Kuelekea Ujamaa Mamboleo - Toward Neo-Socialism

Kuelekea Ujamaa Mamboleo - Toward Neo-Socialism

Kuamua who belong to the league of my colleagues the Keplers et al.

Lete vidhibiti vya mchango wa kazi zako na matokeo yake katika kuboresha maisha ya mwanadamu...usilete link ya kubulogu chako kisicho na traffic
 
African Americans wengi sana wamechanganya damu kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa sana baadhi ya hao inventors kurithi genes za ubunifu kutoka wa wazungu.

Kuna uwezekano? How do you prove uwezekano/probability? Hypothetically?
 
Kwenye mivitabu...kwenye maabara....uraiani...mtaani...kiwanja...kwenye madanguro....kwenye msosi....you name it.

Kidhibiti gani cha Einstein umekiona danguroni? Na kipi cha Kepler umekiona kwenye msosi?
 
Kidhibiti gani cha Einstein umekiona danguroni? Na kipi cha Kepler umekiona kwenye msosi?

Nimetaja majina na sehemu randomly....kama unataka kujua michango yao zaidi fanya utafiti mwenyewe...google....nenda maktaba...uliza marafiki (kama unao)

Mfano...Kepler invented an improved version of the [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Refracting_telescope"]refracting telescope[/ame] (the [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Keplerian_Telescope"]Keplerian Telescope[/ame]),
 
Hahaa kumbe ni mambo unayatoa vitabuni tu!

Wikipedia sio kitabu....na kabla hata ya kuwekwa kwenye karatasi yalikuwa ni mawazo ya mtu (Kepler)....kwa hiyo yalikuwa kichwani kwanza...na huko ndio yalikoanzia.
 
Wikipedia sio kitabu....na kabla hata ya kuwekwa kwenye karatasi yalikuwa ni mawazo ya mtu (Kepler)....kwa hiyo yalikuwa kichwani kwanza...na huko ndio yalikoanzia.

Kitabu ni nini? Je, kilichopo ndani ya kitabu sio mawazo ya mtu pia? Na mawazo si huwa yanakuwa kichwani kwanza kabla hayajawekwa kitabuni?

Wikipidia hiyo ambayo unasema sio kitabu ndio hii:

http://infolitweb. blogspot. com/2007/ 10/how-big- is-wikipedia. html


Tuesday, 9 October 2007

How big is Wikipedia?

Nikola Smolenski has produced a visual of what Wikipedia would look like if it was printed in book format. Take a look at the 1250 volumes and how she's calculated it. Might be useful to show to students to give them some idea of the scale : then introduce them to how it's made up, and updated.
Posted by [...]

File: Size of English Wikipedia in August 2007.svg

From Wikimedia Commons, the free media repository




Size_of_English_ Wikipedia_ in_August_ 2007.svg‎ (SVG file, nominally 800 × 300 pixels, file size: 24 KB)
 
Kitabu ni nini? Je, kilichopo ndani ya kitabu sio mawazo ya mtu pia? Na mawazo si huwa yanakuwa kichwani kwanza kabla hayajawekwa kitabuni?

Wikipidia hiyo ambayo unasema sio kitabu ndio hii:

http://infolitweb. blogspot. com/2007/ 10/how-big- is-wikipedia. html


Tuesday, 9 October 2007

How big is Wikipedia?

Nikola Smolenski has produced a visual of what Wikipedia would look like if it was printed in book format. Take a look at the 1250 volumes and how she's calculated it. Might be useful to show to students to give them some idea of the scale : then introduce them to how it's made up, and updated.
Posted by [...]

File: Size of English Wikipedia in August 2007.svg

From Wikimedia Commons, the free media repository




Size_of_English_ Wikipedia_ in_August_ 2007.svg‎ (SVG file, nominally 800 × 300 pixels, file size: 24 KB)

Umeona jina hilo? Nikola Smolenski
 
Imani ya Ujamaa ina nguzo/misingi 5, wewe nini msingi wa imani yako?

Companero:

Ndio maana nilikuuliza kuhusu kwanini kulikuwa na gap kubwa kati ya wasomi wa enzi za wayunani (archimedes) na wasomi wa enzi ya reinassance (wakina Galileo).

Moja ya sababu kubwa ni imani. Wenzetu waChina na watu wa Ulaya mashariki walichukua ujamaa wao kama sera za maendeleo (period). Na sisi tunaofikiri kuwa ujamaa ni imani tunatumia muda mrefu kum-convert mwizi kuwa mjamaa.

Resources zote zinazotumika kumshawishi mtu kuwa mjamaa, zingetumika kwa kazi zingine labda tungekuwa mbali.

Sir Isack Newton, alikwenda kusomea upadri. Lakini katika chimbachimba yake akaona imani aliyofundishwa ilikuwa inatofautiana na mtazamo wake kuhusu Mungu. Na paper zake kuhusu Mungu hazijachapishwa kwa wingi lakini zinapatikana Hebrew University.

Na wewe unayependa kunukuu Biblia, ukisoma mambo ya Newton unaweza kuacha kumtajataja hapa.
 
Companero:

Ndio maana nilikuuliza kuhusu kwanini kulikuwa na gap kubwa kati ya wasomi wa enzi za wayunani (archimedes) na wasomi wa enzi ya reinassance (wakina Galileo).

Moja ya sababu kubwa ni imani. Wenzetu waChina na watu wa Ulaya mashariki walichukua ujamaa wao kama sera za maendeleo (period). Na sisi tunaofikiri kuwa ujamaa ni imani tunatumia muda mrefu kum-convert mwizi kuwa mjamaa.

Resources zote zinazotumika kumshawishi mtu kuwa mjamaa, zingetumika kwa kazi zingine labda tungekuwa mbali.

Sir Isack Newton, alikwenda kusomea upadri. Lakini katika chimbachimba yake akaona imani aliyofundishwa ilikuwa inatofautiana na mtazamo wake kuhusu Mungu. Na paper zake kuhusu Mungu hazijachapishwa kwa wingi lakini zinapatikana Hebrew University.

Na wewe unayependa kunukuu Biblia, ukisoma mambo ya Newton unaweza kuacha kumtajataja hapa.

Ndugu nilishasoma hizo treatise za Newton hasa zile za kuhusu unabii wa kitabu cha Daniel kwenye Biblia na nakubaliana naye hasa kuhusu kile kipindi cha Dark Arges. Ndio maana nashangaa mnaniuliza maswali ya vitabuni alafu hamtaki niwajibu kwa kutumia vitabu. Yes it is the move away from the tyranny of the 'universal' church and its monopoly of the 'truth' that ushered that period you are talking about. Naam mambo ya Renaissance, Reformation and Englightenement yalichochewa na uhuru wa kufikiri bila ukomo baada ya watu kuanza kusoma 'Latin Vulgate' na kuhoji ukiritimba wa wakuu wa dini waliokuwa wameuhodhi 'ukweli' wa kisayansi.

"She moves" - Galileo Galilei on the World Not Being Flat as then Believed by the 'Church.'
 
Ndugu nilishasoma hizo treatise za Newton hasa zile za kuhusu unabii wa kitabu cha Daniel kwenye Biblia na nakubaliana naye hasa kuhusu kile kipindi cha Dark Arges. Ndio maana nashangaa mnaniuliza maswali ya vitabuni alafu hamtaki niwajibu kwa kutumia vitabu. Yes it is the move away from the tyranny of the 'universal' church and its monopoly of the 'truth' that ushered that period you are talking about. Naam mambo ya Renaissance, Reformation and Englightenement yalichochewa na uhuru wa kufikiri bila ukomo baada ya watu kuanza kusoma 'Latin Vulgate' na kuhoji ukiritimba wa wakuu wa dini waliokuwa wameuhodhi 'ukweli' wa kisayansi.

"She moves" - Galileo Galilei on the World Not Being Flat as then Believed by the 'Church.'

Companero:

Ujamaa na historia ya Tanzania siku zote zime-play victim cards. Kwanza watanzania tuna tatizo la kuwa tulivyo. Halafu tunaongeza matatizo kwa ku-play victim cards.

Hivyo kuweka Truth nje kuhusu chanjo matatizo yetu inaweza kutusaidia. Kuliko kung'ang'ania miundo isiyo yetu kama Ujamaa.
 
Zakumi,
Mkuu, kwangu Mimi NDIVYO TULIVYO ina maana nyingi zaidi ya ubunifu maanake unaweza kuwa mbunifu lakini ukashindwa kuendeleza ubunifu huo..nitawazungusha kidogo unajua tena Mkandara kwa kuandika gazeti la mipasho!

Mathlan nchi kama Iraq ni wabunifu wa sayansi na technologia nyingi ambazo wao walishindwa kuzifanyia kazi kitaifa lakini sifa zote zinakwenda ktk nchi za magharibi na magwiji wa kuendeleza ubunifu..Canada walibuni mchezo wa basketball lakini waka invest more katika Hockey kwa sababu ndio mchezo wenye kuingiza revenue zaidi kulingana na soko la mazingira yao. Marekani wakatumia ubnifu huo wa canada kwao kutokana na sababu kama za Canada wakati sisi tunachukua mpira wa soccer kama ni ushabiki na mapenzi ya Kiujamaa..kudumisha udugu, jamii na Upendo.

Kwa hiyo ubunifu wowote hufuatana na investment inayotazama soko na mazingira ya sehemu sii maswala ya kufikiria kwamba Muarobaini unatibu Maleria kisha ukashindwa kuufanyia kazi ukaagiza madawa toka China yanayotokana na Muarobaini..

Hivyo, tofauti kubwa inayojitokeza wazi kati yetu na nchi zilizoendelea ni kwamba sisi tunajaribu sana ku apply makubwa yanayowashinda Ulaya ili twenda na wakati hali yale madogo yenye soko na yanayowaathiri zaidi wananchi tunayaacha wazungu wafanye investment kwa ajili yetu..
Tatizo kubwa la Ujamaa ni kutotazama nje ya box kiuchumi, kila kitu ni mfano wa imani ya mchezo wa mpira wa miguu (soccer) nchini yaani tunafanya mipango ya mchezo kutokana na mapenzi ya mchezo kuunda ushabiki unaolenga ujamaa wa kuunda umoja, undugu na kadhalika. Ukiwa Simba basi wewe Yanga hata wafanye nini huna thamani nao hata kama wana generate billions of revunue..Tupo radhi kushabikia Arsenal au ManU bila sababu zaidi ya Mapenzi ya mchezo lakini wenzetu utakuta ushabiki wao unatokana na yale Arsenal inayoyafanya katika jamii yao...Mpira kwetu ni kujenga urafiki, kudumisha upendo na umoja swala la fedha halipo ktk mikakati yetu...Ni mfumo uliotufanya tuwapende viongozi wetu hata kama they have done nothing ktk jamii yetu kutuendeleza isipokuwa kujenga upendo, Undugu na amani..huo ndio Ujamaa. Sasa turudi kwenye - Ndivyo Tulivyo..

Hii haifanani hata kidogo na Ujamaa. Imesimama peke yake, sii Kenya, South Afrika wala Tanzania tuna tofautiana sana..Priority zetu sisi Ndivyo Tulivyo...Kwa mfano kuna nguvu kubwa ya kuzuia Ukimwi, mabillioni ya fedha yanawekezwa ktk kupambana na Ukimwi lakini in reality wananchi wengi wa Tanzania wanakufa kwa Maleria..Sasa tujiulize inakuwaje wananchi wengi wanakufa kwa Maleria lakini nguvu kubwa inawekwa kwa HIV ambayo kwanza tunategemea misaada toka nje hata hizo Condom tunashindwa kutengeneza lakini tunaweza kutengeneza mifuko ya kubebea nyanya ambayo hugawiwa bure kwa kila mnunuzi..

Hakuna mikakati tunachokifanya zaidi ya ile ya kujipanga kanisani kusubiri misaada na mara zote tunatazama maradhi ya Kiuchumi yanayozikabiri nchi za Ulaya kutibu maradhi....Nikiwa na maana maradhi kama HIV hata kama tusipofanya mikakati ya nguvu, elimu, fedha na dawa zake zitaletwa tu kinachotakiwa ni sheria (policy) kuruhusu dawa hizo zitumike kwani soko lake lipo na elimu ya maradhi haya tunaitegemea kutoka nje..

Nguvu yetu inatakiwa kuelekezwa zaidi kwa Maleria kiuchumi, Tiba, kinga na hata kuuondoa kabisa ni kazi ndogo sana ya kibamaabara ambayo ingeweza ku generate revenue kubwa kwetu kwa sababu Asia na kusini kote kwa sahara tunategemea madawa toka nje wakati raw material inatoka kwetu... Maleria ni ugonjwa unaotibika, ugonjwa unaoweza kukomeshwa kirahisi zaidi, lakini ktk nchi za kusini mwa jangwa la Afrika watu wanakufa wengi kuliko hesabu ya vita ya Iraq na Afghanstan combined!..

Now, nikirudi ktk Ujamaa kitu pekee ambacho nilikipenda kuhusiana na Ujamaa ni ktk kuelewa mazingira unayoishi na kutafuta tiba ya matatizo hayo kulingana na hali iliyopo.. Miaka ya Nyerrere, Maleria ulikuwa ugonjwa mdogo sana, Kipundupindu kilipokuja (1975-76)tulikimaliza within 5yrs kikawa history.. Ukoma na maradhi mengine yote ya tropical yalikuwa na chanjo za kinga na dawa kila zahanati utakayokwenda tena bure kwa kila mwananchi..Hivyo ukiwa na jamii yenye afya ni rahisi kupanga mikakati ya uzalishaji..
Kwa ujumla wa yote Ndivyo Tulivyo ni pale tuliposhindwa kuwa wabunifu au kutumia Ubunifu ktk investments zetu.. Tumeshindwa kufikiria nje ya box kwamba maradhi kama Maleria yanahityaji nguvu zetu kupata dawa za Kinga na ponya kwa sababu soko lipo ndani na nje.Kuna nchi jirani na Asia ambazo zina maradhi kama yetu na wanahitaji dawa hizo hivyo nguvu kubwa iwekwe ktk kufikiria uzalishaji wa dawa za kinga na ponya ya maradhi hayo badala yake tunazidi kusisitiza uagizaji wa dawa hizi toka nje bila kuweka regulations ambazo zitawakinga wananchi na taifa zima kuingia hasara ya dawa feki au kutazama uwezekano wa uzalishaji wa dawa hizo nchini..

Na ukitazama Elimu, mkuu wangu mambo mengi tunayosoma Tanzania ni kuhusu mazingira ya Ulaya. Kuna masomo mengi tunayafundisha Afrika hayafundishwi Ulaya kwa kutazama Afrika wala Asia...Tena unaweza kuta graduates wao hawajui lolote kuhusiana na Wayunani isipokuwa wabunifu wa yale wanayo invest kwao..Sisi tunasoma kila kitu cha wageni hata ktk maswala ambayo hayahusiani kabisa na mazingira yetu wala hatuna interest ya ku invest katika maswala hayo..

Kwa hiyo ktk kila mfumo wa Kisiasa kulikuwepo na mazuri yake na muhimu zaidi tunapozungumzia Ujamaa nadhani tutazame zaidi pande zote mbili ktk mazuri na mapungufu yake.. Binafsi naamini kabisa kwamba Ujamaa uligota zaidi ktk huduma bila kufahamu kwamba biashara ni invisible hand inarahisisha huduma zote kutokna ana ubunifu unaohamasisha investment ktk soko na mazingira itokane na elimu au mtaji..

Hofu kubwa ya Unyonyaji ktk Ujamaa ndicho kiilikuwa kilema cha mapenzi ya Ubepari (biashara) mfano wa Mwanamke anayeogopa kuingia ktk relationship kwa sababu anaogopa bwana atambwaga mara tu akisha fungua miguu..Mara zote hofu kama hii mwanamke huyo hupata taabu kufanikiwa lakini hofu hiyo haimfanyi kutokuwa mwanamke mzuri mwenye tabia nzuri anayefaa kuolewa!..

Imetosha...
 
Back
Top Bottom