ya uamuzi wa wazee wa CHADEMA kumzuia Zitto kugombea uenyekiti) si tu kwamba ni majuto ya kukwama kwa ajenda yao, bali ni mkakati mbadala wa kuendelea kukiumiza chama hicho kwa malengo ya kisiasa. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo.
 
Na Absalom Kibanda

ZITTO Zubeir Kabwe, amefanikiwa kumtikisa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe na chama hicho na kwa hakika bado anaendelea kukiweka roho joho wakati huu anapoendelea kujipanga kisiasa ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani.

Ni wazi kwamba mwangwi wa kishindo cha uamuzi wa Zitto kuamua kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya juu kabisa ya kimadaraka ndani ya chama hicho akikabiliana na Mbowe kabla hajafikia makubaliano na ushauri wa kamati ya wazee wa chama hicho bado unaendelea kukisika ndani na nje ya chama hicho.

Nikiwa miongoni mwa watu ambao tumekuwa tukiitakia mema CHADEMA na hata kuthamini kwa dhati mchango madhubuti wa viongozi wa chama hicho na wanachama wake katika kuimarisha mfumo wa ushindani wa vyama vingi tangu kuzaliwa kwake na hususan kuanzia mwaka 2005 walipomsimamisha Mbowe kuwa mgombea urais, nilipatwa na hofu kubwa kuhusu aina ya mabadiliko ya kiuongozi ambayo chama hicho kinaelekea kuyakamilisha wiki hii.

Si kwamba nilikuwa na hofu kwa kuwa nayaogopa mabadiliko ya kidemokrasia, bali kikubwa kilichokuwa kikinisumbua ni ukweli kwamba, chama hicho kilikuwa kikifanya mabadiliko wakati huu taifa linapojiandaa kwa ajili ya chaguzi kuu mbili, ule wa serikali za mitaa unaokuja siku chache zijazo na Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwakani.

Hofu yangu kuhusu hofu hii ya mabadiliko ambayo yangeweza kuwa ya hatari, ilizidi kuongezeka kila mara nilipokuwa nikiyasoma magazeti ama ya serikali au yale yanayomilikiwa moja kwa moja kwa njia za panya na mawakala au makada wa kimikakati wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Nilipoanza kusoma habari katika magazeti hayo na kuona namna yalivyokuwa yakishabikia kwa mapana na marefu mpasuko ndani ya CHADEMA mara moja kengele ya hatari ilionekana kuanza kugonga kichwani mwangu na mwangwi wake ukanisukuma kuandika makala yangu ya wiki iliyopita iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho; ‘Naliona anguko la Zitto Kabwe’.

Kama hiyo haitoshi, mazungumzo ya ana kwa ana na yale ya njia ya simu ambayo niliyafanya na vijana mbalimbali walio ndani ya CCM wakiwamo wale walio na ushawishi mkubwa katika Jumuiya ya Vijana ya chama hicho tawala (UVCCM) na wabunge na kuwasikia namna walivyokuwa wakiufuatilia kwa umakini mkubwa uchaguzi wa CHADEMA na takriban wote wakisisitiza haja ya kufanyika kwa mabadiliko ya kiuongozi, mara moja niliiona hatari ikija.

Ilipofika hatua ya Zitto kuchukua fomu, ghafla homa ya uchaguzi ndani ya CHADEMA ikazidi kupanda na takriban vijana (siyo wote) wa CCM ambao wamekuwa na mawasiliano ya kirafiki na mwanasiasa mwenzao kijana kwa muda mrefu, walichukua maamuzi ya kumuunga mkono kwa nguvu kubwa na wote wakarejesha hoja nyingi zilizokuwa zikionyesha udhaifu mkubwa wa viongozi takriban wote wa chama hicho.

Ilipofikia hatua hiyo, mara Mbowe, Dk. Willibrod Slaa, Mnyika, Halima Mdee, Grace Kiwelu, John Mnyika na viongozi wengine wote wa CHADEMA ukimuacha Zitto wakaanza kuonekana kuwa ni watu wasiofaa, wakionekana kuwa hivyo ndani ya chama hicho na nje.

Katika mnyumbuliko huo huo, ndani ya CHADEMA ghafla taswira ya Zitto mwenyewe ikaanza kujipambanua na hali ikazidi kuwa bayana aliporejea kutoka nchini Ujerumani alikokuwa amekwenda kwa shughuli maalum ya ushauri kwa rais wa nchi hiyo. Nguvu zake halisi zikaanza kubainika.

Kile ambacho awali kilionekana kuwa ni uamuzi wake wa kujaribu kutikisa tu kiberiti kikaanza kubadilika kwa haraka na mara Zitto akajitokeza na kuwa tishio la wazi kwa uenyekiti wa Mbowe na kwa hakika akaanza kuwa tishio la majaliwa ya kisiasa ya chama hicho na kambi nzima ya upinzani wakati huu akili za Watanzania wadadisi wa mambo wanapoangalia mustakabali mwema wa ushindani mkali wa kidemokrasia hapa nchini. Ni bahati tu kwamba kiberiti kingali kimejaa.

Kwa hakika tafsiri yangu ya haraka haraka ikanipa jibu moja tu tena la haraka kwamba, maamuzi hayo ya Zitto yalikuwa kwa makusudi kwa ujinga wa wapambe wake wa kushindwa kuona mambo kuwa ulikuwa ikilenga kumhakikishia Rais Jakaya Kikwete ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 80 alizokuwa amezipata mwaka 2005.

Ingawa baadhi ya watu wanaweza wakadhani mimi ni mwendawazimu ninapoliangalia tukio la Zitto kugombea uenyekiti wa CHADEMA wakati huu na kuwapo kwa jitihada za makusudi za kumsafishia Kikwete njia mwaka ujao, ukweli unabaki pale pale kwamba, makosa yoyote ya kisiasa yanayoweza kufanywa na viongozi waadilifu ndani ya vyama viwili vya CUF na CHADEMA wakati huu, yana nafasi kubwa ya kumhakikishia Rais wetu ahueni kubwa.

Ukiliacha hilo, mara moja nikakiona kitendo hicho cha Zitto mwanasiasa ambaye siku zote nimekuwa nikimuunga mkono anaposimamia na kupigania masuala ya msingi, cha kuamua kuutumia vibaya mwanya wa kidemokrasia wa kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA kuwa kilichokuwa kikilenga kwa kujua au kutojua, kupunguza makali na kasi ya chama hicho cha kushinda viti vingi katika chaguzi za serikali ya mitaa, udiwani na baadaye ubunge.

Nilipojiridhisha kwamba hayo yote yanaweza kutokea kwa sababu tu ya uamuzi wa Zitto kugombea uenyekiti na yakafuata hata kama atashinda au kushindwa katika mchuano huo, nikaona nitakuwa sikuitendea haki ndoto yangu ya siku zote ya kuona demokrasia ya vyama vingi inastawi katika nchi hii ambayo kwa takriban miaka 20 tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi CCM imeendelea kujivunia rekodi madhubuti dhidi ya upinzani.

Nilipoamua kuandika makala ya karipio na onyo dhidi ya Zitto katika safu hii, baadhi ya wasomaji wangu kwa makusudi au kwa kutojua wakakimbilia kuanza kunihukumu wengine wakisema najipendekeza kwa Mbowe ambaye ni mwajiri wangu, naganga njaa, nakandamiza demokrasia na wengine wakasema eti namzuia Zitto kutumia kipaji chake cha uongozi.

Ushawishi wote wa kundi hilo, ambao kwa kiwango kikubwa ulichagizwa na upotoshwaji mkubwa wa hoja yangu uliokuwa ikiratibiwa kwa karibu na vijana wa ndani wa CHADEMA waliokuwa wakimpigania Zitto na wale wa CCM na mawakala wao serikalini ulishindwa kulizuia Baraza la Wazee wa chama hicho, kumuacha kabla ya kumzuia kijana wao, kukiingiza chama chake na taifa katika balaa kwa kumsafishia Kikwete na chama chake mteremko. Ni jambo la kheri kwamba Zitto kwa dhati au kwa shingo upande aliliona hilo.

Kama alivyoandika Ansbert Ngurumo katika safu yake ya Maswali Magumu katika gazeti hili Jumapili iliyopita, Zitto na wapambe wake ambao nilifikia hatua ya kuwaita wajinga ambao waliamua kufumba macho na kuendelea kushangilia makosa ya kumruhusu Zitto kukimega chama ambacho siku zote amekuwa akionyesha kwa vitendo kubwa anakipenda kwa dhati wanapaswa kutulia na kutafakari kwa kina ni kitu gani hasa CCM na mawakala wake walikuwa wakikitafuta kutoka kwake hata ghafla kuanza kukiombea CHADEMA mema?

Kwa hakika unahitaji kuwa na akili za kuku za kusahau mapema ili kujidanganya kwamba, vijana ambao ni wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji au wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), wabunge, mawaziri na wanasiasa wengine serikalini wanaweza wakawa na mapenzi mema na CHADEMA hata kukiombea mema chama hicho wakati huu wakijua kuwa mwelekeo wa taifa ni Uchaguzi Mkuu ujao.

Hivi kweli wanasiasa katika vyama vya upinzani na Watanzania wengine hawajui kwamba, ndani ya vikao takriban vyote vya CCM na jumuiya zake, katika miezi na siku za hivi karibuni wamekuwa wakijadili namna wanavyoweza kushiriki katika kudhoofisha nguvu za CHADEMA kwa Tanzania Bara (baada ya kuidhoofisha CUF) na CUF kwa upande wa Zanzibar?

Hivi akina Mbowe, Slaa, Zitto, na wazee wa chama hicho wanaoongozwa na Mzee Edwin Mtei wamechukua hatua gani ili kuanzisha mchakato mahususi wa kufanya uchunguzi wa kina utakaowawezesha kubaini ni kwa kiwango gani nguvu za kifedha au za kiushawishi kutoka CCM na kwa mawakala wake zimefanikiwa kupenya akili za vijana na wazee wengi ndani ya chama hicho pasipo kujua au kwa kujua kiasi cha kujikuta wakiwa majeruhi wa kushabikia ujinga ambao kwa vyovyote vile matokeo yake yalikuwa yakiwachulia wao na chama chao anguko la kihistoria?

Maswali kama hayo tunapaswa kujiuliza hata sisi wana habari ambao kama ilivyokuwa kwa vigogo hao wa CHADEMA kwamba ni kwa kiasi gani kalamu zetu zimechochea au kudhoofisha jitihada mahususi ambazo ziko wazi na zinazolenga kukisambaratisha chama hicho cha upinzani ambacho hakuna shaka kimejipambanua kuwa chama shupavu katika miaka ya hivi karibuni?

Wakati sote tukitafuta majibu ya maswali hayo, tunao wajibu wa kutambua kwamba, pamoja na uamuzi wa Zitto kutangaza kujitoa katika kinyang’anyiro cha uenyekiti, ile sumu kali ambayo tayari imeshapenya mishipa ya uongozi ya chama hicho, haina budi kutafutiwa dawa mahususi ya kuipatia tiba ya haraka kwani tayari vijana wa kazi wa CCM na mawakala wao wameshatamba kwamba wameshakiachia vidonda vingi chama hicho ambavyo wanadai vitaendelea kukitesa hadi wakati wa chaguzi zijazo.

Kwa sababu hiyo basi, ninaweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba, kile ambacho leo hii kinaendelea kuelezwa na kusisitizwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa ni demokrasia kandamizi ya ndani ya CHADEMA (eti kwa sababu ya uamuzi wa wazee wa CHADEMA kumzuia Zitto kugombea uenyekiti) si tu kwamba ni majuto ya kukwama kwa ajenda yao, bali ni mkakati mbadala wa kuendelea kukiumiza chama hicho kwa malengo ya kisiasa. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo.

kibanda ameendelea kumshambulia ZITTO na kuwaita kina KITILA WAJINGA.MAKALA HII KAIWEKA TANZANIA DAIMA JUMATANO HII.
 
Last edited:
Kaka kibanda utanisamehe maana uvumilivu umenishinda...



Si kwamba nilikuwa na hofu kwa kuwa nayaogopa mabadiliko ya kidemokrasia, bali kikubwa kilichokuwa kikinisumbua ni ukweli kwamba, chama hicho kilikuwa kikifanya mabadiliko wakati huu taifa linapojiandaa kwa ajili ya chaguzi kuu mbili, ule wa serikali za mitaa unaokuja siku chache zijazo na Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwakani.
Ungewashauri wasiitishe uchaguzi kabisa kama huamini kuwa CHADEMA hawana uwezo wa kuwa na uchaguzi bila ya kuhofia chama kuvunjika. Na kama hali ni hiyo ina maana ulitaka kulaghai watanzania wasimike imani yao katika nyumba isiyo na nguzo hata za kuzuia upepo wa kawaida?
.

Nilipoanza kusoma habari katika magazeti hayo na kuona namna yalivyokuwa yakishabikia kwa mapana na marefu mpasuko ndani ya CHADEMA mara moja kengele ya hatari ilionekana kuanza kugonga kichwani mwangu na mwangwi wake ukanisukuma kuandika makala yangu ya wiki iliyopita iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho; ‘Naliona anguko la Zitto Kabwe’.

Kama hiyo haitoshi, mazungumzo ya ana kwa ana na yale ya njia ya simu ambayo niliyafanya na vijana mbalimbali walio ndani ya CCM wakiwamo wale walio na ushawishi mkubwa katika Jumuiya ya Vijana ya chama hicho tawala (UVCCM) na wabunge na kuwasikia namna walivyokuwa wakiufuatilia kwa umakini mkubwa uchaguzi wa CHADEMA na takriban wote wakisisitiza haja ya kufanyika kwa mabadiliko ya kiuongozi, mara moja niliiona hatari ikija.
Hii haina tofauti na maamuzi ya Mugabe na wenzake wengine wanakandamiza mabadiliko kwa kisingizio kuwa wazungu wanafuatilia sana mabadiliko hayo....acheni kukimbilia kulaumu majirani kwa kuchekelea kelele zetu vyumbani

Ilipofika hatua ya Zitto kuchukua fomu, ghafla homa ya uchaguzi ndani ya CHADEMA ikazidi kupanda na takriban vijana (siyo wote) wa CCM ambao wamekuwa na mawasiliano ya kirafiki na mwanasiasa mwenzao kijana kwa muda mrefu, walichukua maamuzi ya kumuunga mkono kwa nguvu kubwa na wote wakarejesha hoja nyingi zilizokuwa zikionyesha udhaifu mkubwa wa viongozi takriban wote wa chama hicho.
wewe una haki ya kuwa na urafiki nao lakini Zitto kamwe hana haki hiyo. Urafiki wako wewe hauathiri mapenzi mema yako kwa CCM lakini mahusiano yao na Zitto yana athari? Hivi ina maana umeacha kukubaliana na hoja kuwa wapo watanzania wengi wakiwemo waliojirundika CCM ambao wanashindwa kujiunga na CHADEMA kutokana na kukosa imani na bosi wako wanyemjua vilivyo kuliko hao mnaowalaghai kwa umahiri wenu wa uhandisi wa habari?

Ilipofikia hatua hiyo, mara Mbowe, Dk. Willibrod Slaa, Mnyika, Halima Mdee, Grace Kiwelu, John Mnyika na viongozi wengine wote wa CHADEMA ukimuacha Zitto wakaanza kuonekana kuwa ni watu wasiofaa, wakionekana kuwa hivyo ndani ya chama hicho na nje.
Then Zitto ana nguvu sana ndani ya chama? Sasa huoni kama mtu mwenye ushawishi kiasi hicho ndani ya chama ndio angelikuwa dawa bora kwa chokochoko zinazoendelea kwa muda mrefu humo ndani na hata kuweza kutetea uhalali wa hao viongozi wenzake machoni mwa wanachama?

Katika mnyumbuliko huo huo, ndani ya CHADEMA ghafla taswira ya Zitto mwenyewe ikaanza kujipambanua na hali ikazidi kuwa bayana aliporejea kutoka nchini Ujerumani alikokuwa amekwenda kwa shughuli maalum ya ushauri kwa rais wa nchi hiyo. Nguvu zake halisi zikaanza kubainika.
Kumbe ulikuwa unajua kuwa alikuwa ujerumani iweje kwenye makala ile ya mwanzo uzushe kuwa ametoweka kwa style ya kakakuona?

Kile ambacho awali kilionekana kuwa ni uamuzi wake wa kujaribu kutikisa tu kiberiti kikaanza kubadilika kwa haraka na mara Zitto akajitokeza na kuwa tishio la wazi kwa uenyekiti wa Mbowe na kwa hakika akaanza kuwa tishio la majaliwa ya kisiasa ya chama hicho na kambi nzima ya upinzani wakati huu akili za Watanzania wadadisi wa mambo wanapoangalia mustakabali mwema wa ushindani mkali wa kidemokrasia hapa nchini. Ni bahati tu kwamba kiberiti kingali kimejaa.
Kaka, iweje yeye kuwa tishio kwa mwenyekiti kuwe tishio kwa majaliwa ya chama. Ni chama kipi hicho maana yawezekana kuna chama kingine ndani ya chadema kama vile walivyokuwa NARC wa Kenya na vikundi vyao vya kimaslahi ndani ya chama kikuu...

Kwa hakika tafsiri yangu ya haraka haraka ikanipa jibu moja tu tena la haraka kwamba, maamuzi hayo ya Zitto yalikuwa kwa makusudi kwa ujinga wa wapambe wake wa kushindwa kuona mambo kuwa ulikuwa ikilenga kumhakikishia Rais Jakaya Kikwete ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 80 alizokuwa amezipata mwaka 2005.

Ingawa baadhi ya watu wanaweza wakadhani mimi ni mwendawazimu ninapoliangalia tukio la Zitto kugombea uenyekiti wa CHADEMA wakati huu na kuwapo kwa jitihada za makusudi za kumsafishia Kikwete njia mwaka ujao, ukweli unabaki pale pale kwamba, makosa yoyote ya kisiasa yanayoweza kufanywa na viongozi waadilifu ndani ya vyama viwili vya CUF na CHADEMA wakati huu, yana nafasi kubwa ya kumhakikishia Rais wetu ahueni kubwa.
Sio uwendawazimu kaka ni tatizo la mazoea ya kuspin ndio kinachokusumbua. Yaani unataka kujenga picha kuwa Zitto amechukua uamuzi mgumu kama huu ili amlinde Kikwete ambaye hata wewe unajua mpaka sasa hakuna mwenye uwezo wa kumzuia 2010.


Ina maana Kibanda unataka kusema kuwa Zitto ni supporter wa JK? Ina maana unataka kusema hujui ni nani Zitto alikuwa akimsupport wakati wa mchakato wa CCM?

Ukiliacha hilo, mara moja nikakiona kitendo hicho cha Zitto mwanasiasa ambaye siku zote nimekuwa nikimuunga mkono anaposimamia na kupigania masuala ya msingi, cha kuamua kuutumia vibaya mwanya wa kidemokrasia wa kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA kuwa kilichokuwa kikilenga kwa kujua au kutojua, kupunguza makali na kasi ya chama hicho cha kushinda viti vingi katika chaguzi za serikali ya mitaa, udiwani na baadaye ubunge.
Hapa ndio nashindwa kujua hoja hii inatokea wapi. Iweje mwanasiasa mwenye uwezo, mvuto, umaarufu na network kama aliyonayo Zitto ndio awe tishio la kupunguza makali ya CHADEMA na sio bosi wako ambaye watanzania kamwe hawawezi kumuamini kumpa nchi? Na hata wengine kusita kujiunga na CHADEMA hadi kuwe na sura nyingine ya kuaminika na watu makini...


Nilipojiridhisha kwamba hayo yote yanaweza kutokea kwa sababu tu ya uamuzi wa Zitto kugombea uenyekiti na yakafuata hata kama atashinda au kushindwa katika mchuano huo, nikaona nitakuwa sikuitendea haki ndoto yangu ya siku zote ya kuona demokrasia ya vyama vingi inastawi katika nchi hii ambayo kwa takriban miaka 20 tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi CCM imeendelea kujivunia rekodi madhubuti dhidi ya upinzani.
Kaka una uhakika kuwa una ndoto ya kuona demokrasia ya vyama vingi inastawi ama ni mmoja wa wale wachukia CCM tu ambao hupenda kutumia kauli mbiu ya demokrasia kujenga hoja zao wakati wao wenyewe sio waumini wa misingi na utamaduni wa demokrasia hiyo?


Ushawishi wote wa kundi hilo, ambao kwa kiwango kikubwa ulichagizwa na upotoshwaji mkubwa wa hoja yangu uliokuwa ikiratibiwa kwa karibu na vijana wa ndani wa CHADEMA waliokuwa wakimpigania Zitto na wale wa CCM na mawakala wao serikalini ulishindwa kulizuia Baraza la Wazee wa chama hicho, kumuacha kabla ya kumzuia kijana wao, kukiingiza chama chake na taifa katika balaa kwa kumsafishia Kikwete na chama chake mteremko. Ni jambo la kheri kwamba Zitto kwa dhati au kwa shingo upande aliliona hilo.
Kaka kweli una tatizo sio bure. Yaani umeshaanza kujenga kuwa vijembe ulivyopigwa haviwezi kutoka kwa watu independent isipokuwa wafuasi wa Zitto na "mawakala" wa serikali?

Please, mbona huelezi ni vipi Zitto huyuhuyu uliyekuwa ukimsifia kuwa amekuwa akitetea maslahi ya taifa leo hii anapokuja kushindana na mwenyekiti wake anageuka kuwa analeta balaa kwa kumsafishia kikwete. Hivi kati ya Zitto na wewe ni nani mwenye historia ya kumsafishia njia hadi kumwagia maua waridi Kikwete?


Kwa hakika unahitaji kuwa na akili za kuku za kusahau mapema ili kujidanganya kwamba, vijana ambao ni wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji au wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), wabunge, mawaziri na wanasiasa wengine serikalini wanaweza wakawa na mapenzi mema na CHADEMA hata kukiombea mema chama hicho wakati huu wakijua kuwa mwelekeo wa taifa ni Uchaguzi Mkuu ujao. Hivi kweli wanasiasa katika vyama vya upinzani na Watanzania wengine hawajui kwamba, ndani ya vikao takriban vyote vya CCM na jumuiya zake, katika miezi na siku za hivi karibuni wamekuwa wakijadili namna wanavyoweza kushiriki katika kudhoofisha nguvu za CHADEMA kwa Tanzania Bara (baada ya kuidhoofisha CUF) na CUF kwa upande wa Zanzibar?
Unategemea kuwa wakati ninyi mnakuja kumshambulia Zitto ambaye mtu kama wewe ulikuwa katika hali ya kuwasiliana naye hata alipokuwa nje ya nchi na hao watu/makuwadi wa mfumo fisadi watakaa kando kutotumia nafasi hiyo kwa maslahi yao? Kama CHADEMA wameamua kutumia busara zisizo na hekima ambazo sasa zinawanufaisha CCM ulitaka waangalie pembeni wasijigidie ulabu wa ushindi hata kabla ya muda wa kwenda uwanjani haujawadia?


Maswali kama hayo tunapaswa kujiuliza hata sisi wana habari ambao kama ilivyokuwa kwa vigogo hao wa CHADEMA kwamba ni kwa kiasi gani kalamu zetu zimechochea au kudhoofisha jitihada mahususi ambazo ziko wazi na zinazolenga kukisambaratisha chama hicho cha upinzani ambacho hakuna shaka kimejipambanua kuwa chama shupavu katika miaka ya hivi karibuni?
Hivi ni chama kilichonyesha ushupavu ama baadhi ya viongozi wake ambao ni wabunge ndio walioonyesha ushupavu huo? Viongozi ambao wengine wanapothubutu kushindana na wateule wenu wanageuka kuwa wabaya wa kuogopwa na kumalizwa kwa kutumia WINO WENU WA DAMU....

Wakati sote tukitafuta majibu ya maswali hayo, tunao wajibu wa kutambua kwamba, pamoja na uamuzi wa Zitto kutangaza kujitoa katika kinyang’anyiro cha uenyekiti, ile sumu kali ambayo tayari imeshapenya mishipa ya uongozi ya chama hicho, haina budi kutafutiwa dawa mahususi ya kuipatia tiba ya haraka kwani tayari vijana wa kazi wa CCM na mawakala wao wameshatamba kwamba wameshakiachia vidonda vingi chama hicho ambavyo wanadai vitaendelea kukitesa hadi wakati wa chaguzi zijazo. Kwa sababu hiyo basi, ninaweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba, kile ambacho leo hii kinaendelea kuelezwa na kusisitizwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa ni demokrasia kandamizi ya ndani ya CHADEMA (eti kwa sababu ya uamuzi wa wazee wa CHADEMA kumzuia Zitto kugombea uenyekiti) si tu kwamba ni majuto ya kukwama kwa ajenda yao, bali ni mkakati mbadala wa kuendelea kukiumiza chama hicho kwa malengo ya kisiasa. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo.
Acha kuendekeza huu ulemavu wa kufikiri kwa mapana na marefu yake na kukimbilia kulaumu majirani kwa kushindwa kulea familia yako. Kama baba unarudi nyumbani chakari unategemea watoto wanahitaji kwenda kwa jirani kuharibikiwa? Kibanda acha kupotosha na uanze kuface ukweli kuwa tumejenga nyumba bila ya misingi na sasa wakati tunaezeka vigae kaupepo kadugu kanaleta ufa. Badala ya kukimbia ukweli ni muhimu kukubali makosa kabla hatujawaingiza watanzania matatizoni huko tunapoelekea....

Na pia iweje unadai yamepita wakati bado mnaendelea kutumia WINO WA DAMU kusistiza uwongo mliotumia hadi mkauamini kuwa Zitto anatumiwa na wasio wana CHADEMA kama ambavyo mlifanya kwa CHACHA...Ina maana bosi/kamanda wako hajakutaarifu kuwa msitishe vita yenu kwa sasa ili yeye na Zitto waweze kuganga yajayo?
 
Last edited:
Wakuu zangu,
Mtasema yooote mabaya kuhusiana na Zitto lakini ukweli utabakia kwamba Zitto nimtu makini sana ktk Uongozi. Tatizo la Zitto ni uchungu mkubwa ambao humpa hasira akashindwa kujizuia..Ni kama maradhi ambayo huibuka tu pale anapoguswa sehemu za kipimo cha imani yake kwa wananchi.

Mkandara,

Asante kwa post nzuri lakini jana nimesoma Mwanahalisi as if nipo Dar (thanks ..... kwa kuwezesha hili).

Hivi kweli kama alimueSMS Dr. Slaa kuwa hajasaidia CHADEMA kama yeye na Mbowe walivyofanya. Hivi kweli hapa tufikirie mara mbili kweli? kweli kaka kweli. Namchukulia Zitto kama wewe lakini hili andishi kama hatajibu i will put him off.
 
Zitto;

Mie nipo shocked sana na haya mambo yanavyoendelea. Sio sahihi kwa viongozi wenzako kuja kukulaumua na kukubambikia mambo kwa sababu wapo humu kwa majina bandia.

Vile vile sio sahihi pia kwa wewe kuja na jina lako halisi na kuelezea mambo ya ndani ya chama humu.

Ushauri: kuwa mkiya kama Mnyika na Slaa wanavyofanya humu. Au naomba muone Dr Kitila, baada ya Kibanda kuwashambulia nadhani alielewa na kukaa kimya.

Yangu machache tu hayo!
 
Na baadaye akanyakua shule na hospitali zote za waislam kabla ya kumlazimisha Nyerere kuanzisha Bakwata. Baada ya hapo akawashika waislam wote na kuwaweka ndani kwa miezi kumi nane.

Hivi unajua kuwa sababu ya kumpiga Iddi Amini ilikuwa tu kwa vile Iddi Amin alikuwa muislam .... na na na na .... subiri nimalize .... na na na .. hivi unajua kuwa Tanzania ilikuwa nchi ya kiislam kabla ya Nyerere ah no ..... subiri ... kabla ya wakoloni!? upo?

Teh teh teh,

Kuna mengi yamenichekesha sana hapa ila hili linaonekana kushika nafasi ya juu. Kumbe Idi Amin alipigwa kwa sababu za kidini ..... damn you Nyerere...
 
Teh teh teh,

Kuna mengi yamenichekesha sana hapa ila hili linaonekana kushika nafasi ya juu. Kumbe Idi Amin alipigwa kwa sababu za kidini ..... damn you Nyerere...

Solomon,

Wala usicheke ukimaliza meza na panadol ya maumivu ya kichwa!!! humu siyo mchezo ni balaa!!
 
Teh teh teh,

Kuna mengi yamenichekesha sana hapa ila hili linaonekana kushika nafasi ya juu. Kumbe Idi Amin alipigwa kwa sababu za kidini ..... damn you Nyerere...

Solomon,

Wala usicheke ukimaliza meza panadol ya maumivu ya kichwa!! humu balaa!!
 
Teh teh teh,

Kuna mengi yamenichekesha sana hapa ila hili linaonekana kushika nafasi ya juu. Kumbe Idi Amin alipigwa kwa sababu za kidini ..... damn you Nyerere...

Solomon,

Wala usicheke we meza panadol ya maumivu ya kichwa!! humu balaa!!
 
Zitto that was too much. Hii habari ya mwenzio akimwaga ugali na wewe unamwaga mboga itawagharimu sana CHADEMA. Mshapoteza direction kabisa, yani kama ni credibility, graph imeshuka hadi zero na si rahisi kuipandisha.
 
Na Absalom Kibanda


kibanda ameendelea kumshambulia ZITTO na kuwaita kina KITILA WAJINGA.MAKALA HII KAIWEKA TANZANIA DAIMA JUMATANO HII.
Kwenye hiyo makala kibanda hajamtaja kitila, ila amesema washauri wa zitto, wewe ndio umemtaja kitila kama mshauri wa zitto...

Tafadhali kitila huko humu, kutokana na maneno ya kanda2 je wewe ni mmoja wa washauri wa zitto waliomlazimisha ajaze fomu za unyekiti akiwa airport kulekea ujerumani???
 
Zitto;

Mie nipo shocked sana na haya mambo yanavyoendelea. Sio sahihi kwa viongozi wenzako kuja kukulaumua na kukubambikia mambo kwa sababu wapo humu kwa majina bandia.

Vile vile sio sahihi pia kwa wewe kuja na jina lako halisi na kuelezea mambo ya ndani ya chama humu.

Ushauri: kuwa mkiya kama Mnyika na Slaa wanavyofanya humu. Au naomba muone Dr Kitila, baada ya Kibanda kuwashambulia nadhani alielewa na kukaa kimya.

Yangu machache tu hayo!
Mkuu shukran sana kwa maelezo ya mwanzo ila tu umemalizia vibaya kwani wapo viongozi wa juu wa Chadema hapa wakitumia majina bandia na wanamwaga shombo kichizi.. Wao ndio wachochezi wa habari zoote hizi na nina hakika Zitto asingevamia mkenge huu kama sii kuona wao wanazungumza machafu wakijificha nyuma ya majina Bandia. Ni watu ambao hata mim sikudhania wanaweza bwabwaja hovyo kiasi hicho..But kujificha kwao ktk majina bandia doesn't change who they are!
Na binafsi nadhani hakuna mtu mbaya duniani kama yule anayejificha nyuma ya jina au kuvaa ngozi ya kondoo kumbe ni Mbwa Mwitu.
 
Hapa ndio nashindwa kujua hoja hii inatokea wapi. Iweje mwanasiasa mwenye uwezo, mvuto, umaarufu na network kama aliyonayo Zitto ndio awe tishio la kupunguza makali ya CHADEMA na sio bosi wako ambaye watanzania kamwe hawawezi kumuamini kumpa nchi? Na hata wengine kusita kujiunga na CHADEMA hadi kuwe na sura nyingine ya kuaminika na watu makini...

Omar,

Hapa ndipo unapokosea ndugu yangu.

Zitto sio maarufu na mwenye mvuto na network kama unavyoamini. Zitto amefanya mambo kibao hivi karibuni yaliyompunguzia sana heshima na huo mvuto kwa watu wenye independent thinking.

Mshauri rafiki yako akae chini na kujipanga upya. Asidhani kuwa bado ni yule Zitto aliyefukuzwa bungeni.
 
Mkuu shukran sana kwa maelezo ya mwanzo ila tu umemalizia vibaya kwani wapo viongozi wa juu wa Chadema hapa wakitumia majina bandia na wanamwaga shombo kichizi.. Wao ndio wachochezi wa habari zoote hizi na nina hakika Zitto asingevamia mkenge huu kama sii kuona wao wanazungumza machafu wakijificha nyuma ya majina Bandia. Ni watu ambao hata mim sikudhania wanaweza bwabwaja hovyo kiasi hicho..But kujificha kwao ktk majina bandia doesn't change who they are!
Na binafsi nadhani hakuna mtu mbaya duniani kama yule anayejificha nyuma ya jina au kuvaa ngozi ya kondoo kumbe ni Mbwa Mwitu.

well said, ndio maana nasisitiza, hivi JF pamoja na hii motto yetu ya kutaka Tz nzuri, kuna mpambanaji yuko salama??? kwa nini hatujakemea haya yoote, hivi hao wengine tunaowona mashujaa wako salama?? na wakimwona mwenzao anatendea hivi wao wako upande gani? why our belive to these kind of leaders like SLAA, ZITO , n.k are only temporary if any wind comes, we all sway without FOCUSING ON THE MAIN GOAL!

Juzi Zitto alikuwa shujaa, leo eti msaliti,hatuangalii source ni nini! kesho nani atajitokeza kama sio kuwapa CCM faida?

CCM wangeona pamoja na haya yooote people are sticking with Zitto, CHADEMA etc, without any negative comments, CCM wangejua hwajamaa wamedhamiria kutuondoa!kwa hali hii wanalala na kunywa kwa raha zao wakitafuna nchi yetu taratiiiiiiiibu!
 
well said, ndio maana nasisitiza, hivi JF pamoja na hii motto yetu ya kutaka Tz nzuri, kuna mpambanaji yuko salama??? kwa nini hatujakemea haya yoote, hivi hao wengine tunaowona mashujaa wako salama?? na wakimwona mwenzao anatendea hivi wao wako upande gani? why our belive to these kind of leaders like SLAA, ZITO , n.k are only temporary if any wind comes, we all sway without FOCUSING ON THE MAIN GOAL!

Wewe una chuki kali na za kishetani dhidi ya wachaga...... watu kama wewe kujihusisha na JF ni kulishushia hadhi hili jamvi.

Juzi Zitto alikuwa shujaa, leo eti msaliti,hatuangalii source ni nini! kesho nani atajitokeza kama sio kuwapa CCM faida?

CCM wangeona pamoja na haya yooote people are sticking with Zitto, CHADEMA etc, without any negative comments, CCM wangejua hwajamaa wamedhamiria kutuondoa!kwa hali hii wanalala na kunywa kwa raha zao wakitafuna nchi yetu taratiiiiiiiibu!

Zitto kajichanganya mwenyewe na amelewa umaarufu na huo ushujaa unaousema hapo juu. Yeye sio MUNGU kwamba hafanyi makosa. Kawaida ya JF hapa nyani anakomwa giladi hata kama ana jina kubwa la kishujaa.
 
hii Notion ya kijinga ya kuamini Wahaya, Wanyakyusa na wachaga ni wahalifu wakiwa nje ya CCM inatoka wapi?? Hivi ni Wahaya,Wachaga na Wanyakyusa wangapi ambao wamewahi kupewa madaraka ya nchi hii wakiwa ndani ya CCM??

Kosa la Mbowe ni kuwa Mchaga?? kwa sababu Rai ya leo siyo tu imenishangaza bali pia imenufunua macho ya akili yangu kuwa kumbe vurumai yote ya wiki hii ndani ya CHADEMA ni MKAKATI maalumu ya kundi la WANAMTANDAO ndani ya CCM dhidi ya wapinzani wao CHADEMA!!
 
Hii notion ya kijinga ya kuamini kuwa Wahaya, wachaga, Wanyakyusa ni watu hatari wasiopaswa kuongoza siasa za nchi yetu itakwisha lini miongoni mwa wajinga na wachochezi uchwara wa ukabila nchini mweitu?

Mwakasege ni Mnyakyusa watu mahubiri yake wanayaamini, Saida Karoli ni Mhaya nyimbo zake wanazipenda na LUDOVICK UTOH ni Mchaga watu kazi yake wanaifanyia Rejea dhidi ya ubadhirifu uliojaa ndani ya serikali. lakini hawa wote wakithubutu kuingia kwenye Siasa wanaitwa ni watu hatari na wakabila.

Gazeti la Rai toleo la leo limenifanya nijiulize kama vurumai ndani ya CHADEMA ni suala la mapambano ya kupigania Demokrasia ua ni mchezo mchafu unaofanywa na wapinzani wa CHADEMA ili kukisambaritisha chama hicho kabla ya uchaguzi wa mwakani.

Hivi ni Sahihi kusema "Sitta asulubiwa na waislamu ndani ya Kamati Kuu na Halimashauri Kuu" kwa sababu tu wajumbe wengi ndani ya Vikao hivyo ni waislamu na yeye ni mkristo?

Kosa la Mbowe ni kuzaliwa Mchaga Kabila moja na mwanzilishi wa CHADEMA Edwin Mtei? mbona Warioba,Musuguri,Butiku na wengineo walikuwamo ndani ya serikali iliyoongozwa na Ndugu yao Julius Nyerere. Jee na Mwalimu naye alikuwa Mkabila?
 
Hii notion ya kijinga ya kuamini kuwa Wahaya, wachaga, Wanyakyusa ni watu hatari wasiopaswa kuongoza siasa za nchi yetu itakwisha lini miongoni mwa wajinga na wachochezi uchwara wa ukabila nchini mweitu?

Mwakasege ni Mnyakyusa watu mahubiri yake wanayaamini, Saida Karoli ni Mhaya nyimbo zake wanazipenda na LUDOVICK UTOH ni Mchaga watu kazi yake wanaifanyia Rejea dhidi ya ubadhirifu uliojaa ndani ya serikali. lakini hawa wote wakithubutu kuingia kwenye Siasa wanaitwa ni watu hatari na wakabila.

Gazeti la Rai toleo la leo limenifanya nijiulize kama vurumai ndani ya CHADEMA ni suala la mapambano ya kupigania Demokrasia ua ni mchezo mchafu unaofanywa na wapinzani wa CHADEMA ili kukisambaritisha chama hicho kabla ya uchaguzi wa mwakani.

Hivi ni Sahihi kusema "Sitta asulubiwa na waislamu ndani ya Kamati Kuu na Halimashauri Kuu" kwa sababu tu wajumbe wengi ndani ya Vikao hivyo ni waislamu na yeye ni mkristo?

Kosa la Mbowe ni kuzaliwa Mchaga Kabila moja na mwanzilishi wa CHADEMA Edwin Mtei? mbona Warioba,Musuguri,Butiku na wengineo walikuwamo ndani ya serikali iliyoongozwa na Ndugu yao Julius Nyerere. Jee na Mwalimu naye alikuwa Mkabila?

Unapatikana wapi mkuu nikupe kumi bora!!! Tufahamu kuwa Tanzania ina makabila zaidi ya 120!!! Na mimi mpaka leo ninajichanganya na kila kabisa ndani ya ofisi, nyumba za ibada, tunashirikiana shughuli mbalimbali bila kujali. Ni automatic kuwa kwa mtu yeyote duniani undugu upo ila inapokuja suala la utendaji tunaangalia utendaji zaidi. Na hivyo basi hata Chadema mnosema ni chama cha wachagga kwanza waanzilishi ni wachagga na wakajiunga wengine wakiwemo wachagga na makabila mengine na chama kikawa na nguvu sana baada ya kufa kwa NCCR-Mageuzi. Leo hii kwa sababu 2010 is around the corner mnaanza kukibomoa??? Au ndiyo response kwa ile kampeni za Sangara??? Ohooo tuwe makini.

Nataka wana JF wenzangu ambao wana uchungu na nchi hii na wanataka ikomboleke, wajihadhari sana na vibaraka wa CCM na mafisadi ambao wapo hapa jamvini kutumaliza. Wako kazini sasa usiku na mchana, na wanalipwa heavily kwa kazi hii!! Amini usiamini ila habari ndiyo hiyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom