Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Zitto, acha kuandika uongo na kuaminisha umma juu ya matokeo ya vijana .
Matokeo na ambayo ulikuwa nayo wewe kwani ulikuwa meza kuu na mimi sikuwepo meza kuu ni haya;
David Kafulila = 99
John Heche =83
Dady Igogo= 11
Julieth Rushuli= 11.

jumla zilikuwa kura 204.

Idadi ya wajumbe halali walikuwa ni 164.

Naomba uweke rekodi sahihi na ukijua kuwa kusema ukweli daima ndio njia ya kuweza kujenga, umelaumu sana Mrema na Mnyika hata unafikia mahali pa kudanganya.

Waseminari wana kauli moja kuwa ukweli ni mmoja na haugawanyiki.

naomba niishie hapo kwa leo na nitakujua kujibu mengine yote dhidi yangu siku zijazo .

Nawatakia mjadala mwema.

Mpaka kieleweke..Hivi ni kina nani waliosimamia uchaguzi? Hivi ni kina nani waliokuwa wanasambaza, kukusanya na kuhesabu kura? Hivi kati ya hao walikuwa na jukumu hilo ni wangapi walikuwa wakimuunga mkono Zitto na Kafulila na wangapi walikuwa wakiwapinga?

Unataka kusema kuwa kura zilizongezeka zilikuwa za Kafulila na sio za mgombea wenu? Na jee haiwezekani kuwa kura ziliongezwa kumuongezea nguvu Heche bila ya kung'amua kuwa mahesabu yatakataa na baadae ikaonekana bado mmeshindwa ndio mkaamua kutumia busara zisizo na hekima?

omarilyas
 
Mpaka kieleweke..Hivi ni kina nani waliosimamia uchaguzi? Hivi ni kina nani waliokuwa wanasambaza, kukusanya na kuhesabu kura? Hivi kati ya hao walikuwa na jukumu hilo ni wangapi walikuwa wakimuunga mkono Zitto na Kafulila na wangapi walikuwa wakiwapinga?

Unataka kusema kuwa kura zilizongezeka zilikuwa za Kafulila na sio za mgombea wenu? Na jee haiwezekani kuwa kura ziliongezwa kumuongezea nguvu Heche bila ya kung'amua kuwa mahesabu yatakataa na baadae ikaonekana bado mmeshindwa ndio mkaamua kutumia busara zisizo na hekima?

omarilyas

Na wakati huo Zitto alikuwa anafanya nini ili kuzuia haya yasitokee?
 
Omar ndugu yangu,

Mnazidi kulikoroga hapa na kulitia sukari. Kama Zitto anaona chadema iko vibaya hivi, anaweza:

1. Kuanzisha Chama
2. Kujiunga na CCM
3. Kujiunga na CUF au vyama vingine
4. Au kwenda kusoma kama alivyokwisha sema.

Haya mengine ya frame throwing sioni kama yanajenga nafasi yake ndani ya CHADEMA.

Yaani wewe na wenzio chuki na wivu wenu umewaharibu akili kabisa. Yaani mnapomshambulia Zitto hadi kupanga mikakati yenu ya kutumia magazeti kumuua kisiasa hamuoni kama mnabomoa nafasi yake na ya chama chenu.

Kwani si nyie na upambe na chuki zenu ndio mlikuja hapa na kuanza kusema kuwa Zitto anatumiwa na CCM wakati ninyi wenyewe ndio mabingwa wa kupokea "support" ya hao CCM wakati mnagombea uheshimiwa. Yaani mlipomuona Zitto amekubali kujitoa baada ya ushauri/shinikizo la wazee kutokana na heshima yake kwao ninyi mkatafsiri kuwa ni weak na kuanza kuendeleza sumu zenu kama mlivyowafanyia wengine wengi waliowahi kushindana na maslahi yenu.

Yaani mlipokuwa mnamdanganya Mzee Slaa na Mtei kuwa kuna hongo inatembezwa na Zitto ambaye ndio kioo cha kukuwa kwa matumaini makubwa ya watanzania kwa chama chenu hamkuwa mnaona maslahi yake wala ya chama chenu.

Na mlivyogubikwa na prejudices mmeona kwa kuwa sumu ya kuhamia CCM haifanikiwi malengo yake sasa mmegeukia CUF kwa saabu yeye ni muislamu. Halafu watu wakiwatupia nanyi sumu ya ukabila mnakimbia kuwaona wajinga.

Kaka, msijidanganye kuwa mtamuweza Zitto kirahisi kama wenzako hapo kabla na wewe sasa mlivyowaweza wengi wengine. Zitto ni nuru ya matumaini ya wengi wenye kuamini katika demokrasia makini na kamwe hatutanyamaza kuacha hizi propaganda zenu hivyohovyo mlizokariri zikituzimia nuru hiyo..

Na kwa taarifa yako atakayeondoka CHADEMA ni wakuja kama wewe na wenzako ambao Zitto alifanya kuwabeba kwenda huko na sio Zitto aliyeijua CHADEMA wakati wewe unavaa kikaptura kwenda shuleni.

omarilyas
 
Yaani wewe na wenzio chuki na wivu wenu umewaharibu akili kabisa. Yaani mnapomshambulia Zitto hadi kupanga mikakati yenu ya kutumia magazeti kumuua kisiasa hamuoni kama mnabomoa nafasi yake na ya chama chenu.

Zitto kajiharibia mwenyewe na wala asimlaumu yeyote kwa hili.

Kwani si nyie na upambe na chuki zenu ndio mlikuja hapa na kuanza kusema kuwa Zitto anatumiwa na CCM wakati ninyi wenyewe ndio mabingwa wa kupokea "support" ya hao CCM wakati mnagombea uheshimiwa. Yaani mlipomuona Zitto amekubali kujitoa baada ya ushauri/shinikizo la wazee kutokana na heshima yake kwao ninyi mkatafsiri kuwa ni weak na kuanza kuendeleza sumu zenu kama mlivyowafanyia wengine wengi waliowahi kushindana na maslahi yenu.

Zitto alianza kupata support ya ccm pale alipojiunga na kamati ya madini ya Kikwete kabla hajaanza kuchemsha kwenye issue ya Dowans.

Yaani mlipokuwa mnamdanganya Mzee Slaa na Mtei kuwa kuna hongo inatembezwa na Zitto ambaye ndio kioo cha kukuwa kwa matumaini makubwa ya watanzania kwa chama chenu hamkuwa mnaona maslahi yake wala ya chama chenu.

Na mlivyogubikwa na prejudices mmeona kwa kuwa sumu ya kuhamia CCM haifanikiwi malengo yake sasa mmegeukia CUF kwa saabu yeye ni muislamu. Halafu watu wakiwatupia nanyi sumu ya ukabila mnakimbia kuwaona wajinga.

Huu wa kuhamia CUF au CCM ni uamuzi binafsi wa Zitto. Mimi pesa yangu iko kwenye kuhamia CCM. Uswahiba wa Kikwete na Zitto ni mkubwa kuliko wa Zitto na Lipumba.

Kaka, msijidanganye kuwa mtamuweza Zitto kirahisi kama wenzako hapo kabla na wewe sasa mlivyowaweza wengi wengine. Zitto ni nuru ya matumaini ya wengi wenye kuamini katika demokrasia makini na kamwe hatutanyamaza kuacha hizi propaganda zenu hivyohovyo mlizokariri zikituzimia nuru hiyo..

Zitto kazima nuru yake mwenyewe kwenye issue ya madini na issue ya Dowans. Mengine usinilaumu mimi.

Na kwa taarifa yako atakayeondoka CHADEMA ni wakuja kama wewe na wenzako ambao Zitto alifanya kuwabeba kwenda huko na sio Zitto aliyeijua CHADEMA wakati wewe unavaa kikaptura kwenda shuleni.

omarilyas

Mhh .. hii kali Omar ... hapa sina cha kukujibu
 
Na wakati huo Zitto alikuwa anafanya nini ili kuzuia haya yasitokee?

Alukuwa anatekeleza jukumu lake kama mjumbe wa baraza lilokuwa likimchagua rafiki na msaidizi wake wa karibu kuwa mwenyekiti wake na sio kama msimamizi wa uchaguzi kama mlivyokuwa ninyi na wakati huohuo mnamsaidia mgombea wenu eti kumuonyesha Zitto kuwa mnajua siasa.

Yaani ninyi mnataka kujidanganya mmeshaota ndevu za kujua siasa zaidi ya Zitto? Shukuruni Zitto hana chuki binafsi wala rho ya korosho kama mlivyo ninyi ama sivyo mngeadhirika 4th September.

No wonder mkakimbilia Heche kama chaguo lenu. Yaani kama mlishindwa kuishi na Chacha Wangwe mnaweza kujidanganya kumuamini Heche kulinda ndoto na maslahi yenu binafsi? Nawashauri mtakaporudi katika uchaguzi tena mchagua Zombi la kulimanipulate tofauti huyo ambaye ni wazi mtakapoanza kutaka kumburuza angewageuka na kuwazika na chama chenu..

omarilyas
 
Alukuwa anatekeleza jukumu lake kama mjumbe wa baraza lilokuwa likimchagua rafiki na msaidizi wake wa karibu kuwa mwenyekiti wake na sio kama msimamizi wa uchaguzi kama mlivyokuwa ninyi na wakati huohuo mnamsaidia mgombea wenu eti kumuonyesha Zitto kuwa mnajua siasa.

Yaani ninyi mnataka kujidanganya mmeshaota ndevu za kujua siasa zaidi ya Zitto? Shukuruni Zitto hana chuki binafsi wala rho ya korosho kama mlivyo ninyi ama sivyo mngeadhirika 4th September.

No wonder mkakimbilia Heche kama chaguo lenu. Yaani kama mlishindwa kuishi na Chacha Wangwe mnaweza kujidanganya kumuamini Heche kulinda ndoto na maslahi yenu binafsi? Nawashauri mtakaporudi katika uchaguzi tena mchagua Zombi la kulimanipulate tofauti huyo ambaye ni wazi mtakapoanza kutaka kumburuza angewageuka na kuwazika na chama chenu..

omarilyas

Omar,

Unaandika haya yote kama msemaji wa Zitto au unaongea kwa niaba yako mwenyewe?
 
Mpaka kieleweke..Hivi ni kina nani waliosimamia uchaguzi? Hivi ni kina nani waliokuwa wanasambaza, kukusanya na kuhesabu kura? Hivi kati ya hao walikuwa na jukumu hilo ni wangapi walikuwa wakimuunga mkono Zitto na Kafulila na wangapi walikuwa wakiwapinga?

Unataka kusema kuwa kura zilizongezeka zilikuwa za Kafulila na sio za mgombea wenu? Na jee haiwezekani kuwa kura ziliongezwa kumuongezea nguvu Heche bila ya kung'amua kuwa mahesabu yatakataa na baadae ikaonekana bado mmeshindwa ndio mkaamua kutumia busara zisizo na hekima?

omarilyas

Omar

Mimi nilialikwa kwenye mkutano wa BAVICHA. Aliyesimamia mkutano alikuwa Mbunge Mwera, yeye aliyonyesha wazi kumchukia John Heche toka wakati anajieleza, labda sababu ya mivutano yao ya Tarime. Hawa wanajuana kwa kuwa waliogombea ubunge pamoja mwaka 2008.

Msimamizi msaidizi alikuwa Aidan Ndowa, huyu anatoka Kigoma anapotoka kafulila, msimamo wake hata wewe ulipokuwa Kigoma unaujua vizuri. Huyu ndiye aliyekuwa na makaratasi ya kura na kushikilia ya ziada.

Mwingine ni Ali Chitanda, huyu ni mpambe wa Zitto ambaye alimteua kuwa Afisa Vijana wakati Dr Slaa akiwa safarini na kumbadilisha idara aliyekuwa chini ya Mnyika. Maamuzi yale ya kumuondoa Mnyika kurugenzi ya vijana yamefanya mpaka leo CHADEMA haina mkurugenzi wa vijana. Pengine hii ndio imefanya hata Mnyika hakugombea Uenyekiti wa vijana, pengine alijua mapema kuwa Zitto hamtaki kama ambavyo amedhihirisha kwa maneno yake hapa JF. Chitanda ndiye aliyegawa karatasi kwa wajumbe

Wa mwisho ni Danda Juju Martin, huyu ni afisa aliyetumwa na Zitto kufanya kampeni Nyanda za juu. Unakumbuka huyu iliandikwa kuwa alipigwa chombe kwa sababu ya kusambaza maneno ya kuwachafua Mbowe na Mnyika. Huyu alisambaza na kukusanya karatasi za kura, huyu alituhumiwa kuwa ndiye aliyeandika kura za nyongeza.

Kura zilizozidi haziwezi kuhusishwa na John Heche kwa sababu yeye alilalamika kabla kuwa kuna taarifa kuwa kuna kura za nyongeza. Akapuuzwa. Akalalamika pia kuwa mbele ya meza kura zinaongezwa. Hakusikilizwa.

Gazeti la Leo limemnukuu Mwenyekiti wa Vijana wa Singida akieleza kura zilivyoibiwa, na jinsi Zitto alivyofurahia hali hiyo na kuondoka akisema kuwa 'leo vijana lazima watwangane'!

Nenda kamuulize Zitto, je anamtetea Kafulila kwa sababu anatoka naye wilaya moja au kwa sababu ndiye aliyekuwa akimtuma Habari Corporation kwenye kufanya majadiliano na kina Muhingo kuhusu namna ya kutetea mitambo ya Dowans dhidi ya hoja za CHADEMA na kina Mwakyembe?

serayamajimbo
 
Omar,

Unaandika haya yote kama msemaji wa Zitto au unaongea kwa niaba yako mwenyewe?

Yaleyale, mkishazoe kutumikia watu basi kila mtu ni lazima atumikiwe. Haya ni maoni yangu na nitaendelea kuwapa hata mkisema nini. ukitaka kujua zaidi nenda: www.omarilyas.blogspot.com

Acheni kujidanganya kuwa mtafanikiwa kupambana na Zitto. Tunaomjua na kutambua umuhimu wake katika kujenga demokrasia ya kweli na yenye uwezo wa kufanikisha kuona ndoto zetu za tanzanianjema kwa wote kamwe hatutawaacha mkipiga ramli zenu hapa....

omarilyas
 
Yaleyale, mkishazoe kutumikia watu basi kila mtu ni lazima atumikiwe. Haya ni maoni yangu na nitaendelea kuwapa hata mkisema nini. ukitaka kujua zaidi nenda: www.omarilyas.blogspot.com

Acheni kujidanganya kuwa mtafanikiwa kupambana na Zitto. Tunaomjua na kutambua umuhimu wake katika kujenga demokrasia ya kweli na yenye uwezo wa kufanikisha kuona ndoto zetu za tanzanianjema kwa wote kamwe hatutawaacha mkipiga ramli zenu hapa....

omarilyas

Omar,

Usiendelee kudhani kuwa Zitto ni MUNGU. Yeye ni binadamu kama wengine na anakosema. Zitto ana makosa yake mengi tu na nimekwisha yasema hapa. Kuhusu uongozi wa CHADEMA, nadhani labda unanifananisha mimi na mtu ambaye unadhania kuwa ni kiongozi wa CHADEMA.

Binafsi, mimi sijali sana vyama vinachagua vipi viongozi wake. Nikiwa US kipindi fulani, Democrats walikuwa wanataka kuchagua mwenyekiti wao baada ya kushindwa na Republicans mwaka 2004. Ile process ilikuwa so ugly na tangu siku hiyo niliapa kuwa sitafuatilia mambo ya ndani ya vyama na chaguzi zao.

Nimekupeni ushauri ku-cool down na kujipanga vizuri ila naona mmeamua kubomoana. Binafsi naamini kuwa Zitto ana mpango wa kuhama Chadema na anatafuta pa kutokea. Kuhusu future yake, mimi sio MUNGU kuamua kile kitakachotokea kwa Zitto in the future.
 
Zitto alianza kupata support ya ccm pale alipojiunga na kamati ya madini ya Kikwete

Namfagilia sana Zitto, lakini toka alipoingia Ikulu kupeleka ile kazi ya Tume ya Rais, Zitto Kabwe has never been the same. Akiwa mkweli siku akistaafu akaandika memoir, maana anapenda vitabu, atasema - kama ni mkweli - kwamba siku zile alijifunza kelele pekee hazilipi, lazima ujue ku negotiate power, kiswahili "kula na kipofu."
 
Kama Jamvi liliwapinga CCM walivyokaa kumuambia Dr.Bilali atoe Jina lake kumpinga Karume...na mifano lukuki CCM imefanya...on the name ya "Mshikamano wa Chama"...akina Dr. Bilali..na wenzake..like Nape walivyotoa Majina yao...Kitendo cha Chadema kufanya upuuzi huu....unaofanana na CCM....!!!

Hivi kwanini wasingeache Zitto akagombea na Mbowe "dhana ya kujifia yenyewe" ktk BOX la kura...?

What i can smell from Uamuzi wa Wazee wa Chadema wanajua wajumbe wao wanaakili za "Kushikiwa"...Kumuacha Zitto agombee na Mbowe kungeleta matokeo ambayo Wenye Chama Hawakujiandaa nayo Mapema...!!!

na Kama Zitto angetangaza mapema azma yake ya kugombea Uenyekiti....basi hivi tungekuwa tunazungumza Lugha nyingine kabisa....maana Zengwe lingekuwa kubwa kuliko Hili....!!!
 
Mwingine ni Ali Chitanda, huyu ni mpambe wa Zitto ambaye alimteua kuwa Afisa Vijana wakati Dr Slaa akiwa safarini na kumbadilisha idara aliyekuwa chini ya Mnyika. Maamuzi yale ya kumuondoa Mnyika kurugenzi ya vijana yamefanya mpaka leo CHADEMA haina mkurugenzi wa vijana.

Wa mwisho ni Danda Juju Martin, huyu ni afisa aliyetumwa na Zitto kufanya kampeni Nyanda za juu. Unakumbuka huyu iliandikwa kuwa alipigwa chombe kwa sababu ya kusambaza maneno ya kuwachafua Mbowe na Mnyika. Huyu alisambaza na kukusanya karatasi za kura, huyu alituhumiwa kuwa ndiye aliyeandika kura za nyongeza.

Kura zilizozidi haziwezi kuhusishwa na John Heche kwa sababu yeye alilalamika kabla kuwa kuna taarifa kuwa kuna kura za nyongeza. Akapuuzwa. Akalalamika pia kuwa mbele ya meza kura zinaongezwa. Hakusikilizwa.

haya nitayafuatilia kwa umakini kujua ukweli wake

Pengine hii ndio imefanya hata Mnyika hakugombea Uenyekiti wa vijana, pengine alijua mapema kuwa Zitto hamtaki kama ambavyo amedhihirisha kwa maneno yake hapa

Ama ndio imefanya Mnyika akaamua kujihusisha na propaganda hizi zinazoendelea hapa. Hata hivyo si kweli kuwa Mnyika hakugombea kwa sababu ya Zitto ila alisoma upepo akajua ni jinsi gani wanachadema haswa wa mikoani wasivyowapenda watu wa makao makuu. Lakini pia Mnyika ameponzwa na utekelezaji wake wa uongozi hapo makao makuu ambao wengi wao wamekuwa wakiona kama kujifanya anajua. Haya ni maoni ninayoyapata kila ninapojaribu kuhoji kulikoni kuhusu Mnyika ambaye kwangu mimi bado naamini ni mpambanaji muhimu katika kufanikisha ndoto yetu ya muda mrefu ya kujenga upinzani makini na Tanzania njema kwa wote.

Vilevile siamini kama Zitto ana kinyongo na Mnyika wakati hadi sasa anaamini kuwa anamuhitaji sana Myika kama atakabdhiwa jukumu la ukatibu mkuu hapo. Ukweli ni kuwa wakati sina habari na wengine suala la Mnyika na Halima Mdee kwa kweli linanitatiza sana hata mimi ninapofikiria jinsi ndoto ya kujenga upinzani makini zikipotea....Hawa ni watu muhimu sana kwa Zitto na naamini hawa pamoja na Zitto wanahitaji kukaa chini kuzungumzia kulikoni soon

Gazeti la Leo limemnukuu Mwenyekiti wa Vijana wa Singida akieleza kura zilivyoibiwa, na jinsi Zitto alivyofurahia hali hiyo na kuondoka akisema kuwa 'leo vijana lazima watwangane'

Unategemea angesemaje wakati naye ni sehemu ya spining inayoendelea?

Ni gazeti lipi hilo? Kama ni gzeti linalohusiana na Jesse Kwayu, Kibanda na yule Said Kubenea sishangai maana ndio waliopewa kazi ya "kummaliza kisiasa" Zitto. Magazeti mengine yapo kufaidika na hili sekeseke ambalo kama hao wanaojiona maadui wa Zitto wangeuwa na busara zenye hekima wangeweza kufanya liwe changamoto na sio sekeseke kama lilivyo sasa.

Nenda kamuulize Zitto, je anamtetea Kafulila kwa sababu anatoka naye wilaya moja au kwa sababu ndiye aliyekuwa akimtuma Habari Corporation kwenye kufanya majadiliano na kina Muhingo kuhusu namna ya kutetea mitambo ya Dowans dhidi ya hoja za CHADEMA na kina Mwakyembe?

Hivi kaka hiyo kazi ya uandishi huwa unaifanyaje endapo unafikia kuamini spining hizi. Yaani mnadanganya mpaka mnaanza kuamini uongo wenu. Kafulila ni msaidizi wa Zitto siku nyingi katika masuala mengi tu lakini pia Zitto anaamini kuwa ushujaa na umakini wake unaweza kuwa asset muhimu kwa uchaguzi ujao katika moja ya majimbo ya kigoma....

Nimjuavyo mimi Kafulila angembwatukia Zitto endapo angefanya kitu kama hicho. Hulka hiyo ndiyo inayomfanya Kafulila awe adui number mbili kwa sasa kwa hao wanaoleta majungu humu....ndiyo maana mara baada ya Zitto kuamua kukubali kujitoa wakajiunga kwa pamoja kufanya kampeni dhidi yake ndipo Zitto akagundua kuwa wenzake hawako genuine na kulinda maslahi ya chama ila maslahi yao wenyewe tu na akaanza kumfanyia kampeni za wazi Kafulila.

omarilyas




 
Last edited:
Acheni kujiuliza maswali mepesi haya....ina maana mtu ana haki ya kufikiria kivyake ama kufanya makosa kivyake hadi atumiwe. Mradi ninyi mnajioda ni wepesi wa kutumiwa basi kila mtu atakuwa anatumiwa....

No wonder we keep blaming umasikini na ujinga wetu kwa wazungu.....

Also, Mnyika anaweza kuwa smart na ambaye Zitto alimuamini sana na hata hivi juzi alikuwa akifikiria jinsi gani ya kushirikiana naye hapo mbeleni. Lakini haimanishi kuwa hana makosa na ni malaika asiyeweza kufanya maovu anayotuhumiwa kuyafanya...unadhani kila anayeandika haa anatumia jina lake kama mimi, zitto na wengineo?

omarilyas
Badala ya CCM ningefarijika sana kama ningesoma OMARY HOVYOHOVYO! Toka unakua mpaka leo bado tu haubadiliki. Kuna haja ya kuanzisha bendi ya mipasho!
 
Namfagilia sana Zitto, lakini toka alipoingia Ikulu kupeleka ile kazi ya Tume ya Rais, Zitto Kabwe has never been the same. Akiwa mkweli siku akistaafu akaandika memoir, maana anapenda vitabu, atasema - kama ni mkweli - kwamba siku zile alijifunza kelele pekee hazilipi, lazima ujue ku negotiate power, kiswahili "kula na kipofu."

Kuingia kwenye kamati ya madini ya Kikwete ilikuwa turning point ya maisha ya Zitto kisiasa. Yaliyofuatia na yatakayofuatia baada ya hapo ni historia.

Zitto mwenyewe amejaribu sana kila mara kueleza mafanikio ya kuingia kwake kwenye ile kamati lakini kila mara amejikuta akikosa hata kimoja cha kusema.
 
Humu ndani naona kuna majina 2 au 3 yameandikwa Zitto..akitofautisha herufi..na pia Kuna Jingine la Kabwe...!!!..Mhhh....?

Both Chadema na Zitto wana makosa kama kila mmoja ameamua kuweka "Uharo" wa Mwezie... Washabiki wa Chadema wanaona kuwa sasa hawamuhitaji Zitto...Zitto anaona hatakiwi...ikiwa washabiki wa Chama wanamponda Zitto na Viongozi wa Chama wako Kimya....ni message ambayo kwa mtu kawaida anatafsiri mie "Sitakiwi..."
 
...

Ni gazeti lipi hilo? Kama ni gzeti linalohusiana na Jesse Kwayu, Kibanda na yule Said Kubenea sishangai maana ndio waliopewa kazi ya "kummaliza kisiasa" Zitto. Magazeti mengine yapo kufaidika na hili sekeseke ambalo kama hao wanaojiona maadui wa Zitto wangeuwa na busara zenye hekima wangeweza kufanya liwe changamoto na sio sekeseke kama lilivyo sasa.



...

omarilyas

Omar,

Usitafute mchawi. Zitto anajimaliza mwenyewe.

1. Kuingia kamati ya madini ya Kikwete
2. Issue ya Dowans
3. Hili swala la kuflip flop kwenye kugombea
 
Omar

Kama Kubenea, Kibanda, Ansbert Ngurumo na Jesse wanampinga Zitto katika haya anayoyafanya ni watu makini zaidi ambao nawaunga mkono kwa hoja zao kuliko Balile, Muhingo, Msacky na Charles Charles wanaomtetea.

Zitto anasema Kibanda anafanya hivyo kwa kuwa ni Mkristu na mfanyakazi wa Mbowe, hebu muulize kwamba Kubenea muislamu na si mfanyakazi wa Mbowe kwanini anampinga?

Zitto anasema kwamba Jesse Kwayu anampinga kwa kuwa ni mchaga mmachame, lakini hailezi ni kwa vipi Mchaga Msacky anamuunga mkono na kupotosha habari za CHADEMA kwenye Mwananchi.

Zitto alimfananisha Mwakyembe na Hitler aliposema Rostam ni mhindi, alimuita kuwa ni mbaguzi. Lakini leo Zitto badala ya kujibu hoja za Nipashe anamtuhumu Jesse kwa kuwa ni mmachame!

Inaelekea Zitto ana chembe za udini, ukabila na ubaguzi; akikosa majibu ya hoja anazusha mambo yenye kuibua hisia ili kupata huruma.

Zitto anadalili za U-Augustine Mrema.

serayamajimbo
 
Humu ndani naona kuna majina 2 au 3 yameandikwa Zitto..akitofautisha herufi..na pia Kuna Jingine la Kabwe...!!!..Mhhh....?

Both Chadema na Zitto wana makosa kama kila mmoja ameamua kuweka "Uharo" wa Mwezie... Washabiki wa Chadema wanaona kuwa sasa hawamuhitaji Zitto...Zitto anaona hatakiwi...ikiwa washabiki wa Chama wanamponda Zitto na Viongozi wa Chama wako Kimya....ni message ambayo kwa mtu kawaida anatafsiri mie "Sitakiwi..."

Zitto inabidi asikilize ushauri wa wanaccm kama wewe na afanye maamuzi mapema ya kujiunga na chama la kijani. Kilichomtokea Zitto kwenye kamati ya madini ya Kikwete anakijua mwenyewe na nadhani ni wakati muafaka wa Kikwete kulipa fadhila kwa Zitto.
 
Omar,

Usiendelee kudhani kuwa Zitto ni MUNGU. Yeye ni binadamu kama wengine na anakosema. Zitto ana makosa yake mengi tu na nimekwisha yasema hapa. Kuhusu uongozi wa CHADEMA, nadhani labda unanifananisha mimi na mtu ambaye unadhania kuwa ni kiongozi wa CHADEMA.

Binafsi, mimi sijali sana vyama vinachagua vipi viongozi wake. Nikiwa US kipindi fulani, Democrats walikuwa wanataka kuchagua mwenyekiti wao baada ya kushindwa na Republicans mwaka 2004. Ile process ilikuwa so ugly na tangu siku hiyo niliapa kuwa sitafuatilia mambo ya ndani ya vyama na chaguzi zao.

Nimekupeni ushauri ku-cool down na kujipanga vizuri ila naona mmeamua kubomoana. Binafsi naamini kuwa Zitto ana mpango wa kuhama Chadema na anatafuta pa kutokea. Kuhusu future yake, mimi sio MUNGU kuamua kile kitakachotokea kwa Zitto in the future.

Ungekuwa unatoa hoja zako honestly naamini ungepitia makala niliyoandika katika hiyo blog hapo na ukajua kwa nini nasimama katika mstar huu hapa. Tatizo kwa kuwa mna utando wa kufikiri na muono wenu wa kisiasa unakuwashaped na CNN zenu tu basi mmekuwa wazembe kiasi cha kuja na conclusion zilizojichokea.

Alipochagua kuingia ndani ya tume ya madini kujua ukweli wa hali ilivyo katika sekta hiyo na kupata nafasi ya kuingiza maoni yake humo ambayo mengi yapo katika ripoti hiyo mkamuona kalaghaiwa na Kikwete.

Alipoamua kusimama kushindana na Mbowe mnakuja na kutumia na CCM na hao MAFISADI wenzenu ambao walichowazidi ni kuwa wao wana access zaidi yenu na hivyo kufaidika kuliko ninyi kama aliyosema PENGO.

Sasa amekuja hapa kuwaeleza kuwa mbinu zenu za kusambaza sumu na kumfrustrate kama mlivyozoea kuwafanyia wengine hapo awali haziwezi kuwasaidia zaidi ya kuwaumiza wenyewe mnakimbilia kuwa anatoa siri. Nani kasema mtanzania hapaswi kujua siri chafu kama hizo?

Aliposimama kupinga kutumika katika spining ya CCM inayoongozwa na Mwakyembe na wenziwe kuwadanganya watanzania kuwa there is a hope in CCM mkakimbilia kuwa amenunuliwa.

Cheap minds, cheap conclusions, cheap spinings

Kuhusu UMALAIKA kamwe sina imani za kuamini kuna kiumbe hapa duniani anaweza kuwa na umalaika na ndio maana mimi na yeye huwa tunatofautiana mengi sana na huwa namweleza bila ya kusita. Sasa mnataka muendelee kumwaga sumu zenu hapa halafu mnategemea ninyamaze. La hasha, hilo halitawezekana kama ambavyo mbinu zenu za kumchanganya ili awazilie chama ama mumfanye mliyoanza kuyazoea.

omarilyas
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom